Wednesday, June 15, 2011

Tatizo sio Posho ni haki na usawa katika kugawana keki ya taifa....

SISHANGAI kwanini baadhi ya wabunge hawajagutukia mtego uliopo katika kashikashi ya posho iwepo au isiwepo. Kwa tunaojaribu kuangali mbali na kuona mbele tunatambua kwamba tatizo hapa sio POSHO bali ni ile hali ya umaskini wa kutisha aliyonayo Mtanzania wa kawaida.


Kwa bahati mbaya waheshimiwa wabunge wetu wanachokiona ni kutaka kuporwa na pengine na wale 'walioneemeka kwa njia nyingine' hata kile ambacho bado wao wanakiona ni kidogo.

Wale waliokwishazunguka mijini na vijijini baada ya kubaini kwamba wanaweza kutumia matatizo na dhiki mbalimbali za wananchi kama mtaji wa kisiasa hawajachelewa kufanya hivyo.
Na wale wanaokurupuka na majibu ya haraka haraka bila shaka watajikuta wanajiumbua wenyewe na kubaki wameshangaa ni kitu gani kinachoendelea.

Wenzetu wasingelikuwa wanasumbuliwa na ule ugonjwa niliowahi kuusilimisha kwa jina la 'ndivyotunavyofikir' wangekuwa wajanja kidogo tu, wangelitambua wanaowawakilisha wanauliza na wanataka majibu ya ni nini taifa hili linalovuna na kinachovunwa kinagawanywa vipi ?

Ni vigumu kuandika makala kama hii bila kuegemea upande wa walalahoi na wasiofaidika na mfumo uliopo lakini nitajaribu kutokupendelea upande wowote kwa mara ya kwanza.

Mlipuko wa mawasiliano rahisi kati ya mtu na mtu kupitia simu za mkononi, redio, televisheni, tovuti, blogi, twitter na facebook mijini na vijijini vinawaarifu wananchi mambo mengi kupita hata uwezo wao wa kuyatafakari na kuyachambua. Lakini, kila mmoja akihabarika kiasi cha kuanza kuuuliza je hicho kinachovunwa na taifa ni
nani anayekipata, yuko wapi hapa nchini, anakipata wakati gani, na kwanini anapata yeye na sio wengine ?

Dakika moja tu inatosha kwa mtoto wa mkulima kule kijijini kufahamu kutoka kwa mwanawe kwamba senti anazomtumia inabidi zipungue kwa sababu uwezo wake wa kifedha sasa umeterereka. Gharama mbalimbali zimepanda na wa kulaumiwa ni serikali na chama tawala. Kwa maneno mengine, kazi ya kuwaumbua, kuwasingizia, kuwapakazia na kulaumu viongozi na serikali imekuwa rahisi kufikishwa hadi kijijini -ambako watu kwa kawaida walikuwa wamelala na wasioamin kwamba serikali inaweza kuwa na nia mbaya na wanachi wake achilia mbali kuwafanyia ubaya huku ikijua inawafanyia ubaya.


Je, kuna usawa na haki katika kile kinachopatikana kwa maana wananchi wote wana fursa sawa, wako huru kukifanya au kuna wanaojichagua na kufaidi wao tu. Na kama kuna matatizo, je, kuna wanaoyashughulikia matatizo hayo kwa wakati na kwa manufaa ya jamii husika.
Au kila kiongozi toka ngazi ya chini hadi juu yuko 'bize' na mambo mengine lakini sio matatizo ya wananchi. Na je, wale wanaotumwa kwenda kuwawakilisha wananchi je wanafanya hivyo au wanawakilisha watu au taasisi nyingine ?


Je, mfumo na miundo ya kiuchumi na kijamii iliyopo inaonesha kuwa na uwezekano wa kuwapa wananchi fursa ya kutatua matatizo yao na kujiendeleza wao wenyewe bila kuhadaiwa na siasa au wanasiasa au watu wengine ?

Hii ni miaka ambayo wananchi watakuwa wanauliza maswali yaliyokuwa hayaulizwi sana huko nyuma. Mathalani, wanaweza kuuliza je, hao wanaopata kilicho kikubwa na zaidi ya wengine kutoka kwenye keki ya taifa wanastahili kupata wanachokipata. Au wanakipata kitu wasichokitolea jasho, yaani, wasichokistahili kwa uhalali kabisa, kwa maana kuwepo kwao ni mzigo tu kwa wananchi na watu hao hawasaidii wananchi kuapta unafuu wowote katika maisha yao ?

Yaani, wanaopata zaidi wanakula haramu na jasho la wananchi bue kwa kupata zaidi au wanapendelewa au wanajipendelea bila kuwa na sababu yoyote ya kuridhisha? Utakumbuka wale tulioikuwa tunasoma sekondari za kulala au hata za siku ambazo kuna chakaula cha mchana au jioni. Katika dhambi kubwa niliyowahi kujisikia ni ile ya kujimegea mimi binafsi wali mwingi na mboga nyingi kuliko wanafunzi wenzangu tuliokuwa tunakula kwenye meza moja. Nilifanya hivyo baada ya kuguswa na kosa nililolifanya. Nikaugawa tena wali wangu kwa kuwapunguzia wenzangu na mimi kubakiwa na kiasi kidogo kuliko wao. Kuanzia hapo, palikuwa hapana swali ni nani anastahili kugawa chakula katika meza yetu.

Swali dada na hili ni lile la nani wanaopata kidogo au wanaokosa kabisa ? Na kama kukosa kwao kunatokana na wao kuwa duni, wajinga, wavivu na wasiojituma kwa kiasi hicho au kwa kuwa wamezidiwa tu ujanja na uelewa na wale waliotangulia kupata mitaji na wanaowaongoza?

Kwanini wanakosa ? Kwanini hawatosheki, hawaridhiki na hawashibi kwa yale mazuri viongozi na wanasiasa wanayoamini tayari wamekwishawafanyia toka kuwepo kwao madarkaani?

Na je, mfumo mapokeo tuliourithi na tulio nao hadi leona uloanzia toka tukiwa na watu milioni 9 (1960) unafaa baada ya miaka 50 ambako tunakadiriwa kuwa watu milioni 50 ? Au kwa maneno mengine, kama Karl Marx alivyohoji, je, mahesabu yetu ya 'production' na 'reproduction' na 'redistribution' ya mapato ya taifa yapo sawa na sio yameachiwa huru mno kiasi ambacho tunachezea bomu la tofauti kubwa ya kipato kati ya walionacho na wasionacho?

Tanzania inafikisha miaka 50 ya Uhuru wa benderea ikiwa na tofauti kubwa kati ya mtu wa kipato cha chini na yule wa kipato cha juu pengine kwa uwiano wa 1: 10,000. Hii sio tu ni hatari bali ni aibu na fedheha kwa nchi ambayo Mungu na kiongozi wake wa mwanzo alishawaonyesha ubaya wa tofauti kubwa namna hii kati ya walionacho na wasio nacho.

Na kama Wahenga walivyosema,' Mwenye shibe, hamjui mwenye njaa', jambo hilo sasa, yaani walionacho kushindwa kujua kwanini kuna umasikini na kwanini watu hawana fedha mifukoni mwao na majumbani mwao, limefikia hadi kwenye ngazi za juu za uongozi wetu? Majemadari wanaotakiwa kuwatoa Watanzania toka kwenye umasikini hawajui upana, urefu na kina cha umasikini nchini mwao na miongoni mwa watu wao!!

Upo uwezekano mkubwa kwa nchi hii na viongozi kujiabisha kuhusu hali ya maisha ya Mtanzania kutokana na kulewa na sifa za viongozi wa nje na wale wanaowatumia kisiasa kwa faida zao wanazozijua wao wenyewe.

Katika kupanga tufanye nini wakati wa kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru tuwe waangalifu sana ili sherehe hizo zisiwe chanzo cha kujiaibisha na kujifedhehesha badala ya nafasi nzuri ya kurekebisha makosa yaliyopo na kuifanya siku hiyo siku ya kuzindua yale yatakayowapa wananchi matumaini na faraja.

Ni wakati muafaka kwa hiyo kuoanisha suala la 'posho ya wabunge' na lile la 'riziki ya kila siku ya mwananchi wa kawaida' na wawakilishi wetu kujiuliza kama hakuna uhusiano kati yake na hali halisi ya yule wanayemwakilisha bila kuzingatia dhiki na umaskini wake huko bungeni na kulipa hilo uzito unaostahili bila kuburuzwa na mtu au taasisi yoyote ambayo imeamua kufumbia macho jambo hili ?
Au kuna wanaowafunga macho kwa kitambaa cha khaki tena khaki nyeusi katika usiku mweusi wa hali halisi ya kiuchumi ya Mtanzania?

Je tunaweza kuongeza kinachovunwa? Kwa njia gani na mbinu zipi na mikakati ipi ya chapchapu ? Na hivi ukiwauliza Watanzania kwanini wao ni masikini na wewe una wajibu wa kuwatoa toka kwenye umaskini je, unawajibika kweli na je, unawatendea haki Watanzania masikini? Je, Taasisi ya Utafiti kuhusu umaskini hapa nchini imefikia wapi na yale ambayo imekwishayatafiti hadi wa leo yamefanyiwa kazi kiasi gani? Kwa maneno mengine, je, taasisi hiyo imekuwa na manufaa yaliyokusudiwa kwa Watanzania masikini au imewashibisha tu waliomo katika taasisi hiyo na nyingine kama hizo?

Na, je, ukiritimba katika masuala ya uongozi wa kijamii na uchumi ndio utakaotusaidia kutoka kwenye umasikini na matatizo yetu au tunaung'ang'ania tu kwa sababu ya mazoea na uoga wa kujaribu kilicho kipya?

Maana kuna wanaoamini kwamba serikali kuu inapswa kugawa madaraka ya maamuzi na utekelezaji sio tu kwa mikoa, wilaya, vyama vya kisiasa, mashirika ya kiserikali na yasiyo ya kiserikali, makundi mbalimbali ya kijamii na watu mmoja mmoja kushiriki na kuchangia kikamilifu katika kuziona na kuzitumia fursa za kiuchumi na kijamii zilizopo nchini kuliko tulivyowahi kufanza huko siku za nyuma na vilevile kuyatafakari matatizo mbalimbali yanayowakabili Watanzania na kisha kuweka mkakati unaosadikisha kwamba 'utatuaji matatizo kila sekta, katika kila jamii' kila kona nchini ndiyo ajenda yetu ya kwanza kwa kila mpango tulionao na tutakaokuwa nao.
Tuiaminishe pia jamii yetu kwamba tukijipanga upya, kimkakati, kiakili na kwa hekina na busara zaidi tunaweza kupatia ufumbuzi sisi wenyewe matatizo na changamoto nyingi zinazotukabili.

Na pale msaada wa serikali, sekta binafsi na wasamaria wema inapohitajika inakuwa ni pale ambapo hatuna ujanja kwani kiakili, kiteknolojia na kirasilimali nyinginezo tumekwama na hatuna ujanja.

Nguvu na akili-jamii na ujasiriamali-kijamii ndio njia pekee ya kuinua ubora wa maisha ya Mtanzania.

Serikali yetu lazima ifike siku irudie maneno ya Mwalimu Nyerere kwamba, 'Serikali na Watanzania hatuna fedha. Na fedha na mtaji wetu ni akili, nguvu, maarifa, juhudi na bidii zetu wenyewe katika kutatua matatizo na changamoto mbalimbali zinazotukabili.'


Serikali ikiendelea kujifanya ndio bwana mkubwa, tajiri, ina mali, ina uwezo, ina nguvu na inaweza kila kitu na haishindwi na chochote lazima kuna siku tataibika na tutakwama.

Ninaamini ni Watanzania ndio wanaostahili kuwa BWANA MKUBWA, MATAJIRI, MFANO WA MUKTADIRI, KWA MAPENZI NA BARAKA ZA MWENYEZI MUNGU WANAWEZA KILA JAMBO, HAWASHINDWI NA LOLOTE na wingi, nguvu, matakwa na maslahi yao ndiyo yanayopasa kutawala na kuendesha nchi hii na sio vinginevyo. Demokrasia kwanza, mengine ni mazungumzo baada ya habari.

Tunaweza kumlaumu Mtanzania kuwa chanzo cha kukosa mahitaji yake ya msingi, maradhi, ujinga na umaskini wake lakini tusisahau kwamba upo uwezekano pia ikawa ni mundo na mifumo tuliyo nayo na ukiritimba wa serikali katika mipango, maamuzi na utekelezaji wake vikawa ndio sababu ya umasikini wa Mtanzania.

Katiba, wabunge na posho...

LABDA wabunge wanaotaka wasilipwe posho wameaona kile wanachokula hakilingani na kazi wanayowafanyia masikini wa Kitanzania katika jitihada zao za kutuondoa na umaskini, ujinga na maradhi.

Wametangulia Katiba katika kuleta mabadiliko ya kimsingi yanayohitajika, kwa maana ya kwamba, kipato cha kila kiongozi wa Kitanzania kwanza, kinatakiwa kinaoanishwa na mchango wake katika kupiga vita umaskini, ujinga na maradhi awali ya yote. Na kwa upande mwingine ipo haja kujenga miundo na mifumo inayomsaidia mwananchi kuondakana na umaskini badala ya miundo inayomwingiza mwananchi kwenye umaskini zaidi.

Wakati tunasubiri ujio wa Katiba mpya na namna itakayolishughulikia suala la keki ya taifa na inavyostahili kugawanywa kwa namna ambayo kila Mtanzania anakuwa na arri na motisha ya juu kuiondoa nchi hii kwenye daraja la tatu na umaskini mkubwa kwenda kwenye daraja la pili la kiuchumi kidunia lenye nafuu, utu na ubinadamu zaidi.

Saturday, June 11, 2011

Tofauti kati ya Uchumi-nchi na Uchumi-mtu

KUNA msemo ambao hudhalilisha sana matumizi ya takwimu katika taarifa mbalimbali unaosema kuna aina tatu za uongo (Ona kitabu cha Lies, Damn Lies and Statistics). Kuna uongo wa kawaida, halafu kuna uongo mweupeee na uongo wa tatu unaitwa TAKWIMU !

Katika kitabu hicho mwandishi anajaribu kuoensha kwamba uongo ulio mbaya na wa hatari zaidi ni takwimu kwa sababu wanaoziandaa takwimu huziandaa aghalabu kupotosha ukweli ulivyo; wanaozitangaza takwimu wanajua wanasema uongo lakini wanaamini katika uongo huo na wanaosikia uongo huo hawajui waamini lipi kati ya takwimu kadhaa zinazokuja kivyakevyake kila moja ikiwa na ajenda yake ya siri.

Uchumi-nchi ( Macroeconomics ) na uchumi-mtu ( Microeconomics) vyote huwasilishwa kinadharia katika takwimu zinazohusiana na maeneo husika. Mara nyingi sio rahisi kuchukua takwimu na hesabu za kila eneo kwa hiyo wakati mwingine watu huchagua kati ya maeneo kadhaa na kuwasilisha kile wanachoamini kinazungumza kwa faida ya wengine wote.

Ndio maana leo kuna Watanzania wanaoshindwa kuelewa na wanaoshangaa kwanini wakati nchi inaendelea kwa kasi kubwakutokana na takwimu zinazoonesha kuwa eti pato la Mtanzania sasa ni zaidi ya dola 500 kwa mwaka na kuwa pato la taifa linakuwa kwa asilimia sita kama sio zaidi ya hapo kuna Watanzania wasioliona hili na kulisifia na kuwasifia viongozi wao.

Ukiwauliza wataalamu wa uchumi kama sijakosea tatizo hili linaletwa na viongozi wetu kujikita zaidi katika masuala ya uchumi-nchi na kujisahau au kuwaachia wababaishaji kusimamia masuala ya uchumi-mtu.

Kwa tafsiri uchumi-nchi ni uchumi-jumla wa nchi ambao daima hutoa picha kubwa kiuchumi kwa nchi na hauangazii tu hali ya kiuchumi ya mtu mmoja mmoja. Japo chumi hizi mbili zinategemeana, zinaingiliana na kuoana sana lakini kila moja ina nafasi na wajibu wake katika jamii husika. Kwa upande mmoja, maendeleo ya nchi kiujumla huwa kivutio kwa wawekezaji, wabia wa kibiashara na kiuchumi na watalii na watu kama hao, wakati hilo halimpi sababu mwananchi mjini au kijijini kufarajika kwa sababu anaweza awe ananufaika na uchumi-nchi au kinyume cha hivyo.

Hali ilivyo kwa Tanzania ni asilimia ndogo sana ya Watanzania ndio wanaonufaika na takwimu na hali halisi ya uchumi-nchi . Hawa wanaonufaika ni pamoja na viongozi wa nchi wanaolipwa mishahara na marupurupu mazuri na wakati mwingine hawalipi kodi mbalimbali; wawekezaji na wafanyabiashara na wenye viwanda wanaoweza kuwabebesha walaji gharama zinazoongezeka katika biashara au viwanda vyao na hivyo kubakia pale pale kiuchumi hata kama mfumuko wa bei na gharama mbalimbali zimezidi kuongezeka mno katika kipindi kilichopita.

Wengine wanaonufaika na uchumi-nchi katika hali ambayo bei na mfumuko wa bei vimekuwa vikikuwa siku hadi siku ni wale waliomo katika mashirika ya kimatiafa, mashirika ya kiserikali na walanguzi wa kila aina na ukubwa.

Kwa hiyo uchumi-nchi unaoweza kuwa umekua au unakua lakini faida yote inaenda kwa wale wanaolipwa mishahara na marupurupu na posho nene, wawekezaji, wafanyabiashara, wenye viwanda, makampuni makubwa ya kitalii, waagizaji mafuta na peteroli, wenye viwanda, wafanyakazi wa mashirika ya kimataifa, wafuasi wa chama kinachotawala na watu kama hao tu na sio kwa Mtanzania wa kawaida.

Katika hali kama hii nchi inakuwa kama timu ambayo wachezaji fulani kwa kuitwa wachezaji nyota basi wanalipwa mamilioni ya fedha huku wachezaji wenzao wakipata chini ya nusu ya kile wenzao wanachokipata. Kimya kimya wachezaji walio wengi (asilimia 90) wanaamua kuwaachia wachezaji wanaolipwa vizuri sana ndani ya timu wacheze wenyewe na timu ishinde. Eti timu inaachiwa kucheza bila kucheza kama timu. Wote kwa kuitazama Real Madrid na Chelsea tunajua ni kitu gani kitakachotokea.

Ili nchi kama timu ishinde inahitaji zaidi ya viwango vya kukua uchumi, wawekezaji, mipango na bajeti za serikali. Nchi inahitaji kwanza, watu waamini kwamba wamo katika safari moja na sio kila mtu ana safari yake. Pili, lazima tuwe na visheni moja ya kule tuendako sio kila mtu awe na dira au ndoto binafsi ya kule anakotaka kwenda. Tatu, lazima tujenge uchumi wetu kama timu moja, kama kitu kimoja na sio kinyume cha hiyvo. Nne, lazima akilini mwetu sote tuwe na picha ya kile tunachotaka kukijenga kama vile mfano wa nyumba inayotakiwa kujengwa. Na mwisho lakini sio jambo dogo akili zetu ziione nchi nzima, mikoa, wilaya, tarafa, kata, miji, vijiji na mitaa kama MFUMO MMMOJA mkubwa ulio na mifumo kadhaa midogo midogo nayo yote ikiingiliana kila wakati na kwamba mfumo mdogo mmoja mdogo ukiwa na tatizo basi mifumo mingine yote midogo na huo mkubwa utakuwa katika matatizo pia. Na mfumo huo mkubwa itambulike pia ni sehemu ya mfumo mkubwa kabisa wa dunia na ulimwengu kiujumla ambao kwa sasa watambulika kama utandawazi. Nasi tukiwa na jukumu la kujipanga kwa namna ambayo kwayo tunanufaika badala ya kuathirika vibaya na huo utandawazi.

Tumewahi kuzungumzia huko nyuma kuwa mahitaji muhimu ya binadamu ni pamoja na maji, chakula, mahitaji ya kijamii, mavazi, makazi/nyumba, afya na tiba, elimu na usalama wa watu na mali zao. Vitu hivi ndivyo vinavyostahili kutumika kama kigezo cha kuamua uchumi umekua au haujakua katika medani ya uchumi-mtu na wala sio takwimu za aina nyingine.

Tuwaulize wanauchumi wetu kama Tanzania ya mwaka jana wa bejeti walikuwa na hali bora zaidi au mbaya zaidi katika suala la upatikanaji maji, chakula,mahiraji ya kijamii kama huduma mbalimbali za usafiri ikiwemo wa daladala, usafi na umeme ? Majibu ya hili pengine yatawafungua macho waliofunga macho na walio katika usingizi wa kuridhika na kutosheka na hali kama ilivyo.

Je, wanauchumi wetu walio huru nchini wanasema kwamba Watanzania wameacha kuvaa mitumba kama Mwinyi na Mkapa walivyotuacha au bado tunaendea na mtumba.

Je, hivi leo ni rahisi kujenga na kumiliki nyumba kama ilivyokuwa mwaka jana au hali imezidi kuwa mbaya zaidi. Jibu kwa hili nalo litatuonesha kama tuna sababu ya kukenua meno au ya kufunga vinywa kwa hasira ya ukata na kutokuridhika.

Wanauchumi wetu waambaje katika masuala ya afya na tiba na kama shida na dhiki za kina mama na watoto na wagonjwa wengine katika mahospitali yetu zimeisha au bado zinaendelea. Ziada ya ndogondogo ikiwa je, wale mbu wa Muhimbili wametushinda au tumewadhinda ? Kama mbu hao wametushinda nina mashaka kama tumepiga hatua yoyote mbele ya maana na inayoonekana.

Hali hii ya kuutazama uchumi kutoka juu na kushindwa kuutazama toka chini utaendelea kujenga msimamo na mtazamo wa wale walioko madarakani kujijali zaidi wao wenyewe kwanza na wale wanaowaweka madarakani na kamwe 'haiwezekani' wao kuwa na mipango na sera zinazotoka chini kwenda juu, yaani, kumneemesha kwanza mnyonge kisha ndio vigogo na vizito waneemeke zaidi ya walivyoneemeka. Na hiki ndio chanzo cha wao kuona kwa miwani yenye lensi kubwa uchumi-nchi na kutazamia uchumi-mtu kwa miwani yenye lensi ndogo.

Isitoshe uchumi wowote unaojengwa kwa kutegemea zaidi rasilimali na uwekezaji nyonyaji-sana toka nje hauwezi kamwe kuleta maendeleo linganifu ya uchumi-nchi na uchumi-mtu. Na hili benki ya dunia na IMF wameliona na wanalitambua na ndio maana wanaishauri serikali kupitia upya mikataba na wawekezaji katika sekta ya madini na migodi.

Aidha, nchi inayoshindwa kucheza na kuoanisha mahesabu na takwimu kwa nadharia na vitendo katika masuala ya pande-toaji/ugavi (supply) na pande-mahitaji (demand) katika ngazi ya uchumi-mtu haiwezi kamwe kuwa na maendeleo endelevu na ambayo huwa nadra kuguswa vibaya au kuathirika na kile kinachotokea ndani na nje ya nchi. Hili kama alivyosema Shaaban Robert linahitaji KIASI. Vigogo na vizito wakpata zaidi ya KIASI na walalahoi wakikosa chini ya KIASI basi inakuwa muhali na vigumu sana kujenga pia mtaji wa kijamii ambao hutegemea watu na sio fedha katika nchi husika.

Tunafanya kosa kubwa sana kiuchumi na hususan kibajeti kwa kukosa kuwa na mipango na mikakati adhimu ya kulifanya soko la ndani lifanye kazi kubwa linaloweza kuifanya kwa kujishughulisha zaidi na soko la nje, tena kwa upande wa manunuzi ya vitu vya anasa kwa sana.

Katika kipindi tulichomo na hali tuliyo nayo kiuchumi tulitakiwa tutumie muda mkubwa zaidi na fedha nyingi zaidi za kukuza uchumi-mtu kwanza na sio vinginevyo. Bajeti ya hivi majuzi haioneshi kuwa rafiki wa Malengo ya Milenia (MDGs) ukitazama mgawo wa bajeti ulivyokwenda. Na wala hakuna panapoonesha ni kwa namna na njia gani Tanzania katika kipindi cha bajeti kijacho itajitahidi kuhakikisha wananchi wake wanapata angalau sehemu ya kuridhisha ya mahitaji yao ya msingi. Pengine kwa viongozi kuamini kuwa kwa kuwa uchumi-nchi unakuwa basi watu wana fedha tele mifukoni mwao, kitu ambacho si kweli.

Friday, June 3, 2011

Taarab asili ni Urithi usiostahili kupotea

KWENYE miaka ya hivi karibuni kumekuwa na jitihada zenye mwelekeo potofu katika vyombo vya habari mbalimbali kupotosha maana na dhana halisi ya taarabu na kile ambacho taarabu inastahili kuwa na kuitwa.

Baada ya Watanzania kugeukawavivu wa kila kitu ikiwemo kupiga ala za muziki na kutaka mteremko katika kila jambo wale waliozuka na mitindo inayotumia mashairi au tungo zenye vina na mizani au isivyo hivyo wakaona urahisi ni kuita miziki yao 'modern taarab'. Miziki hiyo ninakaata sio taarabu bali inastahili kuitwa mipasho, kiduku, rusha na roho au mnanda na vitu kama hivyo lakini sio kamwe taarabu.

Muziki wa taarabu una asili na fasili yake katika watu wa pwani na visiwani na maeneo ya mwambao wa Afrika Mashariki.
Umeathirika kwa kiasi kikubwa na muziki wa Mashariki ya Kati, India na kaswida za Kiislamu.

Sifa moja kubwa ya muziki wa taarabu tofauti na wengi wanavyofikiri sio maneno na mpangilio wake, bali ala za muziki huo na mipangilio yake na ule ufundi wa kila mwanataarabu kuwa bingwa au stadi katika kupiga chombo fulani. Taarabu isipokuwa na ala hizi sio taarabu ni igizo tu kwa kiasi fulani la kitu kama taarabu. Taarab kwa kawaida ni kitulizo cha fikra ndani ya nyumba na katika hadhara isiyoshawishiwa na usasa na umagharibi kiasi cha kupuuza maadili na mila za wahusika.

Ala za taarabu ni nyingi na swahiba wangu Ali Salehe ambaye sio tu shabiki wa taarabu bali ni mtunzi pia wa nyimbo za taarab anaweza baadaye kunipokea hapa na kuelezea zaidi kwanini tunastahili kuwekeza kwenye taarab asilia kama eneo la utamaduni linalostahili kuhifadhiwa na kuenziwa.

Taarabu kama walivyoiendelza kina Siti binti Sadi, Bi Kidude, Juma Bhalo na kina Sheikh Ilyas, Machapurala bila kuwasahau mamia ya wanawake na wanaume wa Kizanzibar na Kimrima waliochangia maendeleo ya tasnia hii adimu lakini iliyo na sifa ya kuwa sehemu muhimu ya utamaduni wa mwambao ya Pwani ya Afrika Mashariki na usiostahili kuachiwa kupotea.

Taarabu ni muziki wa enzi na enzi. Ni sehemu ya utamaduni endelevu na hususan katika mikoa ya pwani ya Afrika Mashariki. Taarab ni ustaarabu, utaratibu, upole na uungwana. Taarabu ni kitulizo cha mawazo na gundi ya kuunganisha familia kama sio ukoo mzima. Sifa ambayo si mipasho, sio rusha roho sio mnanda unayo.

Taarab kiasili sio muziki wa kucheza bali wa kutazama, kusikiliza, kutafakari na kutunza. Huu ni muziki uliokuwa ukisikilizwa na watu wenye fikira, busara na hekima kuwapa muda wa kuwaza na kuwazua juu ya hili au lile. Muziki wa kupayuka, kujiona, msshauzi, kusemana, kutukanana, kuumbuana na wenye nyimbo ambazo hazina staha, usiri wala taadibu ya kuimbwa katika mafumbo hauwezi kuitwa taarab.

Ni muziki ambao kwa kawaida una ala takriban ya ishirini. Na kwa wapenzi halisi wa taarabu hufuatilia upigaji wa kila ala na ufundi au ugwiji wa yule anayetumia ala husika. Aidha, mashairi ya taarab hayaangalii tu mlingano wa vina na mizani bali maudhui na mantiki ya kile kilichomo tena kikiwe kwenye mafumbo kuweza kusomeka vyema na wanaosikiliza wimbo husika.

Ni muziki ambao hutungwa kwa mafumbo na kwa namna ambayo hauzui familia nzima, yaani, babu, bibi,baba,mama, kaka na dada wote kujumuika kwa pamoja bila kutokea chochote ambacho kinaweza kuwafanya washindwe kuzungumza au kutazamana. Taarab kiasili uliunga pamoja familia za wakazi wa mji husika. Tofauti na hiyo inayoitwa 'modern taarab' ambayo kwa kiasi kikubwa inazivunja familia katika kila mji na kijiji.

Siti bint Saad (1928) ndiye nyota wa kwanza wa taarab
ambaye kwa mara ya kwanza badala ya kuimba kwa Kiarabu aliimba kwa Kiswahili. Alifyatua mamia ya santuri za nyimbo India na wapenda muziki wa enzi hizo hakuna aliyekosa wimbo wake nyumbani.

Muziki wa taarab asili hauna tofauti na 'Classical Music' wa Ulaya au 'Country Music' wa Marekani. Miziki hiyo ilikuwepo, imekuwepo na itakuwepo bila kubadilika wala kuitwa kwa jina jingine wala kupigwa kwa namna nyingine tofauti na ilivyokuwa, ilivyo sasa na itakavyokuwa kesho.
Ni sehemu ya kudumu ya utamduni wa watu na sio kitu cha kupita na kusahaulika.

Aina hizo za miziki pamoja na kuzuka kwa miziki ya kila aina Ulaya na Marekani bado inatambulika kwa nembo na jina lake. Country ni country na classical ni classical. Hapajakuwepo muziki mwingine uliopewa umodern kuhusiana na miziki hii, hakuna kitu kama modern country au modern classic.

Rouget katika Music and Trance anafafanua kwamba neno taarab linatokana na neno la kiarabu 'tariba' likiwa na maana ya hisia za kusisimka, kudhihirisha au kutaka kufanya kitu fulani kama vile kuimba au kucheza taarab.

Taarab asili ilingia kwanza hapa Afrika Mashariki kupitia Zanzibar kunako miaka ya 1870. Aliileta Sultan Seyyid Barghash ambaye alileta kikundi cha wanamzuki toka Misri kukaa kwenye jumba lake la Kifalme.

Tofauti na viongozi wetu wa leo, Barghash aliwapeleka Wazanzibari kadhaa wakiongozwa na IbrahimMohammed kwenda kusomea muzki nchini Misri nao waliporudi waliunda kikundi cha kwanza pengine cha taarabu Afrika Mashariki kilichoitwa Zanzibar Taarab Orchestra.

Kunako 1905 kikundi cha pili cha taarabu kilizaliwa huko huko Unguja kikiitwa Ikwhani Safaa Musical Club. Kikundi hicho kipo hadi wa leo, lakini kama vilivyo vikundi vingine vya taarab 'hasa' havina msaada wowote wa maana toka kwa yeyote yule, kwani inavyoelekea wengi pamoja na viongozi wa serikali wametekwa na rusharoho na mipasho.

Taarab asili haistahili kuonekana kama ni taarab tu. Ni zaidi ya taarab. Hii ni hazina ya utamaduni katika mwambao wa Afrika Mashariki kuanzisa Lamu hadi Kilwa na Sofala.


Kama jitihada zinavyofanyika kukarabati na kutunza maeneo kama vile Mji Mkongwe Zanzibar, Bagamoyo na Kilwa ili iendelee kuwepo basi upo umuhimu pia wa wanaohusika katika serikali zetu kuhakikisha kuwa muziki wa taarab asili na wanamuziki wake wanakumbukwa na kuenziwa na kisha kizazi kipya kinajengwa ili kuendeleza muziki huu kwa faida ya vizazi vijavyo. Kwa maana, ukweli ni kwamba taarab asili ikipotea ndio utakuwa mwisho wa taarab hapa Afrika Mashariki.

Kwanini tuhifadhi taarab asilia

Kwa bahati mbaya wengi tumezoea kuchukulia vitu kama ardhi, fedha, nyumba, magari kuwa ndio rasilimali tu. Lakini muziki wa kiasili nao ni rasilimali muhimu kimaendeleo na kisaikolojia. Bila urithi wa namna hii tutakuwa ni taifa lipolipo tu ambalo si jambo zuri.

Pamoja na mambo mengine kuifufua, kuitunza na kuiendelza taarab asili ni jambo lenye faida kadhaa ikiwemo kuendeleza mila na utamaduni wetu; kuzileta familia pamoja mara kwa mara; kujenga maadili bora katika jamii; kuwa na muziki usioendana kinyume na maadili ya dini; kukuza na kuendeleza ushairi na Kiswahili; kuwa kivutio kwa wageni wa leo na kesho
na kuzienzi na kuendeleza ala asili za muziki na upigaji wake.

Ninatoa wito maalum pia kwa vyombo vya habari kuacha kuuchanganya umma juu ya muziki wa taarab. Tafadhali Bi Hindu, Dida, Mzee Chapuo, Bi Chau, Miriam wa Migomba, Kristina wa Mbezi kwa kuturahisisishia hili kwa kubaini kwamba Afrika Mashariki kuna taarab moja tu, nayo ni taarab asilia ambayo kwa kawaida hupigwa na vyombo vingi, hutumia mafumbo na usiri katika nyimbo zake na hauchezwi achilia mbali kunenguliwa na kutingishiwa mawowowo.

Miziki inayojiita modern taarab iitwe kwa majina yao yanayostahili kama ni kiduku basi kiduku, kama ni rusha roho basi rusha roho fulani, kama ni mipasho basi ni mipasho na kama ni mnanda uitwe mnanda
na miziki hii isiruhusiwe kutumia mgongo wa taarab kujijenga isipostahili.

Nikiri kuwa nilitaka sana nitembelee Lamu, Malindi, Mombasa, Tanga na Zanzibar kuzungumza na wakereketwa wenzangu wa taarabu asili kabla ya kuandika makala haya lakini haikuwezekana. Ninaamini, hata hivyo kupitia makala haya ujumbe unaweza kufika kwa kiasi fulani.

Ninawashauri wanaharakati wa kulinda na kuendeleza utamaduni wetu kuangalia uwezekano wa haya yafuatayo: Kusaidia juhudi binafsi zilizopo za kufufua na kuendeleza vikundi vya taarabu kupitia vilabu na vyuo vya upigaji ala za asili za taarab (mathalani juhudi za Bi Hamndani, Zanzibar) ; Kushirikiana na UNESCO kuhifadhi taarab asili kwa kutumia TEKNOHAMA;
Kuwatafuta wanataarab asil waliko na kuwaunganisha ili kuufufua na kuchochea kuwepo kwa muziki huo kiasili na kuongeza vionjo viwili vitatu vya kuvutia familia zaidi kuliko mtu mmoja mmoja.

Aidha, kusaidia vikundi vilivyopo lakini havina ala za kutosha za muziki toka Misri na Uarabuni; kuenzi Ushairi katika vyombo vya habari kukuza vipaji vya washairi chipukizi na
kuchukulia Taarab asili kama urithi usiostahili kupotea kwa msaada wa UNESCO na wapenda utamaduni wetu wengineo.


http://www.gmail.com
sammy.i.makilla@gmail.com

Tuesday, May 24, 2011

Simu za mkononi, rushwa na mapato bwereree…

WATU husema kila jambo lina wakati wake. Juma hili limeshuhudia taarifa za tafiti kadhaa ambazo pamoja na mambo mengine zimeonesha kuwa kinachowakera sana Watanzania hivi leo ni rushwa na mengine yanafuatia.Ni kipindi kilichoshuhudia pia ahadi toka kwa kiongozi mkuu wa ndugu zetu wa Usalama wa Raia kwamba wanakuja na mikakati mipya ya kulifanya jeshi hilo liwe safi na linalokubalika, sio tu na Watanzania bali na Afrika nzima kama mfano wa kuigwa.

Kutokana na wao polisi kuonesha angalau nia ya kufanya jambo jema makala haya ninawatunza wao pamoja na yaliyomo ambayo yanaongeza kuwapanua mawazo juu ya kile kinachostahili kufanyika ili azma yao isiwe wimbo utakaosahaulika baada ya muda si mrefu.Kwanza, tukubaliane kwamba, matatizo ya jeshi la polisi sio rushwa tu. Kuna matatizo mengi ambayo kwa umoja wao ndiyo yanayochangia watu kuwa na alama ya ulizo kila saa juu ya utendaji kazi wa jeshi hilo.

Baadhi ya matatizo ya jeshi hilo ni yale ya baadhi yao kukosa wito; tamaa ya kutaka kutajirika haraka haraka kutokana na kujifananisha na wengine; wakubwa wenye ajenda zao nje ya usalama wa raia na mali zao; elimu ndogo ya uraia na uzalendo na uamsho wa chini juu ya wajibu wa polisi katika kukuza na kuimarisha demokrasia changa.Aidha, polisi wana matatizo ya zana na vifaa vichache na duni; kukosa

maendeleo katika matumizi ya teknohama, makazi bora, maslahi ridhishi, nafasi finyu za kujiendeleza ili kukabiliana na mazingira ya nchi na ya dunia yanayobadilika kila leo.Lakini la ajabu kwa upande wangu mimi ni kuwa matatizo haya yote yanaweza kutatuliwa kwa jeshi hilo likisaidiwa na serikali kujipanga upya ili kumaliza ile hali ya mitaa na barabara zetu kuonekama kama vile hazina au hazifuati sheria hata kidogo.

Muulize mtu yeyote anayetoka nchi iliyostaarabika na

atakuambia anachokiogopa sasa hapa nchini zaidi ya rushwa ni kutokuwa na utawala wa kisheria unaofanya kazi.Hili linaashiria kwamba, kuna kazi kubwa sana ya kuleta mabadiliko ya msingi sio tu ndani ya jeshi la polisi, lakini pia katika jamii ya Kitanzania ambayo imeachiwa kwenda upogo na serikali kadhaa zilizotangulia pengine katika ile hali ya wazazi kumdekeza mwana na kumuachia kufanyaatakalo bila kuadabishwa.

Kwa hiyo kama tunataka mapinduzi ya kweli tukubali kuwa

tuanze na kukataa maadili na tabia mbovu tulizozilea hadi wa leo. Hili sio jambo dogo. Linahitaji waliopewa dhamana ya kutuongoza kukutana na wataalamu wa saikolojia na sosholojia ili hatimaye pawe na mkakati wa kupakua toka akilini mwa Watanzania takataka na uchafu mwingine uliomo humo na kisha kusafisha akili na bongo zetu sawasawa halafu kuanza kupandikiza uadilifu, haki, uaminifu, ukweli, utu na ubinadamu ndani yetu.Wakati tunasubiri hayo yatokee; maana kama tunavyowajua wanasiasa duniani hawana haraka na jambo, pengine ipo haja ya kuzungumzia mambo mawili matatu ambayo jeshi la polisi, serikali, kampuni za

simu za mikononi na watu kama 2-Mobile na wale wengine wenye majukwaa ya kupokea na kurushia taarifa wanaweza kuifanya ili jeshi letu la polisi litimize ndoto yake ya kuwa chombo safi na kinachokubalika na jamii.Kabla ya kufanya hivyo, lazima awali ya yote tubainishe ni nini hasa majukumu ya jeshi hilo.

Nitafanya hivyo kwa kuuliza maswali kwamba: Hivi katika karne hii ya sayansi na teknolojia ni kazi ya polisi kukamata magari barabarani ? Hivi usalama wa watembeao kwa miguu

na hasa watoto, wazee na walemavu unamtegemea nani? Hivi ukiwa na madereva ambao hawaheshimu 'zebra-crossing' na taa za barabarani utasema una polisi wa usalama barabarani au wa hatari barabarani?

Hivi unaweza kuwa na askari 10 au 20 ambao eti kazi yao ni kuandika maelezo ya wanaoletwa vituoni ukasema unawatumia jamaa hao vizuri? Hivi kweli tunashindwa kujipanga kwamba, kazi ya ulinzi iwe barabarani, viwandani au nyumbani ni ya watu wanaolipwa mshahara kufanya kazi hiyo?Wakati unafikiria majibu ya maswali hayo mimi ninapendekeza yafuatayo:

Idadi ya polisi wanaobaki vituoni ipunguzwe kwa kiasi kikubwa kwa kutumia kompyuta na nakala-igizwa [templates) kwa kuwa makosa yote yanayoweza kufanyika hapa nchini yanajulikana na yanaweza kuandaliwa nakala-igizwa hizo na kazi ya wanaokaa nyuma ya kompyuta ni kujaza maelezo kidogo kwa kubadili majina, tarehe, namba au idadi za vitu na sehemu mbalimbali, mahali pa tukio na maelezo binafsi machache ili katika dakika 2 au tatu maelezo ya mtu yawe yamedakwa, kuchapwa na kusainiwa. Hili litaongeza idadi ya askari

watakaokuwa majiani na mitaani kunasa uhalifu na kusaidia watoto, wazee na walemavu na watu wengine wenye matatizo binafsi.SMS na Usalama Barabarani.

Hakika aliyegundua ujumbe mfupi anatufungua macho kwenye mengi ambayo hata bado hatujaanza kuyafikiria. Hebu tuangalie hili la usalama barabarani, rushwa na matumizi ya teknohama.Je, makosa yote yanayoweza kufanywa iwe na gari, dereva, konda au abiria na kadhalika barabarani

yanajulikana? Tunaweza kuyapa haya namba maalumu? Na je, kuna polisi, dereva wa daladala au konda asiyekuwa na simu ya mkononi?Ndugu Mwema unaweza kuongea na Vodacom, Zain, Zantel na Tigo na wale wenye majukwaa ya kuhifadhi, kupokea na kutuma ujumbe ili wakueleze kama inawezekana kwa mambo haya kufanyika:

1. Usalama barabarani kutuma ujumbe makao ya Usalama Barabarani kwa kubonyeza kitufe chake kwenye simu na kujaza maelezo muhimu ambayo yote yako kwa namba kuhusu kosa lililofanywa na daladala fulani ?
2. Makao makuu husika kupokea taarifa hiyo na kuhifadhi kumbukumbu na kisha kumtumia papo kwa hapo dereva wa daladala husika kuwa kafanya kosa

fulani, mahala fulani, saa fulani na kwamba alipe faini kiasi fulani ?
3. Makao Makuu ya Usalama kuwa na 'Caution Money' toka kwa wenye daladala itakayotunzwa nao na kukatwa wakati daladala ya mtu hiyo imetozwa faini?
4. Dereva wa daladala kumuarifu tajiri yake alipe faini hiyo kwa kutumia simu yake ya mkononi.
5. Fedha hiyo kuingia kwenye mfumo wa Daladala-Pesa/Barabara-Pesa wa Usalama Barabarani ambao utatumika kuongeza ubora wa maisha ya watumishi wote

wa Jeshi la Polisi pamoja na wanaofanya vizuri sana pia kutunzwa bonasi na bakshishi nyingine?

Na je, bajeti ya serikali nayo hatima ya yote haitatunishwa na

mfuko unaotokana na kuhakikisha kuwasheria za usalama zinafuatwa na kunakuwepo na utawala wa kisheria nchini? Angalizo: Kama wazo hili linakubalika na

kutekelezwa ikumbukwe kwamba, kila mvunja sheria za barabarani anayeripotiwa sio tu atalipa faini bali atalipia ujumbe uliotumwa kumripoti na ujumbe mwingine

utakaofuatia hadi alipe faini ikiwa ni pamoja na ujumbe wa kumkumbusha kwamba hajalipa faini aliyotozwa.

Aidha, raia ndani ya basi au barabarani wataweza

kumripoti dereva yeyote mzembe ili mradi simu zao ziwe zimesajiliwa na majina yao yanajulikana na wanaweza kutoa ushahidi. 'Lotto' ya Usalama barabarani inaweza kuwazawadia pia watu kama hao.Huu ni mfano mmoja tu, lakini ninaamini Tanzania ya leo ina watu wengi tu wenye akili kama mchwa baadhi yao wakiwemo humo humo ndani ya jeshi la polisi basi mjaribu kuona pia njia nyingine zinazofaa zaidi ya mawazo ninayotoa mimi.Ninachokisema mimi ni kuwa upo

uwezekano wa jeshi la polisi kuwa na watu wachache vituoni na wengi wao wakawa mitaani; na huko mitaani kuna uwezekano mkubwa wa kutumia simu za mikononi kunasa na kuripoti makosa ya barabarani bila askari kulazimika kuandika kitu zaidi ya kubonyeza namba na maelezo ndani ya simu yake; na taarifa hizo kupokelewa makao makuu kupitia watoa huduma za simu za mkononi/wenye majukwaa ya kutuma na kupokea ujumbe na juu ya yote simu hizo hizo za mkononi

kutumiwa na wenye daladala kulipa faini za papo kwa hapo.Hili si wazo jipya, ila muktadha wake ni mpya. Sio wazo litakoeleweka au kukubalika kirahisi na wengi

kwani huenda likawa linachangia moja kwa moja kuondoa vitendo vya madereva, abiria na usalama barabarni vinavyochangia kuwepo kwa rushwa kwa kukata

kabisa mzizi wa fitina.

Nimezoea kutoa mawazo bure na sitarajii kunufaika chochote na mawazo haya kama ambavyo sijawahi kunufaika na wazo langu lolote huko nyuma. Hivyo mtu asije kunishuku kwamba, ninatumiwa na wamiliki wa kampuni za simu za mikononi kuwapatia biashara mpya bali nalitoa hili toka dhati ya moyo

wangu ili kuchangia usalama barabarani na kutokomeza kabisa rushwa vitu ambavyo vinamkera yule, wewe na mimi.

Simu za mkononi, rushwa na mapato bwereree…

WATU husema kila jambo lina wakati wake. Juma hili limeshuhudia taarifa za tafiti kadhaa ambazo pamoja na mambo mengine zimeonesha kuwa kinachowakera sana Watanzania hivi leo ni rushwa na mengine yanafuatia.Ni kipindi kilichoshuhudia pia ahadi toka kwa kiongozi mkuu wa ndugu zetu wa Usalama wa Raia kwamba wanakuja na mikakati mipya ya kulifanya jeshi hilo liwe safi na linalokubalika, sio tu na Watanzania bali na Afrika nzima kama mfano wa kuigwa.

Kutokana na wao polisi kuonesha angalau nia ya kufanya jambo jema makala haya ninawatunza wao pamoja na yaliyomo ambayo yanaongeza kuwapanua mawazo juu ya kile kinachostahili kufanyika ili azma yao isiwe wimbo utakaosahaulika baada ya muda si mrefu.Kwanza, tukubaliane kwamba, matatizo ya jeshi la polisi sio rushwa tu. Kuna matatizo mengi ambayo kwa umoja wao ndiyo yanayochangia watu kuwa na alama ya ulizo kila saa juu ya utendaji kazi wa jeshi hilo.

Baadhi ya matatizo ya jeshi hilo ni yale ya baadhi yao kukosa wito; tamaa ya kutaka kutajirika haraka haraka kutokana na kujifananisha na wengine; wakubwa wenye ajenda zao nje ya usalama wa raia na mali zao; elimu ndogo ya uraia na uzalendo na uamsho wa chini juu ya wajibu wa polisi katika kukuza na kuimarisha demokrasia changa.Aidha, polisi wana matatizo ya zana na vifaa vichache na duni; kukosa

maendeleo katika matumizi ya teknohama, makazi bora, maslahi ridhishi, nafasi finyu za kujiendeleza ili kukabiliana na mazingira ya nchi na ya dunia yanayobadilika kila leo.Lakini la ajabu kwa upande wangu mimi ni kuwa matatizo haya yote yanaweza kutatuliwa kwa jeshi hilo likisaidiwa na serikali kujipanga upya ili kumaliza ile hali ya mitaa na barabara zetu kuonekama kama vile hazina au hazifuati sheria hata kidogo.

Muulize mtu yeyote anayetoka nchi iliyostaarabika na

atakuambia anachokiogopa sasa hapa nchini zaidi ya rushwa ni kutokuwa na utawala wa kisheria unaofanya kazi.Hili linaashiria kwamba, kuna kazi kubwa sana ya kuleta mabadiliko ya msingi sio tu ndani ya jeshi la polisi, lakini pia katika jamii ya Kitanzania ambayo imeachiwa kwenda upogo na serikali kadhaa zilizotangulia pengine katika ile hali ya wazazi kumdekeza mwana na kumuachia kufanyaatakalo bila kuadabishwa.

Kwa hiyo kama tunataka mapinduzi ya kweli tukubali kuwa

tuanze na kukataa maadili na tabia mbovu tulizozilea hadi wa leo. Hili sio jambo dogo. Linahitaji waliopewa dhamana ya kutuongoza kukutana na wataalamu wa saikolojia na sosholojia ili hatimaye pawe na mkakati wa kupakua toka akilini mwa Watanzania takataka na uchafu mwingine uliomo humo na kisha kusafisha akili na bongo zetu sawasawa halafu kuanza kupandikiza uadilifu, haki, uaminifu, ukweli, utu na ubinadamu ndani yetu.Wakati tunasubiri hayo yatokee; maana kama tunavyowajua wanasiasa duniani hawana haraka na jambo, pengine ipo haja ya kuzungumzia mambo mawili matatu ambayo jeshi la polisi, serikali, kampuni za

simu za mikononi na watu kama 2-Mobile na wale wengine wenye majukwaa ya kupokea na kurushia taarifa wanaweza kuifanya ili jeshi letu la polisi litimize ndoto yake ya kuwa chombo safi na kinachokubalika na jamii.Kabla ya kufanya hivyo, lazima awali ya yote tubainishe ni nini hasa majukumu ya jeshi hilo.

Nitafanya hivyo kwa kuuliza maswali kwamba: Hivi katika karne hii ya sayansi na teknolojia ni kazi ya polisi kukamata magari barabarani ? Hivi usalama wa watembeao kwa miguu

na hasa watoto, wazee na walemavu unamtegemea nani? Hivi ukiwa na madereva ambao hawaheshimu 'zebra-crossing' na taa za barabarani utasema una polisi wa usalama barabarani au wa hatari barabarani?

Hivi unaweza kuwa na askari 10 au 20 ambao eti kazi yao ni kuandika maelezo ya wanaoletwa vituoni ukasema unawatumia jamaa hao vizuri? Hivi kweli tunashindwa kujipanga kwamba, kazi ya ulinzi iwe barabarani, viwandani au nyumbani ni ya watu wanaolipwa mshahara kufanya kazi hiyo?Wakati unafikiria majibu ya maswali hayo mimi ninapendekeza yafuatayo:

Idadi ya polisi wanaobaki vituoni ipunguzwe kwa kiasi kikubwa kwa kutumia kompyuta na nakala-igizwa [templates) kwa kuwa makosa yote yanayoweza kufanyika hapa nchini yanajulikana na yanaweza kuandaliwa nakala-igizwa hizo na kazi ya wanaokaa nyuma ya kompyuta ni kujaza maelezo kidogo kwa kubadili majina, tarehe, namba au idadi za vitu na sehemu mbalimbali, mahali pa tukio na maelezo binafsi machache ili katika dakika 2 au tatu maelezo ya mtu yawe yamedakwa, kuchapwa na kusainiwa. Hili litaongeza idadi ya askari

watakaokuwa majiani na mitaani kunasa uhalifu na kusaidia watoto, wazee na walemavu na watu wengine wenye matatizo binafsi.SMS na Usalama Barabarani.

Hakika aliyegundua ujumbe mfupi anatufungua macho kwenye mengi ambayo hata bado hatujaanza kuyafikiria. Hebu tuangalie hili la usalama barabarani, rushwa na matumizi ya teknohama.Je, makosa yote yanayoweza kufanywa iwe na gari, dereva, konda au abiria na kadhalika barabarani

yanajulikana? Tunaweza kuyapa haya namba maalumu? Na je, kuna polisi, dereva wa daladala au konda asiyekuwa na simu ya mkononi?Ndugu Mwema unaweza kuongea na Vodacom, Zain, Zantel na Tigo na wale wenye majukwaa ya kuhifadhi, kupokea na kutuma ujumbe ili wakueleze kama inawezekana kwa mambo haya kufanyika:

1. Usalama barabarani kutuma ujumbe makao ya Usalama Barabarani kwa kubonyeza kitufe chake kwenye simu na kujaza maelezo muhimu ambayo yote yako kwa namba kuhusu kosa lililofanywa na daladala fulani ?
2. Makao makuu husika kupokea taarifa hiyo na kuhifadhi kumbukumbu na kisha kumtumia papo kwa hapo dereva wa daladala husika kuwa kafanya kosa

fulani, mahala fulani, saa fulani na kwamba alipe faini kiasi fulani ?
3. Makao Makuu ya Usalama kuwa na 'Caution Money' toka kwa wenye daladala itakayotunzwa nao na kukatwa wakati daladala ya mtu hiyo imetozwa faini?
4. Dereva wa daladala kumuarifu tajiri yake alipe faini hiyo kwa kutumia simu yake ya mkononi.
5. Fedha hiyo kuingia kwenye mfumo wa Daladala-Pesa/Barabara-Pesa wa Usalama Barabarani ambao utatumika kuongeza ubora wa maisha ya watumishi wote

wa Jeshi la Polisi pamoja na wanaofanya vizuri sana pia kutunzwa bonasi na bakshishi nyingine?

Na je, bajeti ya serikali nayo hatima ya yote haitatunishwa na

mfuko unaotokana na kuhakikisha kuwasheria za usalama zinafuatwa na kunakuwepo na utawala wa kisheria nchini? Angalizo: Kama wazo hili linakubalika na

kutekelezwa ikumbukwe kwamba, kila mvunja sheria za barabarani anayeripotiwa sio tu atalipa faini bali atalipia ujumbe uliotumwa kumripoti na ujumbe mwingine

utakaofuatia hadi alipe faini ikiwa ni pamoja na ujumbe wa kumkumbusha kwamba hajalipa faini aliyotozwa.

Aidha, raia ndani ya basi au barabarani wataweza

kumripoti dereva yeyote mzembe ili mradi simu zao ziwe zimesajiliwa na majina yao yanajulikana na wanaweza kutoa ushahidi. 'Lotto' ya Usalama barabarani inaweza kuwazawadia pia watu kama hao.Huu ni mfano mmoja tu, lakini ninaamini Tanzania ya leo ina watu wengi tu wenye akili kama mchwa baadhi yao wakiwemo humo humo ndani ya jeshi la polisi basi mjaribu kuona pia njia nyingine zinazofaa zaidi ya mawazo ninayotoa mimi.Ninachokisema mimi ni kuwa upo

uwezekano wa jeshi la polisi kuwa na watu wachache vituoni na wengi wao wakawa mitaani; na huko mitaani kuna uwezekano mkubwa wa kutumia simu za mikononi kunasa na kuripoti makosa ya barabarani bila askari kulazimika kuandika kitu zaidi ya kubonyeza namba na maelezo ndani ya simu yake; na taarifa hizo kupokelewa makao makuu kupitia watoa huduma za simu za mkononi/wenye majukwaa ya kutuma na kupokea ujumbe na juu ya yote simu hizo hizo za mkononi

kutumiwa na wenye daladala kulipa faini za papo kwa hapo.Hili si wazo jipya, ila muktadha wake ni mpya. Sio wazo litakoeleweka au kukubalika kirahisi na wengi

kwani huenda likawa linachangia moja kwa moja kuondoa vitendo vya madereva, abiria na usalama barabarni vinavyochangia kuwepo kwa rushwa kwa kukata

kabisa mzizi wa fitina.

Nimezoea kutoa mawazo bure na sitarajii kunufaika chochote na mawazo haya kama ambavyo sijawahi kunufaika na wazo langu lolote huko nyuma. Hivyo mtu asije kunishuku kwamba, ninatumiwa na wamiliki wa kampuni za simu za mikononi kuwapatia biashara mpya bali nalitoa hili toka dhati ya moyo

wangu ili kuchangia usalama barabarani na kutokomeza kabisa rushwa vitu ambavyo vinamkera yule, wewe na mimi.

Simu za mkononi, rushwa na mapato bwereree…

WATU husema kila jambo lina wakati wake. Juma hili limeshuhudia taarifa za tafiti kadhaa ambazo pamoja na mambo mengine zimeonesha kuwa kinachowakera sana Watanzania hivi leo ni rushwa na mengine yanafuatia.Ni kipindi kilichoshuhudia pia ahadi toka kwa kiongozi mkuu wa ndugu zetu wa Usalama wa Raia kwamba wanakuja na mikakati mipya ya kulifanya jeshi hilo liwe safi na linalokubalika, sio tu na Watanzania bali na Afrika nzima kama mfano wa kuigwa.

Kutokana na wao polisi kuonesha angalau nia ya kufanya jambo jema makala haya ninawatunza wao pamoja na yaliyomo ambayo yanaongeza kuwapanua mawazo juu ya kile kinachostahili kufanyika ili azma yao isiwe wimbo utakaosahaulika baada ya muda si mrefu.Kwanza, tukubaliane kwamba, matatizo ya jeshi la polisi sio rushwa tu. Kuna matatizo mengi ambayo kwa umoja wao ndiyo yanayochangia watu kuwa na alama ya ulizo kila saa juu ya utendaji kazi wa jeshi hilo.

Baadhi ya matatizo ya jeshi hilo ni yale ya baadhi yao kukosa wito; tamaa ya kutaka kutajirika haraka haraka kutokana na kujifananisha na wengine; wakubwa wenye ajenda zao nje ya usalama wa raia na mali zao; elimu ndogo ya uraia na uzalendo na uamsho wa chini juu ya wajibu wa polisi katika kukuza na kuimarisha demokrasia changa.Aidha, polisi wana matatizo ya zana na vifaa vichache na duni; kukosa

maendeleo katika matumizi ya teknohama, makazi bora, maslahi ridhishi, nafasi finyu za kujiendeleza ili kukabiliana na mazingira ya nchi na ya dunia yanayobadilika kila leo.Lakini la ajabu kwa upande wangu mimi ni kuwa matatizo haya yote yanaweza kutatuliwa kwa jeshi hilo likisaidiwa na serikali kujipanga upya ili kumaliza ile hali ya mitaa na barabara zetu kuonekama kama vile hazina au hazifuati sheria hata kidogo.

Muulize mtu yeyote anayetoka nchi iliyostaarabika na

atakuambia anachokiogopa sasa hapa nchini zaidi ya rushwa ni kutokuwa na utawala wa kisheria unaofanya kazi.Hili linaashiria kwamba, kuna kazi kubwa sana ya kuleta mabadiliko ya msingi sio tu ndani ya jeshi la polisi, lakini pia katika jamii ya Kitanzania ambayo imeachiwa kwenda upogo na serikali kadhaa zilizotangulia pengine katika ile hali ya wazazi kumdekeza mwana na kumuachia kufanyaatakalo bila kuadabishwa.

Kwa hiyo kama tunataka mapinduzi ya kweli tukubali kuwa

tuanze na kukataa maadili na tabia mbovu tulizozilea hadi wa leo. Hili sio jambo dogo. Linahitaji waliopewa dhamana ya kutuongoza kukutana na wataalamu wa saikolojia na sosholojia ili hatimaye pawe na mkakati wa kupakua toka akilini mwa Watanzania takataka na uchafu mwingine uliomo humo na kisha kusafisha akili na bongo zetu sawasawa halafu kuanza kupandikiza uadilifu, haki, uaminifu, ukweli, utu na ubinadamu ndani yetu.Wakati tunasubiri hayo yatokee; maana kama tunavyowajua wanasiasa duniani hawana haraka na jambo, pengine ipo haja ya kuzungumzia mambo mawili matatu ambayo jeshi la polisi, serikali, kampuni za

simu za mikononi na watu kama 2-Mobile na wale wengine wenye majukwaa ya kupokea na kurushia taarifa wanaweza kuifanya ili jeshi letu la polisi litimize ndoto yake ya kuwa chombo safi na kinachokubalika na jamii.Kabla ya kufanya hivyo, lazima awali ya yote tubainishe ni nini hasa majukumu ya jeshi hilo.

Nitafanya hivyo kwa kuuliza maswali kwamba: Hivi katika karne hii ya sayansi na teknolojia ni kazi ya polisi kukamata magari barabarani ? Hivi usalama wa watembeao kwa miguu

na hasa watoto, wazee na walemavu unamtegemea nani? Hivi ukiwa na madereva ambao hawaheshimu 'zebra-crossing' na taa za barabarani utasema una polisi wa usalama barabarani au wa hatari barabarani?

Hivi unaweza kuwa na askari 10 au 20 ambao eti kazi yao ni kuandika maelezo ya wanaoletwa vituoni ukasema unawatumia jamaa hao vizuri? Hivi kweli tunashindwa kujipanga kwamba, kazi ya ulinzi iwe barabarani, viwandani au nyumbani ni ya watu wanaolipwa mshahara kufanya kazi hiyo?Wakati unafikiria majibu ya maswali hayo mimi ninapendekeza yafuatayo:

Idadi ya polisi wanaobaki vituoni ipunguzwe kwa kiasi kikubwa kwa kutumia kompyuta na nakala-igizwa [templates) kwa kuwa makosa yote yanayoweza kufanyika hapa nchini yanajulikana na yanaweza kuandaliwa nakala-igizwa hizo na kazi ya wanaokaa nyuma ya kompyuta ni kujaza maelezo kidogo kwa kubadili majina, tarehe, namba au idadi za vitu na sehemu mbalimbali, mahali pa tukio na maelezo binafsi machache ili katika dakika 2 au tatu maelezo ya mtu yawe yamedakwa, kuchapwa na kusainiwa. Hili litaongeza idadi ya askari

watakaokuwa majiani na mitaani kunasa uhalifu na kusaidia watoto, wazee na walemavu na watu wengine wenye matatizo binafsi.SMS na Usalama Barabarani.

Hakika aliyegundua ujumbe mfupi anatufungua macho kwenye mengi ambayo hata bado hatujaanza kuyafikiria. Hebu tuangalie hili la usalama barabarani, rushwa na matumizi ya teknohama.Je, makosa yote yanayoweza kufanywa iwe na gari, dereva, konda au abiria na kadhalika barabarani

yanajulikana? Tunaweza kuyapa haya namba maalumu? Na je, kuna polisi, dereva wa daladala au konda asiyekuwa na simu ya mkononi?Ndugu Mwema unaweza kuongea na Vodacom, Zain, Zantel na Tigo na wale wenye majukwaa ya kuhifadhi, kupokea na kutuma ujumbe ili wakueleze kama inawezekana kwa mambo haya kufanyika:

1. Usalama barabarani kutuma ujumbe makao ya Usalama Barabarani kwa kubonyeza kitufe chake kwenye simu na kujaza maelezo muhimu ambayo yote yako kwa namba kuhusu kosa lililofanywa na daladala fulani ?
2. Makao makuu husika kupokea taarifa hiyo na kuhifadhi kumbukumbu na kisha kumtumia papo kwa hapo dereva wa daladala husika kuwa kafanya kosa

fulani, mahala fulani, saa fulani na kwamba alipe faini kiasi fulani ?
3. Makao Makuu ya Usalama kuwa na 'Caution Money' toka kwa wenye daladala itakayotunzwa nao na kukatwa wakati daladala ya mtu hiyo imetozwa faini?
4. Dereva wa daladala kumuarifu tajiri yake alipe faini hiyo kwa kutumia simu yake ya mkononi.
5. Fedha hiyo kuingia kwenye mfumo wa Daladala-Pesa/Barabara-Pesa wa Usalama Barabarani ambao utatumika kuongeza ubora wa maisha ya watumishi wote

wa Jeshi la Polisi pamoja na wanaofanya vizuri sana pia kutunzwa bonasi na bakshishi nyingine?

Na je, bajeti ya serikali nayo hatima ya yote haitatunishwa na

mfuko unaotokana na kuhakikisha kuwasheria za usalama zinafuatwa na kunakuwepo na utawala wa kisheria nchini? Angalizo: Kama wazo hili linakubalika na

kutekelezwa ikumbukwe kwamba, kila mvunja sheria za barabarani anayeripotiwa sio tu atalipa faini bali atalipia ujumbe uliotumwa kumripoti na ujumbe mwingine

utakaofuatia hadi alipe faini ikiwa ni pamoja na ujumbe wa kumkumbusha kwamba hajalipa faini aliyotozwa.

Aidha, raia ndani ya basi au barabarani wataweza

kumripoti dereva yeyote mzembe ili mradi simu zao ziwe zimesajiliwa na majina yao yanajulikana na wanaweza kutoa ushahidi. 'Lotto' ya Usalama barabarani inaweza kuwazawadia pia watu kama hao.Huu ni mfano mmoja tu, lakini ninaamini Tanzania ya leo ina watu wengi tu wenye akili kama mchwa baadhi yao wakiwemo humo humo ndani ya jeshi la polisi basi mjaribu kuona pia njia nyingine zinazofaa zaidi ya mawazo ninayotoa mimi.Ninachokisema mimi ni kuwa upo

uwezekano wa jeshi la polisi kuwa na watu wachache vituoni na wengi wao wakawa mitaani; na huko mitaani kuna uwezekano mkubwa wa kutumia simu za mikononi kunasa na kuripoti makosa ya barabarani bila askari kulazimika kuandika kitu zaidi ya kubonyeza namba na maelezo ndani ya simu yake; na taarifa hizo kupokelewa makao makuu kupitia watoa huduma za simu za mkononi/wenye majukwaa ya kutuma na kupokea ujumbe na juu ya yote simu hizo hizo za mkononi

kutumiwa na wenye daladala kulipa faini za papo kwa hapo.Hili si wazo jipya, ila muktadha wake ni mpya. Sio wazo litakoeleweka au kukubalika kirahisi na wengi

kwani huenda likawa linachangia moja kwa moja kuondoa vitendo vya madereva, abiria na usalama barabarni vinavyochangia kuwepo kwa rushwa kwa kukata

kabisa mzizi wa fitina.

Nimezoea kutoa mawazo bure na sitarajii kunufaika chochote na mawazo haya kama ambavyo sijawahi kunufaika na wazo langu lolote huko nyuma. Hivyo mtu asije kunishuku kwamba, ninatumiwa na wamiliki wa kampuni za simu za mikononi kuwapatia biashara mpya bali nalitoa hili toka dhati ya moyo

wangu ili kuchangia usalama barabarani na kutokomeza kabisa rushwa vitu ambavyo vinamkera yule, wewe na mimi.

Nani anayestahili mshahara mzuri?

Nani anayestahili mshahara mzuri?


KATIKA nchi nyingi za Kiafrika na zilizobaki nyuma kimaendeleo, hadi leo suala la mapato kutokana na mishahara lina walakini ambao unachangia nchi hizo

kubakia masikini miaka nenda rudi.

Walakini huu ni kule kuonekana kutokuwa na haki au uwiano kati ya mshahara mtu anaoupata na mchango wake kwa maendeleo ya nchi na watu wake.

Mfumo huu wa mishahara umerithiwa toka kwa wakoloni ambao walikuwa wameamua kujilipa wao walivyopenda bila kujali kuwa wanajenga au wanaharibu nchi.

Hivi leo ili mradi tu unaingia kwenye duru za utawala katika ngazi kuanzia ile ya wilaya kwenda za juu una uhakika wa kulipwa mshahara na masurufu mengine

manono bila ya kuwepo kwa taratibu za kuangalia kama mchango wako una thamani ya mshahara unaolipwa.

Katika hali kama hii kuna idara, wilaya, mikoa na wizara ambazo watu wanaamini kuwa zinaingiza hasara mara mbili kwani kuna watu wasiochangia maendeleo ya

sehemu husika au pengine wanavuruga mambo huko, lakini bado pia wanalipwa vizuri tu.

Hatusemi viongozi hawastahili kulipwa vizuri. La hasha. Lakini kuna ulazima katika miaka hii ya sasa ambayo watumishi wote wa umma wanaweza wakafutwa kazi

na watu wengine pengine wenye uwezo mkubwa zaidi yao kuchukua nafasi hiyo na kazi yao ikawa bora zaidi kuliko ilivyokuwa huko nyuma, kuhakikisha kuwa

tunaoanisha mapato ya mtu na mchango wake kwa maendeleo ya jamii na yale ya nchi kuanzia ngazi ya udiwani hadi uwaziri.

Kwa maneno mengine, kila shilingi anayolipwa mtu lazima ionekane yeye anachangia kurudisha shilingi ngapi katika hazina ya nchi.

Dunia ya leo imebadilika. Nchi haiwezi kuendeshwa kama biashara isiyokuwa na hasara na faida. Ikiendeshwa kwa namna hiyo, yanayotokea Ugiriki hivi leo

yanaweza kuwa ni mambo ya kawaida katika nchi zetu baada ya miaka michache.

Ni lazima tuendeshe nchi zetu kama vile tunaendesha makampuni binafsi ya watu ambayo yanajali na kufuatilia kwa karibu thamani ya mtu na mchango wake kwa

faida na ufanisi wake; vilevile haikubaliki kufanya matumizi ya fujo yanayoweza kuhatarisha hatima ya chombo husika.

Kwa maneno mengine, Tanzania ni kampuni kama kampuni nyingine yoyote. Wananchi wake ni waweka hisa katika serikali yao. Ama serikali hiyo inaweza

kuendeshwa kifaida au kihasara na wao ama wakafaidika na faida hizo au wakala hasara kutokana na uongozi mbovu.

Njia za mawasiliano, elimu na maarifa yaliyopo, maendeleo ya teknolojia mbalimbali na changamoto mbalimbali zinazoukabili ulimwengu zinatulazimisha

kuhakikisha kuwa tunaachana na utamaduni uliopitwa na wakati wa kuamini eti serikali haiwezi kufilisiwa au kuishiwa.

Lakini, kubwa zaidi ni lile la mabadiliko ya kimtazamo na kimsimamo kuhusu ni watu gani ambao kwa kweli ndio wanaostahili kulipwa mishahara mizuri ili kazi yao

izae matunda yatakayochangia watu wengine pia kupata mapato na maisha mazuri.

Kuna mamna mbili za uwezekano hapa. Unaweza ukalipa kundi la watu ambao hawana mchango wowote katika kuwawezesha kihali na kimali wananchi na

hivyo fedha yote ikaishia kwenye matumbo ya watu na miradi isiyochangia kabisa maendeleo ya nchi na watu wake, auunaweza ukawa na mfumo wa uzalishaji na

ugawaji mapato ambao unayapa makundi muhimu katika jamii uwezo wa kifedha ambao unakuwa ni chachu katika maendeleo ya watu wengine.

Kwa maneno mengine, taifa linaingiza mapato kila mwaka, lakini ni nani anayepata mapato haya na anayafanyia kitu gani, nayo yanachangia vipi maendeleo ya

nchi na watu wake? Aidha, ni muhimu kujua ni kwa namna gani nchi inaweza ikawa na mfumo wa fedha hususan katika matumizi ambao hauchangii kujenga kila

siku tabaka la wenye nacho na wasio nacho.

Ni vizuri kuangalia kuwa je, mishahara wanayopata mawaziri, makatibu wao, wakuu wa idara na mamlaka mbalimbali, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya na

wengineo kama inaendana na mchango wao kwa maeneo husika. Maana upo uwezekano wa kumlipa mtu mshahara kwa miaka 5 hata 10 na mtu huyu asiwe na

chochote cha kuonyesha katika eneo lake la kazi. Ndio maana kuna wanaopendekeza katika nafasi mbalimbali za ajira; iwe kwa kuchaguliwa au kuteuliwa

panakuwa na mshahara wa kushikilia nafasi hiyo na ziada ya hapo iwe inalipwa baada ya kuona mhusika amefanya mambo yanayonekana katika eneo lake.

Kuna wanaouliza kwanini nchi kama Imarati, Malaysia, China viongozi wanajirudisha nyuma kwanza ili wananchi wapate na pale wananchi wanapokwamuliwa

kiuchumi na kijamii ndipo viongozi nao wanapoanza kujiangalia.

Tumeua karibu mashirika yote ya umma, lakini yaliyobakia mikononi mwa serikali ndiyo yaliyochoka kuliko wengine. Tatizo ni nini. Mbona Uchina bado wanamiliki

mashirika mengi ya umma na inasemakana sasa yanafanya maajabu ikilinganishwa na zamani?

Nchi au mkoa au kampuni sio fedha au mtaji au majengo au mitambo au ardhi bali ni watu. Tatizo letu kubwa hapa inaelekea liko katika kumsoma, kumwelewa na

kumtumia mwanadamu kwa namna ambayo anaridhika, anafurahia na anakuwa radhi kujitoa ili kuchangia maendeleo ya wenzake na nchi yake. Binadamu yeyote

anayeona kwamba yeye anatumika tu kama chombo au mashine na wenzake au serkali yake hawezi kuwa na uaminifu, utiifu, uadilifu na kujituma kama yule

anayejiona yeye ni mbia au mwenye hisa katika taasisi husika.

Mfanyakazi kama mtoto hukua kwa jinsi umleavyo. Mtoto ukimlea bila mapenzi, kwa kumwita mwizi, mwongo na kumwaminisha kwamba kushindwa kwake kuwa

na maisha bora sio kosa la mzazi bali ni la mtoto unategemea nini kwa kizazi chako hicho?

Huko Malaysia, China, India na Imarati pamoja na nchi nyingi tu za Kiarabu na zile za Marekani ya Kusini na Kati ambao kimaendeleo hatukuwa tumepishana sana

kwenye miaka ya 60 wameligundua hili. Ni pale tu walipoanza kumpa mtu wao thamnani na kumuamini ndipo watu wao walipoanza kufanya maajabu.
Ninaamini tukiwa na siasa na sera za kujifunza kutoka kwa wengine ziara kwenye nchi kama hizo zinaweza kutufungua moyo, roho, macho na masikio kwa kiasi

kikubwa.

Wakati mwingine, huwa najiuliza kwamba, hivi wanasayansi, watafiti, walimu, madaktari, manesi, walinzi na wanausalama, wahandisi, wajenzi na watu wengine

kama hao wanaochangia moja kwa moja kukua kwa pato la nchi ndio wangelikuwa wanalipwa vizuri kuliko wanasiasa; nchi yetu ingelikuwa wapi?

Huko Norway leo kwa kuwa mwalimu au daktari analipwa vizuri mno hafikirii kabisa ubunge au uwaziri au ubalozi. Kwao huwa ni shughuli kutafuta watu wa kujaza

nafasi kama hizo, kiasi ambacho wakati mwingine vivutio hupaswa kuwekwa ili watu wazikubali nyadhifa kama hizo.

Ni kawaida ya binadamu sikuzote kutaka apate yeye hata kama wengine wanakosa. Kwa Waafrika husemekana wapo wanaoshughulikia wengine ili wakose

kabisa.

Hayo yote tisa, kumi ni kwamba, haitakaa hata siku moja mtu kuridhika na anachokipata kama mshahara au kipato kingine. Na anayejua kiatu kinamfinya wapi

hawezi kukaa kimya bila kuonyesha na hasa pale anapojua kuwa kuna mianya kama sio mitaro na mahandaki yaliyoruhusiwa kupitisha kile ambacho kilistahili

kwenda kwake kwenda kwa wengine.
Vilevile nchi kujikuta ina watumishi wa umma wasio na ubunifu wala uzuzi katika kuwawezesha watu kuzitumia fursa za kiuchumi zilizopo na pia kugeuza matatizo

kuwa ni fursa za watu na nchi kuingiza pato zaidi. Wa mbili, kwa kweli, havai moja!


Kampuni, kujitangaza na mchango kwa jamii..... Sammy Makilla KWANZA , nisionekane kwamba sina shukrani. Ninazishukuru kampuni zote za Tanzania na za

nje ambazo hivi leo zinapigana vikumbo sio tu katika kujitangaza, bali la zaidi katika kuirudishia jamii ( kama wanavyosema wao) kile jamii inachowapa wao. Hata

hivyo, kuna mambo kadhaa ambayo yamekuwa yakiendelea kama sehemu ya kujitangaza na sehemu ya kuisaidia jamii ambayo kidogo yananitatiza. Mathalani,

hivi kweli kupiga rangi nyumba kama sio banda bovu ni njia nzuri ya kujitangaza ? Sitaki jibu sasa hivi hebu fikiria wewe kwanza. Swali jingine, hivi kuwahimiza watu

katika nchi maskini wao wenyewe kutumia ili ndio washinde zawadi nayo pia ni njia sahihi ya kuitangaza na kuirudishia jamii kile inachopata toka kwa wanajamii

husika? Halafu tujiulize pia maswali haya: Jamii yetu iko wapi ? Tunataka iende na ifike wapi na lini? Kwanini ? Na kuna matatizo au vikwazo gani vinavyochangia

jamii yetu kuwa hapa ilipo kiujumla kama jamii maskini? Lengo la makala haya ya leo ni kuonesha kwamba kupaka rangi nyumba mbovu; kuhamasisha watu

kutumia (consumerism) na kuwahimiza watu wajione tofauti na wanajamii wenzao kwa hili au lile pengine inaweza ikawa sio njia sahihi ya kujitangaza na

kuirudishia jamii kile kinachostahili kurudishwa.

Nitajaribu kuonyesha mambo mbadala ambayo kama yakifanyika kampuni hizo zenye kujisikia zina wito wa kuwajibika kijamii zitakuwa zimefanya mambo bora na

ya maana kweli kweli. Maana kinachofanyika hivi sasa na kampuni mbalimbali nchini ni sawa sawa na kumpa mtu mzima 'pipi' au kitu kingine kitamu, kama vile

bado mtu ni mtoto wakati ugonjwa wake ni wa kiutu uzima." Yapo mambo mengi yanayoweza kufanywa na makampuni hapa nchini ambayo sio tu yatachangia

kubadili maisha ya wananchi bali pia kuongeza maradufu au zaidi faida za makampuni hayo. Nitajaribu kuorodhesha na kuelezea kwa uchache baadhi ya mambo

hayo nikitaraji kuwa huwa ni mwanzo wa mjadala wa ushirikiano kati ya wananchi na makampuni mbalimbali hapa nchini yatakayolenga sisi wote kuwa washindi.

Ni muhimu kama kweli kampuni zinataka zionekane zina nia ya kumsaidia Mtanzania kujiingiza katika kurahisisha kupatikana kwa zana za uzalishaji mali katika

kilimo na viwanda vidogo vidogo kwa mamilioni ya vijana wa nchi hii, ambao sio rahisi kupata mtu wa kuwaajiri. Kitendo cha kuwawezesha watu hawa kujiajiri ni

kitendo kitakachohakikisha makampuni hayo siku za mbele kuwa na wateja wanaongezeka badala ya kupungua. Kitendo hicho kinaimarisha amani na

mshikamano nchini kitu muhimu kwa mafanikio ya makampuni yote nchini. Ninaamini kwamba njia nyingine ya kuwajibika kijamii kiutu-uzima ni kuwasaidia walimu

na wahadhiri kwa hali na mali ili walimu na wahadhiri wawe na hali bora kimaisha na hivyo kuboresha elimu zaidi katika ngazi ya msingi, sekondari na vyuo.

Ninaamini, mathalani, kampuni A inaweza ikawadhamini walimu kadhaa wa mahesabu; kampuni B Kemia; kampuni C Fizikia; kampuni D-Utalii; kampuni

E-Biashara na kadhalika. Wao wenyewe wataamua nini cha kufanya, lakini mwisho wa siku walimu hao wanajikuta wana muda zaidi wa kujitolea kuboresha elimu

kuliko ilivyo hivi sasa. Kampuni zitaweza kujitangaza kwa walimu au wahadhiri hao kuitwa. Kwa mfano, mwalimu wa mahesabu wa Sasatel, Ali Bakari wa shule ya

Benjamin Mkapa amesema… Sambamba na hili ni kuwasaidia madaktari na wauguzi ili wafanze tiba na uganga bora zaidi. Hapo napo kitakachofanyika kwa

mfano ni kampuni moja kudhamini madaktari wa magonjwa ya watoto kwa kupunguza gharama na kuchangia pengine mkopo wa ujenzi wa nyumba au

ununuzi/utunzaji wa gari kwa mhusika au ulipiaji ada wa mtoto wa daktari au muuguzi nao pia wakaitangaza kampuni husika, mwalimu wa kemia wa Pepsi Cola,

Mary Mangesho amesema kwamba ....... Tunapokuja kwenye ngazi ya wananchi wengi ni muhimu kuangalia upatikanaji wa nishati ya nafuu zaidi, hususan

umeme wa mafuta, maji, jua au upepo kwa matumizi ya nyumbani chapuchapu ili kuchangia kupanda kwa ubora wa hali ya maisha ya mwananchi, kumkinga na

maradhi ya kutumia nishati hafifu na za hatari na vilevile kumrahisishia ununuzi na matumizi ya vifaa bora vya nyumbani vinavyohitaji nishati hiyo pia ikiwemo vile vya

kampuni zitakazochangia kupatikana kwa nishati hiyo. Tatizo jingine kubwa katika miji yetu ni lile la upatikanaji maji. Kampuni zikichangia kufanya upatikanaji maji

kirahisi vitakuwa vimemkomboa mwanamke na kazi inayotumia muda wake mwingi, lakini siyo ya uzalishaji mali moja kwa moja. Muda unaookolewa hivi

utawasaidia watu hao kujiajiri katika kazi yenye kipato na tija zaidi na hivyo kuwapa uwezo wa kununua bidhaa zaidi kutoka kwa makampuni mbalimbali hapa

nchini. Kazi hii ya ufikivu wa maji majumbani na mashuleni sio rahisi na hatuwezi kuwaachia watu au makampuni fulani tu au serikali yenyewe kuifanikisha. Pale

inapowezekana wale wenye uwezo na hasa makampuni makubwa nayo yachangie pia kwa wanajamii kupata maji safi na salama. Vilevile upatikanaji wa maji ya

uhakika utachangia sio haba kuwa na miti, bustani na maua yanayopendezesha mitaa na miji yetu. Na hili nalo litachangia kujenga mvuto wa miji yetu kwa watalii

kwa miji yetu kuonekana ni ya kistaarabu zaidi. Vijana wengi wa kitanzania hawana ajira. Na hakuna njia bora zaidi ya kuwasaidia kuliko ile ya kuwawezesha wao

wenyewe kujiajiri. Ni kweli wanamichezo sasa hivi wanapata fursa hiyo, lakini vijana wote sio wana michezo. Kadhalika sio michezo yote inayofadhiliwa kwa kiasi

hicho; kwa hiyo bado kuna umuhimu wa kuyaangalia wanayoweza kufanya vijana ikiwa ni pamoja na kazi za kilimo, viwanda vidogo vidogo, sanaa, uigizaji filamu,

uandishi wa vitabu, uchoraji katuni, uchekeshaji, matumizi ya kompyuta kuzalisha vitu mbalimbali na kuona ni kwa namna gani kampuni zinaweza kujipanga na

kuwasaidia vijana wetu ili wajikomboe kiuchumi na wakati huo huo waweze kutoa mchango wao unaohitajika sana katika maendeleo ya nchi yetu. Katika hili

kampuni zinaweza kujipanga na kuanzisha mfuko wa maendeleo ya ujasiriamali miongoni mwa vijana Tanzania ambao utasimamiwa na watu wanaoaminika na

wenye utaalamu unaostahili na kazi yake kubwa itakuwa ni kuwahamasisha vijana kuja na mawazo juu ya nini kinachoweza kuwakomboa. Kisha taasisi hiyo

iwape elimu na maarifa katika masuala hayo pamoja na kuwafungua macho kwa kuwapeleka nchi za nje kujifunza zaidi ujasiriamali katika eneo husika. Baada ya

hapo itawafadhili kwa mkopo usio na riba utakaochangia uanzishwaji na uendelezaji wa wazo na hatimaye mradi wao. Katika mikoa Kando ya Ziwa kuna tatizo

sugu la kisasi na wizi wa mifugo ambalo juzi limeishia kwa mauaji ya watu 17 wa ukoo mmoja kuuawa kikatili. Huko mradi wa kisaikolojia na kijamii ili kumaliza

ubabe na ukatili miongoni mwa watu wa mikoa ya Kanda ya Ziwa ungelitoa mchango mkubwa katika kumaliza tatizo hilo ambalo serikali na vyombo vyake mpaka

hivi leo vinakiri ni zito kuliko wanavyofikira wao. Kuna hatari ya ujinga kurudi tena Tanzania je hatuwezi kupeleka sinema za kila mwezi kwa magari huko vijijini ili

kuwaongezea elimu, burudani na starehe wananchi ? Bila shaka mradi huu sio tu utafanya kazi hizo hapo juu bali pia utakuwa ni njia kubwa ya matangazo ya

biashara husika kufika vijijini kirahisi.
Kinachohitajika hapa ni kwa kampuni hizo kuja na kuanzisha kampuni ya kupeleka sinema mitaani na vijijini itakayokuwa ikijiendesha yenyewe kibiashara. Jambo

lingine linaloweza kufanywa na kampuni zinazoamini kuwa wananchi ni wabia wao wa kudumu ni kuchangia kuifanya mitaa, vitongoji, vijiji na miji yetu kuwa safi na

salama zaidi. Bila maneno mengi wote tunajua umuhimu wa usafi na usalama katika maisha yetu. Hili likifanyika ni dhahiri kampuni hizo zitakuwa zinajiongezea sio

tu heshima bali kuaminiwa kwao mbele ya macho ya wananchi. Hali kadhalika kampuni hizo zinaweza kusaidia kuwepo kwa usafiri wa kistaarabu na heshima

zaidi kwa umma kwa kuwaleta wataalamu na ikiwezekana wawekezaji waweze kushauri watu na nchi ni mambo gani yanaweza kufanywa ili wenye daladala na

mabasi mengineyo wafanye kazi zao kiungwana na kistaarabu zaidi. Wito mwingine ni ule wa kufadhili michezo mbalimbali zaidi ya mpira wa miguu kupitia shule

za msingi, sekondari na vyuo vikuu. Hakika nchi hii haiwezi kuendelea kimichezo kama shule na vyuo havishirikishwi kikamilifu katika kuandaa wachezaji na

washindani wa kesho. Kubwa zaidi katika hili ni kwamba, kwa kufanya hivyo kutachangia pia umoja, udugu na mshikamano wa wanafunzi na vijana wa Kitanzania

popote walipo. Pamoja na hili ni lile la kusaidia kuanzishwa kwa ujenzi wa viwanja vya michezo kwa kila shule, chuo, kata, kijiji na mji nchini kama kusudio la awali

la kuwa na miundombinu ya kisasa nchi nzima itakayotuwezesha pia kujiandaa kwa kuwa wenyeji wa mashindano makubwa ya kimataifa siku za baadaye.