HUU si wakati mbaya wa kuanza kuzungumzia kama nchi yetu baada ya
miaka hamsini ya utawala wa marais wanaume, haijfafikia sasa kumruhusu
mwanamke awe kiongozi wa Tanzania.
Ikumbukwe kuna juhudi mbalimbali zinazofanyika ili kuwapendelea
wanawake washike nafasi nyingi kadri iwezekanavyo bungeni, serikalini
na kwingineko. Na kilichobakia ni Ikulu nayo kuwa na rais mwanamke kwa
mara ya kwanza.
Ieleweke, hata hivyo, hatumtaki mwanamke kwa sababu tu ya uanawake
wake, na kuwa tofauti na mwanamme, bali tunamtaka mwanamke mwenye
akili, uwezo, jasiri na anayeweza kuwadhihirishia wanaume kuwa wao
katika miaka 50 ya mwanzo ya uhuru wetu walikuwa wakiichezea shilingi
yetu chooni, na ndiyo maana imeporomoka kiasi hicho.
Isitoshe, hii ni njia muafaka kabisa ya kuzima uchu, uroho, tamaa na
njaa ya ukubwa miongoni mwa wanaume katika vyama vyetu hivi leo ambao
badala ya kuwaondolea Watanzania matatizo yao mbalimbali wameanza
kugombania nani atakuwa rais 2015 kama vile wote bila aibu wala haya
wana mihadi na Mwenyezi Mungu, kwamba, hadi kufikia hapo atakuwa bado
kawaridhia fursa ya kupumua na kutanua katika dunia hii.
Kwa miaka zaidi ya hamsini sasa tumeona marais wanaume wakifanya kazi
kwa staili, kipaumbele na mikakati na mbinu zao mbalimbali. Kuna
wakati tulianza kwenda mbele, lakini bahati mbaya upepo wa shetani
ukatukumba tukaua ushirika, vyama vya kijamii, halmashauri za miji na
miundo mingine muafaka ya wakati huo na hivyo kupoteza zaidi ya miaka
20 ya kimaendeleo kwa makosa ya siasa zisizo na ushindani au
kudhibitiwa. Ninaamini, huko tunakokwenda ushindani utakuwa na
kudhibitiana na kudhibitiwa na kujidhibiti yatakuwa mambo ya kila siku
na ya kawaida. Na kwamba mwenye sifa na vigezo vya kutosha ndiye
atakayekuwa kiongozi na wababishaji na wasanii hawatakaa tena wapewe
nafasi. Ninaamini hadi kufikia hapo uigizaji sinema utakuwa umefikia
kiwango cha juu kabisa na watu kama hao kwenda kutafuta utajiri huu na
sio kuja kulazimisha kuwa viongozi na wakubwa wetu tena. Na mwanamke
atakayekuja kuwa rais hatakuwa msanii au muigizaji bali mtendaji,
mleta mabadiliko ya kweli na mwanamapinduzi ya kiuchumi na kijamii.
Sifa za wanawake kama viongozi
Wanaume kama walivyozoea kusema uongo kwa wake, wapenzi , watoto na
jamaa zao ndivyo walivyogeuka kuwa waongo wakubwa pia katika siasa na
serikali.
Fursa ya kuwa na rais mwanamke, ambao kimsingi ni wastu wasiopenda
uongo ingawa wapo wanaopenda uongo na umbeya pia, ni fursa ya kuanza
kusafisha serikali na vyama vya siasa huko tunakokwenda. Ili
tuondokane kabisa na tabia inayojijenga hivi sasa kwamba ukienda
kuajiriwa na gazeti, redio au televisheni fulani unaajiriwa ili kwenda
kuandika au kutangaza uongo. Watu kwa njaa ya ajira na malezi ya
watoto na watu tegemezi wanakubali kuuza utu na ubinadamu wao kwa
kujidhalilisha kuandika na kutangaza uongo mweupee, ili tu mtu apate
kujisetiri. Hii ni aibu kubwa kuliko mfano, lakini ndipo hapa ambapo
wanasiasa wanaume leo wametufikisha.
Aidha, wanawake ni viumbe wenye kiasi na kutosheka, tofauti na
wanaume. Hii ina maana kwamba mwanamke akishapata vitu vya msingi
anavyohitaji katika maisha yake kwa kawaida hawi na tamaa zaidi kama
inavyokuwa kwa wanaume. Kwa hiyo kujilimbikizia ni sifa ambayo
mwanamke hanayo sana, ila panapokuwa na kasosro za kiakili, kitamaa na
kimaumbile kwa mhusika.
Mwanamke pia ni mzuri katika iktisadi. Uwekevu ni tabia ya kuifanya
shilingi elfu kumi itoshe siku tatu badala ya siku moja. Wanawake
wanayo sifa hii, lakini ni wanaume wachache sana wanayo. Na ndiyo
maana ukianza kumsema mwanamme kuwa anatumia vibaya, mbadhirifu,
hatunzi fedha ni mwepesi kununa. Lakini huu ni ukweli mwanamme daima
mbadhirifu. Na tunayaona hatuhitaji kuambiwa.
Sifa nyingine ya wanawake ni ile ya kuwa waaminifu (ingawa wanaokuwa
kinyume cha hivyo, hukubuku kuzidi hata wanaume), na hivyo angala kuwa
na watendaji chini ya rais mwanamke kama huyo ambaye watu wengi
wataiga mfano wake na hivyo kurejesha imani zaidi kwa wananchi. Ambao
hivi leo, hawaamini wanasiasa na hususana wabunge wao, kutokana na
yale yanayoendelea ndani na nje ya majimbo yao.
Katika miaka kadhaa, niliyokuwa mkuu kwenye makampuni na idara
mbalimbali, ilitokea aghalabu kuwategemea na kuwaamini wasaidizi wangu
wanawake zaidi ya nilivyowaamini wanaume. Wanaume huwa na sababu elfu
za kukuelezea wameshindwa kufanya jambo fulani kwa sababu hii au ile.
Matatizo mengi yanayowakabili Watanzania leo, yanawagusa zaidi
wakinamama kuliko wanaume. Mathalani, unapoongelea suala la watoto na
malezi, tatizo hili linabebwa kwa zaidi ya asilimia 90 na wanawake.
Hili linaendana na tatizo la mayatima na watoto wa mitaani. Hakuna
mama anayependa kumuona mwanawe au mtoto wa mwenzie katika uyatima au
kukosa mlezi. Hili haliwaumi sana wanaume. Pengine, kuwepo kwa rais
mwanamke kutatoa msukumo zaidi kwa upande huu.
Marais wanaume na wanasiasa kwa ujumla na mangimeza kwa upande
mwingine wamejenga mazingira ya kuwapa matunzo, malezi na uangalizi
viongozi wazee wastaafu. Lakini wazee wa kawaida hakuna anayewajali.
Kuwepo kwa rais mwanamke na ule ukweli kwamba sio wanaume bali ni
wanawake wanaosumbuka zaidi katika kuwatunza wazee wetu, upo uwezekano
mkubwa kwamba sera nzuri na zenye kufanya kazi zitabuniwa na kiongozi
huyo, kutokana na kuelewa uzito na ugumu wa kuwatunza wazee na kuwapa
matumaini huku ukijua fika wanasubiri kwenda safari yao wasiorejea
tena!
Ahadi nyingi zilizotolewa na rais aliyeko madarakani zilihusu
urahisishaji upatikanaji maji mijini na vijijini. Ni dhahiri ahadi
zilizo nyingi hazitatimizwa. Na ukweli ni kuwa anayesumbuliwa sana na
dhiki hii sio mwanamme, ni mwanamke, iwe mjini au vijijini ambapo sasa
kuna tofauti ndogo sana kati yao.
Kwa kutambua uzito wa tatizo la maji kwa wanawake, kiongozi mwanamke,
atajitoa kwa hali na mali, kuona anawasaidia wemzake kugeuza dhiki na
tatizo hili kuwa historia isiyopendeza katika nchi hii.
Hivi leo ugumu wa maisha nchini umefanya tatizo la utafutaji na
upatikanaji kuni, mkaa na nishati nyinginezo kuwa ghali na gumu zaidi
katika kila familia. Na mhusika mkuu au muathirika mkuu hapa sio
mwingine ila ni mwanamke.
Ni dhahiri, rais mwanamke atafanya kila awezalo ili adha na kero ya
gharama na upatikanaji wa nishati kwa njia inayorahisisha maisha ya
mwanamke mijini na vijijini yawe ni mambo yatakayopigwa vita kwa
ukucha na jino na kwa wepesi wa radi au tetemeko la ardhi.
Hivi sasa vijana wengi wanakimbilia mjini na hivyo kuwaachia mama na
dada zao kazi zote za sulubu kiasi ambacho wanawake wengi vijijini
wanachoka na kupoteza uzuri wao wakiwa na miaka 30 tu. Hii si haki, ni
lazima rais ajaye ahakikishe kwamba tunawarahisishia wanawake maisha
huko vijijini kwa namna ambayo wanawake wanaendelea kuwa wabichi na
wenye mvuto hata wakiwa na miaka 40. Na hili ni jambo linalowezekana
kama wanawake watakataa kuendelea wabeba mifuko ya wanaume nchini, na
wao kumchagua mwanamke mwenzao kuwa rais wa kwanza mwanamke katika
kizazi hiki na wakati huu tulio nao. Maana ukweli ni mwanamke tu,
ndiye anayeweza kuamua rais ajaye awe mwanamke au mwanamme!
Picha nyingi tulizoziona wakati wa mgomo wa madaktari nchini,
hazikuonyesha wanaume bali wanawake. Na wanaume ni wale wababe
waliokuwa wakidiriki pamoja na kuugua kwao kusema kwamba madaktari
poa, waendelee tu na mgomgo wao mbona wanasiasa wanakwiba mchana
kweupe?
Ninahakika rais mwanamke siyo tu ataimarisha huduma na afya tofauti na
viongozi wa sasa, bali ataiwezesha nchi kuwa na huduma za kisasa na
kukomesha kabisa nchi kupoteza mabilioni kwa ajili ya kwenda tibia
watu nchi za nje, kwani mahospitali ya hapa nyumbani nayo yatakuwa
yanatibu pia wagonjwa kutoka nchi za nje katika wakati wake.
Tahadhari: Ili kumpata kiongozi bora na atakayekuwa mfano kwa wanawake
na wanaume ni vizuri kuepuka wanawake wenye uchama kupindukia; wenye
tabia ya kuzomea na kukashifu wenye mitazamo tofauti; wapigaji
vigelegel ovyo na wale wanaobebwa sio kwa sababu ya akili na uwezo wao
bali kwa sababu ya jinsia yao. Aidha, huu si wakati wa kuwa na
viongozi wanaopenda kwenda nchi za nje wasikojifunza lolote la
kuibadili nchi yao, bali wakati wa kuwa na kiongozi anayependa kwenda
vijijini na kujifunza mbinu na mikakati ya kuufuta umaskini huko huko
vijijini, na wakati huohuo kuwatunuku wanavijiji utajiri na neema, na
hivyo nchi yetu nzima kuwa tajiri na ustawi wa hali ya juu zaidi
kimaisha.
Monday, February 20, 2012
Friday, February 3, 2012
Wizara ya Afya, Uongozi na Muundo wake vinakwenda na wakati?
KWA UJUMLA pamoja na bajeti kubwa na misaada mbalimbali ambayo Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii hupata bado sekta hii sikuzote imekuwa katika tatizo hili au lile.
Tatizo hili la madaktari kugoma ni tatizo lililokuwa njiani na kila mtu akawa analiona, lakini wengi wakaamua kuficha kichwa chao mchangani kama vile mbuni afanyavyo anavyoona hatari i mbele yake. Hili ni kosa kwa sababu unatoa nafasi kwa nadhara makubwa zaidi kutokea.
Isitoshe hili ni moja tu kati ya matatizo ambayo wizara hiyo inakabiliana nayo. Yapo mengine mengi, makubwa kwa madogo ambayo kama petroli yanahitaji mtu kupita tu na kijinga cha moto na moto ukalipuka. Hivyo, kutafuta mchawi wa matatizo ya sekta ya afya kunakoishia kumtaja mtu mmoja au wawili sio kitu cha busara wala hekima na hakimsaidiii yoyote ndani au nje ya wizara husika.
Binafsi ninaamini kuna matatizo yafuatayo katika wizara husika: Utawala, uaminifu na uwezo wa mameneja wa mahospitali;
madaktari kufunguka macho zaidi juu ya haki zao zisizotekelezwa; manesi na wafnyakazi wasaidizi katika mahospitali mbalimbali kugeuzwa wafanyakazi maskini na ombaomba; wagonjwa kukosa mahitaji, ulinzi na maangalizi ya msingi.
Aidha ni makosa kwa upande wangu kwa wizara hiyo kubebeshwa idara kama ile
ya Ustawi wa jamii na makundi yake ambayo kwa maono yangu ni mzigo ambao nao unahitaji ubebaji wa aina yake ili kutendea haki sawa pande zote mbili, yaani Idara ya Afya na ile Idara ya Ustawi wa Jamii.
Vilevile, huu ni wakati wa kuangalia upya kama uoga wetu wa kuiachia mikoa na wilaya kuwa huru zaidi katika mipanga, mikakati, oganaizesheni na utekelezaji wa majukumu ya sekta ya afya nchini ni kitu kinachosaidia kupungua au kuongeza matatizo katika sekta hiyo.
Matatizo mengine ninayoyaona kwa upande wangu ni lile la ujira, maslahi na posho za watumishi wa ngazi za kati na chini katika wizara hiyo; kukosa utawala na menejimenti bora ya rasilimali watu katika sekta muhimu kama hii; muundo wa wizara uliopitwa na wakati;
kukosa aina yoyote ya ushindani kati ya wafanyakazi na kati ya mahospitali nchini; kukosa mifuko maalum kwa mahospitali na watumishi inayoweza kuchangia kuleta ahueni kwa njia moja au nyingine; udhibiti dhaifu wa rasilimali na hususan fedha wizarani na kukosekana na ubunifu na uvumbuzi katika sekta nzima ya afya nchini.
Ninaamini sina akili wala uwezo wa kutoa majawabu kwa changamoto zinazokabili wizara hii, kwani kitakwimu na kitaalamu sijajaliwa uwezo wa kufundwa na kuelewa kila jambo lipasalo. Nitajaribu tu kutoa mawazo ya kijuu juu ambayo kwayo waelewa zaidi wanaweza kujenga juu yake na hatimaye ufumbuzi wa matatizo ya kudumu au ya muda mrefu kwa wizara na changamoto zake yakapatikana.
Sekta hii ni nyeti. Inahitaji mameneja na watawala ambao wanaoana na kuiva vizuri na watumishi wa ngazi za juu na chini. Ukiwaweka watu wanaojiona ni wakubwa, bora na muhimu zaidi kuliko wengine basi misingi yote ya kuwa na wizara yenye mafanikio unakuwa umebomolewa fumba na kufumbua. Siingili kwa undani zaidi juu ya hili, lakini kwa wote wanaoelewa ukweli huu tutakuwa kwa uahkika katika frekwensi moja hapa.
Ikiwezekana majopo ya wataalamu husika yatastahili kuwashauri wakubwa wa nchi nani anafaa kwa nafasi ya uwaziri, unaibu waziri na nafasi za juu katika wizara na mahospitali kwa namna wazi na bora zaidi kuliko iliyopo hivi sasa. Kubwa la kuzingatiwa ni kuwa na watu wenye uwezo wa juu kiutendaji katika masuala ya utawala, uaminifu na uwezo wa kiumeneja katika mahospitali na sekta ya afya na tiba kwa ujumla.
Madaktari kutokana na yale yanayotokea kwingineko hivi duniani wameona mengi ambayo yamewasaidia kufunguka macho juu ya mambo mengi. Ni vizuri viongozi wa wizara wakajua kuwa wanayoyajua kuhusu sekta hiyo na mahospitali katika nchi zenye maisha bora ingawa maskini na
madaktari wetu nao wamefunguka macho zaidi juu ya haki zao zisizotekelezwa.
Aidha, manesi na wafnyakazi wasaidizi katika mahospitali mbalimbali wamechoka kugeuzwa wafanyakazi maskini na ombaomba katika nchi yao na kukosa uwezo wa kuwalisha na kuwasomesha vizuri watoto wao ila kwa kungojea bakshishi kutoka kwa wakubwa ambao ndio chanzo cha wadhifa wao kimshahara, kimaslahi na kihali ya maisha.
Katika nchi ambayo kuna tatizo kubwa la ajira na vifaa vinavyotakiwa na mahospitali vinaweza kutengenezwa na magenge ya seremakala au mawelda (wachomaji na waundaji vitu vya bati na chuma) toka Mwenge, Keko, Kawe na kwingineko nchini na wagonjwa kukosa mahitaji, samani, vifaa, ulinzi na maangalizi ya msingi, basi wanaosimamia wizara husika ni kama vile wapo wapo tu, na ni ile aina ya uongozi ambayo huachia matatizo kuendelea kuwa matatizo katika sehemu husika, hata ukiwaachia miaka hamsini kufanya kazi mahala hapo.
Aidha ni makosa kwa upande wangu kwa wizara hiyo kubebeshwa idara kama ile
ya Ustawi wa jamii na makundi yake ambayo kwa maono yangu ni mzigo ambao nao unahitaji ubebaji wa aina yake ili kutendea haki sawa pande zote mbili, yaani Idara ya Afya na ile Idara ya Ustawi wa Jamii.
Kwa maneno mengine ni makosa kuwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kama wizara moja badala ya kuwa ni wizara mbili. Ndio maana hivi leo utunzaji na usaidizi kwa wazee, watoto watundu wanaoishinda jamii na familia zao, mayatima, walemavu, albino, wajane, ombaomba na watu kama hao ni mambo yanayofanyika kiubabaishaubabaishaji tu na kuruhusu wajanja kujinufaisha kutokana na ombwe lililopo.
Vilevile, huu ni wakati wa kuangalia upya kama uoga wetu wa kuiachia mikoa na wilaya kuwa huru zaidi katika mipanga, mikakati, oganaizesheni na utekelezaji wa majukumu ya sekta ya afya nchini ni kitu kinachosaidia kupungua au kuongeza matatizo katika sekta hiyo.
Muundo mpya, majukumu mapya
Ninavyoamini ni kuwa wizara ya Afya ingeliachiwa tu kushughulikia majukumu ya upatikanaji dawa, uendeshaji mahospitali na uratibu wa shughuli za kinga, afya na tiba nchini na si zaidi ya hapo.
Shughuli na majukumu yote yanayosalia, kwa maoni yangu, yangestahili kupewa Taasisi huru ambazo utendaji wake sio utakuwa na ufanisi na ufanifu zaidi bali pia unaweza ukawa ungiza fedha zaidi kuliko ya zinavyotumia.
Pamoja na wizara kugawanywa katika sehemu zaidi ya mbili ningelipendekeza pia kwamba
hata wizara ya afya asilia yenyewe igawanywe katika:
Taasisi ya Hospitali za Ngazi ya Rufaa nchini; Taasisi ya Hospitali za Ngazi ya Mkoa nchini; Taasisi ya Hospitali za Ngazi ya Wilaya nchini;
Taasisi za Hospitali Binafsi na zahananti; Taasisi za Hospitali za Kijamii na Hospitali za Kiimani nchini; Taasisi ya Utafiti kwa Tiba Mbadala na Tiba za Kisunna na Taasisi Maalum ya Kuoanisha na Kuunganisha nguvu na uwezo wa taasisi za sekta za afya kwa ufanisi na ufanifu zaidi nchini.
Dhamira kuu ya uanzishwaji wa taaisisi kama hizo hapo juu zinatokana na ule ukweli kwamba wizara na hospitali zetu kwa hali ilivyo haziwwezi kujitosheleza katika mahitaji yao yote bila kuwa watundu, wabunifu, wavumbuzi na wanaoweza kupanua wigo wa wagonjwa wanaotibiwa hadi nje ya mipaka yetu. Hiki ni kitu kinachowezakana, kinataka tu serikali iliyo angavu na inayotoa fursa kwa wenye mawazo mapya kuonekana, kufnayiwa kazi, kutunzwa na kuenziwa.
Matatizo mengine ninayoyaona kwa upande wangu ni lile la ujira, maslahi na posho za watumishi wa ngazi za kati na chini katika wizara hiyo. Katika nchi kama Norway hivi leo kuna watu wachache wanaotaka uanasiasa au uwaziri kwa sababu kazi wanazozifanya zinawalipa vizuri zaidi kuliko uwaziri au ubunge.
Kwa kugeuza miguu juu na kichwa chini sera hii muhimu ya kipato cha mtu, leo tunaishiwa kuwa na watu wa ajabu wanaopewa nafasi za ubunge, baadhi yao wakifanya pati na kualika wasichana wenye sketi fupi tu kuliko wote kuhudhuria pati hizo !!! Hawa ndio wabunge wetu, na hii ni nchi yetu, na yote haya tumeyataka sisi wenyewe!
Wizara husika na mahospitali ni maeneo yanayohitaji idara nzito ya rasilimali watu. Ukikosa utawala na menejimenti bora ya rasilimali watu katika sekta muhimu kama hii; na kuwa na muundo wa wizara uliopitwa na wakati;
na ukakosa aina yoyote ya ushindani kati ya wafanyakazi na kati ya mahospitali na taasisi au idara zake nchini ni dhahiri unajenga mwanzo mzuri wa matatizo na shinikizo zisizokwisha wakati wote huko mbele ya safari. Ni muhimu kuvuta hatua moja nyuma na kuona ni kwa namna gani jambo hili linaweza kufikiriwa na kuzingatiwa na kisha kuingizwa katika mbinu na mikakati ya ujenzi wa wizara mpya yenye mtazamo chana unaojiandaa kabla kupambana na kila aina ya changamoto mbele yake.
Umefika wakati wa kujiuliza pia kama ni shahi kwa wizara na mahospitali mikoani na wilayani kukosa mifuko maalum kwa mahospitali na watumishi inayoweza kuchangiwa na wenye fedha na uwezo nchini iwe ni watu binafsi au mashirika au taasisi za kidini au vyama vya kisiasa !
Mifuko kama hii si haba inaweza kuchangia kuleta nyingine katika mahospitali na zahanati zetu katika maeneo mbalimbali ya taifa letu.
Ipo haja pia ya kuangalia kama tuna udhibiti imara au dhaifu wa rasilimali na hususan fedha wizarani. Aidha, kuona kama matumizi ya wizara hiyo ni yale ambayo kweli yanastahili kufanyika na wizara husika au ni matumizi ambayo hayastahili kuwa na nafasi katika wizara kama hiyo. Maana ukiwa na wizara inayotumia mabilioni kulipia matangazo ya biashara kwangu binafsi ni walakini mkubwa na unastahili kutazamwa na CAG kwa undani zaidi ya kawaida anayoifanya.
Wizara ambayo inaviza na kudumaza akili, uwezo, ubunifu na uvumbuzi katika rasilimali watu zake ni wizara inayojichimbia kabura lake wakati yenyewe ingali hai kwa kupenda. Na wizara ikiwa hivyo basi hilo huashiria kukosekana na kuadimika kwa ubunifu na uvumbuzi katika sekta nzima ya afya nchini.
Ni muhimu pia kujenga ushindani kati ya hospitali, vituo vya afya na zahanati nchini na hata kati ya hospitali za rufaa kibiashara na kijamii pia. Na wale wanaokuwa bora kutunzwa kwa mujibu wa taratibu na kanuni zitakazokubaliwa na wadau wote. Bila ya ushindani, tutaendelea kuachia wasiostahili kuzawadiwa, na wanaostahili kuzawadiwa kutokupata lolote na hivyo kuwavunja moyo na imani.
Lazima wizara na hospitali za rufaa, mikoa na wilaya kuwa na mfuko maalum (Health and Medicare Foundation) wa fedha za kuchangia na msaada kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya hospitali na vilevile kuendesha tafiti mbalimbali ambazo zitawasaidia interns na waganga kufanya utafiti utaowangezea kipato chao kwa namna moja au nyingine.
Tunastahili pia kuuwatumia vijana wa Kitanzania wasio na ajira kutengeneza vitanda, magodoro, mipira ya wagonjwa na samani na vifaa vinavyohitajika mahospitalini na kwa hiyo tukaua ndege wawili kwa jiwe moja.
Huu ni wakati pia wa kuziwezesha na kuziipa hospitali za mipakani changamoto na uwezo wa kutibu wagonjwa toka nje ya mipaka yetu na kwa uwekezaji huu sekta ya afya na tiba isibaki kuwa ya matumizi tu, bali pia inayoiingia taifa pato la haja.
Kinachohitajika ni kuboresha majengo na mandhari ya hospitali husika, kuwapa madaktari na watumishi wengine motisha ya kutosha, na kisha kuweka vifaa vya kisasa katika mahospitali hayo na hivyo kuiingizia nchi fedha za kigeni na uwezo wa kupunguza gharama kwa wagonjwa wa ndani..
Tatizo hili la madaktari kugoma ni tatizo lililokuwa njiani na kila mtu akawa analiona, lakini wengi wakaamua kuficha kichwa chao mchangani kama vile mbuni afanyavyo anavyoona hatari i mbele yake. Hili ni kosa kwa sababu unatoa nafasi kwa nadhara makubwa zaidi kutokea.
Isitoshe hili ni moja tu kati ya matatizo ambayo wizara hiyo inakabiliana nayo. Yapo mengine mengi, makubwa kwa madogo ambayo kama petroli yanahitaji mtu kupita tu na kijinga cha moto na moto ukalipuka. Hivyo, kutafuta mchawi wa matatizo ya sekta ya afya kunakoishia kumtaja mtu mmoja au wawili sio kitu cha busara wala hekima na hakimsaidiii yoyote ndani au nje ya wizara husika.
Binafsi ninaamini kuna matatizo yafuatayo katika wizara husika: Utawala, uaminifu na uwezo wa mameneja wa mahospitali;
madaktari kufunguka macho zaidi juu ya haki zao zisizotekelezwa; manesi na wafnyakazi wasaidizi katika mahospitali mbalimbali kugeuzwa wafanyakazi maskini na ombaomba; wagonjwa kukosa mahitaji, ulinzi na maangalizi ya msingi.
Aidha ni makosa kwa upande wangu kwa wizara hiyo kubebeshwa idara kama ile
ya Ustawi wa jamii na makundi yake ambayo kwa maono yangu ni mzigo ambao nao unahitaji ubebaji wa aina yake ili kutendea haki sawa pande zote mbili, yaani Idara ya Afya na ile Idara ya Ustawi wa Jamii.
Vilevile, huu ni wakati wa kuangalia upya kama uoga wetu wa kuiachia mikoa na wilaya kuwa huru zaidi katika mipanga, mikakati, oganaizesheni na utekelezaji wa majukumu ya sekta ya afya nchini ni kitu kinachosaidia kupungua au kuongeza matatizo katika sekta hiyo.
Matatizo mengine ninayoyaona kwa upande wangu ni lile la ujira, maslahi na posho za watumishi wa ngazi za kati na chini katika wizara hiyo; kukosa utawala na menejimenti bora ya rasilimali watu katika sekta muhimu kama hii; muundo wa wizara uliopitwa na wakati;
kukosa aina yoyote ya ushindani kati ya wafanyakazi na kati ya mahospitali nchini; kukosa mifuko maalum kwa mahospitali na watumishi inayoweza kuchangia kuleta ahueni kwa njia moja au nyingine; udhibiti dhaifu wa rasilimali na hususan fedha wizarani na kukosekana na ubunifu na uvumbuzi katika sekta nzima ya afya nchini.
Ninaamini sina akili wala uwezo wa kutoa majawabu kwa changamoto zinazokabili wizara hii, kwani kitakwimu na kitaalamu sijajaliwa uwezo wa kufundwa na kuelewa kila jambo lipasalo. Nitajaribu tu kutoa mawazo ya kijuu juu ambayo kwayo waelewa zaidi wanaweza kujenga juu yake na hatimaye ufumbuzi wa matatizo ya kudumu au ya muda mrefu kwa wizara na changamoto zake yakapatikana.
Sekta hii ni nyeti. Inahitaji mameneja na watawala ambao wanaoana na kuiva vizuri na watumishi wa ngazi za juu na chini. Ukiwaweka watu wanaojiona ni wakubwa, bora na muhimu zaidi kuliko wengine basi misingi yote ya kuwa na wizara yenye mafanikio unakuwa umebomolewa fumba na kufumbua. Siingili kwa undani zaidi juu ya hili, lakini kwa wote wanaoelewa ukweli huu tutakuwa kwa uahkika katika frekwensi moja hapa.
Ikiwezekana majopo ya wataalamu husika yatastahili kuwashauri wakubwa wa nchi nani anafaa kwa nafasi ya uwaziri, unaibu waziri na nafasi za juu katika wizara na mahospitali kwa namna wazi na bora zaidi kuliko iliyopo hivi sasa. Kubwa la kuzingatiwa ni kuwa na watu wenye uwezo wa juu kiutendaji katika masuala ya utawala, uaminifu na uwezo wa kiumeneja katika mahospitali na sekta ya afya na tiba kwa ujumla.
Madaktari kutokana na yale yanayotokea kwingineko hivi duniani wameona mengi ambayo yamewasaidia kufunguka macho juu ya mambo mengi. Ni vizuri viongozi wa wizara wakajua kuwa wanayoyajua kuhusu sekta hiyo na mahospitali katika nchi zenye maisha bora ingawa maskini na
madaktari wetu nao wamefunguka macho zaidi juu ya haki zao zisizotekelezwa.
Aidha, manesi na wafnyakazi wasaidizi katika mahospitali mbalimbali wamechoka kugeuzwa wafanyakazi maskini na ombaomba katika nchi yao na kukosa uwezo wa kuwalisha na kuwasomesha vizuri watoto wao ila kwa kungojea bakshishi kutoka kwa wakubwa ambao ndio chanzo cha wadhifa wao kimshahara, kimaslahi na kihali ya maisha.
Katika nchi ambayo kuna tatizo kubwa la ajira na vifaa vinavyotakiwa na mahospitali vinaweza kutengenezwa na magenge ya seremakala au mawelda (wachomaji na waundaji vitu vya bati na chuma) toka Mwenge, Keko, Kawe na kwingineko nchini na wagonjwa kukosa mahitaji, samani, vifaa, ulinzi na maangalizi ya msingi, basi wanaosimamia wizara husika ni kama vile wapo wapo tu, na ni ile aina ya uongozi ambayo huachia matatizo kuendelea kuwa matatizo katika sehemu husika, hata ukiwaachia miaka hamsini kufanya kazi mahala hapo.
Aidha ni makosa kwa upande wangu kwa wizara hiyo kubebeshwa idara kama ile
ya Ustawi wa jamii na makundi yake ambayo kwa maono yangu ni mzigo ambao nao unahitaji ubebaji wa aina yake ili kutendea haki sawa pande zote mbili, yaani Idara ya Afya na ile Idara ya Ustawi wa Jamii.
Kwa maneno mengine ni makosa kuwa na Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii kama wizara moja badala ya kuwa ni wizara mbili. Ndio maana hivi leo utunzaji na usaidizi kwa wazee, watoto watundu wanaoishinda jamii na familia zao, mayatima, walemavu, albino, wajane, ombaomba na watu kama hao ni mambo yanayofanyika kiubabaishaubabaishaji tu na kuruhusu wajanja kujinufaisha kutokana na ombwe lililopo.
Vilevile, huu ni wakati wa kuangalia upya kama uoga wetu wa kuiachia mikoa na wilaya kuwa huru zaidi katika mipanga, mikakati, oganaizesheni na utekelezaji wa majukumu ya sekta ya afya nchini ni kitu kinachosaidia kupungua au kuongeza matatizo katika sekta hiyo.
Muundo mpya, majukumu mapya
Ninavyoamini ni kuwa wizara ya Afya ingeliachiwa tu kushughulikia majukumu ya upatikanaji dawa, uendeshaji mahospitali na uratibu wa shughuli za kinga, afya na tiba nchini na si zaidi ya hapo.
Shughuli na majukumu yote yanayosalia, kwa maoni yangu, yangestahili kupewa Taasisi huru ambazo utendaji wake sio utakuwa na ufanisi na ufanifu zaidi bali pia unaweza ukawa ungiza fedha zaidi kuliko ya zinavyotumia.
Pamoja na wizara kugawanywa katika sehemu zaidi ya mbili ningelipendekeza pia kwamba
hata wizara ya afya asilia yenyewe igawanywe katika:
Taasisi ya Hospitali za Ngazi ya Rufaa nchini; Taasisi ya Hospitali za Ngazi ya Mkoa nchini; Taasisi ya Hospitali za Ngazi ya Wilaya nchini;
Taasisi za Hospitali Binafsi na zahananti; Taasisi za Hospitali za Kijamii na Hospitali za Kiimani nchini; Taasisi ya Utafiti kwa Tiba Mbadala na Tiba za Kisunna na Taasisi Maalum ya Kuoanisha na Kuunganisha nguvu na uwezo wa taasisi za sekta za afya kwa ufanisi na ufanifu zaidi nchini.
Dhamira kuu ya uanzishwaji wa taaisisi kama hizo hapo juu zinatokana na ule ukweli kwamba wizara na hospitali zetu kwa hali ilivyo haziwwezi kujitosheleza katika mahitaji yao yote bila kuwa watundu, wabunifu, wavumbuzi na wanaoweza kupanua wigo wa wagonjwa wanaotibiwa hadi nje ya mipaka yetu. Hiki ni kitu kinachowezakana, kinataka tu serikali iliyo angavu na inayotoa fursa kwa wenye mawazo mapya kuonekana, kufnayiwa kazi, kutunzwa na kuenziwa.
Matatizo mengine ninayoyaona kwa upande wangu ni lile la ujira, maslahi na posho za watumishi wa ngazi za kati na chini katika wizara hiyo. Katika nchi kama Norway hivi leo kuna watu wachache wanaotaka uanasiasa au uwaziri kwa sababu kazi wanazozifanya zinawalipa vizuri zaidi kuliko uwaziri au ubunge.
Kwa kugeuza miguu juu na kichwa chini sera hii muhimu ya kipato cha mtu, leo tunaishiwa kuwa na watu wa ajabu wanaopewa nafasi za ubunge, baadhi yao wakifanya pati na kualika wasichana wenye sketi fupi tu kuliko wote kuhudhuria pati hizo !!! Hawa ndio wabunge wetu, na hii ni nchi yetu, na yote haya tumeyataka sisi wenyewe!
Wizara husika na mahospitali ni maeneo yanayohitaji idara nzito ya rasilimali watu. Ukikosa utawala na menejimenti bora ya rasilimali watu katika sekta muhimu kama hii; na kuwa na muundo wa wizara uliopitwa na wakati;
na ukakosa aina yoyote ya ushindani kati ya wafanyakazi na kati ya mahospitali na taasisi au idara zake nchini ni dhahiri unajenga mwanzo mzuri wa matatizo na shinikizo zisizokwisha wakati wote huko mbele ya safari. Ni muhimu kuvuta hatua moja nyuma na kuona ni kwa namna gani jambo hili linaweza kufikiriwa na kuzingatiwa na kisha kuingizwa katika mbinu na mikakati ya ujenzi wa wizara mpya yenye mtazamo chana unaojiandaa kabla kupambana na kila aina ya changamoto mbele yake.
Umefika wakati wa kujiuliza pia kama ni shahi kwa wizara na mahospitali mikoani na wilayani kukosa mifuko maalum kwa mahospitali na watumishi inayoweza kuchangiwa na wenye fedha na uwezo nchini iwe ni watu binafsi au mashirika au taasisi za kidini au vyama vya kisiasa !
Mifuko kama hii si haba inaweza kuchangia kuleta nyingine katika mahospitali na zahanati zetu katika maeneo mbalimbali ya taifa letu.
Ipo haja pia ya kuangalia kama tuna udhibiti imara au dhaifu wa rasilimali na hususan fedha wizarani. Aidha, kuona kama matumizi ya wizara hiyo ni yale ambayo kweli yanastahili kufanyika na wizara husika au ni matumizi ambayo hayastahili kuwa na nafasi katika wizara kama hiyo. Maana ukiwa na wizara inayotumia mabilioni kulipia matangazo ya biashara kwangu binafsi ni walakini mkubwa na unastahili kutazamwa na CAG kwa undani zaidi ya kawaida anayoifanya.
Wizara ambayo inaviza na kudumaza akili, uwezo, ubunifu na uvumbuzi katika rasilimali watu zake ni wizara inayojichimbia kabura lake wakati yenyewe ingali hai kwa kupenda. Na wizara ikiwa hivyo basi hilo huashiria kukosekana na kuadimika kwa ubunifu na uvumbuzi katika sekta nzima ya afya nchini.
Ni muhimu pia kujenga ushindani kati ya hospitali, vituo vya afya na zahanati nchini na hata kati ya hospitali za rufaa kibiashara na kijamii pia. Na wale wanaokuwa bora kutunzwa kwa mujibu wa taratibu na kanuni zitakazokubaliwa na wadau wote. Bila ya ushindani, tutaendelea kuachia wasiostahili kuzawadiwa, na wanaostahili kuzawadiwa kutokupata lolote na hivyo kuwavunja moyo na imani.
Lazima wizara na hospitali za rufaa, mikoa na wilaya kuwa na mfuko maalum (Health and Medicare Foundation) wa fedha za kuchangia na msaada kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya hospitali na vilevile kuendesha tafiti mbalimbali ambazo zitawasaidia interns na waganga kufanya utafiti utaowangezea kipato chao kwa namna moja au nyingine.
Tunastahili pia kuuwatumia vijana wa Kitanzania wasio na ajira kutengeneza vitanda, magodoro, mipira ya wagonjwa na samani na vifaa vinavyohitajika mahospitalini na kwa hiyo tukaua ndege wawili kwa jiwe moja.
Huu ni wakati pia wa kuziwezesha na kuziipa hospitali za mipakani changamoto na uwezo wa kutibu wagonjwa toka nje ya mipaka yetu na kwa uwekezaji huu sekta ya afya na tiba isibaki kuwa ya matumizi tu, bali pia inayoiingia taifa pato la haja.
Kinachohitajika ni kuboresha majengo na mandhari ya hospitali husika, kuwapa madaktari na watumishi wengine motisha ya kutosha, na kisha kuweka vifaa vya kisasa katika mahospitali hayo na hivyo kuiingizia nchi fedha za kigeni na uwezo wa kupunguza gharama kwa wagonjwa wa ndani..
Thursday, December 22, 2011
Dar kimaafa ni bomu litakalolipuka wakati wowote
NI DHAHIRI suala la kuishi au kuhama mabondeni, hususan Jangwani, ni
suala 'lililosiasaishwa' na haiwezekani chama kilichoko madarakani na
serikali kuwahamisha wakazi wa maeneo haya kwa nguvu kama nguvu
inavyotumika sehemu zingine kutokana na kuhitajika kwa mtaji wa kisiasa.
Haiwezekani pia kidira, kisera, kifedha, kiteknolojia na kiuwezo kwa Dar es
salaam ambayo ni pua na mdomo na bahari kuwa na miundo mbinu
itakaloliwezesha jiji litapike maji yote ya mvua yaende baharini kama tu
imeshidwa kutapisha maji taka na ya matumizi ya kawaida kwenda baharini.
Ugumu wa hili umedhirishwa na kauli zinazopingana juu ya kuhama au
kutokuhama mabondeni zinazotolewa na viongozi wa serikali na chama
tawala. Haiwezekani katika muda mfupi na siamini kama suala hilo limo
katika kipaumbele cha serikali. Je, kiuhalisia kinachobakia kushauri ni kitu
gani ? Nitajaribu ingawa ninajua ni mtihani mkubwa kufanya hivyo katika
makala yangu leo. Ila kama kawaida tutarajie amri zisizotekelezeka na ahadi zisizotimizwa.
Kipindi cha pili cha awamu ya nne kilianza kwa bishara njemba katika
angalau za masula ya nyumba na makazi, lakini kadri muda unavyokwenda
imedhihirika kuwa hizo zilikuwa ni nguvu za soda tu.
Biashara hizo zilitokana kwanza na kuteuliwa kwa mwanamke aliyeswahi
kushika wadhifa wa juu katika shilrika la masula ya nyumba na makazi na
kauli zake za mwanzo ambazo zilionekana kama angelikuwa na uhuru wa
kufanya yale anayofikiria kichwani kwake leo angalau tungelianza angalau
kuona ishara za kuwa na mipngo miji katika nchi ambayo kwa mapana na
marefu na kwa ujumla yake ilikwishazika kabisa suala la mipango miji na
ujenzi uaoangalia na kutahadhari na yanayoweza kutokea kesho na kesho
kutwa.
Jambo moja linalochangia udhaifu katika utawala na menejimenti yetu ya
nyumba na makazi ni sheria za kubembelezana na kuvumiliana. Na siku hizi
umezuka mtindo kuwa pakijengwa kijiwe cha chama tawala mahala fulani,
basi mahala hapo panahesabika kuwa sehemu ambayo hata kama sheria
zimevunjwa, hazikuvunjwa!
Hizi ni siasa za kutafuta kupendwa na umaarufu, huku mtu akijua fika kwa
kuruhusu kinachofanyika kiendelee kufanyika basi mwisho wake ni zahama,
dhiki na vifo kwa wale wanouhurumiwa na kvumililiwa. Ninaamini wakati
umefika kwa nchi yetu kujenga heshima ya kuwa na utawala wa kisheria
ambao haushawishiwi vinginevyo na wanasiasa kwa malengo yao binafsi.
Pamoja na ujenzi wa nyumba mabondeni ipo mifano mingi ya kimaafa
maafa tu inayosubiri cheche moja tu, moto au bomu kulipuka.
Mifano hiyo ni pamoja na vituo vya zima moto na upatikanaji maji kuwa mbali
na maeneo ambayo janga la moto linaweza likazuka.
Manispaa mbalimbali za maji zimeruhusu au kuachia watu kujenga kuta au
vizuizi vya aina mbalimbali ambavyo vinaweza vikachangia si haba ukubwa
wa maafa na hasa yale ya maji na mafuriko.
Tembelea sehemu mbalimbali za jiji la Dar es salaam na utakuta makumi
kama sio mamia ya vituo vya petroli ambavyo vimejenga kando ya masoko
au ndani ya makazi ya watu.
Watalii mbalimbali hivi sasa wanahofia kuja Tanzania kutokana na
kukosekana usalama wa kutosha mabarabarani . Jambo linalosababishwa
na malori, daladala, bajaji, pikipiki, mikokoteni na vyombo vingine vya
uchukuzi kutofuata sheria zilizopo na kukosa uungwana na ustaarabu katika
maingiliano ya watu njiani.
Aidha, kumekuwa na kauli kadhaa za kisheria zisizotekelezwa juu ya hili au
lile, mojawapo likiwa ni amri inayokataza watu kuishi mabondeni toka zama
za Mzee Makamba alipokuwa mkuu wa mkoa wa jijimkoa.
Nchi haiwezi kamwe kujengwa kwa siasa za kujipendekeza, kutaka
kuonekana wema na wazuri na wengine wabaya na unafiki mwingine kama
huo. Ni lazima tufike mahala ambapo sheria zetu zinalinda na kutunza roho
za watu, kisha utamaduni, imani na mali za watu . Mengine ni uzandiki wa
kisiasa ulio na melngo binafsi dhidi ya yale yanayostahili kuwa ya umma.
Ninaamini, wakati tunatoa michango yetu kuhusu katiba yetu mpya itulinde
vipi tokana na wale tunaowapa ukubwa tutahakikisha kuwa ulinzi na
usalama wa roho za watu, utamaduni na mali zao unapewa uzito
unaostahili.
Kama azma yetu basi itakuwa ni hivyo ni dhahiri kubainisha hapa kwamba
huwezi ukalinda na kuthamini maisha ya wananchi wako kama wewe kama
serikali na mkusanyaji mkuu wa kodi na mirabaha unashindwa kuwapatia
wananchi unaowaongoza mahitaji yao ya msingi. Mahitaji hayo ya msingi ni
pmoja na nyumba na makazi bora na salama.
Nyumba kama hitaji la msingi
Kichekesho kwa wazungu na wageni wengi wanaotembelea nchi hii ni pale
wanapokuta kuwa kila Mtanzania ana mradi wa kujenga nyumba. Pengine
hawaelewi umasikini na kudunduliza kwetu na jinsi tunavyozaliana kwa
wingi, lakini bado ukweli unabakia pale pale wengi wanatushangaa
wanapoona badala ya kujenga vitu vya kututajirisha tunajenga vitu vya
kutumasikinisha.
Ukiweka siasa pembeni, nyumba ni hitaji la msingi la kila mwanadamu.
Inasemekana baada ya chakula na maji basi nyumba ni muhimu kuliko kitu
kingine. Kutokana na ukweli huu, serikali iliyokuwa makini haiwezi
kulichukulia suala hili kimzahaha mzaha au kuliona ni mzigo na kulisukuma
ili libebwe na watu wengine. Bila watu kuwa na nyumba bora na salama hata
kama watajishughulisha na mengi mazuri katika uzalishaji na ujenzi wa
nchi, fumba na kufumbua, siku moja vyote vinaweza kuoshwa au kufagiliwa
mbali na maafa ya aina hii au ile.
Serikali inayoona mbali na mbele, kwa hiyo, huwa inachukulia suala la
mipango na mikakati ya nyumba na makazi kama jiwe la msingi la
maendeleo la taifa na watu husika. Inafanya hivyo, kwa kuzingatia kuwa vita
vyote vingine vinavyokabili watu wake vikiwemo vile vya ujinga, njaa, maradhi
na umaskini ni vita vitakavyokuwa rahisi sana kuibuka kidedea kama
washindi wasioshindika.
Katika muktadha huu, hoja yangu hapa ni kwamba tusianze kumwaga
machozi ya mamba huku tukijua fika kwamba siasa zetu za kujipendekeza
zimechangia si haba kuwapotezea Watanzania wenzetu ambao kama sheria
zingelikuwa zinawalinda na rasilimali za nchi zinatumika kuwanufaisha wao
na sio vinginevyo hivi leo wasingelikuwa marehemu.
Ninasema hivyo, kwa kudhihirisha kuwa ulegevu na urojorojo wa seriikali
yetu ambayo kwa kushangaza sana inakuwa na nguvu ya kupambana na
waandamanaji toka vyama vya upinzani au wafuasi wa dini fulani
wanapotaka kuandamana au kuwasekwa ndani na kuwashtaki waandishi wa
habari kwa kutumia sheria za kidhalimu na kikoloni na zilizopitwa na wakati
kwa sababu tu waandishi hao wa habari wameandika kisichowafurahisha
wanasiasa walioko madarakani unachangia si haba nchi hii kuwa na
matatizo ya kila namna, kutokuendelea na kupiga maktaimu wakati watawala
wakidanganywa na takwimu na taarfifa za wapambe wao kwamba mambo ni
saaafii.
Mradi wa kuondokana na makazi ya mabondeni
Mathalani, kama serikali yetu ingelikuwa haifanyi kazi kisanii, basi mara tu
baada ya kutangaza marufuku ya kujenga na kuishi mabondeni
nilichotegemea kuona ni serikali hiyo kujenga nyumba za angalau chumba
kimoja na ukumbi kwa familia husika katika maeneo mengine na kisha
kupitia benki na taasisi nyingine za fedha, misaada na ukopeshaji kurejesha
gharama zake kwa kuwalipisha wananchi masikini kwa kiwango
wanachoweza kulipa hadi deni lao liishe. Je, tunakumbuka mikopo ya miaka
25 hadi 50 ya Benki ya Dunia kwa watanzania miaka ya huko nyumba.
Serikali yetu kwa kutumia utajiri, madini, mali asili zetu na kodi zetu hivi
inashindwa kufanya jambo kama hili au haina nafasi na watu wake ambao ni
maskini? Utaratibu huu utaendana hata na matarajio ya katiba ya kiutawala iliyopo na
utaanza kujenga kutoa fursa sawa kiustawi ili kuleta uwiano na usawa wa
kimaendeleo miongoni mwa Watanzania.
Hitaji la nyumba na makazi kama hitaji la msingi likishatoshelezwa, kinachobakia ni kwa wananchi kujiingiza katika ushindani mbalimbali wa kujiendeleza kielimu, kikazi, kibiashara, kihuduma, kisanaa, kimichezo na kadhalika na kuwa bora zaidi nchini na
duniani.
Kwa maneno mengine, safari ya kweli na dhati kuelekea kwenye
maendeleo ya Watanzania inakuwa ndio imeanza na sio vinginevyo.
Nyumba zilizo kwenye maeneo safi, bora na salama zitachangia sio haba
kuwapa mamilioni ya Watanzania utulivu wa akili na kiroho. Ni kitu
kitakachorahisisha miingiliano ya kijamii na kupatikana kwa huduma za
utumaji na upokeaji barua kupitia makasha nyumbani na sio ofisi za posta
mbali na waishipo watu. Hali kadhalika, kuishi kwenye makazi salama, mandhari nzuri
na yanayopendeza vitawapa Watanzania moyo wa amani, utu, huruma na mapenzi zaidi.
Na kubwa zaidi litawapa Watanzania nafasi kubwa zaidi ya kujiheshimu na
kujithamini na sio kujiona wao sio lolote sio chochote.
Nyumba bora na salama zitawapa watoto wa kimaskini nafasi ya kusoma
katika mazingira bora zaidi na kufanya vizuri zaidi katika shule na vyuo.
Nyumba bora na salama na zenye nafasi zitawapa watoto wa makini fursa
ya kuwa watundu, wenye kujaribu na wazua ujasiriamali wa kila aina siku
zote daima.
Nyumba bora, salama katika miji ambayo utawala wa kisheria sio tu
unasemekana kuwepo bali kufuatwa kwa herufi na silabi na zenye
kuhudumiwa ipasavyo na huduma zote muhimu za kijaami unaweza
kuifanya Tanzania fumba na kufumbua kuwa chaguo la watalii duniani na
mapato ya utalii peke yake yakatuwezesha kujivua nguo za mitumba ya
umaskini na kuvaa nguo mpya za raia wanaoheshimiwa, kujiheshimu na
kutoa mchango wao muhimu katika maendeleo ya dunia yao na wakati wao.
Kubwa zaidi ni lile la kwamba kuanzia hapo hayo hapo juu
yatakapozingatiwa watu wetu sio tu itakuwa ni rahisi kupata huduma zote
muhimu binadamu anazohitaji, bali kubwa zaidi maisha na mali zao
zitakuwa salama wakati wote.
suala 'lililosiasaishwa' na haiwezekani chama kilichoko madarakani na
serikali kuwahamisha wakazi wa maeneo haya kwa nguvu kama nguvu
inavyotumika sehemu zingine kutokana na kuhitajika kwa mtaji wa kisiasa.
Haiwezekani pia kidira, kisera, kifedha, kiteknolojia na kiuwezo kwa Dar es
salaam ambayo ni pua na mdomo na bahari kuwa na miundo mbinu
itakaloliwezesha jiji litapike maji yote ya mvua yaende baharini kama tu
imeshidwa kutapisha maji taka na ya matumizi ya kawaida kwenda baharini.
Ugumu wa hili umedhirishwa na kauli zinazopingana juu ya kuhama au
kutokuhama mabondeni zinazotolewa na viongozi wa serikali na chama
tawala. Haiwezekani katika muda mfupi na siamini kama suala hilo limo
katika kipaumbele cha serikali. Je, kiuhalisia kinachobakia kushauri ni kitu
gani ? Nitajaribu ingawa ninajua ni mtihani mkubwa kufanya hivyo katika
makala yangu leo. Ila kama kawaida tutarajie amri zisizotekelezeka na ahadi zisizotimizwa.
Kipindi cha pili cha awamu ya nne kilianza kwa bishara njemba katika
angalau za masula ya nyumba na makazi, lakini kadri muda unavyokwenda
imedhihirika kuwa hizo zilikuwa ni nguvu za soda tu.
Biashara hizo zilitokana kwanza na kuteuliwa kwa mwanamke aliyeswahi
kushika wadhifa wa juu katika shilrika la masula ya nyumba na makazi na
kauli zake za mwanzo ambazo zilionekana kama angelikuwa na uhuru wa
kufanya yale anayofikiria kichwani kwake leo angalau tungelianza angalau
kuona ishara za kuwa na mipngo miji katika nchi ambayo kwa mapana na
marefu na kwa ujumla yake ilikwishazika kabisa suala la mipango miji na
ujenzi uaoangalia na kutahadhari na yanayoweza kutokea kesho na kesho
kutwa.
Jambo moja linalochangia udhaifu katika utawala na menejimenti yetu ya
nyumba na makazi ni sheria za kubembelezana na kuvumiliana. Na siku hizi
umezuka mtindo kuwa pakijengwa kijiwe cha chama tawala mahala fulani,
basi mahala hapo panahesabika kuwa sehemu ambayo hata kama sheria
zimevunjwa, hazikuvunjwa!
Hizi ni siasa za kutafuta kupendwa na umaarufu, huku mtu akijua fika kwa
kuruhusu kinachofanyika kiendelee kufanyika basi mwisho wake ni zahama,
dhiki na vifo kwa wale wanouhurumiwa na kvumililiwa. Ninaamini wakati
umefika kwa nchi yetu kujenga heshima ya kuwa na utawala wa kisheria
ambao haushawishiwi vinginevyo na wanasiasa kwa malengo yao binafsi.
Pamoja na ujenzi wa nyumba mabondeni ipo mifano mingi ya kimaafa
maafa tu inayosubiri cheche moja tu, moto au bomu kulipuka.
Mifano hiyo ni pamoja na vituo vya zima moto na upatikanaji maji kuwa mbali
na maeneo ambayo janga la moto linaweza likazuka.
Manispaa mbalimbali za maji zimeruhusu au kuachia watu kujenga kuta au
vizuizi vya aina mbalimbali ambavyo vinaweza vikachangia si haba ukubwa
wa maafa na hasa yale ya maji na mafuriko.
Tembelea sehemu mbalimbali za jiji la Dar es salaam na utakuta makumi
kama sio mamia ya vituo vya petroli ambavyo vimejenga kando ya masoko
au ndani ya makazi ya watu.
Watalii mbalimbali hivi sasa wanahofia kuja Tanzania kutokana na
kukosekana usalama wa kutosha mabarabarani . Jambo linalosababishwa
na malori, daladala, bajaji, pikipiki, mikokoteni na vyombo vingine vya
uchukuzi kutofuata sheria zilizopo na kukosa uungwana na ustaarabu katika
maingiliano ya watu njiani.
Aidha, kumekuwa na kauli kadhaa za kisheria zisizotekelezwa juu ya hili au
lile, mojawapo likiwa ni amri inayokataza watu kuishi mabondeni toka zama
za Mzee Makamba alipokuwa mkuu wa mkoa wa jijimkoa.
Nchi haiwezi kamwe kujengwa kwa siasa za kujipendekeza, kutaka
kuonekana wema na wazuri na wengine wabaya na unafiki mwingine kama
huo. Ni lazima tufike mahala ambapo sheria zetu zinalinda na kutunza roho
za watu, kisha utamaduni, imani na mali za watu . Mengine ni uzandiki wa
kisiasa ulio na melngo binafsi dhidi ya yale yanayostahili kuwa ya umma.
Ninaamini, wakati tunatoa michango yetu kuhusu katiba yetu mpya itulinde
vipi tokana na wale tunaowapa ukubwa tutahakikisha kuwa ulinzi na
usalama wa roho za watu, utamaduni na mali zao unapewa uzito
unaostahili.
Kama azma yetu basi itakuwa ni hivyo ni dhahiri kubainisha hapa kwamba
huwezi ukalinda na kuthamini maisha ya wananchi wako kama wewe kama
serikali na mkusanyaji mkuu wa kodi na mirabaha unashindwa kuwapatia
wananchi unaowaongoza mahitaji yao ya msingi. Mahitaji hayo ya msingi ni
pmoja na nyumba na makazi bora na salama.
Nyumba kama hitaji la msingi
Kichekesho kwa wazungu na wageni wengi wanaotembelea nchi hii ni pale
wanapokuta kuwa kila Mtanzania ana mradi wa kujenga nyumba. Pengine
hawaelewi umasikini na kudunduliza kwetu na jinsi tunavyozaliana kwa
wingi, lakini bado ukweli unabakia pale pale wengi wanatushangaa
wanapoona badala ya kujenga vitu vya kututajirisha tunajenga vitu vya
kutumasikinisha.
Ukiweka siasa pembeni, nyumba ni hitaji la msingi la kila mwanadamu.
Inasemekana baada ya chakula na maji basi nyumba ni muhimu kuliko kitu
kingine. Kutokana na ukweli huu, serikali iliyokuwa makini haiwezi
kulichukulia suala hili kimzahaha mzaha au kuliona ni mzigo na kulisukuma
ili libebwe na watu wengine. Bila watu kuwa na nyumba bora na salama hata
kama watajishughulisha na mengi mazuri katika uzalishaji na ujenzi wa
nchi, fumba na kufumbua, siku moja vyote vinaweza kuoshwa au kufagiliwa
mbali na maafa ya aina hii au ile.
Serikali inayoona mbali na mbele, kwa hiyo, huwa inachukulia suala la
mipango na mikakati ya nyumba na makazi kama jiwe la msingi la
maendeleo la taifa na watu husika. Inafanya hivyo, kwa kuzingatia kuwa vita
vyote vingine vinavyokabili watu wake vikiwemo vile vya ujinga, njaa, maradhi
na umaskini ni vita vitakavyokuwa rahisi sana kuibuka kidedea kama
washindi wasioshindika.
Katika muktadha huu, hoja yangu hapa ni kwamba tusianze kumwaga
machozi ya mamba huku tukijua fika kwamba siasa zetu za kujipendekeza
zimechangia si haba kuwapotezea Watanzania wenzetu ambao kama sheria
zingelikuwa zinawalinda na rasilimali za nchi zinatumika kuwanufaisha wao
na sio vinginevyo hivi leo wasingelikuwa marehemu.
Ninasema hivyo, kwa kudhihirisha kuwa ulegevu na urojorojo wa seriikali
yetu ambayo kwa kushangaza sana inakuwa na nguvu ya kupambana na
waandamanaji toka vyama vya upinzani au wafuasi wa dini fulani
wanapotaka kuandamana au kuwasekwa ndani na kuwashtaki waandishi wa
habari kwa kutumia sheria za kidhalimu na kikoloni na zilizopitwa na wakati
kwa sababu tu waandishi hao wa habari wameandika kisichowafurahisha
wanasiasa walioko madarakani unachangia si haba nchi hii kuwa na
matatizo ya kila namna, kutokuendelea na kupiga maktaimu wakati watawala
wakidanganywa na takwimu na taarfifa za wapambe wao kwamba mambo ni
saaafii.
Mradi wa kuondokana na makazi ya mabondeni
Mathalani, kama serikali yetu ingelikuwa haifanyi kazi kisanii, basi mara tu
baada ya kutangaza marufuku ya kujenga na kuishi mabondeni
nilichotegemea kuona ni serikali hiyo kujenga nyumba za angalau chumba
kimoja na ukumbi kwa familia husika katika maeneo mengine na kisha
kupitia benki na taasisi nyingine za fedha, misaada na ukopeshaji kurejesha
gharama zake kwa kuwalipisha wananchi masikini kwa kiwango
wanachoweza kulipa hadi deni lao liishe. Je, tunakumbuka mikopo ya miaka
25 hadi 50 ya Benki ya Dunia kwa watanzania miaka ya huko nyumba.
Serikali yetu kwa kutumia utajiri, madini, mali asili zetu na kodi zetu hivi
inashindwa kufanya jambo kama hili au haina nafasi na watu wake ambao ni
maskini? Utaratibu huu utaendana hata na matarajio ya katiba ya kiutawala iliyopo na
utaanza kujenga kutoa fursa sawa kiustawi ili kuleta uwiano na usawa wa
kimaendeleo miongoni mwa Watanzania.
Hitaji la nyumba na makazi kama hitaji la msingi likishatoshelezwa, kinachobakia ni kwa wananchi kujiingiza katika ushindani mbalimbali wa kujiendeleza kielimu, kikazi, kibiashara, kihuduma, kisanaa, kimichezo na kadhalika na kuwa bora zaidi nchini na
duniani.
Kwa maneno mengine, safari ya kweli na dhati kuelekea kwenye
maendeleo ya Watanzania inakuwa ndio imeanza na sio vinginevyo.
Nyumba zilizo kwenye maeneo safi, bora na salama zitachangia sio haba
kuwapa mamilioni ya Watanzania utulivu wa akili na kiroho. Ni kitu
kitakachorahisisha miingiliano ya kijamii na kupatikana kwa huduma za
utumaji na upokeaji barua kupitia makasha nyumbani na sio ofisi za posta
mbali na waishipo watu. Hali kadhalika, kuishi kwenye makazi salama, mandhari nzuri
na yanayopendeza vitawapa Watanzania moyo wa amani, utu, huruma na mapenzi zaidi.
Na kubwa zaidi litawapa Watanzania nafasi kubwa zaidi ya kujiheshimu na
kujithamini na sio kujiona wao sio lolote sio chochote.
Nyumba bora na salama zitawapa watoto wa kimaskini nafasi ya kusoma
katika mazingira bora zaidi na kufanya vizuri zaidi katika shule na vyuo.
Nyumba bora na salama na zenye nafasi zitawapa watoto wa makini fursa
ya kuwa watundu, wenye kujaribu na wazua ujasiriamali wa kila aina siku
zote daima.
Nyumba bora, salama katika miji ambayo utawala wa kisheria sio tu
unasemekana kuwepo bali kufuatwa kwa herufi na silabi na zenye
kuhudumiwa ipasavyo na huduma zote muhimu za kijaami unaweza
kuifanya Tanzania fumba na kufumbua kuwa chaguo la watalii duniani na
mapato ya utalii peke yake yakatuwezesha kujivua nguo za mitumba ya
umaskini na kuvaa nguo mpya za raia wanaoheshimiwa, kujiheshimu na
kutoa mchango wao muhimu katika maendeleo ya dunia yao na wakati wao.
Kubwa zaidi ni lile la kwamba kuanzia hapo hayo hapo juu
yatakapozingatiwa watu wetu sio tu itakuwa ni rahisi kupata huduma zote
muhimu binadamu anazohitaji, bali kubwa zaidi maisha na mali zao
zitakuwa salama wakati wote.
Friday, December 16, 2011
CUF na hatima ya upinzani Tanzania...
WATANZANIA mnamo mwaka 1990 waliupokea mfumo wa vyama vingi kwa matumaini makubwa ya mageuzi na mabadiliko chanya katika mfumo wao wa kisiasa, kijamii na kiuchumi. Awali CUF kilihofiwa kuwa chama chenye udini, akheri, ni dhahiri inaweza kuwa au isiwe hivyo, ila kilicho wazi ni kuwa CUF baada ya muafaka ni chama cha Kizanzibari zaidi na sio cha Kitanzania, achilia mbali kuwa cha Kitanganyika.
Watu wengi waliamini mfumo wa vyama vingi utaleta ushindani wa kweli katika siasa, uchumi, teknolojia, utamaduni na rasilimali ziendazo kwa wanajamii ili kila mtu na kila jamii ipate kilicho bora kabisa na sio kitu hafifu, dhaifu na vilivyochakachuliwa.
Hata hivyo, ushindani katika sekta nyingine ulitegemea sana kuwepo na mafanikio ya ushindani wa dhati na wa kweli katika siasa. Ushindani huo katika siasa hadi hivi wa leo haujafika, haujaonekana na kwa siasa zilizopo ndani na nje ya chama tawala haionekani kama utapatikana kwenye awamu hii.
La kusikitisha ni kuwa siasa za mfumo wa vyama vingi Tanzania zimeiga neno kwa neno siasa za Kimarekani zinazotawaliwa na wenye fedha, na wasio na fedha kuwa wasindikizaji kama sio wanunuliwaji. Na kinachopandwa hakiashirii mema kwa nchi hii na watu wake hapo baadaye.
Kubwa tunalojifunza hapa ni kwamba kutokana na kukwamishwa kuwepo kwa ushindani wa kweli wa kisiasa ndani na nje ya bunge, viongozi wetu wanawapotezea wananchi muda na nafasi nyingi na nyinginezo za kuondokana na umaskini wao kwa kutumia fursa na changamoto ambazo aghalabu huzaliwa tu katika mfumo wenye ushindani wa kweli kisiasa. Hili linapaswa lionekane na lieleweke na wote, waliomo kwenye upinzani na wanaoongoza chama tawala hivi sasa ili maamuzi yanayofaa yafanywe kwa faida ya nchi na watu wake.
Ilitegemewa kuwa vyama vya upinzani vingekuwa vingi, lakini kuna viwili au vitatu vitakavyoungana na kukipa changamoto ya kutosha chama tawala. Kiasi ambacho chama tawala kisingeweza kufanya maamuzi yoyote ya maana kiurahisi bila ushirikiano na vyama vingine na kuwaelimisha na kuwaridhisha wabunge au wawakilishi wake kwenye mazungumzo mbalimbali.
Kinachoonekana leo, hata hivyo, ni kuongezeka vyama vya siasa visivyo na kichwa wala miguu, huku vile vilivyokuwepo vikizidi kudhoofika kwa njia moja au nyingine.
Zipo sababu mbalimbali zinazotolewa kuhusu udhaifu wa upinzani. Baadhi ya viongozi wa vyama tawala wanaamini kwamba vyama hivyo vimeanzishwa kwa shinikizo la IMF na Benki ya dunia, na hili pengine linaathiri mahusiano ya chama tawala na vyama hivyo kwa chama tawala kuona ndicho pekee chenye ridhaa na uhalali kwa wananchi lakini sio vya upinzani.
Aidha, vyama vingi vya upinzani pamoja na sheria ya kuvilazimisha kuwa na wanachama angalau 200 katika angalau mikoa 10 ni vyama vilivyokosa mizizi ya kweli mijini na vijijini na vinaishi kwa kubangaizabangaiza tu. Wakati hili linatokea chama tawala kwa kushika funguo za hazina na kuwa katika nafasi ya kufanya maamuzi kadhaa kwa manufaa yake, hakina dhiki kama hiyo, ila pale kinapoingizwa mkenge kama ilivyotokea kwenye suala la rada.
Kutokana na chama tawala na viongozi wake kuwa na uwezo wa kifedha (ambao hatuna uhakika na chimbuko lake, maana hakionekani kuwa na miradi ya maana ya kukiingizia kipato na wanachama wake wengi sio walipa ada wala watoa michango mikubwa) kimetumia njaa na umaskini wa vyama vya upinzani kwa manufaa yake kwa njia mbalimbali, ambazo hatuna sababu ya kuingilia kwa undani zaidi hapa. Pamoja na hayo kutokana na siasa kuitwa mchezo mchafu tumeshuhudia mambo ambayo yanatia mashaka kuhusu ukweli na uhalali wake katika maeneo mbalimbali ya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kimaendeleo kwa ujumla.
Kisiasa kwa mfano tumeona baadhi ya vyama vikisingizia vingine udini, wakati ndivyo vinavyolea udini kwa mlango wa nyuma; tumeona uoza na ufisadi ukiswafishwa na kuitwa utakatifu; tumeona wabunge wakizomewa na kukashifiwa kwa kuwa na msimamo fulani; tumeona wabunge wakitumiwa kwa manufaa ya chama na serikali na siyo ya wananchi; tumeona watu wakisingiziwa uongo na wengine kujiita na kutaka kuonekana watakatifu na kadhalika; na juu ya yote tumewaona wanafiki na wasioitakia nchi yetu mema wakijifanya wao ndio wenye uchungu mkubwa kabisa na nchi yetu kuliko watu wengine.
CUF na Zanzibar....
Baada ya kukerwa na ugomvi wa ndugu wa Unguja na Pemba, sisi sote tulivuta pumzi na kushukuru Mungu na tukafata wahenga waliyosema: ' Ndugu wakigombana, chukua kisegerema chako uende kulima; na ndugu wanapopatana, chukua kapu lake ukavune!'
Hebu turudi nyuma kidogo, hata hivyo, je, CUF kiliundwa makusudi na mahsusi kwa ajili ya muafaka wa Zanzibar? Au nini kilichotokea?
Pamoja na ukweli kwamba cham hicho kilistahili kuwa na wanachama 200 katika kila mkoa angalau kwa mikoa 10 Tanzania bara na visiwani ni vipi chama hicho kikamezwa kabisa na Wazanzibari? Kiasi kwamba kama chama hicho hakikuhusiswa na Uzanzibari na Upemba kilikuwa kikihusishwa na Uislamu kwa heri au shari ?
Je, katika hali ambayo tunayo leo, yaani, kuwepo sio tu muafaka bali pia serikali ya Umoja wa Kizanzibari, ukweli hauonekani kwamba chama cha CUF hakikuwa chama cha Tanzania bali cha Kizanzibari?
Iweje baada ya viongozi wa Kizanzibari kupewa ubunge na vyeo mbalimbali katika serikali yao ya Umoja wa kitaifa harakati zao za kisiasa kama upinzani unaotarajiwa kuwa imara katika kuikabili CCM bara kudhoofu na kuwa hoi bin taabani?
Katika matukio ya kitaifa na hususan Bungeni, tumeona watunga sheria wa CUF kwa heri au shari wakiunga mkono au kupinga moja kwa moja lolote lile ambalo Chama tawala liliunga mkono au kupinga ?
Na hivi Hazina, Tume ya Uchaguzi na Msajili wa vyama vya siasa wanastahili kulipa CUF na CCM kama chama kimoja au vyama viwili kwa hali kama hii?
Wamasheria wanasemaje kuhusu CUF hapa Tanzania kama ni chama cha Upinzani au chama tawala au chama kilicho katikati ya hayo ?
Na Watanzania waliohadaiwa na wapanda mabasi ya muafaka wakidhani wanapelekwa kwenye upinzani imara na wa kweli wana kila haki ya kushuka na kupanda basi jengine.
Vijana wa chama ambacho kimefikia kuwauza bila wao wenyewe kujua wanauzwa ili viongozi wachache wa chama hicho wapate ukubwa na sio maendeleo ya watu na nchi yao sio laiki yao kukaa kimya labda wakose kiongozi wa kuwafungua macho na kuwaongoza kwenda kule wanakosatahili kuelekea na sio vinginevyo.
Maana ya kuwa na upinzani nchini haiwezi kubadilika. Upinzani unahitajika kama njia muhimu ya kisiasa kwa wanasiasa wa mrengo fulani kupimwa kiuwezo, kufuatiliwa, kudhibitiwa na kutathminiwa kimatendo na kimatokeo kama na wanasiasa wenzao na wananchi kwa ujumla kama wanaweza au hawawezi kazi waliyoiomba.
Huu ni mfumo ambao ukiutumia vibaya unaweza ukairuhusu nchi kutawaliwa na kuendeshwa na chuya na pumba wakati nafaka zimetupwa jalalani. Au kwa upande mwingine mfumo wa vyama vingi ni mfumo unaoweza pia kuchangia sio haba nchi kuwa na viongozi safi, wenye uwezo, wenye nia ya kujenga nchi na watu wao na wenye mitazamo na dira za kimaendeleo zinazohitajika kufikisha nchi na watu wake kule wanakotaka kwenda.
Upinzani hauwezi kustawi kama katika nchi husika bado watu wana wasiwasi kwamba upinzani ni uasi, vita na uhaini. Ni lazima watu na hasa vijijini waliko wananchi wengi wakubali kwamba mfumo wa vyama vingi ni kitu kizuri na anayeutega au kudhoofisha ni adui wa nchi na watu wake. Na kwamba upinzani si ubaya, si uasi na sio vita wala uhaini. Na kwamba vita na uhaini hutokea pale demokrasia inapohujumiwa na wale walioko madarakani kukataa kushindwa na kuwanyima washindi haki yao kwa njia halali au haramu.
Juu ya yote upinzani hauwezi kujengwa na wazee ambao daima wanalilia kupewa nishani ili watambuliwe kwa kile kisichotambulika wala kueleweka. Upinzani wa kweli utajengwa na vijana waliofunguka macho na wanaotambua kwamba nchi hii haiwezi kujengwa kwa kuigeuza shamba la bibi kama sio la nyanya, ila kwa mikoa na wilaya za nchi hii kujiendesha kama makampuni huru yenye visheni na misheni ya kile kinachostahili kuzalishwa, kuundwa au kuhudumiwa kwa ufanifu na ufanisi wa hali ya juu kwa kasi ambayo itatuwezesha kuuaga ulimwengu wa tatu kwa haraka zaidi kuliko tunavyotarajia.
Watu wengi waliamini mfumo wa vyama vingi utaleta ushindani wa kweli katika siasa, uchumi, teknolojia, utamaduni na rasilimali ziendazo kwa wanajamii ili kila mtu na kila jamii ipate kilicho bora kabisa na sio kitu hafifu, dhaifu na vilivyochakachuliwa.
Hata hivyo, ushindani katika sekta nyingine ulitegemea sana kuwepo na mafanikio ya ushindani wa dhati na wa kweli katika siasa. Ushindani huo katika siasa hadi hivi wa leo haujafika, haujaonekana na kwa siasa zilizopo ndani na nje ya chama tawala haionekani kama utapatikana kwenye awamu hii.
La kusikitisha ni kuwa siasa za mfumo wa vyama vingi Tanzania zimeiga neno kwa neno siasa za Kimarekani zinazotawaliwa na wenye fedha, na wasio na fedha kuwa wasindikizaji kama sio wanunuliwaji. Na kinachopandwa hakiashirii mema kwa nchi hii na watu wake hapo baadaye.
Kubwa tunalojifunza hapa ni kwamba kutokana na kukwamishwa kuwepo kwa ushindani wa kweli wa kisiasa ndani na nje ya bunge, viongozi wetu wanawapotezea wananchi muda na nafasi nyingi na nyinginezo za kuondokana na umaskini wao kwa kutumia fursa na changamoto ambazo aghalabu huzaliwa tu katika mfumo wenye ushindani wa kweli kisiasa. Hili linapaswa lionekane na lieleweke na wote, waliomo kwenye upinzani na wanaoongoza chama tawala hivi sasa ili maamuzi yanayofaa yafanywe kwa faida ya nchi na watu wake.
Ilitegemewa kuwa vyama vya upinzani vingekuwa vingi, lakini kuna viwili au vitatu vitakavyoungana na kukipa changamoto ya kutosha chama tawala. Kiasi ambacho chama tawala kisingeweza kufanya maamuzi yoyote ya maana kiurahisi bila ushirikiano na vyama vingine na kuwaelimisha na kuwaridhisha wabunge au wawakilishi wake kwenye mazungumzo mbalimbali.
Kinachoonekana leo, hata hivyo, ni kuongezeka vyama vya siasa visivyo na kichwa wala miguu, huku vile vilivyokuwepo vikizidi kudhoofika kwa njia moja au nyingine.
Zipo sababu mbalimbali zinazotolewa kuhusu udhaifu wa upinzani. Baadhi ya viongozi wa vyama tawala wanaamini kwamba vyama hivyo vimeanzishwa kwa shinikizo la IMF na Benki ya dunia, na hili pengine linaathiri mahusiano ya chama tawala na vyama hivyo kwa chama tawala kuona ndicho pekee chenye ridhaa na uhalali kwa wananchi lakini sio vya upinzani.
Aidha, vyama vingi vya upinzani pamoja na sheria ya kuvilazimisha kuwa na wanachama angalau 200 katika angalau mikoa 10 ni vyama vilivyokosa mizizi ya kweli mijini na vijijini na vinaishi kwa kubangaizabangaiza tu. Wakati hili linatokea chama tawala kwa kushika funguo za hazina na kuwa katika nafasi ya kufanya maamuzi kadhaa kwa manufaa yake, hakina dhiki kama hiyo, ila pale kinapoingizwa mkenge kama ilivyotokea kwenye suala la rada.
Kutokana na chama tawala na viongozi wake kuwa na uwezo wa kifedha (ambao hatuna uhakika na chimbuko lake, maana hakionekani kuwa na miradi ya maana ya kukiingizia kipato na wanachama wake wengi sio walipa ada wala watoa michango mikubwa) kimetumia njaa na umaskini wa vyama vya upinzani kwa manufaa yake kwa njia mbalimbali, ambazo hatuna sababu ya kuingilia kwa undani zaidi hapa. Pamoja na hayo kutokana na siasa kuitwa mchezo mchafu tumeshuhudia mambo ambayo yanatia mashaka kuhusu ukweli na uhalali wake katika maeneo mbalimbali ya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kimaendeleo kwa ujumla.
Kisiasa kwa mfano tumeona baadhi ya vyama vikisingizia vingine udini, wakati ndivyo vinavyolea udini kwa mlango wa nyuma; tumeona uoza na ufisadi ukiswafishwa na kuitwa utakatifu; tumeona wabunge wakizomewa na kukashifiwa kwa kuwa na msimamo fulani; tumeona wabunge wakitumiwa kwa manufaa ya chama na serikali na siyo ya wananchi; tumeona watu wakisingiziwa uongo na wengine kujiita na kutaka kuonekana watakatifu na kadhalika; na juu ya yote tumewaona wanafiki na wasioitakia nchi yetu mema wakijifanya wao ndio wenye uchungu mkubwa kabisa na nchi yetu kuliko watu wengine.
CUF na Zanzibar....
Baada ya kukerwa na ugomvi wa ndugu wa Unguja na Pemba, sisi sote tulivuta pumzi na kushukuru Mungu na tukafata wahenga waliyosema: ' Ndugu wakigombana, chukua kisegerema chako uende kulima; na ndugu wanapopatana, chukua kapu lake ukavune!'
Hebu turudi nyuma kidogo, hata hivyo, je, CUF kiliundwa makusudi na mahsusi kwa ajili ya muafaka wa Zanzibar? Au nini kilichotokea?
Pamoja na ukweli kwamba cham hicho kilistahili kuwa na wanachama 200 katika kila mkoa angalau kwa mikoa 10 Tanzania bara na visiwani ni vipi chama hicho kikamezwa kabisa na Wazanzibari? Kiasi kwamba kama chama hicho hakikuhusiswa na Uzanzibari na Upemba kilikuwa kikihusishwa na Uislamu kwa heri au shari ?
Je, katika hali ambayo tunayo leo, yaani, kuwepo sio tu muafaka bali pia serikali ya Umoja wa Kizanzibari, ukweli hauonekani kwamba chama cha CUF hakikuwa chama cha Tanzania bali cha Kizanzibari?
Iweje baada ya viongozi wa Kizanzibari kupewa ubunge na vyeo mbalimbali katika serikali yao ya Umoja wa kitaifa harakati zao za kisiasa kama upinzani unaotarajiwa kuwa imara katika kuikabili CCM bara kudhoofu na kuwa hoi bin taabani?
Katika matukio ya kitaifa na hususan Bungeni, tumeona watunga sheria wa CUF kwa heri au shari wakiunga mkono au kupinga moja kwa moja lolote lile ambalo Chama tawala liliunga mkono au kupinga ?
Na hivi Hazina, Tume ya Uchaguzi na Msajili wa vyama vya siasa wanastahili kulipa CUF na CCM kama chama kimoja au vyama viwili kwa hali kama hii?
Wamasheria wanasemaje kuhusu CUF hapa Tanzania kama ni chama cha Upinzani au chama tawala au chama kilicho katikati ya hayo ?
Na Watanzania waliohadaiwa na wapanda mabasi ya muafaka wakidhani wanapelekwa kwenye upinzani imara na wa kweli wana kila haki ya kushuka na kupanda basi jengine.
Vijana wa chama ambacho kimefikia kuwauza bila wao wenyewe kujua wanauzwa ili viongozi wachache wa chama hicho wapate ukubwa na sio maendeleo ya watu na nchi yao sio laiki yao kukaa kimya labda wakose kiongozi wa kuwafungua macho na kuwaongoza kwenda kule wanakosatahili kuelekea na sio vinginevyo.
Maana ya kuwa na upinzani nchini haiwezi kubadilika. Upinzani unahitajika kama njia muhimu ya kisiasa kwa wanasiasa wa mrengo fulani kupimwa kiuwezo, kufuatiliwa, kudhibitiwa na kutathminiwa kimatendo na kimatokeo kama na wanasiasa wenzao na wananchi kwa ujumla kama wanaweza au hawawezi kazi waliyoiomba.
Huu ni mfumo ambao ukiutumia vibaya unaweza ukairuhusu nchi kutawaliwa na kuendeshwa na chuya na pumba wakati nafaka zimetupwa jalalani. Au kwa upande mwingine mfumo wa vyama vingi ni mfumo unaoweza pia kuchangia sio haba nchi kuwa na viongozi safi, wenye uwezo, wenye nia ya kujenga nchi na watu wao na wenye mitazamo na dira za kimaendeleo zinazohitajika kufikisha nchi na watu wake kule wanakotaka kwenda.
Upinzani hauwezi kustawi kama katika nchi husika bado watu wana wasiwasi kwamba upinzani ni uasi, vita na uhaini. Ni lazima watu na hasa vijijini waliko wananchi wengi wakubali kwamba mfumo wa vyama vingi ni kitu kizuri na anayeutega au kudhoofisha ni adui wa nchi na watu wake. Na kwamba upinzani si ubaya, si uasi na sio vita wala uhaini. Na kwamba vita na uhaini hutokea pale demokrasia inapohujumiwa na wale walioko madarakani kukataa kushindwa na kuwanyima washindi haki yao kwa njia halali au haramu.
Juu ya yote upinzani hauwezi kujengwa na wazee ambao daima wanalilia kupewa nishani ili watambuliwe kwa kile kisichotambulika wala kueleweka. Upinzani wa kweli utajengwa na vijana waliofunguka macho na wanaotambua kwamba nchi hii haiwezi kujengwa kwa kuigeuza shamba la bibi kama sio la nyanya, ila kwa mikoa na wilaya za nchi hii kujiendesha kama makampuni huru yenye visheni na misheni ya kile kinachostahili kuzalishwa, kuundwa au kuhudumiwa kwa ufanifu na ufanisi wa hali ya juu kwa kasi ambayo itatuwezesha kuuaga ulimwengu wa tatu kwa haraka zaidi kuliko tunavyotarajia.
Tusipoangalia demokrasia yetu inaweza kuwa wizi….
SI MTU mwingine ila baba wa ukomunisti, Karl Marx ambaye miaka zaidi ya 120 alitahadharisha kwamba demokrasia kama ilivyokuwa katika nchi za Magharibi ni mfumo wenye udhaifu, mapungufu na kasoro nyingi.
Alionya kwamba demokrasia isipodhibitiwa na wananchi wenyewe ikaachiwa kwa wajanja wachache katika jamii inaweza kugeuka wizi wa mchana kweupe na wa kutisha ambao umehalalishwa na una nguvu za kisheria.
Kiasi ambacho jambo likishaamuliwa huwezi kulipinga kwa kutumia sheria ila kwa njia nyingine.
Alidai wale wanaoitwa wawakilishi wa wananchi wanaweza kuamua kupiga kura ya 'ndiyo' ili kuifagia na kuisafisha hazina au Benki Kuu ya nchi ikawa nyeupe na isibakiwe hata na shilingi moja kwa ajili ya matumizi yao binafsi.
Nina wasiwasi kama huko sio kwa mfumo tulionao leo, wa demokrasia ya chama kimoja iliyojificha ndani ya mfumo wa vyama vingi kama sio tunakokwenda.
Hakuna anayepinga wabunge kupata posho na maslahi zaidi na hata kufanya israfu na kufuru ndogondogo. Kwa mfano, wabunge wenzao wa Kenya wameidhinisha bunge lao kununua viti vipya vya bunge kwa mabilioni ya fedha za Kenya. Kiti kimoja kitakuwa chanunuliwa kwa takriban shilingi milioni tatu. Piga hesabu kwa viti zaidi ya mia tatu bungeni uone mambo hayo. Tofauti na Tanzania viti hivyo havitoki nje vitatoka magereza ya Kenya ambako kuna maseremala wenye hadhi ya kimataifa. Lakini huu ni uwakilishi wa walio nacho kuwawakilisha wasio nacho, ambao wanaamini ili kufanya kazi zao vizuri na kwa starehe lazima anasa na starehe nazo ziingizwe hadi bungeni kwa namna moja au nyingine. Na matajiri kumbukeni hawatopenda wawakilishi wenu waonekane kuteseka au kuwa na maisha ya dhiki au kufanya kazi katika mazingira magumu, kwa hiyo mkiwaruhusu au msipowaruhusu wao watawafadhili bila shida. Ili kuepukana na aibu hii na fedheha ya kufadhiliwa na wenye pesa basi gharama hizo huonekana ni za lazima na zisizoepukika.
Maswali ya kujiuliza
Swali kuu la kujiuliza ni kigezo au vigezo gani vinavyotumika kihistoria na kimapokeo na katika mazingira na hali halisi au muktadha uliopo hivi leo ? Swali hili linazaa maswali yafuatayo:
. Wabunge wetu wana umuhimu na utakatifu gani wa kustahili kulipwa vizuri kuliko madaktari, wahadhiri, wahandisi, walimu, manesi na watu wengine kama hao?
. Hivi kweli hiki tunachokiona katika luninga, yaani, bunge la kusifia na kujisifia na kujipalilia na bunge la NDIIIIYO.... ndicho Watanzania watakachokubali kwacho wabunge kulipwa kihalali na sio kidhulumati ?
. Hivi bunge letu kazi yake ni kutatua matatizo ya wananchi na kuwawezesha wananchi wetu au kazi yake ni kuwapatia fursa wabunge ya kutumbua na kutanua?
. Je, badala ya kuwa na bunge moja tukawa pia na bunge la makundi ya kimaslahi, yaani, bunge la pili muda wa vikao hautafupishwa kiasi wabunge wakashughulikia matatizo yetu badala ya swahifa na swahifa za maneno na porojo?
. Hivi kila mkoa ukiwa na waziri wake mkuu, mawaziri na wawakishi wake nao wakashughulikia moja kwa moja mipango na bajeti zao bunge au mabunge ya kitaifa hayatahitaji tu wiki moja kila baada ya miezi mitatu kuzungumzia mambo makubwa ya kitaifa badala ya utaratibu wa sasa unaotudumaza badala ya kutukuza?
. Hivi na wanaopiga porojo, wanaolala, wanaozomea na kupiga vigelegele nao wanastahili posho hii?
. Mfumo wetu wa bunge hivi unalandana na ule wa kikoloni au kibepari ambao umejengwa katika hoja kuwa watu ni matajiri na sio masikini au vipi?
. Huko Malasyia viongozi wakiwemo wabunge walijipa miaka kadhaa ili kwanza wawatoe wananchi kutoka kwenye umaskini wa kutisha na kisha ndio wabunge wakaanza kulipwa vizuri na kutanua, je, wabunge wetu wanapoanza kwa kutanua kuna uwezekano wowote kweli kwa sisi kukombolewa kiuchumi na kijamii? Wanakubaliana na falsafa ya wabunge wa Malaysia au hawajaona ndani? Ukizingatia hulka au saikolojia ya binadamu, tuna ubavu wa kuifikia Malaysia hata 2100 kwa namna za posho kama hizi za wabunge wetu ?
. Kuna uwiano gani kati ya kile wabunge wanachofanikisha kiuchumi na kijamii kwa wananchi na kile wanacholipwa ?
. Je, uwezo wetu wa kukusanya kodi na kipato chetu cha kila mwaka unaturuhusu kulipa posho hii?
. Je, mabilioni ya fedha yatakayolipwa kwa namna hii hayawezi kuwekezwa kwanza katika mradi utakaozalisha ili posho hiyo itokane na kinachozalishwa na sio kuiingizia hazina shimo jipya la kuchotwa fedha kila mwaka? Hivi wabunge wetu wana akili za uwekezaji au wanazisikia tu na wanataka wawe nazo wananchi lakini si wao wenyewe?
. Je, kwanini mhadhiri, mwalimu, polisi, daktari na nesi nao wasipate posho kama hii? Hasa ukizingatia mazingira magumu wanayofanya kazi na majukumu watumishi hawa waliyonayo kwa wananchi wenzao ?
. Je, uwezo wetu wa kiakili unatufanya tujali faida au manufaa makubwa zaidi kwa idadi iliyo kubwa zaidi au kinyume cha hayo?
. Ni miradi mingapi mbadala ambayo ingesaidia watu wenye kipato cha chini kuondokana na umaskini inakwamishwa kwa hatua hii?
Sababu za baadhi ya wabunge kuridhika na hili
Wabunge nao ni binadamu na mahitaji yao yanaongezeka kutokana na ukubwa walio nao na tamaa zao za kifahari licha ya umaskini wa watu wao; wanataka kulimbikiza ili kushinda uchaguzi ujao; uwakilishi unakuwa fursa ya wao kunyanyuka kiuchumi kama sio kutajirika kirahisi zaidi na mfumo uliopo unatumika kuwanunua bila kujua ili wawasaliti wanaowawakilisha na kutetea walioko mamlakani hata katika yale yanayowahujumu wawakilishwa wao. Aidha katika mfumo ambao wizi wa kura umehalalishwa kinyemela na mbunge hachaguliwi ila kwa kugawa fedha kwanza, wawakilishi hulazimika baadaye kulipa madeni ya watu au kudunduliza tena kile kilichokuwa akiba yao walichokitumia ili wapate kura za wananchi.
Kwanini wabunge wanajisahau
. Wabunge ni binadamu na katika mfumo unaostawi kwa ubinafsi wa kichama na umimi, ubinafsi hauonekani ni kitu kibaya;
. Wabunge walio wengi hawaingii bungeni kutetea maslahi ya wengine ila kulinda na kuendeleza maslahi yao binafsi na jamaa zao;
. Katika mfumo ambao umekwaza na unakinza fani na tasnia nyingine (k.m. mishahara njiwa kwa wahadhiri, walimu, manesi na madaktari ) kimshahara au kiujira, kimasurufu na kimaslahi matokeo yake ni wengi kukimbilia siasa hata kama hawapendi siasa na wanaziona ni uchafu kwa sababu ya fedha au kipato na siyo kwa sababu ya wito;
. Wabunge hawachaguliwi tena kama wawakilishi na watetezi wa wanajamii fulani bali kama watumishi wa chama fulani;
. Mawasiliano kati ya wanaowawakilisha na wabunge huisha mara baada ya mbunge kuchaguliwa;
. Mbunge hafanyi kazi zake ili wananchi wake waneemeke na kutajirika bali kukisaidia chama chake kurudi tena madarakani;
. Nguvu ya serikali na vyombo vya serikali hutumika kukijenga chama tawala na kuvidhoofisha vyama vingine na kutokana na udhaifu wa vyama vingi wabunge kuamini kuwepo kwao kisiasa kunategemea chama tawala kushinda;
. Baadhi ya vyama vingine nyongeza ya posho inapotolewa asilimia kubwa haiendi mfukoni kwa mwakilishi bali kwa chama husika, yaani, nyongeza ya posho ni mlango mzuri wa kustawisha udokozi wa vilivyo vya serikali ili kuwajenga wanasiasa na vyama vyao, na;
. Wawakilishi walio wengi hawaujui umaskini wa wanaowawakilisha. Na wengi huishi katika ukale badala ya kuangalia hali halisi iliyopo hivi leo majimboni mwao.
Majibu ya maswali hayo hapo juu na mengine kama hayo nina hakika ndiyo yatakayoamua hatima ya wabunge na wanasiasa wetu na mustakabali wa nchi yetu bila kujali masuala ya itikadi, msimamo, mtazamo, chama na serikali iliyopo madarakani.
Tanzania tuitakayo
Tanzania tuitakayo haiwezi kupatikana kwa kuwa na wabunge walioshiba na wasiyemjua mwenye njaa, na wakuu wa mikoa wanaokokota badala ya kuongoza mikoa; kwani wao bado waamini wana njaa pia; kwa kutanguliza mbele ubinafsi badala ya jamii; na bwabwaja wa kuzungumza lakini wachache wa vitendo; na vyama na wanasiasa ambao wanajilinganisha na matajiri na kuishi kama wao kama sio kuwapita; na wanaotetea maslahi ya chama au serikali badala ya wananchi wao; na wenye fedha wanaoingia bungeni ili kutajirika zaidi na sio kuwanyanyua wanaowawaklisha; na watu wanaokubali kutumiwa na wengine kwa manufaa ya wengine na sio ya watu wao; na watu wasiojua nchi ilipo na inapotakiwa kwenda.
Ninaelewa maswali hayo hapo juu sio rahisi kuyajibu achilia mbali kuyajibu kwa haraka sana. Ila yanadhihirisha kitu kimoja, muswaada wa katiba si 'blue' wala 'green' wala 'white' paper ya serikali unahitaji muda na wasaa kuusoma na kuutafakari. Na kwamba kama wanaharakati, kazi yetu moja kubwa ni kuitumia katiba ama kuondoa vipengele vyote vinavyowapendelea kiujira na kimaslahi wale wasiozalisha na kuwakamua wanaozalisha kwa upande mmoja na kuviingiza vipengele vipya vyote vinavyohitajika ili kuondokana na dhuluma hii ya kiujira na kimapato ilioyoanzishwa na wakoloni, kulelewa na watawala wetu wa jana na sasa na likachukuliwa kama msahafu au biblia na lisilogusika au kurekebishwa na watawala wetu wa leo. Muktadha huu si msahafu, si biblia na mapinduzi hayaepukiki ili tuwe na Tanzania yenye usawa, haki, utu na ubinadamu zaidi. Tanzania mtu anayelipwa kwa kigezo cha kile alichokisomea na kuhitimu na sio kwa kubebwa kisiasa bila hoja na sababu za msingi. Mungu tusaidie!
Alionya kwamba demokrasia isipodhibitiwa na wananchi wenyewe ikaachiwa kwa wajanja wachache katika jamii inaweza kugeuka wizi wa mchana kweupe na wa kutisha ambao umehalalishwa na una nguvu za kisheria.
Kiasi ambacho jambo likishaamuliwa huwezi kulipinga kwa kutumia sheria ila kwa njia nyingine.
Alidai wale wanaoitwa wawakilishi wa wananchi wanaweza kuamua kupiga kura ya 'ndiyo' ili kuifagia na kuisafisha hazina au Benki Kuu ya nchi ikawa nyeupe na isibakiwe hata na shilingi moja kwa ajili ya matumizi yao binafsi.
Nina wasiwasi kama huko sio kwa mfumo tulionao leo, wa demokrasia ya chama kimoja iliyojificha ndani ya mfumo wa vyama vingi kama sio tunakokwenda.
Hakuna anayepinga wabunge kupata posho na maslahi zaidi na hata kufanya israfu na kufuru ndogondogo. Kwa mfano, wabunge wenzao wa Kenya wameidhinisha bunge lao kununua viti vipya vya bunge kwa mabilioni ya fedha za Kenya. Kiti kimoja kitakuwa chanunuliwa kwa takriban shilingi milioni tatu. Piga hesabu kwa viti zaidi ya mia tatu bungeni uone mambo hayo. Tofauti na Tanzania viti hivyo havitoki nje vitatoka magereza ya Kenya ambako kuna maseremala wenye hadhi ya kimataifa. Lakini huu ni uwakilishi wa walio nacho kuwawakilisha wasio nacho, ambao wanaamini ili kufanya kazi zao vizuri na kwa starehe lazima anasa na starehe nazo ziingizwe hadi bungeni kwa namna moja au nyingine. Na matajiri kumbukeni hawatopenda wawakilishi wenu waonekane kuteseka au kuwa na maisha ya dhiki au kufanya kazi katika mazingira magumu, kwa hiyo mkiwaruhusu au msipowaruhusu wao watawafadhili bila shida. Ili kuepukana na aibu hii na fedheha ya kufadhiliwa na wenye pesa basi gharama hizo huonekana ni za lazima na zisizoepukika.
Maswali ya kujiuliza
Swali kuu la kujiuliza ni kigezo au vigezo gani vinavyotumika kihistoria na kimapokeo na katika mazingira na hali halisi au muktadha uliopo hivi leo ? Swali hili linazaa maswali yafuatayo:
. Wabunge wetu wana umuhimu na utakatifu gani wa kustahili kulipwa vizuri kuliko madaktari, wahadhiri, wahandisi, walimu, manesi na watu wengine kama hao?
. Hivi kweli hiki tunachokiona katika luninga, yaani, bunge la kusifia na kujisifia na kujipalilia na bunge la NDIIIIYO.... ndicho Watanzania watakachokubali kwacho wabunge kulipwa kihalali na sio kidhulumati ?
. Hivi bunge letu kazi yake ni kutatua matatizo ya wananchi na kuwawezesha wananchi wetu au kazi yake ni kuwapatia fursa wabunge ya kutumbua na kutanua?
. Je, badala ya kuwa na bunge moja tukawa pia na bunge la makundi ya kimaslahi, yaani, bunge la pili muda wa vikao hautafupishwa kiasi wabunge wakashughulikia matatizo yetu badala ya swahifa na swahifa za maneno na porojo?
. Hivi kila mkoa ukiwa na waziri wake mkuu, mawaziri na wawakishi wake nao wakashughulikia moja kwa moja mipango na bajeti zao bunge au mabunge ya kitaifa hayatahitaji tu wiki moja kila baada ya miezi mitatu kuzungumzia mambo makubwa ya kitaifa badala ya utaratibu wa sasa unaotudumaza badala ya kutukuza?
. Hivi na wanaopiga porojo, wanaolala, wanaozomea na kupiga vigelegele nao wanastahili posho hii?
. Mfumo wetu wa bunge hivi unalandana na ule wa kikoloni au kibepari ambao umejengwa katika hoja kuwa watu ni matajiri na sio masikini au vipi?
. Huko Malasyia viongozi wakiwemo wabunge walijipa miaka kadhaa ili kwanza wawatoe wananchi kutoka kwenye umaskini wa kutisha na kisha ndio wabunge wakaanza kulipwa vizuri na kutanua, je, wabunge wetu wanapoanza kwa kutanua kuna uwezekano wowote kweli kwa sisi kukombolewa kiuchumi na kijamii? Wanakubaliana na falsafa ya wabunge wa Malaysia au hawajaona ndani? Ukizingatia hulka au saikolojia ya binadamu, tuna ubavu wa kuifikia Malaysia hata 2100 kwa namna za posho kama hizi za wabunge wetu ?
. Kuna uwiano gani kati ya kile wabunge wanachofanikisha kiuchumi na kijamii kwa wananchi na kile wanacholipwa ?
. Je, uwezo wetu wa kukusanya kodi na kipato chetu cha kila mwaka unaturuhusu kulipa posho hii?
. Je, mabilioni ya fedha yatakayolipwa kwa namna hii hayawezi kuwekezwa kwanza katika mradi utakaozalisha ili posho hiyo itokane na kinachozalishwa na sio kuiingizia hazina shimo jipya la kuchotwa fedha kila mwaka? Hivi wabunge wetu wana akili za uwekezaji au wanazisikia tu na wanataka wawe nazo wananchi lakini si wao wenyewe?
. Je, kwanini mhadhiri, mwalimu, polisi, daktari na nesi nao wasipate posho kama hii? Hasa ukizingatia mazingira magumu wanayofanya kazi na majukumu watumishi hawa waliyonayo kwa wananchi wenzao ?
. Je, uwezo wetu wa kiakili unatufanya tujali faida au manufaa makubwa zaidi kwa idadi iliyo kubwa zaidi au kinyume cha hayo?
. Ni miradi mingapi mbadala ambayo ingesaidia watu wenye kipato cha chini kuondokana na umaskini inakwamishwa kwa hatua hii?
Sababu za baadhi ya wabunge kuridhika na hili
Wabunge nao ni binadamu na mahitaji yao yanaongezeka kutokana na ukubwa walio nao na tamaa zao za kifahari licha ya umaskini wa watu wao; wanataka kulimbikiza ili kushinda uchaguzi ujao; uwakilishi unakuwa fursa ya wao kunyanyuka kiuchumi kama sio kutajirika kirahisi zaidi na mfumo uliopo unatumika kuwanunua bila kujua ili wawasaliti wanaowawakilisha na kutetea walioko mamlakani hata katika yale yanayowahujumu wawakilishwa wao. Aidha katika mfumo ambao wizi wa kura umehalalishwa kinyemela na mbunge hachaguliwi ila kwa kugawa fedha kwanza, wawakilishi hulazimika baadaye kulipa madeni ya watu au kudunduliza tena kile kilichokuwa akiba yao walichokitumia ili wapate kura za wananchi.
Kwanini wabunge wanajisahau
. Wabunge ni binadamu na katika mfumo unaostawi kwa ubinafsi wa kichama na umimi, ubinafsi hauonekani ni kitu kibaya;
. Wabunge walio wengi hawaingii bungeni kutetea maslahi ya wengine ila kulinda na kuendeleza maslahi yao binafsi na jamaa zao;
. Katika mfumo ambao umekwaza na unakinza fani na tasnia nyingine (k.m. mishahara njiwa kwa wahadhiri, walimu, manesi na madaktari ) kimshahara au kiujira, kimasurufu na kimaslahi matokeo yake ni wengi kukimbilia siasa hata kama hawapendi siasa na wanaziona ni uchafu kwa sababu ya fedha au kipato na siyo kwa sababu ya wito;
. Wabunge hawachaguliwi tena kama wawakilishi na watetezi wa wanajamii fulani bali kama watumishi wa chama fulani;
. Mawasiliano kati ya wanaowawakilisha na wabunge huisha mara baada ya mbunge kuchaguliwa;
. Mbunge hafanyi kazi zake ili wananchi wake waneemeke na kutajirika bali kukisaidia chama chake kurudi tena madarakani;
. Nguvu ya serikali na vyombo vya serikali hutumika kukijenga chama tawala na kuvidhoofisha vyama vingine na kutokana na udhaifu wa vyama vingi wabunge kuamini kuwepo kwao kisiasa kunategemea chama tawala kushinda;
. Baadhi ya vyama vingine nyongeza ya posho inapotolewa asilimia kubwa haiendi mfukoni kwa mwakilishi bali kwa chama husika, yaani, nyongeza ya posho ni mlango mzuri wa kustawisha udokozi wa vilivyo vya serikali ili kuwajenga wanasiasa na vyama vyao, na;
. Wawakilishi walio wengi hawaujui umaskini wa wanaowawakilisha. Na wengi huishi katika ukale badala ya kuangalia hali halisi iliyopo hivi leo majimboni mwao.
Majibu ya maswali hayo hapo juu na mengine kama hayo nina hakika ndiyo yatakayoamua hatima ya wabunge na wanasiasa wetu na mustakabali wa nchi yetu bila kujali masuala ya itikadi, msimamo, mtazamo, chama na serikali iliyopo madarakani.
Tanzania tuitakayo
Tanzania tuitakayo haiwezi kupatikana kwa kuwa na wabunge walioshiba na wasiyemjua mwenye njaa, na wakuu wa mikoa wanaokokota badala ya kuongoza mikoa; kwani wao bado waamini wana njaa pia; kwa kutanguliza mbele ubinafsi badala ya jamii; na bwabwaja wa kuzungumza lakini wachache wa vitendo; na vyama na wanasiasa ambao wanajilinganisha na matajiri na kuishi kama wao kama sio kuwapita; na wanaotetea maslahi ya chama au serikali badala ya wananchi wao; na wenye fedha wanaoingia bungeni ili kutajirika zaidi na sio kuwanyanyua wanaowawaklisha; na watu wanaokubali kutumiwa na wengine kwa manufaa ya wengine na sio ya watu wao; na watu wasiojua nchi ilipo na inapotakiwa kwenda.
Ninaelewa maswali hayo hapo juu sio rahisi kuyajibu achilia mbali kuyajibu kwa haraka sana. Ila yanadhihirisha kitu kimoja, muswaada wa katiba si 'blue' wala 'green' wala 'white' paper ya serikali unahitaji muda na wasaa kuusoma na kuutafakari. Na kwamba kama wanaharakati, kazi yetu moja kubwa ni kuitumia katiba ama kuondoa vipengele vyote vinavyowapendelea kiujira na kimaslahi wale wasiozalisha na kuwakamua wanaozalisha kwa upande mmoja na kuviingiza vipengele vipya vyote vinavyohitajika ili kuondokana na dhuluma hii ya kiujira na kimapato ilioyoanzishwa na wakoloni, kulelewa na watawala wetu wa jana na sasa na likachukuliwa kama msahafu au biblia na lisilogusika au kurekebishwa na watawala wetu wa leo. Muktadha huu si msahafu, si biblia na mapinduzi hayaepukiki ili tuwe na Tanzania yenye usawa, haki, utu na ubinadamu zaidi. Tanzania mtu anayelipwa kwa kigezo cha kile alichokisomea na kuhitimu na sio kwa kubebwa kisiasa bila hoja na sababu za msingi. Mungu tusaidie!
Tusipoangalia demokrasia yetu inaweza kuwa wizi….
SI MTU mwingine ila baba wa ukomunisti, Karl Marx ambaye miaka zaidi ya 120 alitahadharisha kwamba demokrasia kama ilivyokuwa katika nchi za Magharibi ni mfumo wenye udhaifu, mapungufu na kasoro nyingi.
Alionya kwamba demokrasia isipodhibitiwa na wananchi wenyewe ikaachiwa kwa wajanja wachache katika jamii inaweza kugeuka wizi wa mchana kweupe na wa kutisha ambao umehalalishwa na una nguvu za kisheria.
Kiasi ambacho jambo likishaamuliwa huwezi kulipinga kwa kutumia sheria ila kwa njia nyingine.
Alidai wale wanaoitwa wawakilishi wa wananchi wanaweza kuamua kupiga kura ya 'ndiyo' ili kuifagia na kuisafisha hazina au Benki Kuu ya nchi ikawa nyeupe na isibakiwe hata na shilingi moja kwa ajili ya matumizi yao binafsi.
Nina wasiwasi kama huko sio kwa mfumo tulionao leo, wa demokrasia ya chama kimoja iliyojificha ndani ya mfumo wa vyama vingi kama sio tunakokwenda.
Hakuna anayepinga wabunge kupata posho na maslahi zaidi na hata kufanya israfu na kufuru ndogondogo. Kwa mfano, wabunge wenzao wa Kenya wameidhinisha bunge lao kununua viti vipya vya bunge kwa mabilioni ya fedha za Kenya. Kiti kimoja kitakuwa chanunuliwa kwa takriban shilingi milioni tatu. Piga hesabu kwa viti zaidi ya mia tatu bungeni uone mambo hayo. Tofauti na Tanzania viti hivyo havitoki nje vitatoka magereza ya Kenya ambako kuna maseremala wenye hadhi ya kimataifa. Lakini huu ni uwakilishi wa walio nacho kuwawakilisha wasio nacho, ambao wanaamini ili kufanya kazi zao vizuri na kwa starehe lazima anasa na starehe nazo ziingizwe hadi bungeni kwa namna moja au nyingine. Na matajiri kumbukeni hawatopenda wawakilishi wenu waonekane kuteseka au kuwa na maisha ya dhiki au kufanya kazi katika mazingira magumu, kwa hiyo mkiwaruhusu au msipowaruhusu wao watawafadhili bila shida. Ili kuepukana na aibu hii na fedheha ya kufadhiliwa na wenye pesa basi gharama hizo huonekana ni za lazima na zisizoepukika.
Maswali ya kujiuliza
Swali kuu la kujiuliza ni kigezo au vigezo gani vinavyotumika kihistoria na kimapokeo na katika mazingira na hali halisi au muktadha uliopo hivi leo ? Swali hili linazaa maswali yafuatayo:
. Wabunge wetu wana umuhimu na utakatifu gani wa kustahili kulipwa vizuri kuliko madaktari, wahadhiri, wahandisi, walimu, manesi na watu wengine kama hao?
. Hivi kweli hiki tunachokiona katika luninga, yaani, bunge la kusifia na kujisifia na kujipalilia na bunge la NDIIIIYO.... ndicho Watanzania watakachokubali kwacho wabunge kulipwa kihalali na sio kidhulumati ?
. Hivi bunge letu kazi yake ni kutatua matatizo ya wananchi na kuwawezesha wananchi wetu au kazi yake ni kuwapatia fursa wabunge ya kutumbua na kutanua?
. Je, badala ya kuwa na bunge moja tukawa pia na bunge la makundi ya kimaslahi, yaani, bunge la pili muda wa vikao hautafupishwa kiasi wabunge wakashughulikia matatizo yetu badala ya swahifa na swahifa za maneno na porojo?
. Hivi kila mkoa ukiwa na waziri wake mkuu, mawaziri na wawakishi wake nao wakashughulikia moja kwa moja mipango na bajeti zao bunge au mabunge ya kitaifa hayatahitaji tu wiki moja kila baada ya miezi mitatu kuzungumzia mambo makubwa ya kitaifa badala ya utaratibu wa sasa unaotudumaza badala ya kutukuza?
. Hivi na wanaopiga porojo, wanaolala, wanaozomea na kupiga vigelegele nao wanastahili posho hii?
. Mfumo wetu wa bunge hivi unalandana na ule wa kikoloni au kibepari ambao umejengwa katika hoja kuwa watu ni matajiri na sio masikini au vipi?
. Huko Malasyia viongozi wakiwemo wabunge walijipa miaka kadhaa ili kwanza wawatoe wananchi kutoka kwenye umaskini wa kutisha na kisha ndio wabunge wakaanza kulipwa vizuri na kutanua, je, wabunge wetu wanapoanza kwa kutanua kuna uwezekano wowote kweli kwa sisi kukombolewa kiuchumi na kijamii? Wanakubaliana na falsafa ya wabunge wa Malaysia au hawajaona ndani? Ukizingatia hulka au saikolojia ya binadamu, tuna ubavu wa kuifikia Malaysia hata 2100 kwa namna za posho kama hizi za wabunge wetu ?
. Kuna uwiano gani kati ya kile wabunge wanachofanikisha kiuchumi na kijamii kwa wananchi na kile wanacholipwa ?
. Je, uwezo wetu wa kukusanya kodi na kipato chetu cha kila mwaka unaturuhusu kulipa posho hii?
. Je, mabilioni ya fedha yatakayolipwa kwa namna hii hayawezi kuwekezwa kwanza katika mradi utakaozalisha ili posho hiyo itokane na kinachozalishwa na sio kuiingizia hazina shimo jipya la kuchotwa fedha kila mwaka? Hivi wabunge wetu wana akili za uwekezaji au wanazisikia tu na wanataka wawe nazo wananchi lakini si wao wenyewe?
. Je, kwanini mhadhiri, mwalimu, polisi, daktari na nesi nao wasipate posho kama hii? Hasa ukizingatia mazingira magumu wanayofanya kazi na majukumu watumishi hawa waliyonayo kwa wananchi wenzao ?
. Je, uwezo wetu wa kiakili unatufanya tujali faida au manufaa makubwa zaidi kwa idadi iliyo kubwa zaidi au kinyume cha hayo?
. Ni miradi mingapi mbadala ambayo ingesaidia watu wenye kipato cha chini kuondokana na umaskini inakwamishwa kwa hatua hii?
Sababu za baadhi ya wabunge kuridhika na hili
Wabunge nao ni binadamu na mahitaji yao yanaongezeka kutokana na ukubwa walio nao na tamaa zao za kifahari licha ya umaskini wa watu wao; wanataka kulimbikiza ili kushinda uchaguzi ujao; uwakilishi unakuwa fursa ya wao kunyanyuka kiuchumi kama sio kutajirika kirahisi zaidi na mfumo uliopo unatumika kuwanunua bila kujua ili wawasaliti wanaowawakilisha na kutetea walioko mamlakani hata katika yale yanayowahujumu wawakilishwa wao. Aidha katika mfumo ambao wizi wa kura umehalalishwa kinyemela na mbunge hachaguliwi ila kwa kugawa fedha kwanza, wawakilishi hulazimika baadaye kulipa madeni ya watu au kudunduliza tena kile kilichokuwa akiba yao walichokitumia ili wapate kura za wananchi.
Kwanini wabunge wanajisahau
. Wabunge ni binadamu na katika mfumo unaostawi kwa ubinafsi wa kichama na umimi, ubinafsi hauonekani ni kitu kibaya;
. Wabunge walio wengi hawaingii bungeni kutetea maslahi ya wengine ila kulinda na kuendeleza maslahi yao binafsi na jamaa zao;
. Katika mfumo ambao umekwaza na unakinza fani na tasnia nyingine (k.m. mishahara njiwa kwa wahadhiri, walimu, manesi na madaktari ) kimshahara au kiujira, kimasurufu na kimaslahi matokeo yake ni wengi kukimbilia siasa hata kama hawapendi siasa na wanaziona ni uchafu kwa sababu ya fedha au kipato na siyo kwa sababu ya wito;
. Wabunge hawachaguliwi tena kama wawakilishi na watetezi wa wanajamii fulani bali kama watumishi wa chama fulani;
. Mawasiliano kati ya wanaowawakilisha na wabunge huisha mara baada ya mbunge kuchaguliwa;
. Mbunge hafanyi kazi zake ili wananchi wake waneemeke na kutajirika bali kukisaidia chama chake kurudi tena madarakani;
. Nguvu ya serikali na vyombo vya serikali hutumika kukijenga chama tawala na kuvidhoofisha vyama vingine na kutokana na udhaifu wa vyama vingi wabunge kuamini kuwepo kwao kisiasa kunategemea chama tawala kushinda;
. Baadhi ya vyama vingine nyongeza ya posho inapotolewa asilimia kubwa haiendi mfukoni kwa mwakilishi bali kwa chama husika, yaani, nyongeza ya posho ni mlango mzuri wa kustawisha udokozi wa vilivyo vya serikali ili kuwajenga wanasiasa na vyama vyao, na;
. Wawakilishi walio wengi hawaujui umaskini wa wanaowawakilisha. Na wengi huishi katika ukale badala ya kuangalia hali halisi iliyopo hivi leo majimboni mwao.
Majibu ya maswali hayo hapo juu na mengine kama hayo nina hakika ndiyo yatakayoamua hatima ya wabunge na wanasiasa wetu na mustakabali wa nchi yetu bila kujali masuala ya itikadi, msimamo, mtazamo, chama na serikali iliyopo madarakani.
Tanzania tuitakayo
Tanzania tuitakayo haiwezi kupatikana kwa kuwa na wabunge walioshiba na wasiyemjua mwenye njaa, na wakuu wa mikoa wanaokokota badala ya kuongoza mikoa; kwani wao bado waamini wana njaa pia; kwa kutanguliza mbele ubinafsi badala ya jamii; na bwabwaja wa kuzungumza lakini wachache wa vitendo; na vyama na wanasiasa ambao wanajilinganisha na matajiri na kuishi kama wao kama sio kuwapita; na wanaotetea maslahi ya chama au serikali badala ya wananchi wao; na wenye fedha wanaoingia bungeni ili kutajirika zaidi na sio kuwanyanyua wanaowawaklisha; na watu wanaokubali kutumiwa na wengine kwa manufaa ya wengine na sio ya watu wao; na watu wasiojua nchi ilipo na inapotakiwa kwenda.
Ninaelewa maswali hayo hapo juu sio rahisi kuyajibu achilia mbali kuyajibu kwa haraka sana. Ila yanadhihirisha kitu kimoja, muswaada wa katiba si 'blue' wala 'green' wala 'white' paper ya serikali unahitaji muda na wasaa kuusoma na kuutafakari. Na kwamba kama wanaharakati, kazi yetu moja kubwa ni kuitumia katiba ama kuondoa vipengele vyote vinavyowapendelea kiujira na kimaslahi wale wasiozalisha na kuwakamua wanaozalisha kwa upande mmoja na kuviingiza vipengele vipya vyote vinavyohitajika ili kuondokana na dhuluma hii ya kiujira na kimapato ilioyoanzishwa na wakoloni, kulelewa na watawala wetu wa jana na sasa na likachukuliwa kama msahafu au biblia na lisilogusika au kurekebishwa na watawala wetu wa leo. Muktadha huu si msahafu, si biblia na mapinduzi hayaepukiki ili tuwe na Tanzania yenye usawa, haki, utu na ubinadamu zaidi. Tanzania mtu anayelipwa kwa kigezo cha kile alichokisomea na kuhitimu na sio kwa kubebwa kisiasa bila hoja na sababu za msingi. Mungu tusaidie!
Alionya kwamba demokrasia isipodhibitiwa na wananchi wenyewe ikaachiwa kwa wajanja wachache katika jamii inaweza kugeuka wizi wa mchana kweupe na wa kutisha ambao umehalalishwa na una nguvu za kisheria.
Kiasi ambacho jambo likishaamuliwa huwezi kulipinga kwa kutumia sheria ila kwa njia nyingine.
Alidai wale wanaoitwa wawakilishi wa wananchi wanaweza kuamua kupiga kura ya 'ndiyo' ili kuifagia na kuisafisha hazina au Benki Kuu ya nchi ikawa nyeupe na isibakiwe hata na shilingi moja kwa ajili ya matumizi yao binafsi.
Nina wasiwasi kama huko sio kwa mfumo tulionao leo, wa demokrasia ya chama kimoja iliyojificha ndani ya mfumo wa vyama vingi kama sio tunakokwenda.
Hakuna anayepinga wabunge kupata posho na maslahi zaidi na hata kufanya israfu na kufuru ndogondogo. Kwa mfano, wabunge wenzao wa Kenya wameidhinisha bunge lao kununua viti vipya vya bunge kwa mabilioni ya fedha za Kenya. Kiti kimoja kitakuwa chanunuliwa kwa takriban shilingi milioni tatu. Piga hesabu kwa viti zaidi ya mia tatu bungeni uone mambo hayo. Tofauti na Tanzania viti hivyo havitoki nje vitatoka magereza ya Kenya ambako kuna maseremala wenye hadhi ya kimataifa. Lakini huu ni uwakilishi wa walio nacho kuwawakilisha wasio nacho, ambao wanaamini ili kufanya kazi zao vizuri na kwa starehe lazima anasa na starehe nazo ziingizwe hadi bungeni kwa namna moja au nyingine. Na matajiri kumbukeni hawatopenda wawakilishi wenu waonekane kuteseka au kuwa na maisha ya dhiki au kufanya kazi katika mazingira magumu, kwa hiyo mkiwaruhusu au msipowaruhusu wao watawafadhili bila shida. Ili kuepukana na aibu hii na fedheha ya kufadhiliwa na wenye pesa basi gharama hizo huonekana ni za lazima na zisizoepukika.
Maswali ya kujiuliza
Swali kuu la kujiuliza ni kigezo au vigezo gani vinavyotumika kihistoria na kimapokeo na katika mazingira na hali halisi au muktadha uliopo hivi leo ? Swali hili linazaa maswali yafuatayo:
. Wabunge wetu wana umuhimu na utakatifu gani wa kustahili kulipwa vizuri kuliko madaktari, wahadhiri, wahandisi, walimu, manesi na watu wengine kama hao?
. Hivi kweli hiki tunachokiona katika luninga, yaani, bunge la kusifia na kujisifia na kujipalilia na bunge la NDIIIIYO.... ndicho Watanzania watakachokubali kwacho wabunge kulipwa kihalali na sio kidhulumati ?
. Hivi bunge letu kazi yake ni kutatua matatizo ya wananchi na kuwawezesha wananchi wetu au kazi yake ni kuwapatia fursa wabunge ya kutumbua na kutanua?
. Je, badala ya kuwa na bunge moja tukawa pia na bunge la makundi ya kimaslahi, yaani, bunge la pili muda wa vikao hautafupishwa kiasi wabunge wakashughulikia matatizo yetu badala ya swahifa na swahifa za maneno na porojo?
. Hivi kila mkoa ukiwa na waziri wake mkuu, mawaziri na wawakishi wake nao wakashughulikia moja kwa moja mipango na bajeti zao bunge au mabunge ya kitaifa hayatahitaji tu wiki moja kila baada ya miezi mitatu kuzungumzia mambo makubwa ya kitaifa badala ya utaratibu wa sasa unaotudumaza badala ya kutukuza?
. Hivi na wanaopiga porojo, wanaolala, wanaozomea na kupiga vigelegele nao wanastahili posho hii?
. Mfumo wetu wa bunge hivi unalandana na ule wa kikoloni au kibepari ambao umejengwa katika hoja kuwa watu ni matajiri na sio masikini au vipi?
. Huko Malasyia viongozi wakiwemo wabunge walijipa miaka kadhaa ili kwanza wawatoe wananchi kutoka kwenye umaskini wa kutisha na kisha ndio wabunge wakaanza kulipwa vizuri na kutanua, je, wabunge wetu wanapoanza kwa kutanua kuna uwezekano wowote kweli kwa sisi kukombolewa kiuchumi na kijamii? Wanakubaliana na falsafa ya wabunge wa Malaysia au hawajaona ndani? Ukizingatia hulka au saikolojia ya binadamu, tuna ubavu wa kuifikia Malaysia hata 2100 kwa namna za posho kama hizi za wabunge wetu ?
. Kuna uwiano gani kati ya kile wabunge wanachofanikisha kiuchumi na kijamii kwa wananchi na kile wanacholipwa ?
. Je, uwezo wetu wa kukusanya kodi na kipato chetu cha kila mwaka unaturuhusu kulipa posho hii?
. Je, mabilioni ya fedha yatakayolipwa kwa namna hii hayawezi kuwekezwa kwanza katika mradi utakaozalisha ili posho hiyo itokane na kinachozalishwa na sio kuiingizia hazina shimo jipya la kuchotwa fedha kila mwaka? Hivi wabunge wetu wana akili za uwekezaji au wanazisikia tu na wanataka wawe nazo wananchi lakini si wao wenyewe?
. Je, kwanini mhadhiri, mwalimu, polisi, daktari na nesi nao wasipate posho kama hii? Hasa ukizingatia mazingira magumu wanayofanya kazi na majukumu watumishi hawa waliyonayo kwa wananchi wenzao ?
. Je, uwezo wetu wa kiakili unatufanya tujali faida au manufaa makubwa zaidi kwa idadi iliyo kubwa zaidi au kinyume cha hayo?
. Ni miradi mingapi mbadala ambayo ingesaidia watu wenye kipato cha chini kuondokana na umaskini inakwamishwa kwa hatua hii?
Sababu za baadhi ya wabunge kuridhika na hili
Wabunge nao ni binadamu na mahitaji yao yanaongezeka kutokana na ukubwa walio nao na tamaa zao za kifahari licha ya umaskini wa watu wao; wanataka kulimbikiza ili kushinda uchaguzi ujao; uwakilishi unakuwa fursa ya wao kunyanyuka kiuchumi kama sio kutajirika kirahisi zaidi na mfumo uliopo unatumika kuwanunua bila kujua ili wawasaliti wanaowawakilisha na kutetea walioko mamlakani hata katika yale yanayowahujumu wawakilishwa wao. Aidha katika mfumo ambao wizi wa kura umehalalishwa kinyemela na mbunge hachaguliwi ila kwa kugawa fedha kwanza, wawakilishi hulazimika baadaye kulipa madeni ya watu au kudunduliza tena kile kilichokuwa akiba yao walichokitumia ili wapate kura za wananchi.
Kwanini wabunge wanajisahau
. Wabunge ni binadamu na katika mfumo unaostawi kwa ubinafsi wa kichama na umimi, ubinafsi hauonekani ni kitu kibaya;
. Wabunge walio wengi hawaingii bungeni kutetea maslahi ya wengine ila kulinda na kuendeleza maslahi yao binafsi na jamaa zao;
. Katika mfumo ambao umekwaza na unakinza fani na tasnia nyingine (k.m. mishahara njiwa kwa wahadhiri, walimu, manesi na madaktari ) kimshahara au kiujira, kimasurufu na kimaslahi matokeo yake ni wengi kukimbilia siasa hata kama hawapendi siasa na wanaziona ni uchafu kwa sababu ya fedha au kipato na siyo kwa sababu ya wito;
. Wabunge hawachaguliwi tena kama wawakilishi na watetezi wa wanajamii fulani bali kama watumishi wa chama fulani;
. Mawasiliano kati ya wanaowawakilisha na wabunge huisha mara baada ya mbunge kuchaguliwa;
. Mbunge hafanyi kazi zake ili wananchi wake waneemeke na kutajirika bali kukisaidia chama chake kurudi tena madarakani;
. Nguvu ya serikali na vyombo vya serikali hutumika kukijenga chama tawala na kuvidhoofisha vyama vingine na kutokana na udhaifu wa vyama vingi wabunge kuamini kuwepo kwao kisiasa kunategemea chama tawala kushinda;
. Baadhi ya vyama vingine nyongeza ya posho inapotolewa asilimia kubwa haiendi mfukoni kwa mwakilishi bali kwa chama husika, yaani, nyongeza ya posho ni mlango mzuri wa kustawisha udokozi wa vilivyo vya serikali ili kuwajenga wanasiasa na vyama vyao, na;
. Wawakilishi walio wengi hawaujui umaskini wa wanaowawakilisha. Na wengi huishi katika ukale badala ya kuangalia hali halisi iliyopo hivi leo majimboni mwao.
Majibu ya maswali hayo hapo juu na mengine kama hayo nina hakika ndiyo yatakayoamua hatima ya wabunge na wanasiasa wetu na mustakabali wa nchi yetu bila kujali masuala ya itikadi, msimamo, mtazamo, chama na serikali iliyopo madarakani.
Tanzania tuitakayo
Tanzania tuitakayo haiwezi kupatikana kwa kuwa na wabunge walioshiba na wasiyemjua mwenye njaa, na wakuu wa mikoa wanaokokota badala ya kuongoza mikoa; kwani wao bado waamini wana njaa pia; kwa kutanguliza mbele ubinafsi badala ya jamii; na bwabwaja wa kuzungumza lakini wachache wa vitendo; na vyama na wanasiasa ambao wanajilinganisha na matajiri na kuishi kama wao kama sio kuwapita; na wanaotetea maslahi ya chama au serikali badala ya wananchi wao; na wenye fedha wanaoingia bungeni ili kutajirika zaidi na sio kuwanyanyua wanaowawaklisha; na watu wanaokubali kutumiwa na wengine kwa manufaa ya wengine na sio ya watu wao; na watu wasiojua nchi ilipo na inapotakiwa kwenda.
Ninaelewa maswali hayo hapo juu sio rahisi kuyajibu achilia mbali kuyajibu kwa haraka sana. Ila yanadhihirisha kitu kimoja, muswaada wa katiba si 'blue' wala 'green' wala 'white' paper ya serikali unahitaji muda na wasaa kuusoma na kuutafakari. Na kwamba kama wanaharakati, kazi yetu moja kubwa ni kuitumia katiba ama kuondoa vipengele vyote vinavyowapendelea kiujira na kimaslahi wale wasiozalisha na kuwakamua wanaozalisha kwa upande mmoja na kuviingiza vipengele vipya vyote vinavyohitajika ili kuondokana na dhuluma hii ya kiujira na kimapato ilioyoanzishwa na wakoloni, kulelewa na watawala wetu wa jana na sasa na likachukuliwa kama msahafu au biblia na lisilogusika au kurekebishwa na watawala wetu wa leo. Muktadha huu si msahafu, si biblia na mapinduzi hayaepukiki ili tuwe na Tanzania yenye usawa, haki, utu na ubinadamu zaidi. Tanzania mtu anayelipwa kwa kigezo cha kile alichokisomea na kuhitimu na sio kwa kubebwa kisiasa bila hoja na sababu za msingi. Mungu tusaidie!
Friday, November 25, 2011
Jinsi ya kuifanya Dar safi na ya kupendeza
KAMA jiji hili ambalo ndilo lenye Ikulu na wizara na idara zote muhimu nchini linataka liondokane na uchafu, harufu mbaya mpaka misikitini na makanisani, kinyesi kinachozibuliwa wakati wa mvua barabarani na mandhari za kuchukiza sasa ni wakati wa kuirudisha kazi ya usafi wa jiji kwa wanajamii kwa kiasi fulani badala ya kutoa tenda na kukodisha mchakato wote kwa watu wasio na uwezo na wasiokidhi mahitaji na matakwa ya usafi wa jiji hili.
Serikali kuu na serikali za mitaa zitatakiwa kutoa ushirikiano maalum ili kufanikisha azma hii.
Tofauti na mambo mengine, ningelipendekeza kazi hii ipewe umuhimu wa juu hata machoni kwa watu wa nje wanaotaka kuisadia nchi yetu katika masuala ya utunzaji mazingira na usafi.
Kinachopendekezwa hapa ni kuachana na utitiri wa magari na matrekta mabovu katika kazi ya kukusanya na kusomba taka kuzipeleka huko zinakotupwa. Badala yake kutoa ajira pana na za kudumu kwa kina vijana wetu wenye matoroli, maguta, pikipiki, vipawatila, bajaji, mikokoteni na wilibaroo kufanya kazi ya kukusanya taka mitaani na kwenda kutupwa kwenye eneo maalum litakalokuwa na shimo kubwa la kutupwa taka zilizotenganishwa kiaina na kiufundi na kisha kuchakatwa hadi kuzalishwa bidhaa mpya inayoweza kutumika majumbani, viwandani na mashambani.
Umuhimu wa serikali kuu na serikali za mitaa ni katika kupatikana kwa maeneo maalum ya kuchimbwa mashimo hayo mitaani au kwenye kata; ujenzi wa miundo mbinu rahisi ya kukokotosha taka kuwa bidhaa hitajika; kuwaandaa vijana kimafunzo tayari kwa kazi za kutenganisha taka na kuzibeba kwenda kwenye maeneo husika; na kuhakikisha bajeti ya usafi toka serikalini na misaada ya wafadhili inaelekezwa kwenye mambo haya badala ya kuliwa na wajanja wachache huko walipo.
Italazimu pia kwa viongozi na maofisa wote wa jiji na katika wizara husika, ambao wameomba kupewa hisa na chochote na wawekezaji katika miradi mipya tarajiwa ya kurejelea taka kupewa ruhusa maalum na serikali kuu ya kuwekeza kwenye makampuni bila kutoa chochote !
Aidha wanajamii kwa kushirikiana na serikali kuu na za mitaa watapaswa kuwa na kisima cha maji kilichochimbwa kwenye eneo au kina ambacho maji hayakauki kamwe ili kuhakikisha mji unakuwa na mandhari nzuri na ya kuvutia wakati wote. Maji hayo pia yatatumika kusaidia kazi za kupooza na kulainisha bidhaa katika kituo kikuu cha kubadili taka kuwa mali na utajiri. Ndoto ya kuwa na mifumo mizuri ya kuvuna mvua itakuwa ziada ambayo si mbovu katika hili.
Kila nyumba italazimika kupatiwa pipa pacha nne au kwa maneno mengine pipa ambalo lina sehemu nne: moja kwa ajili ya kutupwa chupa na glasi: la pili kwa ajili ya kutupwa karatasi: la tatu kwa ajili ya kutupwa mabaki ya vyakula na la mwisho kwa ajili ya kutupwa taka ambazo ni hatari kwa afya ya binadamu na taka mchanganyiko nje ya hizo hapo juu.
Vijana wakusanyaji watafunzwa jinsi ya kuzihamisha taka hizo toka mapipa hayo kwenda mifuko maalum ambayo itachukua taka kwa mpangilio huo huo huo na kuzipeleka kwenye kituo kikuu cha taka kwenye mtaa au kata kwa ajili ya kurejelewa upya kuzalisha kinachowezekana kuzalishwa.
Zitakapofikishwa kituoni hapo taka zitakuwa tayari zimetenganishwa kwa utaratibu huo hapo juu na hivyo kuingizwa kwenye moja kwa moja kwenye eneo zitakazofanyiwa kazi ili kuzalisha umeme au kutoa bidhaa fulani itakayotumika kama bidhaa mpya tena madukani au sokoni. Mabaki ya vyakula yanatarajiwa kutengenezwa kuwa mbolea asili isiyo na dawa yoyote ambayo itauzwa kwenye mifuko maalum kwa wakulima na watunza bustani.
Watumishi wizara ya ardhi wataaswa kwamba ili kuleta uwiano kati ya klutenda dhambai na mema- nchini ni muhimu kwao pamoja na kuuza maeneo wazi kwa mabwanyenye wetu wapya, sasa kutoa maeneo kwa ajili ya uchimbaji mashimo makubwa ya uhifadhi wa taka zitakazochakatwa na kuwa bidhaa mpya au kuzalisha umeme kwa ajili ya faida ya wakazi walio wengi jijini.
Wataalamu wa vyama vya siasa vyenye vijiwe mjini wataombwa wautumie utaalamu huo ili kugeuza vijana wetu toka 'majoblesi alwatani', wababaishaji na kupe wenye sifa za kimataifa kubadilika kwa kukopeshwa mitaji ya kununua toroli, maguta na vifaa kama hivyo ili kuwa wakusanyaji na wabebaji taka watakaoipa heshima mpya jiji la Dar es salaam.
Wataalamu wa kupiga raia mabomu, kuvunja maandamano na mikutano wataombwa kuutumia utaalamu wao ili kuhamasisha kazi ya usombaji taka kila wakati ili pasiwe na taka hata moja mahala popote jijini kwa kasi ile ile ya upigaji mabomu ya machozi wakati wa maandamano ya upinzani, wafuasi wa dini fulani au wafanyakazi au wanafunzi.
Mameneja wa migodi wataaombwa kuazimisha magreda na makatapila kuja kuchimba mashimo hayo katika mitaa au kata mbalimbali jijini kama walivyofanikisha zoezi la uchimbaji mashimo huko Geita, North Mara na Bulyanhulu,kutegemeana na kiwango cha uzalishaji taka katika maeneo husika.
Badala ya kuwa na magari mabovu yanayosafiri umbali mrefu kuokota na kutupa taka sasa vitoroli, mikokoteni, bajaji, guta na pikipiki zitatengenezwa kwa njia ambayo kwazo zitakuwa zikipeleka taka kwenye maeneo hayo yenye mashimo na miundo mbinu maalum ya kupokea taka zilizotenganishwa na kuanza kuzifanyia mchakato ili zitoe bidhaa za aina mbalimbali na kuzalisha umeme na vitu vingine vitakavyowezekanika.
Taka zinazohitaji kutupwa mbali zitachukuliwa na magari makubwa maalum machache lakini yenye kiwango cha kimataifa kwenda kutupwa mbali kabisa na makazi ya watu na wakati mwingine hata kwenda kufukia mashimo yaliyotokana na kuchimbwa madini yetu katika mikoa ya kaskazini na kusini.
Ukiutazama mtiririko huu mzima utagundua kuwa pendekezo hili lina shabaha ya kugeuza taka kuwa mali kwa namna kadhaa. Kwanza, vijana ambao wana tatizola ajira itabidi sasa wakimbie ajira wao wenyewe. Taka zitageuka fumba na kufumbua mali, maana kila mzigo kutegemeana na aina yake utakuwa ukilipwa fedha nzuri tu mara ukifika kwenye kituo kikuu cha kuchakata taka kwenye mtaa au kata.
Aidha magari mabovu ya kusomba taka amabyo wakati mwingine badala ya kusafisha mji huuchafua yatatoweka. Takataka hizo zitazaa bidhaa ambazo wafanyabiashara na wanunuzi watanufaika kwani zina uwezekano mkubwa wa kuwa za bei rahisi zaidi kuliko nyinginezo. Kisha mbolea itakayozalishwa itakwenda kuzistawisha bustani za Ikulu na Mnazi mmoja na maeneo mengine mjini na hivyo kulipa jiji mandhari ya kukata na shoka kwa uzuri wake. Hali kadhalika, sio tu tatizo la kukatikakatika umeme jijini litakuwa historia bali mradi huu utahakikisha hata nyumba mbavu za mbwa zilizo mabondeni zinapata umeme wa kutosha na wa uhakika kila siku.
Vilevile visima vitakavyoendana na mradi huu vitawahakikishia wakazi wa kila mtaa na kata upatikanaji maji masafi ya uhakika wakati wote, wakati wanasubiri maajabu yatakayofanywa na DAWASCO miaka mitano au kumi ijayo kama bado wako hai. Hili linawezekana, cheza nafasi yako na timiza wajibu wako. Miaka hamsini baada ya uhuru hutakiwi kushindwa na jambo hili.
Wakati ninaandika makala haya watafiti wanaonisaidia wameleta habari kwamba kuna watu tayari wameanza kujituma wenyewe na kuanzisha miradi kama hii. Kama hili ni kweli basi wilaya, mkoa na wizara husika zichangamkie mara moja jambo hili. NIna hakika likipata kuungwa mkono nao ni kitu kinachowezekana na kitakalolifanya jiji la Dar es salaam kuwa jiji la kuigwa na miji mingine sio tu Tanzania bali Afrika nzima.
lle tabia ya kujifanya kuwa serikali inaweza kufanya kila kitu si kitu kizuri. Na katika miaka hii ni kitu kilichopitwa na wakati na kuwazaini wananchi huku tukijua fika tunasema uongo. Kweli Watanzania hawana fedha, yaani, ni maskini. Lakini Watanzania wana kitu kimoja ambcho thamani yake wakati mwingine ni kubwa kuliko fedha. Kitu hicho sio kingine ila akili na nguvu zao. Pakiwa na uongozi unaoona mbali na mbele na unaojua kutumia akili na nguvu hizo na kuwekeza fedha kidogo Watanzania kama watu wengine wana nafasi ya kufanya maajabu mbalimbali duniani.
Serikali kuu na serikali za mitaa zitatakiwa kutoa ushirikiano maalum ili kufanikisha azma hii.
Tofauti na mambo mengine, ningelipendekeza kazi hii ipewe umuhimu wa juu hata machoni kwa watu wa nje wanaotaka kuisadia nchi yetu katika masuala ya utunzaji mazingira na usafi.
Kinachopendekezwa hapa ni kuachana na utitiri wa magari na matrekta mabovu katika kazi ya kukusanya na kusomba taka kuzipeleka huko zinakotupwa. Badala yake kutoa ajira pana na za kudumu kwa kina vijana wetu wenye matoroli, maguta, pikipiki, vipawatila, bajaji, mikokoteni na wilibaroo kufanya kazi ya kukusanya taka mitaani na kwenda kutupwa kwenye eneo maalum litakalokuwa na shimo kubwa la kutupwa taka zilizotenganishwa kiaina na kiufundi na kisha kuchakatwa hadi kuzalishwa bidhaa mpya inayoweza kutumika majumbani, viwandani na mashambani.
Umuhimu wa serikali kuu na serikali za mitaa ni katika kupatikana kwa maeneo maalum ya kuchimbwa mashimo hayo mitaani au kwenye kata; ujenzi wa miundo mbinu rahisi ya kukokotosha taka kuwa bidhaa hitajika; kuwaandaa vijana kimafunzo tayari kwa kazi za kutenganisha taka na kuzibeba kwenda kwenye maeneo husika; na kuhakikisha bajeti ya usafi toka serikalini na misaada ya wafadhili inaelekezwa kwenye mambo haya badala ya kuliwa na wajanja wachache huko walipo.
Italazimu pia kwa viongozi na maofisa wote wa jiji na katika wizara husika, ambao wameomba kupewa hisa na chochote na wawekezaji katika miradi mipya tarajiwa ya kurejelea taka kupewa ruhusa maalum na serikali kuu ya kuwekeza kwenye makampuni bila kutoa chochote !
Aidha wanajamii kwa kushirikiana na serikali kuu na za mitaa watapaswa kuwa na kisima cha maji kilichochimbwa kwenye eneo au kina ambacho maji hayakauki kamwe ili kuhakikisha mji unakuwa na mandhari nzuri na ya kuvutia wakati wote. Maji hayo pia yatatumika kusaidia kazi za kupooza na kulainisha bidhaa katika kituo kikuu cha kubadili taka kuwa mali na utajiri. Ndoto ya kuwa na mifumo mizuri ya kuvuna mvua itakuwa ziada ambayo si mbovu katika hili.
Kila nyumba italazimika kupatiwa pipa pacha nne au kwa maneno mengine pipa ambalo lina sehemu nne: moja kwa ajili ya kutupwa chupa na glasi: la pili kwa ajili ya kutupwa karatasi: la tatu kwa ajili ya kutupwa mabaki ya vyakula na la mwisho kwa ajili ya kutupwa taka ambazo ni hatari kwa afya ya binadamu na taka mchanganyiko nje ya hizo hapo juu.
Vijana wakusanyaji watafunzwa jinsi ya kuzihamisha taka hizo toka mapipa hayo kwenda mifuko maalum ambayo itachukua taka kwa mpangilio huo huo huo na kuzipeleka kwenye kituo kikuu cha taka kwenye mtaa au kata kwa ajili ya kurejelewa upya kuzalisha kinachowezekana kuzalishwa.
Zitakapofikishwa kituoni hapo taka zitakuwa tayari zimetenganishwa kwa utaratibu huo hapo juu na hivyo kuingizwa kwenye moja kwa moja kwenye eneo zitakazofanyiwa kazi ili kuzalisha umeme au kutoa bidhaa fulani itakayotumika kama bidhaa mpya tena madukani au sokoni. Mabaki ya vyakula yanatarajiwa kutengenezwa kuwa mbolea asili isiyo na dawa yoyote ambayo itauzwa kwenye mifuko maalum kwa wakulima na watunza bustani.
Watumishi wizara ya ardhi wataaswa kwamba ili kuleta uwiano kati ya klutenda dhambai na mema- nchini ni muhimu kwao pamoja na kuuza maeneo wazi kwa mabwanyenye wetu wapya, sasa kutoa maeneo kwa ajili ya uchimbaji mashimo makubwa ya uhifadhi wa taka zitakazochakatwa na kuwa bidhaa mpya au kuzalisha umeme kwa ajili ya faida ya wakazi walio wengi jijini.
Wataalamu wa vyama vya siasa vyenye vijiwe mjini wataombwa wautumie utaalamu huo ili kugeuza vijana wetu toka 'majoblesi alwatani', wababaishaji na kupe wenye sifa za kimataifa kubadilika kwa kukopeshwa mitaji ya kununua toroli, maguta na vifaa kama hivyo ili kuwa wakusanyaji na wabebaji taka watakaoipa heshima mpya jiji la Dar es salaam.
Wataalamu wa kupiga raia mabomu, kuvunja maandamano na mikutano wataombwa kuutumia utaalamu wao ili kuhamasisha kazi ya usombaji taka kila wakati ili pasiwe na taka hata moja mahala popote jijini kwa kasi ile ile ya upigaji mabomu ya machozi wakati wa maandamano ya upinzani, wafuasi wa dini fulani au wafanyakazi au wanafunzi.
Mameneja wa migodi wataaombwa kuazimisha magreda na makatapila kuja kuchimba mashimo hayo katika mitaa au kata mbalimbali jijini kama walivyofanikisha zoezi la uchimbaji mashimo huko Geita, North Mara na Bulyanhulu,kutegemeana na kiwango cha uzalishaji taka katika maeneo husika.
Badala ya kuwa na magari mabovu yanayosafiri umbali mrefu kuokota na kutupa taka sasa vitoroli, mikokoteni, bajaji, guta na pikipiki zitatengenezwa kwa njia ambayo kwazo zitakuwa zikipeleka taka kwenye maeneo hayo yenye mashimo na miundo mbinu maalum ya kupokea taka zilizotenganishwa na kuanza kuzifanyia mchakato ili zitoe bidhaa za aina mbalimbali na kuzalisha umeme na vitu vingine vitakavyowezekanika.
Taka zinazohitaji kutupwa mbali zitachukuliwa na magari makubwa maalum machache lakini yenye kiwango cha kimataifa kwenda kutupwa mbali kabisa na makazi ya watu na wakati mwingine hata kwenda kufukia mashimo yaliyotokana na kuchimbwa madini yetu katika mikoa ya kaskazini na kusini.
Ukiutazama mtiririko huu mzima utagundua kuwa pendekezo hili lina shabaha ya kugeuza taka kuwa mali kwa namna kadhaa. Kwanza, vijana ambao wana tatizola ajira itabidi sasa wakimbie ajira wao wenyewe. Taka zitageuka fumba na kufumbua mali, maana kila mzigo kutegemeana na aina yake utakuwa ukilipwa fedha nzuri tu mara ukifika kwenye kituo kikuu cha kuchakata taka kwenye mtaa au kata.
Aidha magari mabovu ya kusomba taka amabyo wakati mwingine badala ya kusafisha mji huuchafua yatatoweka. Takataka hizo zitazaa bidhaa ambazo wafanyabiashara na wanunuzi watanufaika kwani zina uwezekano mkubwa wa kuwa za bei rahisi zaidi kuliko nyinginezo. Kisha mbolea itakayozalishwa itakwenda kuzistawisha bustani za Ikulu na Mnazi mmoja na maeneo mengine mjini na hivyo kulipa jiji mandhari ya kukata na shoka kwa uzuri wake. Hali kadhalika, sio tu tatizo la kukatikakatika umeme jijini litakuwa historia bali mradi huu utahakikisha hata nyumba mbavu za mbwa zilizo mabondeni zinapata umeme wa kutosha na wa uhakika kila siku.
Vilevile visima vitakavyoendana na mradi huu vitawahakikishia wakazi wa kila mtaa na kata upatikanaji maji masafi ya uhakika wakati wote, wakati wanasubiri maajabu yatakayofanywa na DAWASCO miaka mitano au kumi ijayo kama bado wako hai. Hili linawezekana, cheza nafasi yako na timiza wajibu wako. Miaka hamsini baada ya uhuru hutakiwi kushindwa na jambo hili.
Wakati ninaandika makala haya watafiti wanaonisaidia wameleta habari kwamba kuna watu tayari wameanza kujituma wenyewe na kuanzisha miradi kama hii. Kama hili ni kweli basi wilaya, mkoa na wizara husika zichangamkie mara moja jambo hili. NIna hakika likipata kuungwa mkono nao ni kitu kinachowezekana na kitakalolifanya jiji la Dar es salaam kuwa jiji la kuigwa na miji mingine sio tu Tanzania bali Afrika nzima.
lle tabia ya kujifanya kuwa serikali inaweza kufanya kila kitu si kitu kizuri. Na katika miaka hii ni kitu kilichopitwa na wakati na kuwazaini wananchi huku tukijua fika tunasema uongo. Kweli Watanzania hawana fedha, yaani, ni maskini. Lakini Watanzania wana kitu kimoja ambcho thamani yake wakati mwingine ni kubwa kuliko fedha. Kitu hicho sio kingine ila akili na nguvu zao. Pakiwa na uongozi unaoona mbali na mbele na unaojua kutumia akili na nguvu hizo na kuwekeza fedha kidogo Watanzania kama watu wengine wana nafasi ya kufanya maajabu mbalimbali duniani.
Subscribe to:
Posts (Atom)
