UDIKTETA au ukiritimba au mtu kuhodhi mamlaka yote peke yake, iwe kisiasa au kiuchumi au kijamii huashiria kuwa huyo ni mtu au mtu mwenye kikundi cha watu wasiajiamini na wasiokuwa na uhakika na kile wanachokifanya. Aghalabu watu wa namna hii huwa hawajui wanakotoka wala wanakokwenda. Ni mwanzo wa kuficha maovu mengi kwa kuonesha mazuri machache ambayo pengine hayana faida wala manufaa kwa a ya kujichimbia kaburi lake yenyewe. Huanza kwa kutoamini wengine lakini huishia kwa kutojiamini wenyewe na kutoaminiana wenyewe kwa wenyewe na kuishia kujichanganya na kujimaliza wenyewe.
Udikteta huweza kuundwa na mtu mmoja au kikundi cha watu. Udikteta uliopo Tanzania hivi leo ni ule wa kichama. Udikteta huu unajidhirisha kwa chama hicho kutaka kuwa na watu na sauti katika kila jambo hata yale yasiyokihusu- kwa mfano, dini, utamaduni, mila na desturi, mawasiliano, maendeleo ya watu na jamii zao, ushirika, uzalishaji mali na majumuiko mengine ya kijamii kwa hofu hii au ile.
Kwa kuwa wanasiasa waliopo wanaamini kwamba kwa kuwa hawawezi kuitawala nchi bila ya kulazimisha mikoa, wilaya, vijiji na mitaa kuwa chini ya chama tawala basi miundo na mifumo ya kisiasa inayoundwa sio ile ya kufanya maeneo hayo kuwa huru bali maeneo hayo kutawaliwa moja kwa moja au kimzunguko na chama tawala na viongozi wake.
Ni dhahiri basi madaraka mikoani au kuwa na mikoa huru kiuchumi na kijamii sio jambo linaloweza kufanywa na wanasiasa wa chama tawala. Hili ni jambo linalostahili kuwemokwenye katiba na sheria za nchi kama sehemu moja ya kupanua na kuongeza kina cha watu kujitawala, kujiamulia mambo yao wenyewe na demokrasia kiujumla.
Chama tawala kina unafiki mkubwa ambao ni muhimu kuutambua na kuubainisha kwa wadau wa katiba. Kwa kuwa kinatambua nguvu yake inatokana na ujinga, umaskini na magonjwa mbalimbali ya watawaliwa inaelewa fika kuwa kupiga vita mambo hayo ni lazima wanajamii washirikiane ili kufanikiwa. Lakini, ushirikiano wa wananchi kijamii na kiuchumi kutawapa pia wanajamii nguvu na sauti sawa au zaidi ya wanasiasa. Kwa mantiki hii chama cha siasa kinachokubali makundi ya jamii au watu kuwa huru zaidi kiuchumi na kisisasa katika ngazi ya mtaa, kata, wilaya na mkoa huhofia pia kujimaliza kisiasa. Kwa sababu hii, maamuzi yote yanayohusiana na kuyapa makundi ya kijamii nguvu na uwezo zaidi hufanywa polepole mno. Jambo la siku moja huchukua mwezi; la mwezi, mwaka; la mwaka muongo; la muongo karne kama sio zaidi!
Hata hivyo, ili nchi na watu wake kuendelea hakuna njia ya mkato. Njia ni moja tu. Nayo ni ushirikishwaji wananchi katika uundwaji wa katiba na sheria za nchi zinazoendana na wakati tuliomo; ushirikishwaji watu katika maamuzi, mipango, uongozi, utekelezwaji na udhibiti wa masuala yote ya maendeleo na ustawi wa jamii huska ikiwemo kuwa na mikoa huru kiuchumi inayokuwa chini ya viongozi waliochaguliwa na wananchi au wakazi wa mkoa husika.
Kwa kifupi kuna mambo kadhaa yanayoonesha wazi kwamba ili serikali yoyote ifanikiwe ni lazima wananchi wake washiriki na wawe na sauti katika uongozi wa nchi:
. Kukubalika, heshima na uwezo wa serikali kuu huanza kwenye mitaa na jamii mikoani;
. Maendeleo ya kweli ya mkoa yanatokana na kile wananchi wake wanachozalisha na kumiliki na sio vitu vya wageni;
. Serikali zenye nguvu na uwezo za mikoa na mitaa hufanya kazi ya kulinda hazina ya mkoa na mali asili za eneo husika kwa faida ya wakazi wake na nchi nzima;
. Uongozi wa kitaifa hutekeleza miradi ya mikoa aghalabu nusu nusu kutokana na kukurupuka na kwenda kuzima moto unaowaka mkoa mwingine, hivyo kuhamisha fedha kwa ajili ya mkoa mmoja kwenda kuufaa mkoa mwingine isivyo haki;
. Wizi wa kura unaofanyika kirahisi chini ya uchaguzi wa kitaifa utapungua ikiwa kila mkoa unachagua viongozi na serikali yake kwanza wao wenyewe kabla ya uongozi wa kitaifa;
. Serikali huru za mikoa ni shule au chuo pekee kitakachowafundisha viongozi wa baadaye wa kitaifa kwa vitendo huko huko waliko mikoani.
Migogoro ya kisiasa inayotokea Afrika na hususan Tanzania kwa kiasi kikubwa ni kati ya wale wamanaoamini:
. wanasiasa kazi yao ni kutawala na wananchi ni kutawaliwa tu dhidi ya wale wanaoamini wananchi wanastahili kujitawala wenyewe;
. Wanasiasa wanaoamini viongozi wetu wanastahili kuishi kifahari na wale wanaoamini ni lazima wanasiasa wajishushe kwanza na kuwanyanyua watu wao kabla ya wao wenyewe kuwa na maisha mazuri na bora;
. Wanasiasa wanaodhani kuwa kazi ya vyombo vya habari vya umma na vile vya chama tawala ni kufuma na kusambaza urongo na wale wanaoamini hakuna mwenye haki ya kutengeneza na kuuzia wananchi uongo Afrika;
. wanasiasa wanastahili maisha mazuri na bora kuliko raia wengine na wale wanaoamini wananchi wanastahili maisha bora na mazuri kuliko ya wanasiasa;
. wanasiasa wana haki ya kuiba toka hazina za taifa na kuweka fedha toka nchi maskini katika nchi tajiri kwa hifadhi yao ya baadaye na wale wanaoamini huo ni ujinga na kama mwanasiasa ni mwananchi mzalendo hifadhi yake lazima itoke ndani ya jamii yake;
. wanasiasa wetu wanastahili kuwanyenyekea na kuwafuata wale wanasiasa matajiri kwa kila jambo wanalolisema au kutushauri hata likiwa halina maslahi kwa watu wetu;
. wanasiasa wanastahili kuwatumia polisi na pengine jeshi ili kuwasaga wananchi waende kule wao wanakotaka waende dhidi ya wale wanaoamini polisi na jeshi wanastahili kudhibiti wanasiasa kwenda kle wananchi wanakotaka nchi iende;
. wanasiasa wanahitaji kubaki madarakani milele ili walete maendeleo na wale wanaoshani wanahitaji muhula mmoja tu kufanya kazi hiyo;
. wanasiasa wa chama tawala ndio tu wapewe uongozi hata kama hawawezi kazi na wale wanaodhani wanaostahili kuongoza wananchi lazima wachaguliwe na wananchi wa eneo husika;
. wanasiasa wanaoamini wananchi wakielimishwa na wakiondokana na umasikini itakuwa vigumu wao kutawala dhidi ya wale wanaoamini itakuwa rahisi zaidi kwao kutawala;
. wanasiasa wanaoamini kuwa chama cha kisiasa lazima kiwaibie wananchi ili kiendelee kutawala na wanaoamini wananchi wenyewe wanaweza kukika chama uwezo wa kujiendesha;
. wanasiasa wanaoamini ni wanachama wa chama fulani tu wanaostahili kuwa na sauti na kuwa makundi mengine katika jamii hayastahili kuwezeshwa wala kuwa na nguvu iwe ya kisiasa, kijamii au kiuchumi na kadhalika.
Afrika imebadilika, na Afrika ya leo si ya jana. Wale wote wenye fikra pacha za kwanza hawana tena nafasi katika Afrika mpya. Kizungumkuti kinachokuja kitawagia kama ilivyofanyika huko Maghreb pembeni na kuwajaribu wala wenye fikra mbadala pacha hapo juu.
Na njia sahihi ya kufuata kuanzia sasa ni kuhakikisha kuwa tunapelekea madaraka kwa wananchi sio tu mikoani bali mpaka vijijini.
Mikoa Huru ya Ujerumani:
Kwa mfano mikoa ya Ujerumani ni pamoja na Baden-Württemberg, Bavaria (Bayern), Berlin,Brandenburg na Bremen. Kahalika kuna Hamburg, Hesse
(Hessen), Mecklenburg-Vorpommern, Lower Saxony (Niedersachsen), North Rhine-Westphalia (Nordrhein-Westfalen), Rhineland-Palatinate (Rheinland-Pfalz), Saarland, Saxony (Sachsen), Saxony-Anhalt (Sachsen-Anhalt), Schleswig-Holstein na Thuringia (Thüringen).
Mikoa yote hii isipokuwa kwa mkoa mmoja tu ina serikali za pamoja/mseto kati ya vyama viwili au zaidi. KIla mkoa una waziri wake mkuu, baraza lake la mawaziri, wawakilishi wake na taasisi zake na inakuwa huru kwa kiasi kikubwa kwenye masuala yote ya kiuchumi na kijamii. Yale ya ulinzi, usalama, fedha na siasa za nje hushughulikiwa zaidi na serikali ya kitaifa yenye makao yake makuu hivi leo Berlin. Mikoa hii imewezesha kuwa na ushindani wa ndani kwa ndani na hivyo kuipa nguvu Ujerumani katika utandawazi na ushindani wa nje kwa kujikita tu kwenye maeneo inayoamini hakuna anayeweza kuwapita. Wao si watu wa kufanya na kujaribu kila kitu kwa kubahatisha. Hutafuta uhakika kwanza kabla hawajawekeza kwenye jambo fulani.
Sunday, February 27, 2011
Wednesday, February 9, 2011
Utalii, Tanroads na Kujipanga Kimkakati
MAJUMA mawili yaliyopita, siku ya Jumanne, kulikuwa na habari za Kenya kujenga bandari na kiwanja cha ndege mpakani mwa Tanzania. Hili linatokea wakati ambapo mwaka mmoja haujapita toka makala haya kuhoji kuwepo kwa 'bodaposti' katika mipaka yetu ambazo zimefanana sana na vichaka bodaposti hizo zilizomo.
Makala haya yakashauri kwamba wakati umefika sasa kubadilisha bodaposti hizo zifanane na viwanja vya ndege vya kimataifa ili kuwapendezesha na kuwavutia zaidi watalii na wawekezaji kuja kusaidia kukuza na kuendeleza uchumi wetu. Kitu ambacho ni haki yao. Wakati Kenya walisoma, kuitafakari na kuifanyia kazi habari hiyo wenzetu bado wapo usingizini na hakuna kinachoendelea. Bado somo la utandawazi na ushindani usio na mipaka halijaeleweka hata kidogo kwa upande wao.
Kenya inatambua fika kwamba vivutio vikubwa vya utalii hapa Afrika Mashariki viko Tanzania. Walichokifanya ni kutumia akili yao kwani wanajua Watanzania hawatumii zao ila kwa yale yasiyochangia maendeleo yao bali kuyavuruga na kuharibu walichonacho. Nchi ya maneno mengi sana, lakini ya vitendo vifupi na vichache mno, ndivyo tunavyoitwa eti! Nani wa kubisha ?
Kiutalii tunakwenda wapi ?
Hivi kweli tunataka utalii uchangie kupunguza umaskini nchini ? Nina mashaka. Maana tungelikuwa na busara hiyo yale yaliyofanyika Arusha ambayo ni kitovu cha utalii yasingefanyika. Lakini hilo ni dogo tu. Tuje kwenye picha kubwa. Hivi kujitangaza Ulaya, Marekani na kwenye CNN na wengineo kama hako kutatusaidia kweli bila kujipanga hapa nyumbani ? Muhali sana.
Takwimu zinaonesha sekta ya utalii inakuwa haraka kuliko sekta za mazoea za siku za nyuma. Lakini kukua kwa utalii hapa nchini kutategemea sana jinsi tunavyoondokana na picha ya sisi kuwa nchi masikini. Kwa kadri tutakavyoonekana ni masikini (wa kujitakia) tutawaogopesha watu kuja kutalii nchi hii. Na kwa ujumla watu wasiotaka kubadilika na wanaotaka kuvuna pale wasipopanda kitu chochote. Ni lazima serikali ishiriki kikamilifu katika uendelezaji wa sekta hii ili iweze kufanya maajabu katika muda mfupi iwezekanavyo. Na njia mojawapo kama nilivyosema ni ile ya kuwa na mikakati sahihi ya kupunguza kama sio kuundoa kabisa umaskini wa kutupwa.
Tanroads na Wizara husika zijipange upya
Kama kweli tunataka utalii utusaie kupunguza umaskini ni lazima tujipange upya. Ninachokiona sasa ni kuwa wahusika wakuu kila mmoja anakwenda njia yake na analifanya lile analojua yeye. Hili nadhani ni kosa. Ninashauri wale wanaoishi kando ya barabara zetu, Tanroads, SUMATRA, Kituo cha Uwekezaji Tanznia, NSSF, PPF, Wizara ya Utalii, TANAPA, Wenye vyombo vya usafiri, Wasafirishaji Watalii, Wenye mahoteli wafanye kazi pamoja ili barabara zetu zisiwe kama mstari tu unaopita juu ya nchi baliziwe na vivutio vya aina mbalimbali vitakavyogeuza njia husika yenyewe kuwa ni kivutio cha utalii pia.
Tuchukulie mfano wa barabara mbili kuu Tanzania, yaani, ile ya Dar es Salaam-Arusha/Namanga na ile ya Dar es Salaam-Mbeya/Tunduma. Barabara hizi zimejengwa kizamani. Hazina mvuto kwa watalii ila vivutio vya asili na vile vichache watu binafsi walivyoviweka njiani. Lakini hebu tujiulize walichokifanya waliojenga hoteli pale Kitonga na pale Highway Korogwe kimeongeza ubora wa huduma za usaifi njia hizo kwa kiasi gani ? Na, je, mifano hii inaweza kuigwa kwenye mambo mengine ? Je, tunaweza kuwa na sehemu zenye huduma zote muhimu kama vile misikiti au mahala pa kusalia, zahanati, vituo vya mafuta, vyombo vya ulinzi na usalama, mahoteli, viwanja vya michezo mbalimbali,mabwawa ya kuogelea, vyoo safi, bafu, gesti, intaneti, simu, maduka, masoko na kadhalika kwa kila kilomita 70 hivi? Mathalani njia ya Dar-Arusha ukawa na vituo kama hivyo 5 na ile ya Dar-Mbeya kama 10 hivi ? Ninaamini kuwepo barabara kunakuwa na faida endapo watu wanafaidika na barabara hiyo na biashara na miji mipya inazuka. Kazi ya kwenda kuchimba dawa ikiisha hivi kuna mgeni atakayesita kusafiri na mabasi ya TABOA ?
Tujiulize, ni kwa namna gani tutaacha kujenga barabara zisizokuwa na kivutio chochote njia nzima? Maana zikibaki kama zilivyo zinakuwa hazijaongeza thamani wala maslahi yoyote ya maana kwa Mtanzania wa kawaida. Na utunzaje wake pia hapo baadaye unakuwa wa mashaka. Njia bora ni kuwa na ushirikiano na washikadau wote katika kuzifanya barabara zetu na maeneo zinakopita kuwa ni aina fulani ya kivutio cha utalii. Kiasi kwamba mtu anaposafiri kuelekea Arusha au Mbeya asitake kufika huko haraka na ikiwezekana alale siku mbili au tatu njiani kufaidi vivutio mbalimbali anavyokutana navyo njiani. Kwa namna hii pia utalii sasa utashuka hadi chini na kuwanufaisha masikini ili mradi tu twende nao sambamba katika kuhakiki viwango vya ubora vinavyokubalika njia nzima.
Utalii ni kama msichana. Jinsi anavyokuwa mzuri, msafi, mwenye kujua mapishi ya kila aina, mcheshi na mwenye kuvutia kwa kila hali ndivyo wanaume wengi wanavyojigonga gonga kwake kila kukichwa!
Humo mote barabara hizo kuu zinamopita inawezekana kuwa na programu kamambe ya kukuza utalii wa aina mbalimbali ukiwemo ule wa makumbusho, vyakula na vinywaji, miti na mali asili zingine. Aidha, utalii wa kielimu, mafunzo, mikutano na kiutafiti pia unawezekana na ile ya anasa au starehe, michezo na sanaa. Vilevile utalii wa usafi na mazingira bora, mazoezi, tiba na afya na kadhalika.
Kama hili litaendana na kuondokana na bodaposti za kale na badala yake kuwa na vituo vya mpakani sawa na viwanja vya ndege kwa ushirikiano kati ya wananchi, serikali na wawekezaji wa nje na ndani kilichofanywa na Kenya kinaweza kikawa ni hasara badala ya faida. Isipokuwa hakuna muda hata kidogo wa kusubiri. Kama walivyosema wahenga: " Chelewa, chelewa utamkuta mtoto si wako!"
Tanroads isifikirie kiuhandisi au kifundi tu. Ianze kujenga tabia ya kufikiria mambo kibiashara na kiuchumi. Upo uwezekano mkubwa sana wa barabara zetu kusaidia kupunguza umaskini endapo miradi kama iliyooneshwa hapo juu itatekelezwa inavyostahili na sio kiubabaishaji.
Sambamba na hili ni lile la kuwa na barabara moja kuu inayotambaa na bahari ya Hindi katika pwani ya Tanzania kiasi ambacho kwamba tunaweza pia kuwa na Utalii wa pwani ya Tanzania kwa meli, ndege na magari. Na katika yote haya nafuu ya kimaisha na kiuchumi ikapatikana kwa wakazi wa maeneo husika katika muda mfupi tu ujao. Mikoa yetu ya pwani kwa kiasi fulani ni masikini na iko nyuma kimaendeleo kwa sababu bahari, vilivyomo na fukwe zake ambazo ndio rasilimali zao kuu hazijatumika ipasavyo kuvutia watalii katika maeneo hayo.
Katika dunia inayobadilika kila siku ni kosa kubwa kufanya jambo bila kuhusisha mambo mengine yanayoendana na jambo hili. Huu ni mtazamo wa kuyafanya mengi kwa faida kubwa chini ya mwamvuli mmoja, kwa maana kwamba, mambo mengi kwa pamoja yanaweza kufanyika kwa faida kubwa zaidi na kwa manufaa ya wengi zaidi kwa wakati uleule.
Ipo kila sababu kama kweli tunataka kuitumikia nchi hii na watu wake kuifanya Tanroads, Wizara ya Mali Asili, Hazina, TASAF, Benki Kuu, mabenki mbalimbali, makampuni ya mafuta na simu za mkononi kuanza kufikiria kuwapa Watanzania nyavu za kuvua samaki wao wenyewe badala ya kuwadanganya na kipande cha samaki au nguru kila siku.
Makala haya yakashauri kwamba wakati umefika sasa kubadilisha bodaposti hizo zifanane na viwanja vya ndege vya kimataifa ili kuwapendezesha na kuwavutia zaidi watalii na wawekezaji kuja kusaidia kukuza na kuendeleza uchumi wetu. Kitu ambacho ni haki yao. Wakati Kenya walisoma, kuitafakari na kuifanyia kazi habari hiyo wenzetu bado wapo usingizini na hakuna kinachoendelea. Bado somo la utandawazi na ushindani usio na mipaka halijaeleweka hata kidogo kwa upande wao.
Kenya inatambua fika kwamba vivutio vikubwa vya utalii hapa Afrika Mashariki viko Tanzania. Walichokifanya ni kutumia akili yao kwani wanajua Watanzania hawatumii zao ila kwa yale yasiyochangia maendeleo yao bali kuyavuruga na kuharibu walichonacho. Nchi ya maneno mengi sana, lakini ya vitendo vifupi na vichache mno, ndivyo tunavyoitwa eti! Nani wa kubisha ?
Kiutalii tunakwenda wapi ?
Hivi kweli tunataka utalii uchangie kupunguza umaskini nchini ? Nina mashaka. Maana tungelikuwa na busara hiyo yale yaliyofanyika Arusha ambayo ni kitovu cha utalii yasingefanyika. Lakini hilo ni dogo tu. Tuje kwenye picha kubwa. Hivi kujitangaza Ulaya, Marekani na kwenye CNN na wengineo kama hako kutatusaidia kweli bila kujipanga hapa nyumbani ? Muhali sana.
Takwimu zinaonesha sekta ya utalii inakuwa haraka kuliko sekta za mazoea za siku za nyuma. Lakini kukua kwa utalii hapa nchini kutategemea sana jinsi tunavyoondokana na picha ya sisi kuwa nchi masikini. Kwa kadri tutakavyoonekana ni masikini (wa kujitakia) tutawaogopesha watu kuja kutalii nchi hii. Na kwa ujumla watu wasiotaka kubadilika na wanaotaka kuvuna pale wasipopanda kitu chochote. Ni lazima serikali ishiriki kikamilifu katika uendelezaji wa sekta hii ili iweze kufanya maajabu katika muda mfupi iwezekanavyo. Na njia mojawapo kama nilivyosema ni ile ya kuwa na mikakati sahihi ya kupunguza kama sio kuundoa kabisa umaskini wa kutupwa.
Tanroads na Wizara husika zijipange upya
Kama kweli tunataka utalii utusaie kupunguza umaskini ni lazima tujipange upya. Ninachokiona sasa ni kuwa wahusika wakuu kila mmoja anakwenda njia yake na analifanya lile analojua yeye. Hili nadhani ni kosa. Ninashauri wale wanaoishi kando ya barabara zetu, Tanroads, SUMATRA, Kituo cha Uwekezaji Tanznia, NSSF, PPF, Wizara ya Utalii, TANAPA, Wenye vyombo vya usafiri, Wasafirishaji Watalii, Wenye mahoteli wafanye kazi pamoja ili barabara zetu zisiwe kama mstari tu unaopita juu ya nchi baliziwe na vivutio vya aina mbalimbali vitakavyogeuza njia husika yenyewe kuwa ni kivutio cha utalii pia.
Tuchukulie mfano wa barabara mbili kuu Tanzania, yaani, ile ya Dar es Salaam-Arusha/Namanga na ile ya Dar es Salaam-Mbeya/Tunduma. Barabara hizi zimejengwa kizamani. Hazina mvuto kwa watalii ila vivutio vya asili na vile vichache watu binafsi walivyoviweka njiani. Lakini hebu tujiulize walichokifanya waliojenga hoteli pale Kitonga na pale Highway Korogwe kimeongeza ubora wa huduma za usaifi njia hizo kwa kiasi gani ? Na, je, mifano hii inaweza kuigwa kwenye mambo mengine ? Je, tunaweza kuwa na sehemu zenye huduma zote muhimu kama vile misikiti au mahala pa kusalia, zahanati, vituo vya mafuta, vyombo vya ulinzi na usalama, mahoteli, viwanja vya michezo mbalimbali,mabwawa ya kuogelea, vyoo safi, bafu, gesti, intaneti, simu, maduka, masoko na kadhalika kwa kila kilomita 70 hivi? Mathalani njia ya Dar-Arusha ukawa na vituo kama hivyo 5 na ile ya Dar-Mbeya kama 10 hivi ? Ninaamini kuwepo barabara kunakuwa na faida endapo watu wanafaidika na barabara hiyo na biashara na miji mipya inazuka. Kazi ya kwenda kuchimba dawa ikiisha hivi kuna mgeni atakayesita kusafiri na mabasi ya TABOA ?
Tujiulize, ni kwa namna gani tutaacha kujenga barabara zisizokuwa na kivutio chochote njia nzima? Maana zikibaki kama zilivyo zinakuwa hazijaongeza thamani wala maslahi yoyote ya maana kwa Mtanzania wa kawaida. Na utunzaje wake pia hapo baadaye unakuwa wa mashaka. Njia bora ni kuwa na ushirikiano na washikadau wote katika kuzifanya barabara zetu na maeneo zinakopita kuwa ni aina fulani ya kivutio cha utalii. Kiasi kwamba mtu anaposafiri kuelekea Arusha au Mbeya asitake kufika huko haraka na ikiwezekana alale siku mbili au tatu njiani kufaidi vivutio mbalimbali anavyokutana navyo njiani. Kwa namna hii pia utalii sasa utashuka hadi chini na kuwanufaisha masikini ili mradi tu twende nao sambamba katika kuhakiki viwango vya ubora vinavyokubalika njia nzima.
Utalii ni kama msichana. Jinsi anavyokuwa mzuri, msafi, mwenye kujua mapishi ya kila aina, mcheshi na mwenye kuvutia kwa kila hali ndivyo wanaume wengi wanavyojigonga gonga kwake kila kukichwa!
Humo mote barabara hizo kuu zinamopita inawezekana kuwa na programu kamambe ya kukuza utalii wa aina mbalimbali ukiwemo ule wa makumbusho, vyakula na vinywaji, miti na mali asili zingine. Aidha, utalii wa kielimu, mafunzo, mikutano na kiutafiti pia unawezekana na ile ya anasa au starehe, michezo na sanaa. Vilevile utalii wa usafi na mazingira bora, mazoezi, tiba na afya na kadhalika.
Kama hili litaendana na kuondokana na bodaposti za kale na badala yake kuwa na vituo vya mpakani sawa na viwanja vya ndege kwa ushirikiano kati ya wananchi, serikali na wawekezaji wa nje na ndani kilichofanywa na Kenya kinaweza kikawa ni hasara badala ya faida. Isipokuwa hakuna muda hata kidogo wa kusubiri. Kama walivyosema wahenga: " Chelewa, chelewa utamkuta mtoto si wako!"
Tanroads isifikirie kiuhandisi au kifundi tu. Ianze kujenga tabia ya kufikiria mambo kibiashara na kiuchumi. Upo uwezekano mkubwa sana wa barabara zetu kusaidia kupunguza umaskini endapo miradi kama iliyooneshwa hapo juu itatekelezwa inavyostahili na sio kiubabaishaji.
Sambamba na hili ni lile la kuwa na barabara moja kuu inayotambaa na bahari ya Hindi katika pwani ya Tanzania kiasi ambacho kwamba tunaweza pia kuwa na Utalii wa pwani ya Tanzania kwa meli, ndege na magari. Na katika yote haya nafuu ya kimaisha na kiuchumi ikapatikana kwa wakazi wa maeneo husika katika muda mfupi tu ujao. Mikoa yetu ya pwani kwa kiasi fulani ni masikini na iko nyuma kimaendeleo kwa sababu bahari, vilivyomo na fukwe zake ambazo ndio rasilimali zao kuu hazijatumika ipasavyo kuvutia watalii katika maeneo hayo.
Katika dunia inayobadilika kila siku ni kosa kubwa kufanya jambo bila kuhusisha mambo mengine yanayoendana na jambo hili. Huu ni mtazamo wa kuyafanya mengi kwa faida kubwa chini ya mwamvuli mmoja, kwa maana kwamba, mambo mengi kwa pamoja yanaweza kufanyika kwa faida kubwa zaidi na kwa manufaa ya wengi zaidi kwa wakati uleule.
Ipo kila sababu kama kweli tunataka kuitumikia nchi hii na watu wake kuifanya Tanroads, Wizara ya Mali Asili, Hazina, TASAF, Benki Kuu, mabenki mbalimbali, makampuni ya mafuta na simu za mkononi kuanza kufikiria kuwapa Watanzania nyavu za kuvua samaki wao wenyewe badala ya kuwadanganya na kipande cha samaki au nguru kila siku.
Sunday, February 6, 2011
Tatizo Si Vyama Bali Vijana Kukosa Ajira na Tumaini
Tatizo Si Vyama Bali Vijana Kukosa Ajira na Tumaini
UPO msiba mkubwa Tanzania ambao sio mwingine ila ni ule wa viongozi na wananchi kujenga tabia ya kutangaza, kuamua au kutetea jambo fulani baada ya kumsikiliza mtu mmoja au chombo kimoja tu. Huu ni msiba mkubwa ambao unaweza kutufikisha kwenye gharika ya karne kitaifa katika muda sio mrefu kutoka sasa.
Aidha, pamoja na msiba huo ni ajali za kila siku ambako viongozi wetu hufikia kwenye majibu mepesi na ya kirahisi kwa masuala tata na magumu ya kitaifa na kijamii!
Mifano iko mingi. Tanzania inashinda kombe la chalenji kwa fluki basi nchi bila hata kukuza vipaji vyovyote vya maana wala maandalizi inaonekana tayari imepanda juu kisoka (hebu cheki taarifa ya FIFA ya hivi karibuni-mambo ni kinyume chake). TANESCO wanaomba kuongeza bei na wanaruhusiwa mara moja eti gharama zimepanda. Hakuna maelezo ya
wataalamu kwamba badala ya kupandisha bei TANESCO ingeweza ikapunguza gharama moja, mbili, tatu na isihitajike kupandisha bei umeme. Hakuna anayehangaisha akili ili kuangalia wizi na ubadhirifu TANESCO upo kiasi gani, jinsi gani watu wanajiandikia 'overtime' ya masaa 10 kwa kazi ya saa moja na kadhalika.
Tuliambiwa mgawo wa umeme sasa ni historia. [ Wengine leo wanadai wanahabari walinukuu kauli hiyo vibaya. Eti ni mgawo wa Kihistoriaa na sio mgawo utakuwa historia. ]
Inaonekana bado ni hadithi pevu na mpya kabisa. Kiasi kwamba wakati mwingine kuna watu wanaojiuliza kama viongozi wetu ni watu wazima au watoto wadogo? Inashangaza sana.
Kati ya muda ambao kiongozi anaambiwa kuwepo tatizo au fursa au changamoto fulani hadi anatoa kauli juu ya tatizo hilo kuna mambo kadhaa yanayotakiwa kufanyika. Kwanza, apate habari tofauti kutoka vyanzo mbalimbali. Asiwaamini tu maofisa na washauri wake. Apate watu wa kumfanyia kazi ya ziada pembeni ya wale wanaomzunguka. Atafakari ripoti zote
kwa kina. Akutane na wataalamu wa masuala husika na azungumze nao bila kutumia ukubwa wake kupata msimamo wao wa kweli. Kisha aangalie sasa kutokana na maelezo aliyo nayo anafaa kutangaza au kulizungmza jambo hadharani au la. Na kama ni kulitangaza litangazwe likiwa na mashiko yapi ya kiidhibati, kisheria na kiakili, kibusara na kihekima.
Kukurupuka tu baada ya kushauriwa na mtu au kikundi au taasisi moja mtu akajibu maswali mazito ya kitaifa au kimataifa hakika ni msiba usioelezeka nchini hapa. Na matokeo yake mara nyingi inakuwa ni mtu au nchi kujiiaibisha bila sababu ya maana.
Nikimsikiliza mwanasiasa mmoja machachari Tanzania nilibaki kinywa wazi alivyokuwa akielezea kiini cha tatizo la maandamano na vurugu huko Tunisia na Misri. Sina haja ya kurudia alichokisema, lakini upeo na uwezo wake kama kiongozi ulikuwa rahisi sana kuonekana kwa yeyote mwenye utambuzi na tafakuri kama mtu wa kawaida tu na wala sio lazima
awe mwalimu wa menejimenti na oganaizesheni na sayansi ya maamuzi. Hizi ndizo baadhi ya ajali za nchi yetu ambazo zinatokana na kutotambua umuhimu wa kutafuta katika rasilimali watu zetu kile kilicho bora zaidi kwa kila jambo na eneo.
Kinachotokea Afrika Kaskazini si majibu kwa ukame wa demokrasia na usawa katika ugawanyaji rasilimali za nchi ingawa hizi ni baadhi ya sababu.
Ukikumbuka historia ya ulimwengu kunako miaka ya 1960 na kizazi cha 'baby boomers' na 'mahippies' moja kwa moja unaona uhusiano kati ya matukio ya miaka hiyo na kile kitakachotokea katika muongo huu hapa Afrika.
Hali ya hewa na mazingira katika miaka ya 60 na 70 yamechangia Waafrika kuwa na watoto wengi ambao leo ni vijana. Baadhi ya vijana hawa wamezaliwa, wamesoma chekechea, shule ya msingi na sekondari, chuo kikuu na kuishia joblesi mitaani chini ya rais mmoja au wawili au chini ya chama kimoja tu cha kisiasa. Na hao waliokuwa madarakani hawana cha maana walichokifanya kama wenzetu wa Asia na Marekani Kusini kuinua nchi zao kiuchumi na kijamii.
Vijana hao ambao sasa wana miaka 20-40 wameona wazazi wao wakiwa na maisha bora kuliko waliyokuwa nayo wao leo; wameona jinsi viongozi wanavyozidi kujitajirisha; wameona viongozi wanavyowapa wanawake na watoto wao utajiri na nafasi katika utawala; na wameona jinsi nchi zao zinavyoporwa na kuibwa na viongozi wao wenyewe. Na wamefikia mahala wamechafukwa na roho, moyo na akili kiasi kwamba wako tayari wakipepewa na upepe mdogo tu kuwasha moto mkubwa unaoweza kuangamiza jamiii nzima.
Amani na umoja ambao kwa kawaida unakuwa ni wimbo wa vyama vikongwe vilivyotawala Waafrika sasa unakuwa ni wimbo unaowakinaisha na kutokuwaogopesha kabisa vijana.
Vijana wanajua fika amani wala umoja ni muhimu. Lakini kukosa ajira kwao ni kukosa umoja na kukosa riziki kwao ni kukosa amani. Na kukosa matumaini katika maisha ni kukosa mshikamano kabisa na jamii mtu aliyemo.
Hawa ni watu ambao wamekulia chini ya chama kimoja au rais mmoja toka walipozaliwa, kusoma chekechea, kusoma shule ya msingi, sekondari na hata chuo kikuu. Na sasa ni joblesi na watu wasio na matumaini chini ya chama au rais huyohuyo ! Na televisheni, redio, intaneti na simu za mkononi zinawafungua macho kila siku kuwa mtu au chama kimoja kikitawala kwa muda mrefu kinazeeka, kinachoka na kinaridhika na hali ilivyo hata kama kwa kufanya hivyo kuna mateso, dhiki na majonzi makubwa mioyoni mwa walio wengi.
Katika lugha ya kiutafiti tatizo hili la vijana limeelezwa na watu kadhaa kama David Bloom na wenzake kuwa ni tukio la kinchi linaloitwa 'demographic dividend' au mgawo wa ziada wa kimaendeleo unaoletwa na kuwa na watu wengi wenye umri wa kufanya kazi kuliko wasiofanya kazi. Ikiwa viongozi wanaliona hili na kulifanyia kazi ili nguvu na akili hizo zitumike
kuijenga na pengine kuitajirisha nchi basi nchi itakuwa na amani na maendeleo.
Wasipoliona jambo hili na kadri idadi kubwa ya vijana wanavyokuwa hawana kazi na hawachangii lolote la maana katika maendeleo yao binafsi, ya familia zao na ya nchi basi kulipuka na kusambaratika kwa nchi husika ni kitu kisichoepukika. Kwa maneno mengine, 'demographic dividend' hustahili kuwa kitu cha manufaa kwa nchi na watu wake, lakini
chini ya uongozi mbovu, unaoifilisi serikali yake yenyewe, uongozi unaofikiria kuneemeka wenyewe kwanza na sio wananchi na utawala usiojua unakwenda wapi na unafanya nini jambo hili hugeuka kuwa tani za fataki hatari kwa jamii na nchi nzima.
Baadhi ya dhiki na matatizo yanayowakera vijana wa Kiafrika ni pamoja na kushindwa kujikimu wenyewe na kutegemewa wazazi na watu wengine; kuiona nchi yao inakuwa shamba la bibi la wageni; kuona ndani ya serikali kuna wizi na ufisadi wa kutisha; kuona hakuna dalili zozote za uongezwaji au uzalishaji wa ajira mpya nchini; kubebeshwa zigo la gharama za elimu na afya na kudhulumiwa hata kile wanachotakiwa kupewa au kukopeshwa.
Matatizo mengine ni pamoja na dini na madhehebu mbalimbali kukosa dhamira ya kweli kufuta umaskini na kuwasaidia vijana mitaji, mafunzo na uwezeshwaji wa aina mbalimbali ili waweze kujiajiri; miradi mingi ya serikali ya kijamii kuwa ni ya kuwapa watu samaki badala ya kuwapa nyavu; nchi kushindwa kutumia fursa za kiuchumi zilzoletwa na intaneti na teknolojia mpya; viongozi na matajiri kuwapendelea watoto wao kwanza kwa kila kitu na suala la maendeleo na nafuu vijijini kwa vijana na wazee kuchimbiwa hali hai katika kaburi la sahau serikalini na katika vyama vya kisiasa.
Dini na madhehebu yaliyoanzisha shule za msingi, sekondari na vyuo vikuu vilitarajiwa vitatoa elimu kwa bei nafuu zaidi na hasa ukizingatia kwamba dini hizo zinapewa sio tu ruzuku na serikali bali pia na nchi za nje. Kinyume chake, shule za kidini leo zinatisha kwa gharama kubwa, walimu duni na wachache, wababaishaji katika menejimenti ya shule, walaji wazuri
tu lakini wanaowalisha wanafunzi chakula sawa au pengine chakula duni zaidi ya kile cha wafungwa magerezani. Shule hizo za kidini zimegeuzwa ni vyuo vya kuvumilia shida na taabu za kila aina.
Mashirika binafsi na yale ya umma yanajali zaidi kutoa ajira kwa watoto wa wakubwa na matajiri lakini wasiokuwa na majina hawafikirii wala kupewa msaada wa kujiendeleza.
Wanaoshika nafasi za uongozi serikalini wanajli zaidi kuwanufaisha watoto, ndugu na jamaa zao na sio kila kijana wa Kitanzania.
Ili kukabiliana na hali hii ni vyema wananchi wakashinikiza viongozi na vyama vya kisiasa na serikali zao kuhakikisha vitendo sasa viwe vinatangulia kauli. Serikali na wanasiasa wafanye kazi kwanza kuleta nafuu kwa watu ndio maneno yafuate. Ieleweke kwamba hakuna kitu kinachomkatisha tamaa mwanadamu kama vile kupewa ahadi hewa au isiyotekelezwa. Hesabu za haraka haraka zinaonesha kuna ahadi zaidi ya 100 zilizotolewa na wagombea nafasi ya Urais nchini. Kama hivyo ndivyo ni hatari kuachia mambo kwenda kama kawaida bila kuwa na taarifa zinazotoka kila mwezi kuonesha ahadi hizo zinaendeleaje kutekelezwa. Na ahadi zenye uzito hapa ni zile ambazo kwa namna moja au nyingine zinakuwa na manufaa kwa vijana.
Tatizo la ahadi zetu nyingi ni kuwa zinachukua miaka mingi hadi kutimizwa. Tunapaswa kujiangalia na kupanga ahadi kutokana na muda unaohitajika. Ahadi ya kukipa kijiji maji ya kisima isichukue mwaka bali ichukue mwezi mmoja au miwili tu. Shule ikikosa madawati au viti lisiwe jambo la mwezi bali la wiki moja tu. Na pale ambapo jambo kweli linataka miezi kadhaa au miaka liwe ni jambo ambalo kila mtu anakubali kwamba haiwezekani vinginevyo.
Wanasiasa wetu kihistoria hawaheshimu muda. Lakini lazima tubadilike tuwe tunaheshimu na kuuchukulia muda kuwa ni rasilimali adimu kuliko zote duniani. Ahadi lazima zimfae yule anayeahidiwa. Tukishakufa ahadi wala maneno mazuri hayatusaidii kitu. Tutekeleze mambo mapema na kwa wakati ili watu wafaidi tunayoahidi wakiwa hai na sio wakishakuwa wafu. Na hili ndilo linalowatisha vijana. Wanaogopa kwamba hakuna ahadi itakayotimizwa wakati wakiwa hai. Au zikitimizwa watakuwa wazee na hawatafaidika tena na kitu chochote kutokana na uzee na kukosa nguvu na uwezo mwingineo.
Ni muhimu pia kwa vijana wa Tanzania kuanzia sasa kuwa na jumuiya ya kitaifa badala ya jumuiya za kichama ili kuepusha tunayona yakitokea Misri na kwingineko baadaye. Kwanza, kuwagawa vijana katika makundi mbalimbali ni kuwazuia kuwa na umoja wa kitaifa na nguvu na sauti zaidi katika maamuzi ya nchi. Lakini muhimu zaidi ni kuwa vijana wakiwa chini ya Muungano wa Vijana wa Tanzania na sio wa chama hiki au kile watajenga Uzalendo na Utanzania wao kuwa madhubuti zaidi kuliko vinginevyo.
Taasisi kama JKT iliundwa makusudi kuwaleta pamoja vijana wa Kitanzania na kuwafanya wote (masikini kwa tajiri,dini mbalimbali, kabila mbalimbali) kujiona wao ni Watanzania kwanza juu ya kitu kingine. Tukiiachia fursa hii kupotea tutakuja ijutia baadaye.
Nimalizie kwa kusema kwamba, Tanzania haijafikia zilipofikia nchi za Maghreb lakini hatuko mbali sana kama tusipoamka na kubadili muundo wa serikali, mifumo ya uendeshaji nchi, matumizi ya rasilimali za nchi na kuacha kuwatanguliza matajiri, wanasiasa na wageni mbele badala ya kumtanguliza Mtanzania mzawa kwanza.
Ni lazima pia tufanye mambo yetu tofauti na watu wengine. Utofauti huu peke yake ndiyo unaoweza kutufanya tuwe tofauti na pengine kufanikiwa kwa haraka zaidi kuliko Waafrika wengine. Tuna mbegu, ardhi na maji tosha kupanda na kuvuna nchi yenye amani, mshikamano na maendeleo kwa wote. Watakaosababisha mambo kuwa kinyume cha hivyo wamo miongoni mwetu na ni wale wasiojua nchi hii na watu wake wanatakiwa waelekee wapi!
Kila mtu anaafiki Tanzania ina viungo vyote nchi inayohitaji kuandaa pilau safi ya ustawi jamii; uchumi imara; lugha ya Kiswahili inayoweza kumfundisha Mtanzania kila kitu chini ya mbingu; ustaarabu; miji safi na yenye mvuto kwa walio ndani na nje; kilimo kinachotutosheleza na ziada kupatikana; viwanda maridhia kukidhi mahitaji yetu ya ndani na ya nje; utalii wenye vivutio aali na vingine vya kutengnezwa an watu; taasisi za elimu zinazovutia walimu na wanafunzi toka nje, hospitali zinazovutia madaktari na wagonjwa toka nje, migodi ya madini na mali asili zinazoweza kupunguza nusu ya umaskini wetu na masoko na biashara zinazoweza kutufanya wafanyabiashara bora Afrika na kwingineko -ila kinachokosekana ni wapishi wanaoweza kuikubali kazi yao ya upishi wakakaa jikoni kwa muda unaohitajika na sio kama viongozi wetu ambao wanausahau upishi wao na kukaa mezani chakula hicho kipikwe sijui na nani?
UPO msiba mkubwa Tanzania ambao sio mwingine ila ni ule wa viongozi na wananchi kujenga tabia ya kutangaza, kuamua au kutetea jambo fulani baada ya kumsikiliza mtu mmoja au chombo kimoja tu. Huu ni msiba mkubwa ambao unaweza kutufikisha kwenye gharika ya karne kitaifa katika muda sio mrefu kutoka sasa.
Aidha, pamoja na msiba huo ni ajali za kila siku ambako viongozi wetu hufikia kwenye majibu mepesi na ya kirahisi kwa masuala tata na magumu ya kitaifa na kijamii!
Mifano iko mingi. Tanzania inashinda kombe la chalenji kwa fluki basi nchi bila hata kukuza vipaji vyovyote vya maana wala maandalizi inaonekana tayari imepanda juu kisoka (hebu cheki taarifa ya FIFA ya hivi karibuni-mambo ni kinyume chake). TANESCO wanaomba kuongeza bei na wanaruhusiwa mara moja eti gharama zimepanda. Hakuna maelezo ya
wataalamu kwamba badala ya kupandisha bei TANESCO ingeweza ikapunguza gharama moja, mbili, tatu na isihitajike kupandisha bei umeme. Hakuna anayehangaisha akili ili kuangalia wizi na ubadhirifu TANESCO upo kiasi gani, jinsi gani watu wanajiandikia 'overtime' ya masaa 10 kwa kazi ya saa moja na kadhalika.
Tuliambiwa mgawo wa umeme sasa ni historia. [ Wengine leo wanadai wanahabari walinukuu kauli hiyo vibaya. Eti ni mgawo wa Kihistoriaa na sio mgawo utakuwa historia. ]
Inaonekana bado ni hadithi pevu na mpya kabisa. Kiasi kwamba wakati mwingine kuna watu wanaojiuliza kama viongozi wetu ni watu wazima au watoto wadogo? Inashangaza sana.
Kati ya muda ambao kiongozi anaambiwa kuwepo tatizo au fursa au changamoto fulani hadi anatoa kauli juu ya tatizo hilo kuna mambo kadhaa yanayotakiwa kufanyika. Kwanza, apate habari tofauti kutoka vyanzo mbalimbali. Asiwaamini tu maofisa na washauri wake. Apate watu wa kumfanyia kazi ya ziada pembeni ya wale wanaomzunguka. Atafakari ripoti zote
kwa kina. Akutane na wataalamu wa masuala husika na azungumze nao bila kutumia ukubwa wake kupata msimamo wao wa kweli. Kisha aangalie sasa kutokana na maelezo aliyo nayo anafaa kutangaza au kulizungmza jambo hadharani au la. Na kama ni kulitangaza litangazwe likiwa na mashiko yapi ya kiidhibati, kisheria na kiakili, kibusara na kihekima.
Kukurupuka tu baada ya kushauriwa na mtu au kikundi au taasisi moja mtu akajibu maswali mazito ya kitaifa au kimataifa hakika ni msiba usioelezeka nchini hapa. Na matokeo yake mara nyingi inakuwa ni mtu au nchi kujiiaibisha bila sababu ya maana.
Nikimsikiliza mwanasiasa mmoja machachari Tanzania nilibaki kinywa wazi alivyokuwa akielezea kiini cha tatizo la maandamano na vurugu huko Tunisia na Misri. Sina haja ya kurudia alichokisema, lakini upeo na uwezo wake kama kiongozi ulikuwa rahisi sana kuonekana kwa yeyote mwenye utambuzi na tafakuri kama mtu wa kawaida tu na wala sio lazima
awe mwalimu wa menejimenti na oganaizesheni na sayansi ya maamuzi. Hizi ndizo baadhi ya ajali za nchi yetu ambazo zinatokana na kutotambua umuhimu wa kutafuta katika rasilimali watu zetu kile kilicho bora zaidi kwa kila jambo na eneo.
Kinachotokea Afrika Kaskazini si majibu kwa ukame wa demokrasia na usawa katika ugawanyaji rasilimali za nchi ingawa hizi ni baadhi ya sababu.
Ukikumbuka historia ya ulimwengu kunako miaka ya 1960 na kizazi cha 'baby boomers' na 'mahippies' moja kwa moja unaona uhusiano kati ya matukio ya miaka hiyo na kile kitakachotokea katika muongo huu hapa Afrika.
Hali ya hewa na mazingira katika miaka ya 60 na 70 yamechangia Waafrika kuwa na watoto wengi ambao leo ni vijana. Baadhi ya vijana hawa wamezaliwa, wamesoma chekechea, shule ya msingi na sekondari, chuo kikuu na kuishia joblesi mitaani chini ya rais mmoja au wawili au chini ya chama kimoja tu cha kisiasa. Na hao waliokuwa madarakani hawana cha maana walichokifanya kama wenzetu wa Asia na Marekani Kusini kuinua nchi zao kiuchumi na kijamii.
Vijana hao ambao sasa wana miaka 20-40 wameona wazazi wao wakiwa na maisha bora kuliko waliyokuwa nayo wao leo; wameona jinsi viongozi wanavyozidi kujitajirisha; wameona viongozi wanavyowapa wanawake na watoto wao utajiri na nafasi katika utawala; na wameona jinsi nchi zao zinavyoporwa na kuibwa na viongozi wao wenyewe. Na wamefikia mahala wamechafukwa na roho, moyo na akili kiasi kwamba wako tayari wakipepewa na upepe mdogo tu kuwasha moto mkubwa unaoweza kuangamiza jamiii nzima.
Amani na umoja ambao kwa kawaida unakuwa ni wimbo wa vyama vikongwe vilivyotawala Waafrika sasa unakuwa ni wimbo unaowakinaisha na kutokuwaogopesha kabisa vijana.
Vijana wanajua fika amani wala umoja ni muhimu. Lakini kukosa ajira kwao ni kukosa umoja na kukosa riziki kwao ni kukosa amani. Na kukosa matumaini katika maisha ni kukosa mshikamano kabisa na jamii mtu aliyemo.
Hawa ni watu ambao wamekulia chini ya chama kimoja au rais mmoja toka walipozaliwa, kusoma chekechea, kusoma shule ya msingi, sekondari na hata chuo kikuu. Na sasa ni joblesi na watu wasio na matumaini chini ya chama au rais huyohuyo ! Na televisheni, redio, intaneti na simu za mkononi zinawafungua macho kila siku kuwa mtu au chama kimoja kikitawala kwa muda mrefu kinazeeka, kinachoka na kinaridhika na hali ilivyo hata kama kwa kufanya hivyo kuna mateso, dhiki na majonzi makubwa mioyoni mwa walio wengi.
Katika lugha ya kiutafiti tatizo hili la vijana limeelezwa na watu kadhaa kama David Bloom na wenzake kuwa ni tukio la kinchi linaloitwa 'demographic dividend' au mgawo wa ziada wa kimaendeleo unaoletwa na kuwa na watu wengi wenye umri wa kufanya kazi kuliko wasiofanya kazi. Ikiwa viongozi wanaliona hili na kulifanyia kazi ili nguvu na akili hizo zitumike
kuijenga na pengine kuitajirisha nchi basi nchi itakuwa na amani na maendeleo.
Wasipoliona jambo hili na kadri idadi kubwa ya vijana wanavyokuwa hawana kazi na hawachangii lolote la maana katika maendeleo yao binafsi, ya familia zao na ya nchi basi kulipuka na kusambaratika kwa nchi husika ni kitu kisichoepukika. Kwa maneno mengine, 'demographic dividend' hustahili kuwa kitu cha manufaa kwa nchi na watu wake, lakini
chini ya uongozi mbovu, unaoifilisi serikali yake yenyewe, uongozi unaofikiria kuneemeka wenyewe kwanza na sio wananchi na utawala usiojua unakwenda wapi na unafanya nini jambo hili hugeuka kuwa tani za fataki hatari kwa jamii na nchi nzima.
Baadhi ya dhiki na matatizo yanayowakera vijana wa Kiafrika ni pamoja na kushindwa kujikimu wenyewe na kutegemewa wazazi na watu wengine; kuiona nchi yao inakuwa shamba la bibi la wageni; kuona ndani ya serikali kuna wizi na ufisadi wa kutisha; kuona hakuna dalili zozote za uongezwaji au uzalishaji wa ajira mpya nchini; kubebeshwa zigo la gharama za elimu na afya na kudhulumiwa hata kile wanachotakiwa kupewa au kukopeshwa.
Matatizo mengine ni pamoja na dini na madhehebu mbalimbali kukosa dhamira ya kweli kufuta umaskini na kuwasaidia vijana mitaji, mafunzo na uwezeshwaji wa aina mbalimbali ili waweze kujiajiri; miradi mingi ya serikali ya kijamii kuwa ni ya kuwapa watu samaki badala ya kuwapa nyavu; nchi kushindwa kutumia fursa za kiuchumi zilzoletwa na intaneti na teknolojia mpya; viongozi na matajiri kuwapendelea watoto wao kwanza kwa kila kitu na suala la maendeleo na nafuu vijijini kwa vijana na wazee kuchimbiwa hali hai katika kaburi la sahau serikalini na katika vyama vya kisiasa.
Dini na madhehebu yaliyoanzisha shule za msingi, sekondari na vyuo vikuu vilitarajiwa vitatoa elimu kwa bei nafuu zaidi na hasa ukizingatia kwamba dini hizo zinapewa sio tu ruzuku na serikali bali pia na nchi za nje. Kinyume chake, shule za kidini leo zinatisha kwa gharama kubwa, walimu duni na wachache, wababaishaji katika menejimenti ya shule, walaji wazuri
tu lakini wanaowalisha wanafunzi chakula sawa au pengine chakula duni zaidi ya kile cha wafungwa magerezani. Shule hizo za kidini zimegeuzwa ni vyuo vya kuvumilia shida na taabu za kila aina.
Mashirika binafsi na yale ya umma yanajali zaidi kutoa ajira kwa watoto wa wakubwa na matajiri lakini wasiokuwa na majina hawafikirii wala kupewa msaada wa kujiendeleza.
Wanaoshika nafasi za uongozi serikalini wanajli zaidi kuwanufaisha watoto, ndugu na jamaa zao na sio kila kijana wa Kitanzania.
Ili kukabiliana na hali hii ni vyema wananchi wakashinikiza viongozi na vyama vya kisiasa na serikali zao kuhakikisha vitendo sasa viwe vinatangulia kauli. Serikali na wanasiasa wafanye kazi kwanza kuleta nafuu kwa watu ndio maneno yafuate. Ieleweke kwamba hakuna kitu kinachomkatisha tamaa mwanadamu kama vile kupewa ahadi hewa au isiyotekelezwa. Hesabu za haraka haraka zinaonesha kuna ahadi zaidi ya 100 zilizotolewa na wagombea nafasi ya Urais nchini. Kama hivyo ndivyo ni hatari kuachia mambo kwenda kama kawaida bila kuwa na taarifa zinazotoka kila mwezi kuonesha ahadi hizo zinaendeleaje kutekelezwa. Na ahadi zenye uzito hapa ni zile ambazo kwa namna moja au nyingine zinakuwa na manufaa kwa vijana.
Tatizo la ahadi zetu nyingi ni kuwa zinachukua miaka mingi hadi kutimizwa. Tunapaswa kujiangalia na kupanga ahadi kutokana na muda unaohitajika. Ahadi ya kukipa kijiji maji ya kisima isichukue mwaka bali ichukue mwezi mmoja au miwili tu. Shule ikikosa madawati au viti lisiwe jambo la mwezi bali la wiki moja tu. Na pale ambapo jambo kweli linataka miezi kadhaa au miaka liwe ni jambo ambalo kila mtu anakubali kwamba haiwezekani vinginevyo.
Wanasiasa wetu kihistoria hawaheshimu muda. Lakini lazima tubadilike tuwe tunaheshimu na kuuchukulia muda kuwa ni rasilimali adimu kuliko zote duniani. Ahadi lazima zimfae yule anayeahidiwa. Tukishakufa ahadi wala maneno mazuri hayatusaidii kitu. Tutekeleze mambo mapema na kwa wakati ili watu wafaidi tunayoahidi wakiwa hai na sio wakishakuwa wafu. Na hili ndilo linalowatisha vijana. Wanaogopa kwamba hakuna ahadi itakayotimizwa wakati wakiwa hai. Au zikitimizwa watakuwa wazee na hawatafaidika tena na kitu chochote kutokana na uzee na kukosa nguvu na uwezo mwingineo.
Ni muhimu pia kwa vijana wa Tanzania kuanzia sasa kuwa na jumuiya ya kitaifa badala ya jumuiya za kichama ili kuepusha tunayona yakitokea Misri na kwingineko baadaye. Kwanza, kuwagawa vijana katika makundi mbalimbali ni kuwazuia kuwa na umoja wa kitaifa na nguvu na sauti zaidi katika maamuzi ya nchi. Lakini muhimu zaidi ni kuwa vijana wakiwa chini ya Muungano wa Vijana wa Tanzania na sio wa chama hiki au kile watajenga Uzalendo na Utanzania wao kuwa madhubuti zaidi kuliko vinginevyo.
Taasisi kama JKT iliundwa makusudi kuwaleta pamoja vijana wa Kitanzania na kuwafanya wote (masikini kwa tajiri,dini mbalimbali, kabila mbalimbali) kujiona wao ni Watanzania kwanza juu ya kitu kingine. Tukiiachia fursa hii kupotea tutakuja ijutia baadaye.
Nimalizie kwa kusema kwamba, Tanzania haijafikia zilipofikia nchi za Maghreb lakini hatuko mbali sana kama tusipoamka na kubadili muundo wa serikali, mifumo ya uendeshaji nchi, matumizi ya rasilimali za nchi na kuacha kuwatanguliza matajiri, wanasiasa na wageni mbele badala ya kumtanguliza Mtanzania mzawa kwanza.
Ni lazima pia tufanye mambo yetu tofauti na watu wengine. Utofauti huu peke yake ndiyo unaoweza kutufanya tuwe tofauti na pengine kufanikiwa kwa haraka zaidi kuliko Waafrika wengine. Tuna mbegu, ardhi na maji tosha kupanda na kuvuna nchi yenye amani, mshikamano na maendeleo kwa wote. Watakaosababisha mambo kuwa kinyume cha hivyo wamo miongoni mwetu na ni wale wasiojua nchi hii na watu wake wanatakiwa waelekee wapi!
Kila mtu anaafiki Tanzania ina viungo vyote nchi inayohitaji kuandaa pilau safi ya ustawi jamii; uchumi imara; lugha ya Kiswahili inayoweza kumfundisha Mtanzania kila kitu chini ya mbingu; ustaarabu; miji safi na yenye mvuto kwa walio ndani na nje; kilimo kinachotutosheleza na ziada kupatikana; viwanda maridhia kukidhi mahitaji yetu ya ndani na ya nje; utalii wenye vivutio aali na vingine vya kutengnezwa an watu; taasisi za elimu zinazovutia walimu na wanafunzi toka nje, hospitali zinazovutia madaktari na wagonjwa toka nje, migodi ya madini na mali asili zinazoweza kupunguza nusu ya umaskini wetu na masoko na biashara zinazoweza kutufanya wafanyabiashara bora Afrika na kwingineko -ila kinachokosekana ni wapishi wanaoweza kuikubali kazi yao ya upishi wakakaa jikoni kwa muda unaohitajika na sio kama viongozi wetu ambao wanausahau upishi wao na kukaa mezani chakula hicho kipikwe sijui na nani?
Subscribe to:
Posts (Atom)