NI CHINI ya asilimia 5 ya Watanzania wanaolalamikia tatizo la Umeme nchini. Asilimia 95 ya Watanzania hawana sababu ya kulalamika kwa sababu miaka 50 baada ya Uhuru hawana wala hawamo katika mpango wa kupata umeme.
Kwa hiyo, mgao wa umeme unaoendelea, na jinsi tatizo hilo lilivyopata wapiga makelele mbalimbali toka ndani na nje ya nchi, upo uwezekano mkubwa kwamba ufumbuzi wake uanweza ukawa pia ni ufumbuzi wa asilimia 95 ya Watanzania waliosahaulika nao kupata umeme. Kama laana yao kwa asilimia 5 ya wanaonufaika na matunda ya uhuru wa nchi hii itasitishwa.
Inavyoelekea bado tatizo la umeme linaloikumba Tanzania kwa hivi sasa halijaweleka na wote, yaani, viongozi na wananchi. Katika hali kama hii ni vigumu kuona mwanga upande wa pili wa pango, hususan, kuhusiana na uwezekano wa suala hilo kupata ufumbuzi bila kuchelewa mambo yakaharibika zaidi kuliko ilivyo sasa, kisiasa na kiuchumi.
Maana tatizo letu kama nchi nyingi za Kiafrika ni lile la kushindwa kuwa na miundo na mifumo inayofanya kazi kwa sababu mbalimbali zikiwemo zile za nchi kuongozwa kwa kufuata mipango, ahadi na misaada kutoka nje. Na kushindwa kabisa kujikwanyua toka kwenye makucha ya ubepari mamboleo, matapeli wa kimataifa na mabwana wa watwana. Uongozi wowote unaojenga tabia ya ombaomba, hujenga nchi ya ombaomba. Nyumba au uongozi wowote unaojivuna na unaothamini watu wake kikwelikweli hukataa kujenga tabia ya ombaomba. Watazame ombaomba mitaani Dar es salaam na familia zao ujiulize kama watu hawa kweli wanaweza kuja kubadilika baadaye. Haiwezekani. Badala yake ,hujenga tabia ya kupenda kujitegemea, kukinaishwa na kusaidiwa na kujivunia kama wenzetu wa Korea ya Kaskazini walivyofanya kunako miaka ya 1950 pale walipotengeneza trekta lao wenyewe la kwanza na badala ya kwenda mbele, gia zote zikawa ni za rivasi tu.
Kiongozi yeyote anayewadharau raia wake: kwa kuwaita wavivu, wezi, wategaji, wababaishaji atambue sio raia wake wenye tatizo bali ni yeye mwenye tatizo. Kwa kifupi, mdharau chake na kuthamini wengine na vya wengine hawezi kamwe kuwa kiongozi wa kutumaniwa wala kutegemewa kuleta mabadiliko ya kimsingi katika jamii husika. China au Korea Kusini au Brazl au India au Malaysia -ingelifanya hivyo, isingekua hapo ilipo leo.
Kuwathamini kupindukia watu toka nje na kutowathmini ipasavyo raia wako mwenyewe ni mwanzo wa jengo la nchi lisilo na msingi madhubuti.
Haya ni mambo yaliyotufikisha hapa tulipo ambapo leo pamoja na kuwa na wasomi wa masuala ya umeme na nishati, hawatumiki kwa ajili hiyo, na wanaofanya maamuzi juu ya masulala hayo ni wanasiasa ambao bila shaka ni mbumbumbu katika masuala hayo na uelewa wao unategemea maelezo wanayopata kutoka kwa wanaojua wanachokizungumza.
Aidha, kutokana na hayo hapo juu imekuwa vigumu kwetu kupambanua kati ya yale ambayo tunatakiwa tuyafanye sisi wenyewe ima-fa-ima na yale ambayo kwa sababu fulani fulani tunalazimika kuomba msaada au ushirikiano toka kwa wengine.
Hakuna asiyetambua kwamba, ili tuendelee nchi yetu inahitaji : chakula, maji; hewa safi; mazinigira salama; afya bora na usalama kwa watu wetu; umeme au nishati mbadala; reli ya kisasa; barabara zinazopitika bila usumbufu wakati wote; makazi bora kwa watu; usafiri wa anga na majini; masoko yanayofikika ndani na nje ya nchi; ushauri mzuri kwa waliotutangulia; utafiti na kuyaelezea kwa urahisi masuala mbalimbali ili yaeleweke na wengi nchini na elimu inayosaidia kutatua matatizo yetu au kutumia fursa za maendeleo zilizopo ndani ya mipaka yetu na nje ya mipaka yetu.
Tujihusishe na hili suala la umeme tu na hayo mengine tuyaache hadi wakati mwingine. Inshallah. Kuna vitu ambavyo 'piga-ua' ni lazima Watanzania waiunde au watengeneze wao wenyewe kwa kutumia watu wetu waliosoma na wasiosoma ili mradi ni wabunifu, watundu na wanaoweza kujaribu bila kukatishwa tamaa na kushindwa katika maisha yao yote. Hata wakishindwa mara ngapi! Na mimi siamini kama tukiwatumia wasomi wetu, wataalamu wetu, mameneja wetu, wanajeshi wetu na vijana wetu kikamilifu tuna sababu ya kushindwa zaidi ya mara mbili tatu tu! Tunashindwa kwa sababu hatuwatumii watu wetu ipasavyo! Tunashindwa kwa sababu wanasiasa wetu wamejifanya pia wao ndio wataalamu na magwiji wa uchumi na maendeleo ya jamii.
Lakini kama tutawatumia maprofesa wetu wa vyuo vikuu na wanafunzi wao katika taaluma ya umeme na nishati sio tu tunaweza kupata ufumbuzi wa muda mfupi bali wa kudumu wa matatizo yetu.
Ni kitu cha kuhuzunisha kuwa pengine kutokana na viongozi wetu wa vyuo vikuu kujikita zaidi kwenye siasa badala ya uchumi na uzalishaji mali, mahala kama Chuo Kikuu cha Dar es salaam, chenye idara ya Uhandisi wa umeme hakina mifano yoyote inayofanya kazi kama vile mashamba ya upepo wa umeme au ya solar energy au uzalishaji umeme kwa njia nyingine mikoani - na inayoweza kulipiwa na kufadhalilwa na kupanuliwa kukidhi mahitaji yetu ya umeme.
Msiba mmoja mkubwa kwa taifa letu ni lile la kuwa na elimu na wasomi wanaojengwa ili na wao kutegemea vitu na mitambo inayozalishwa nje kwa maendeleo ya watu na nchi yetu.
Ni kwa njia hii tu ndiyo tutaweza kupata maendeleo ya kweli, ya kudumu na endelevu na sio kwa kutegemea kila kitu kitoke kwa wengine.
Vitu hivyo ni pamoja na mashine na mitambo kwa ajili ya uzalishaji umeme; utekaji, uvutaji na usmbazaji na umwagiliaji maji; uchimbaji madini; ujenzi wa bandari; ujenzi wa reli; ujenzi wa viwanja vya ndege; ujenzi wa barabara; ujenzi wa madaraja; miundombinu ya mawasiliano; na zana au vifaa mbalimbali vinavyohitajika katika ujenzi wa majengo na makazi katika nchi.
Msingi wa nchi yoyote usipoanzia katika mambo hayo hapo juu, nchi haiwezi kamwe kuuacha umaskini, achilia kuwa na maendeleo endelevu. Mpango na mkakati wowote unaoshindwa kuibua mambo haya, kisha kuyatafakari, kuyainisha na kuyapa kipaumbele katika maendeleo ya nchi ni mpango au mkakati unaofaa kutupwa jalalani pindi unapogundulika kwamba upo na unagharamiwa na kodi za wananchi. Ni mpango unaoihukumu nchi kubaki kwenye makucha ya wakoloni, mabepari na mabeberu kwa faida zao na wala sio kwa faida ya nchi na watu wake. Ni mapango unaowalazimisha watu wa nchi fulani wawe ombaomba, huku rasilimali za nchi zikichotwa kwenda kuwafanya watoa sadaka matajiri na matajiri zaidi. Ni mpango na mkakati unaomfanya raia wa nchi hii kuwa mtumwa wa wakoloni wa zamani na vibarakala wao na utandawazi na mumiani wake.
Kwa maneno mengine matatizo yetu mengi, likiwemo hilo la umeme ni matatizo yanayoweza kupatiwa ufumbuzi wa haraka na kudumu kwa kutumia vyema rasilimali watu yetu na rasimali watu toka nje pamoja na matumizi sahihi ya rasilimali zetu nyingine.
Hili linaweza kufaulu tu katika nchi ambayo haijvunii na haiwalindi mafisadi kama sehemu ya uongozi wake; inayotambua maendeleo yetu kama rasilimali zetu zinatumika vizuri, yanaweza kugharamiwa na watakaopata ujuzi na uzoefu katika mipango yetu mbalimbali ya maendeleo nchini, wakati watakapokwenda kuwafanyia Waafrika wengine kazi kama hii. Fisadi wa Kitanzania, ni mwizi anayejiibia shati lake mwenyewe. Fisadi wa kimataifa, haibi cha ndani, hukwapua cha nje kuja kuwafaa wenzake walio nyumbani na sio vinginevyo. Na uwezo wa kutajirika kwa kutumia rasilimali za wengine, ikiwa ni pamoja na umeme, kutokana na nchi zinazotuzunguka Watanzania tunao, isipokuwa hatuna uongozi unaoona wala kuelewa hili.
Vilevile, hili huweza kufanyika tu katika nchi ambayo chama tawala hakiendeshi nchi kana kwamba ni wabunge wake tu na wanachama wake wenye uwezo wa kuwa mawaziri, wakuu wa mikoa, wakuu wa wilaya, makatibu wakuu, wakurugenzi, mamaneja, majaji, mabalozi na wafanyakazi nchi za nje na wasimamizi wa taasisi mbalimbali. Bali kinaendesha nchi kwa kutumia akili, uwezo na michango ya Watanzania wote bila kujali ni wafuasi wa chama tawala au la.
Miaka hamsini baada ya Uhuru dunia imeipa fursa kubwa nchi yetu ya kuchagua na kuwakaribisha wataalamu tofauti toka sehemu mbalimbali duniani wenye ujuzi na uzoefu wa kila aina kuanzia watengnenezaji baiskeli hadi waunda satelaiti na roketi. Hawa ni binadamu wenzetu amabo leo ni 'jobless' pamoja na utaalamu au elimu na uzoefu wao, walioko huko Marekani, Ulaya Magharibi, Ulaya Mashariki, Marekani ya Kusini na Asia. Watu ambao tukiwapatia nyumba, gari na mshahara wa kukidhi mahitaji yao ya msingi wapo tayari kuja nchini hapa kusaidiana na sisi kuifanya nchi yetu iendelee kwa kasi na haraka zaidi. Kinachotakiwa ni kutambua hili na kujipanga kulishughulikia kwa namna ambayo litakuwa ni la faida kwetu sote, kwao na sisi kadhalika. Ni rahisi, kulizungumza hili kwa maneno, lakini ukweli ni kwmba kwa uoga, uziwi na upofu wa viongozi wetu hususan kuhusiana na yale yanayoandikwa na magazeti ni GUMU KAMA GAMBA LA KOBE.
Ila kwa bahati nzuri, kutokana na kukua kwa demokrasia nchini hapa upo uwezekano kwamba hili likifumbiwa macho na watawala, haliwezi kuachwa kuokotwa na wapinzani na wanaharakati wengine wenye mapenzi ya dhati ya nchi yao na uchungu na umasikini wa wananchi wenzao.
Sunday, July 24, 2011
Umeme: Mipango, mikakati na nishati mbadala muhimu
Katika miaka hii ambayo hali ya hewa inaendelea kubadilika na hatuna ahadi wala uhakika na mvua na kwa hiyo maji yanayotiririka katika mito na mabwawa tuliyoandaa kuzalisha umeme ni makosa makubwa kuendelea kutegemea umeme wa tabaini zinazoendeshwa na maji.
Hali yetu kama nchi sasa ni afadhali ukilinganisha na Somalia. Lakini upo uwezekano mkubwa wa ukame ulioikumba nchi hii iliyo kaskazini ya Tanzania na Kenya pia kuikumba nchi yetu.
Kutokana na ukweli huu, wale wanaoshika nafasi za uongozi nchini wanapaswa kuona mbali na mbele zaidi kuliko mwananchi wa kawaida.
Tatizo letu kwa hiyo siyo tu tatizo la ukame na kukosa mvua na maji ya kuzalisha umeme bali pia ni upungufu wa mipango na mikakati ya upatikanaji nishati ya uhakika na isiyoathirika na hali ya hewa kwa kadri inavyobadilika.
Tatizo pacha ni lile la serikali kudharau na kupuuza ushauri wa watu mbalimbali kuhusiana na muundo, kazi na nafasi ya shirka la umeme la taifa (TANESCO) katika kutafuta jawabu kamili na la kuridhisha la tatizo la umeme nchini.Shirika ambalo hivi leo limebatizwa na kuitwa 'TANZANIA ELELCTRIC SUFFOCATION COMPANY'- Ni dhahiri kwamba shirika ambalo miaka 50 baada ya uhuru limeweza kuwapatia asilimia 5 tu ya Watanzania umeme halina akili wala uwezo wa kufanya makubwa zaidi ya hayo ambayo tayari limekwishayafanya. Limefikia upeo wa uwezo na ubunifu wake.
Uendeshaji wa mashirika ya umma umefanana na ule wa mzazi ambaye alimshonea mwanaye suti akiwa na miaka 10 na leo mtoto huyo ambaye ana miaka 20 eti anatakiwa kuvaa suti ileile aliyoivaa akiwa na miaka 10. Watanzania tulikuwa milioni 9 mwaka 1960. Tuliyoyafanya wakati huo hayawezi kufanywa miaka hamsini baadaye na tukiwa takriban Watanzania milioni hamsini.
Baadhi ya watu wameshawahi shirika hilo livunjwe katika sehemu nne. Uzalishaji umeme, usambazaji umeme, utengenezaji vifaa vya umeme na uunganishaji na uhudumiaji miundo-mbinu ya umeme. Na sio lazima kufanya kazi zote hizi, bali shirika/serikali iruhusu Watanzania binafsi, wanajamii na wawekezaji kuendesha shughuli hizo kwa ufanisi na ufanifu zaidi.
Wapo pia waliopendekeza kwamba kila mkoa uwe na shirika lake la umeme, badala ya kuwa na shirika la umeme la taifa, kwa kutumia rasilimali za mkoa na ubia na wawekezaji wa ndani na nje. Hawa waliamini katika falsafa ya Schumacher kwamba 'Kidogo ni kizuri na chema zaidi,' au kwa Kiingereza: 'Small is Beautiful.' Kilal mkoa ungelitafuta chanzo chake binafsi cha uzalishaji umeme bila ya kutegemea tu maji. Hili lingeliendana pia na kifungu cha katiba kinachohusiana na kuwepo na ulinganifu katika maendeleo ya taifa-kitu ambacho kimeshindikana kabisa katika sekta hii ya nishati.
Niliposikiliza mahojiano ya Mh. Jakaya Kikwete na BBC akiwa ziarani Afrika Kusini sikuweza kuacha kuona kwamba majibu yake hayakuwa yenye kuonesha imani na matumaini kwamba tatizo la umeme liko ndani ya mikono ya Watanzania . Kilichojitokeza ni kwamba ni serikali ndiyo tu iliyokuwa ikitarajiwa kulitatua tatizo hilo. Aidha, serikali ilikuwa inapaswa kulipa fedha zote za ununuzi wa mitambo ya uzalishaji umeme papo kwa hapo. Kitu ambacho sio sahihi.
Ninaamini, Watanzania wakihamasishwa kama walivyokatwa kodi na haki zao mbalimbali ili kuanzisha mashirika ya umma (yaliyokuja kubinafsishwa bila wao kulipwa chochote) wana sababu, uwezo na nia ya kuchangia kumaliza tatizo la umeme lakini kwa sharti kuwa wanakuwa nao ni wamiliki wa mashirika yatakayoanzishwa kama sehemu ya ufumbuzi wa tatizo hili.
Vilevile, watengenezaji wa mitambo ya umeme wako tayari kukodisha mitambo yao na vile vile kuuza mitambo hiyo kwa mtu kulipia kidogo kidogo hadi deni liishe.
Hata hivyo kinachoonekan hapa ni kuwa mtazamo wa ndani kwa suala hili haupo na badala yake tuna mtazamo wa nje tu. Ikiwa ni pamoja na kuamini kuwa ni lazima tupate msaada au tukope kutoka nje ili tatizo la umeme liishe hapa nchini. Au wakati mwingine, pengine ni ujanja wa kununua vikubwa vikubwa kwa gharama kubwa ili watu wapate chambele au teni pasenti yao.
Sikubaliani kabisa na wale wanaoamini kwamba tatizo la umeme limesababishwa na ufisadi na eti kuna wauza majenereta walioihona serikali ili biashara yao ya majenereta ichanganye vilivyo. Japo kuwa majenereta yanauzwa kwa fujo hivi leo, lakini adha na gharama za uendeshaji majenereta ikiwemo kwa taasisi za serikali pia, kama vile gharama za dizeli au petroli; kelele; uchafu wa mazingira; nguvu kazi ya ziada katika kuzihudumia
ni mambo yanayoitia hoja hiyo hapo juu mashakani.
Uwekezaji katika sekta hii ya umeme unawezekana kabisa kutokea ndani ya nchi. Kwa maana kwamba, kama serikali ilivyoanzisha mashirika kwa kutumia kodi za wananchi upo uwezekano wa wananchi na wawekezaji kuchangia asilimia fulani na wawekezaji wa nje wakachangia asilimia fulani. Inapendekezwa ili makampuni ya umeme yawe ni ya Watanzania basi Watanzania wamiliki asilimia 51-60 na wawekezaji toka kwingineko asilimia 40-49.
Ufumbuzi wa tatizo la umeme, hali kadhalika, utakuwa mgumu bila kufahamu mchango wa siasa katika udhairu, kudumaa na kuserereka kwa TANESCO pamoja na misaada yote ambayo shirika hili limekuwa likipata toka kwa wafadhili wa nje na malipo ya gharama kubwa za umeme kuliko nchi nyingine yoyote Afrika. Wapo wanaodai kwamba shirika hilo liligeuzwa shamba la bibi na baadhi ya wanasiasa. Kwa maneno machache, shirika hilo, halijawahi kuendeshwa kibiashara bila kuingiliwa na wanasiasa. Pamoja na mifano mingi ya uwezo mdogo wa mameneja wa Kitanzania kusimamia miradi mikubwa hazijafanyika jitihada za dhati kumpata meneja toka nje mwenye uwezo na dhati ya kutusaidia Watanzania tuondokane na tatizo hili la umeme. Netsolution, kwa kiasi kikubwa, ilikuwa ni 'dili' lililonufaisha watu binafsi na sio nchi na watu wake.
Vilevile, wanasiasa Tanzania wamejenga tabia ya kuingilia kila fani na kazi nchini na kujifanya wao ni wataalamu zaidi kuliko wataalamu wenyewe. Toka mgao huu wa umeme pamoja na kuwa na vyuo vikuu vinavyotoa shahada mbalimbali za masuala ya umeme hapajawahikuendeshwa warsha au kongamano au angalau semina yoyote iliyowashsirikisha ili michango yao kuhusu ufumbuzi wa tatizo la umeme nchini lipatikane. Hii ni kasoro kubwa sana nchi mwetu, na isipoangaliwa itatuumiza katika kila sekta na nyanja ya maendeleo kwa miaka mingi ijayo.
Kama walivyo wanafunzi wa masomo mengine, wanafunzi wa shahada za uhandisi Tanzania hawapewi fursa za kutosha kutumia elimu yao kwa utafiti na uvumbuzi kwa majibu ya matatizo yetu mbalimbali. Bajeti yetu katika kuchochea utafiti ni ndogo mno, na sidhani kuna bajeti yoyote ya kuhamasisha ubunifu na uvumbuzi nchini miongoni mwa wasomi na wasiokuwa wasomi.
Wakati vijana wa Kenya wanagundua njia mbalimbali za kuzalisha umeme ikiwemo wa kutumia magurudumu ya baiskeli, umeme kwa upepe na sasa umeme kwa chupa ya cocacola na maji, vijana wa Kitanzania wamezungushiwa kitanzi shingoni mwao kinachowatia uoga katika kuanzisha au kuunda kitu chochote kinachoweza kuwa na manufaa kwa jamii yao. Na sio suala la ujinga au kutokujua. Ni kwamba wazazi wao na serikali yao haijakaa mkao wa kudai na kupata kutoka kwa kizazi hiki kipya zaidi ya muziki wa kuiga toka Marekani au kuvaa katakei!
Kati ya vijana wasiosoma sana ni wale ambao wameshawahi kuunda redio, kompyuta, gari, ndege, helikopta, transmita za redio na kadhalika. Lakini kwa kuwa baba na mama zao sio watu wakubwa, vijana hawa wameishia kutishiwa na vyombo vya dola hadi kujenga uoga mkubwa wa kuwa wabunifu na wavumbuzi wa kitu chochote katika maisha yao yaliyobakia. Ni nani anayekosa hapa. Tanzania au mtoto anayehusika?
Hebu, chunguza wewe mwenyewe katika nchi ambayo magazeti yametoa habari za watoto au vijana waliovumbua vitu mbalimbali, je, leo hao watoto wako wapi. Wamesaidiwa au wamehujumiwa, kwa kuwa tu ni watoto wa watu wasiokuwa na uwezo?
Hali yetu kama nchi sasa ni afadhali ukilinganisha na Somalia. Lakini upo uwezekano mkubwa wa ukame ulioikumba nchi hii iliyo kaskazini ya Tanzania na Kenya pia kuikumba nchi yetu.
Kutokana na ukweli huu, wale wanaoshika nafasi za uongozi nchini wanapaswa kuona mbali na mbele zaidi kuliko mwananchi wa kawaida.
Tatizo letu kwa hiyo siyo tu tatizo la ukame na kukosa mvua na maji ya kuzalisha umeme bali pia ni upungufu wa mipango na mikakati ya upatikanaji nishati ya uhakika na isiyoathirika na hali ya hewa kwa kadri inavyobadilika.
Tatizo pacha ni lile la serikali kudharau na kupuuza ushauri wa watu mbalimbali kuhusiana na muundo, kazi na nafasi ya shirka la umeme la taifa (TANESCO) katika kutafuta jawabu kamili na la kuridhisha la tatizo la umeme nchini.Shirika ambalo hivi leo limebatizwa na kuitwa 'TANZANIA ELELCTRIC SUFFOCATION COMPANY'- Ni dhahiri kwamba shirika ambalo miaka 50 baada ya uhuru limeweza kuwapatia asilimia 5 tu ya Watanzania umeme halina akili wala uwezo wa kufanya makubwa zaidi ya hayo ambayo tayari limekwishayafanya. Limefikia upeo wa uwezo na ubunifu wake.
Uendeshaji wa mashirika ya umma umefanana na ule wa mzazi ambaye alimshonea mwanaye suti akiwa na miaka 10 na leo mtoto huyo ambaye ana miaka 20 eti anatakiwa kuvaa suti ileile aliyoivaa akiwa na miaka 10. Watanzania tulikuwa milioni 9 mwaka 1960. Tuliyoyafanya wakati huo hayawezi kufanywa miaka hamsini baadaye na tukiwa takriban Watanzania milioni hamsini.
Baadhi ya watu wameshawahi shirika hilo livunjwe katika sehemu nne. Uzalishaji umeme, usambazaji umeme, utengenezaji vifaa vya umeme na uunganishaji na uhudumiaji miundo-mbinu ya umeme. Na sio lazima kufanya kazi zote hizi, bali shirika/serikali iruhusu Watanzania binafsi, wanajamii na wawekezaji kuendesha shughuli hizo kwa ufanisi na ufanifu zaidi.
Wapo pia waliopendekeza kwamba kila mkoa uwe na shirika lake la umeme, badala ya kuwa na shirika la umeme la taifa, kwa kutumia rasilimali za mkoa na ubia na wawekezaji wa ndani na nje. Hawa waliamini katika falsafa ya Schumacher kwamba 'Kidogo ni kizuri na chema zaidi,' au kwa Kiingereza: 'Small is Beautiful.' Kilal mkoa ungelitafuta chanzo chake binafsi cha uzalishaji umeme bila ya kutegemea tu maji. Hili lingeliendana pia na kifungu cha katiba kinachohusiana na kuwepo na ulinganifu katika maendeleo ya taifa-kitu ambacho kimeshindikana kabisa katika sekta hii ya nishati.
Niliposikiliza mahojiano ya Mh. Jakaya Kikwete na BBC akiwa ziarani Afrika Kusini sikuweza kuacha kuona kwamba majibu yake hayakuwa yenye kuonesha imani na matumaini kwamba tatizo la umeme liko ndani ya mikono ya Watanzania . Kilichojitokeza ni kwamba ni serikali ndiyo tu iliyokuwa ikitarajiwa kulitatua tatizo hilo. Aidha, serikali ilikuwa inapaswa kulipa fedha zote za ununuzi wa mitambo ya uzalishaji umeme papo kwa hapo. Kitu ambacho sio sahihi.
Ninaamini, Watanzania wakihamasishwa kama walivyokatwa kodi na haki zao mbalimbali ili kuanzisha mashirika ya umma (yaliyokuja kubinafsishwa bila wao kulipwa chochote) wana sababu, uwezo na nia ya kuchangia kumaliza tatizo la umeme lakini kwa sharti kuwa wanakuwa nao ni wamiliki wa mashirika yatakayoanzishwa kama sehemu ya ufumbuzi wa tatizo hili.
Vilevile, watengenezaji wa mitambo ya umeme wako tayari kukodisha mitambo yao na vile vile kuuza mitambo hiyo kwa mtu kulipia kidogo kidogo hadi deni liishe.
Hata hivyo kinachoonekan hapa ni kuwa mtazamo wa ndani kwa suala hili haupo na badala yake tuna mtazamo wa nje tu. Ikiwa ni pamoja na kuamini kuwa ni lazima tupate msaada au tukope kutoka nje ili tatizo la umeme liishe hapa nchini. Au wakati mwingine, pengine ni ujanja wa kununua vikubwa vikubwa kwa gharama kubwa ili watu wapate chambele au teni pasenti yao.
Sikubaliani kabisa na wale wanaoamini kwamba tatizo la umeme limesababishwa na ufisadi na eti kuna wauza majenereta walioihona serikali ili biashara yao ya majenereta ichanganye vilivyo. Japo kuwa majenereta yanauzwa kwa fujo hivi leo, lakini adha na gharama za uendeshaji majenereta ikiwemo kwa taasisi za serikali pia, kama vile gharama za dizeli au petroli; kelele; uchafu wa mazingira; nguvu kazi ya ziada katika kuzihudumia
ni mambo yanayoitia hoja hiyo hapo juu mashakani.
Uwekezaji katika sekta hii ya umeme unawezekana kabisa kutokea ndani ya nchi. Kwa maana kwamba, kama serikali ilivyoanzisha mashirika kwa kutumia kodi za wananchi upo uwezekano wa wananchi na wawekezaji kuchangia asilimia fulani na wawekezaji wa nje wakachangia asilimia fulani. Inapendekezwa ili makampuni ya umeme yawe ni ya Watanzania basi Watanzania wamiliki asilimia 51-60 na wawekezaji toka kwingineko asilimia 40-49.
Ufumbuzi wa tatizo la umeme, hali kadhalika, utakuwa mgumu bila kufahamu mchango wa siasa katika udhairu, kudumaa na kuserereka kwa TANESCO pamoja na misaada yote ambayo shirika hili limekuwa likipata toka kwa wafadhili wa nje na malipo ya gharama kubwa za umeme kuliko nchi nyingine yoyote Afrika. Wapo wanaodai kwamba shirika hilo liligeuzwa shamba la bibi na baadhi ya wanasiasa. Kwa maneno machache, shirika hilo, halijawahi kuendeshwa kibiashara bila kuingiliwa na wanasiasa. Pamoja na mifano mingi ya uwezo mdogo wa mameneja wa Kitanzania kusimamia miradi mikubwa hazijafanyika jitihada za dhati kumpata meneja toka nje mwenye uwezo na dhati ya kutusaidia Watanzania tuondokane na tatizo hili la umeme. Netsolution, kwa kiasi kikubwa, ilikuwa ni 'dili' lililonufaisha watu binafsi na sio nchi na watu wake.
Vilevile, wanasiasa Tanzania wamejenga tabia ya kuingilia kila fani na kazi nchini na kujifanya wao ni wataalamu zaidi kuliko wataalamu wenyewe. Toka mgao huu wa umeme pamoja na kuwa na vyuo vikuu vinavyotoa shahada mbalimbali za masuala ya umeme hapajawahikuendeshwa warsha au kongamano au angalau semina yoyote iliyowashsirikisha ili michango yao kuhusu ufumbuzi wa tatizo la umeme nchini lipatikane. Hii ni kasoro kubwa sana nchi mwetu, na isipoangaliwa itatuumiza katika kila sekta na nyanja ya maendeleo kwa miaka mingi ijayo.
Kama walivyo wanafunzi wa masomo mengine, wanafunzi wa shahada za uhandisi Tanzania hawapewi fursa za kutosha kutumia elimu yao kwa utafiti na uvumbuzi kwa majibu ya matatizo yetu mbalimbali. Bajeti yetu katika kuchochea utafiti ni ndogo mno, na sidhani kuna bajeti yoyote ya kuhamasisha ubunifu na uvumbuzi nchini miongoni mwa wasomi na wasiokuwa wasomi.
Wakati vijana wa Kenya wanagundua njia mbalimbali za kuzalisha umeme ikiwemo wa kutumia magurudumu ya baiskeli, umeme kwa upepe na sasa umeme kwa chupa ya cocacola na maji, vijana wa Kitanzania wamezungushiwa kitanzi shingoni mwao kinachowatia uoga katika kuanzisha au kuunda kitu chochote kinachoweza kuwa na manufaa kwa jamii yao. Na sio suala la ujinga au kutokujua. Ni kwamba wazazi wao na serikali yao haijakaa mkao wa kudai na kupata kutoka kwa kizazi hiki kipya zaidi ya muziki wa kuiga toka Marekani au kuvaa katakei!
Kati ya vijana wasiosoma sana ni wale ambao wameshawahi kuunda redio, kompyuta, gari, ndege, helikopta, transmita za redio na kadhalika. Lakini kwa kuwa baba na mama zao sio watu wakubwa, vijana hawa wameishia kutishiwa na vyombo vya dola hadi kujenga uoga mkubwa wa kuwa wabunifu na wavumbuzi wa kitu chochote katika maisha yao yaliyobakia. Ni nani anayekosa hapa. Tanzania au mtoto anayehusika?
Hebu, chunguza wewe mwenyewe katika nchi ambayo magazeti yametoa habari za watoto au vijana waliovumbua vitu mbalimbali, je, leo hao watoto wako wapi. Wamesaidiwa au wamehujumiwa, kwa kuwa tu ni watoto wa watu wasiokuwa na uwezo?
Umeme: Jamii na watu binafsi waaminiwe katika kutafuta ufumbuzi
Nchi zetu za Kiafrika zimejenga utaratibu unaowafanya wananchi waamini kwamba bila serikali matatizo yao hayawezi kutatuliwa. Serikali inaonekana kujua kila kitu,kuwa na fedha zote duniani na kuwa bila mkono au mguu wa serikali hakuna anayeweza kusogea kwenda popote. Na serikali kwa upande wake inaelekea kuamini na kudhani ndiyo peke yake yenye majibu ya matatizo yote ya kiuchumi, kijamii, kisiasa, kiutamaduni na kiteknolojia. Kitu ambacho si kweli.
Guru wa Menejimenti, Profesa Peter Drucker anasema meneja mzuri na anayefanya kazi kwelikweli, hafanyi kazi yoyote. Ndivyo ilivyo pia kwa serikali nzuri na inayofanya kazi kwelikweli. Haifanyi kazi. Tunaposema haifanyi kazi hatuna maana haifanyi chochote au inategea tu. La hasha. Meneja na serikali bora na mfano wa kuigwa hufnaya kazi kwa kupitia watu, idara na taasisi nyingine. Unapoingilia kufanya kazi za watu wengine, idara na taasisi nyingine badla aya wao kuzifanya wenyewe kuna uwezekano mkubwa wa wewe kuvuruga kazi hizo au kutokuwa na tija linganifu wala ufanifu na ufanisi. Ni vizuri viongozi na mameneja wetu walielewe hili na wajipime na kuona kama kweli wanafanya kile ambacho kiongozi au meneja anachotakiwa kukifanya na sio kufanya anayoweza kufanya karani au tarishi. Kama sio waziri au mbunge au mkuu wa mkoa kama sio mkuu wa wilaya.
Tujiulize ni nini nafasi ya jamii katika ufumbuzi wa tatizo la umeme nchini Tanzania. Hivi leo, Benki ya dunia inamwaga misaada kwa ajili ya uanzishwaji wa miradi mbalimbali ya kijamii, jambo linaloashiria uwezekano wa kushirikiana na benki hiyo kuziwezesha jamii mbalimbali kuja na mawazo na mapendekezo kuhusiana na jinsi wanajamii wenyewe wanavyoweza kuchangia katika uzalishaji umeme nchini bila ya kutegemea sana wawekezaji toka nje. Maana wawekezaji hawaji kujenga miundombinu bali kuwekeza katika biashara au uzalishaji mali kwenye eneo walilojikita. Mjenzi wa miundombinu yetu ni lazima awe Mtanzania mwenyewe, mwanajamii katika jamii husika.
Wanajamii wa maeneo mbalimbali nchini hivi leo wanasita kujiunga na shughuli yoyote inayonukia ujamaaujamaa au ushirka ushrika kwani dhana hizo zilichakachuliwa vibaya mno na viongozi waliokuwa chini ya Mwalimu Nyerere. Ni yeye tu inaelekea alikuwa na nia safi na nzuri ya kubadili maisha ya Watanzania na sio wengine, na kama walikuwepo walikuwa wachache sana na walisakamwa kupita kiasi na mafisadi na walilia ubepari wa wakati huo.
Ni vyema pia kuzijua njia mbalimbali za kuzalisha umeme. Kisha kuainisha ni ipi au zipi ambazo zinaweza katika muda mfupi kutupa nafuu katika tatizo hili na zile ambazo zinahitaji muda na uwekezaji mkubwa zaidi.
Ziko njia mbalimbali za kuzalsha umeme zinazojulikana kufikia sasa. Njia hizo ni pamoja na mchakato wa nyuklia; samadi na takataka mbalimbali; mvuke; mashamba ya umeme wa solar; mashamba ya umeme wa upepo; mafuta ya petroli au dizeli na maji.
Tanzania inasemekana haijafikia hali ya kujitosheleza kiuwezo na kiusalama kuzalisha umeme kwa mchakato wa uranium ijapo tumejaliwa madini hayo. Kwa hiyo, hii sio njia ya kutusaidia katika siku za karibu.
Umeme kwa maji ndio huo ambao unatuongezea umaskini, maafa na dhiki zisizokweisha.
Nao huu unaweza kurudia hali yake ya kawaida endapo mipango yetu ya uoteshai miti, utunzaji mazingira na vilivyomo na hususan kwenye maeneo ya vyanzo vya maji milimani au chini ardhini itafanikishwa.
Uzalishaji umeme kwa kutumia samadi na takataka mbalimbali; upepo; mafuta ya petroli au dizeli ndio njia zinazoweza kuchangia haraka zaidi kumaliza tatizo hili.
Kwa jiji kama Dar es salaam uzalishaji umeme kwa kutumia takataka ni kitu kinachowezekana. Na njia hii itaua ndege wawili kwa jiwe moja. Kwanza, utaongeza megawati za umeme kwenye mtandoa wa umeme na pili utafanya jiji hili kuwa safi daima.
Mashamba ya umeme wa solar na upepo kwenye mikoa yenye jua na upepo wa kutosha yanaweza kuchangia gridi ya taifa kwa megawati kadhaa.
Kwenye miji na wilaya ambazo zina upepo wa kutosha ni dhahiri tukishirikiana na nchi kama Denmark na Netherlands tunaweza kupata 'shortcut' za kupata mitambo na vifaa vinavyohitaji na kuzalisha umeme chini ya mwaka mmoja.
Umeme wa jenereta zinazotuchafulia hali ya hewa, mazingira na kutupigia makelele unastahili kudhibitiwa na kuvumuliwa tu kutokana na ukweli kuwa hakuna ujanja mwingine.
Mitaani ili tusichafue zaidi hali ya hewa ni vyema maduka au makampuni kadhaa yakaungana na kununua jenereta kubwa zinazoweza kutosheleza maduka au makampuni yote yaliyo sehemu hiyo badala ya kila mmoja kuwa na kijenereta chake na hivyo kusababisha uchafuzi mkubwa wa mazingira kwa moshi, kelele na hewa ya carbon monoxide.
Inafaa pia kuuliza kama nchi zilizotuzunguka, yaani, Msumbiji, Malawi, Zambia, Kongo Kinshasa, Rwanda (ambayo imefanya kazi nzuri sana katika upatikanaji umeme kwa watu wake), Burundi, Uganda na Kenya zina hali gani kiumeme na tunaweza kushirikiana nazo vipi ili tuzalishe umeme kwa pamoja utakaotusaidia sote kupunguza au kumaliza kabisa tatizo letu la umeme.
Maendeleo ni vigumu kupatikana bila kuwa na mipango mizuri inayotekelezeka. Ni heri nchi kupiga maktaimu kwa mwaka mmoja hata zaidi ili kwanza ihakikishe imejipanga vizuri kabla ya kuwa na mpango wowote wa maendeleo usiotekelezeka.
Katika hili ni muhimu kuona kwamba viongozi mbalimbali wa nchi hii wanawekwa kwa misingi ya kujenga na kuendeleza sehemu husika. Hii ina maana kazi ya mkuu wa shrika fulani, mathalani, TANESCO, lazima iwe ni kulitoa shirika hilo kwenye ngazi ya chini kwenda ngazi ya juu kiutendaji na kiufanisi.
Ndivyo ilivyo pia kwa mwenyekiti wa kijiji, katibu kata, kiongozi wa tarafa, mkuu wa wilaya, mkuu wa mkoa wanavyotakiwa kuwa. Baadhi ya matatizo yetu kama hili la umeme kama watu hawa wangeliachiwa kufanya kazi kama watu huru labda linaweza kumalizwa huko huko kwani wao wanajua eneo lao vyema zaidi kuliko viongozi wa kitaifa na mbunge asiyewatembelea hadi uchaguzi mkuu ujao.
Nilishawahi kuzungumzia kwamba ukiwa na kiongozi halafu kiongozi huyo hana tatizo analolitatua, wala haichangamkii fursa yoyote ili kuongeza kipato au kuyafanya maisha ya walio chini yake kuwa bora zaidi-ni sawa na kuwa na watu bila kiongozi.
Kadhalika, kama una shirika, wilaya, mkoa au wizara ambayo haijulikani inashughulikia tatizo gani au kuchangamkia fursa gani za kimaendeleo katika eneo husika, basi mahala hapo hakuna kiongozi. Kuna mtawala. Na kwa bahati mbaya viongozi wengi tuliokuwa nao hawastahili kuitwa viongzi bali watawala au magavana.
Tofauti ya kiongozi na mtawala ni kwamba, mtawala kazi yake ni kusimamia tu kile kilichopto, yaani, kile ambacho kimeshaanzishwa na wengine. Na sio jukumu lake kubadili chochote au kufanya kazi zaidi ya usimamizi na kutoa taarifa kwa wakubwa wake. Wakati kiongozi, ni mtu mwenye dhamana za kuleta mabadiliko toka hali duni kwenda hali bora zaidi. Kiongozi huonyesha kwa vitendo, hushauri, huelekeza, huelimisha, huwezesha na hutoa motisha ili walioko chini yake walete mabadiliko tarajiwa katika eneo husika.
Kiongozi tofauti na mtawala, huona mbali na mbele zaidi. Ni mtabiri wa namna fulani. Hufahamu fika kwamba haya ya kawaida watu walio chini yake wanayajua na wanaweza kuyashughulikia. Lakini yale ya mbele na yajayo na yasiyo tabirika ndio eneo la kuonesha uongozi wake.
Mathalani, mtawala huwaza jinsi ya kuwalisha watu wake leo leo. Wakati kiongozi anatakiwa kuwaza, kupanga na kuweka mikakati ya watu wake kupata chakula bila tatizo miaka mitano au kumi ijayo.
Mtawala huwaza kutatua tatizo la umeme leo leo, lakini kiongozi hutafakari, hupanga na kuweka mikakati inayouliza maswali ya msingi na yasiyo na majibu ya haraka. Kwa mfano, kama tutakuwa na ukame, yaani, mvua hazitanywesha na umeme wetu unategemea maji, ni njia gani mbadala tutakuwa nazo ili ukame na kukosa mvua kuisisababishe matatizo ya upatikanaji umeme.
Kiongozi mzuri huwatumia walio chini yake kutokana na uwezo na utalaamu walio nao bila kujali watokako wala udhaifu wao. Ubora na kile mtu anachoweza kukifanya katika kutimiza lengo lililoko mbele yake ndio kitu muhimu kuliko vyote. Na kiongozi bora, hatokei hata mara moja, kuwalaumu walio chini yake kwamba wameshindwa kazi fulani. Wakishindwa ina maana ni yeye ameshindwa na sio walio chini yake. Aghalabu, kiongozi mzuri na bora, huwaongoza watu kwa namna ambayo watu wao wanapofanikisha malengo fulani basi watu hao kwa pamoja husema, 'tumeweza, tumeshinda!' na sio kiongozi wetu ameweza, ameshinda!
Kiongozi bora na hususan akiwa wa wilaya au mkoa au nchi hupaswa kujua mambo ambayo mkoa wenyewe unastahili kutengeneza au kuzalisha na yale ambayo kwa muda fulani yapasa kuyapata toka kwa wengine.
Ni kichekesho kwa nchi kuwa na mpango unaotaka kuongeza asilimia ya nyumba zinazopata umeme toka asilimia 5 hadi asilimia ishirini na tano au hamsini, bila ya kuwa na mpango wa uzalishaji mashine, vifua umeme, mitambo na zanatepe mbalimbali zinazohitajika ili nchi yenyewe ijitegemee angalau kwa asilimia 80 kwa vitu vinavyohitajika kuzalisha, kusambaza na kuunganisha umeme nchini.
Kama nilivyodokeza huko nyuma, jambo hili sasa ni rahisi na jepesi kuliko wakati wowote katika historia ya nchi yetu na maendeleo yetu. Maana, hakuna sheria inayosema ili tuendelee lazima tuwatumie tu Watanzania au raia wetu hata kama hawajui na hawajasomea kazi inayotaka kufanyika. Na eti, hata kama kuna wahandisi au mafundi wa umeme,, maprofesa wa umeme, washauri, wanafunzi na watafiti wa masuala ya uzalishaji umeme wasio na kazi wala mafunzo kwa vitendo nchini na nchi za nje lazima tutegemee shirika moja tu nchini kutunusuru na balaa na maafa yanayoikumba nchi na watu wetu leo.
Kutokuona na kutozithamini na kutozitumia rasilimali watu zilizotapakaa huko Marekani, Ulaya Magharibi, Ulaya Mashariki, Russia ya zamani na kwingineko kutafuta ufumbuzi wa matatizo yetu mbalimbali ya kijamii, kiuchumi na kiteknolojia
ni jambo ambalo tutakaa na kuja kulijutia baada ya muda si mrefu kutoka sasa.
Miaka mingi iliyopita kulikuwa na Baba Baa na Baba Waa. Wote wawili walikuwa na mashamba makubwa yenye mimea ya kila aina pamoja na maeneo wazi, yaani, yasiyopandwa chochote. Msimu wa kilimo ulivyofika, Baba Baa alikuwa akiwatafuta vibarua wa kikwao tu, hakutaka wageni walime shamba lake. Aliamini hawajui kulima.Lakini mwenziwe Baba Waa aliwamwagia ajira Warundi, wamakonde, wasafwa, Wanyarandwa bila kubagua. Katika mchanganyiko huu wa watu wenye asili mbalimbali shamba la Baba Waa sio tu lililimwa vizuri bali lilinufaika na mimea mipya, njia mpya za kilimo, kama vile kupiga matuta na kadhalika. Hivi leo wajukuu wa Baba Baa hawana lolote maana shamba lilimshinda na hatimaye akaliuza. Wajukuu wa Baba Baa wangali na shamba la babu yao, na Mungu kawaongezea zaidi kwa kuwa na viwanda, maduka na mahoteli ya kitalii! Tafakari! Akili kichwani mwako!
Guru wa Menejimenti, Profesa Peter Drucker anasema meneja mzuri na anayefanya kazi kwelikweli, hafanyi kazi yoyote. Ndivyo ilivyo pia kwa serikali nzuri na inayofanya kazi kwelikweli. Haifanyi kazi. Tunaposema haifanyi kazi hatuna maana haifanyi chochote au inategea tu. La hasha. Meneja na serikali bora na mfano wa kuigwa hufnaya kazi kwa kupitia watu, idara na taasisi nyingine. Unapoingilia kufanya kazi za watu wengine, idara na taasisi nyingine badla aya wao kuzifanya wenyewe kuna uwezekano mkubwa wa wewe kuvuruga kazi hizo au kutokuwa na tija linganifu wala ufanifu na ufanisi. Ni vizuri viongozi na mameneja wetu walielewe hili na wajipime na kuona kama kweli wanafanya kile ambacho kiongozi au meneja anachotakiwa kukifanya na sio kufanya anayoweza kufanya karani au tarishi. Kama sio waziri au mbunge au mkuu wa mkoa kama sio mkuu wa wilaya.
Tujiulize ni nini nafasi ya jamii katika ufumbuzi wa tatizo la umeme nchini Tanzania. Hivi leo, Benki ya dunia inamwaga misaada kwa ajili ya uanzishwaji wa miradi mbalimbali ya kijamii, jambo linaloashiria uwezekano wa kushirikiana na benki hiyo kuziwezesha jamii mbalimbali kuja na mawazo na mapendekezo kuhusiana na jinsi wanajamii wenyewe wanavyoweza kuchangia katika uzalishaji umeme nchini bila ya kutegemea sana wawekezaji toka nje. Maana wawekezaji hawaji kujenga miundombinu bali kuwekeza katika biashara au uzalishaji mali kwenye eneo walilojikita. Mjenzi wa miundombinu yetu ni lazima awe Mtanzania mwenyewe, mwanajamii katika jamii husika.
Wanajamii wa maeneo mbalimbali nchini hivi leo wanasita kujiunga na shughuli yoyote inayonukia ujamaaujamaa au ushirka ushrika kwani dhana hizo zilichakachuliwa vibaya mno na viongozi waliokuwa chini ya Mwalimu Nyerere. Ni yeye tu inaelekea alikuwa na nia safi na nzuri ya kubadili maisha ya Watanzania na sio wengine, na kama walikuwepo walikuwa wachache sana na walisakamwa kupita kiasi na mafisadi na walilia ubepari wa wakati huo.
Ni vyema pia kuzijua njia mbalimbali za kuzalisha umeme. Kisha kuainisha ni ipi au zipi ambazo zinaweza katika muda mfupi kutupa nafuu katika tatizo hili na zile ambazo zinahitaji muda na uwekezaji mkubwa zaidi.
Ziko njia mbalimbali za kuzalsha umeme zinazojulikana kufikia sasa. Njia hizo ni pamoja na mchakato wa nyuklia; samadi na takataka mbalimbali; mvuke; mashamba ya umeme wa solar; mashamba ya umeme wa upepo; mafuta ya petroli au dizeli na maji.
Tanzania inasemekana haijafikia hali ya kujitosheleza kiuwezo na kiusalama kuzalisha umeme kwa mchakato wa uranium ijapo tumejaliwa madini hayo. Kwa hiyo, hii sio njia ya kutusaidia katika siku za karibu.
Umeme kwa maji ndio huo ambao unatuongezea umaskini, maafa na dhiki zisizokweisha.
Nao huu unaweza kurudia hali yake ya kawaida endapo mipango yetu ya uoteshai miti, utunzaji mazingira na vilivyomo na hususan kwenye maeneo ya vyanzo vya maji milimani au chini ardhini itafanikishwa.
Uzalishaji umeme kwa kutumia samadi na takataka mbalimbali; upepo; mafuta ya petroli au dizeli ndio njia zinazoweza kuchangia haraka zaidi kumaliza tatizo hili.
Kwa jiji kama Dar es salaam uzalishaji umeme kwa kutumia takataka ni kitu kinachowezekana. Na njia hii itaua ndege wawili kwa jiwe moja. Kwanza, utaongeza megawati za umeme kwenye mtandoa wa umeme na pili utafanya jiji hili kuwa safi daima.
Mashamba ya umeme wa solar na upepo kwenye mikoa yenye jua na upepo wa kutosha yanaweza kuchangia gridi ya taifa kwa megawati kadhaa.
Kwenye miji na wilaya ambazo zina upepo wa kutosha ni dhahiri tukishirikiana na nchi kama Denmark na Netherlands tunaweza kupata 'shortcut' za kupata mitambo na vifaa vinavyohitaji na kuzalisha umeme chini ya mwaka mmoja.
Umeme wa jenereta zinazotuchafulia hali ya hewa, mazingira na kutupigia makelele unastahili kudhibitiwa na kuvumuliwa tu kutokana na ukweli kuwa hakuna ujanja mwingine.
Mitaani ili tusichafue zaidi hali ya hewa ni vyema maduka au makampuni kadhaa yakaungana na kununua jenereta kubwa zinazoweza kutosheleza maduka au makampuni yote yaliyo sehemu hiyo badala ya kila mmoja kuwa na kijenereta chake na hivyo kusababisha uchafuzi mkubwa wa mazingira kwa moshi, kelele na hewa ya carbon monoxide.
Inafaa pia kuuliza kama nchi zilizotuzunguka, yaani, Msumbiji, Malawi, Zambia, Kongo Kinshasa, Rwanda (ambayo imefanya kazi nzuri sana katika upatikanaji umeme kwa watu wake), Burundi, Uganda na Kenya zina hali gani kiumeme na tunaweza kushirikiana nazo vipi ili tuzalishe umeme kwa pamoja utakaotusaidia sote kupunguza au kumaliza kabisa tatizo letu la umeme.
Maendeleo ni vigumu kupatikana bila kuwa na mipango mizuri inayotekelezeka. Ni heri nchi kupiga maktaimu kwa mwaka mmoja hata zaidi ili kwanza ihakikishe imejipanga vizuri kabla ya kuwa na mpango wowote wa maendeleo usiotekelezeka.
Katika hili ni muhimu kuona kwamba viongozi mbalimbali wa nchi hii wanawekwa kwa misingi ya kujenga na kuendeleza sehemu husika. Hii ina maana kazi ya mkuu wa shrika fulani, mathalani, TANESCO, lazima iwe ni kulitoa shirika hilo kwenye ngazi ya chini kwenda ngazi ya juu kiutendaji na kiufanisi.
Ndivyo ilivyo pia kwa mwenyekiti wa kijiji, katibu kata, kiongozi wa tarafa, mkuu wa wilaya, mkuu wa mkoa wanavyotakiwa kuwa. Baadhi ya matatizo yetu kama hili la umeme kama watu hawa wangeliachiwa kufanya kazi kama watu huru labda linaweza kumalizwa huko huko kwani wao wanajua eneo lao vyema zaidi kuliko viongozi wa kitaifa na mbunge asiyewatembelea hadi uchaguzi mkuu ujao.
Nilishawahi kuzungumzia kwamba ukiwa na kiongozi halafu kiongozi huyo hana tatizo analolitatua, wala haichangamkii fursa yoyote ili kuongeza kipato au kuyafanya maisha ya walio chini yake kuwa bora zaidi-ni sawa na kuwa na watu bila kiongozi.
Kadhalika, kama una shirika, wilaya, mkoa au wizara ambayo haijulikani inashughulikia tatizo gani au kuchangamkia fursa gani za kimaendeleo katika eneo husika, basi mahala hapo hakuna kiongozi. Kuna mtawala. Na kwa bahati mbaya viongozi wengi tuliokuwa nao hawastahili kuitwa viongzi bali watawala au magavana.
Tofauti ya kiongozi na mtawala ni kwamba, mtawala kazi yake ni kusimamia tu kile kilichopto, yaani, kile ambacho kimeshaanzishwa na wengine. Na sio jukumu lake kubadili chochote au kufanya kazi zaidi ya usimamizi na kutoa taarifa kwa wakubwa wake. Wakati kiongozi, ni mtu mwenye dhamana za kuleta mabadiliko toka hali duni kwenda hali bora zaidi. Kiongozi huonyesha kwa vitendo, hushauri, huelekeza, huelimisha, huwezesha na hutoa motisha ili walioko chini yake walete mabadiliko tarajiwa katika eneo husika.
Kiongozi tofauti na mtawala, huona mbali na mbele zaidi. Ni mtabiri wa namna fulani. Hufahamu fika kwamba haya ya kawaida watu walio chini yake wanayajua na wanaweza kuyashughulikia. Lakini yale ya mbele na yajayo na yasiyo tabirika ndio eneo la kuonesha uongozi wake.
Mathalani, mtawala huwaza jinsi ya kuwalisha watu wake leo leo. Wakati kiongozi anatakiwa kuwaza, kupanga na kuweka mikakati ya watu wake kupata chakula bila tatizo miaka mitano au kumi ijayo.
Mtawala huwaza kutatua tatizo la umeme leo leo, lakini kiongozi hutafakari, hupanga na kuweka mikakati inayouliza maswali ya msingi na yasiyo na majibu ya haraka. Kwa mfano, kama tutakuwa na ukame, yaani, mvua hazitanywesha na umeme wetu unategemea maji, ni njia gani mbadala tutakuwa nazo ili ukame na kukosa mvua kuisisababishe matatizo ya upatikanaji umeme.
Kiongozi mzuri huwatumia walio chini yake kutokana na uwezo na utalaamu walio nao bila kujali watokako wala udhaifu wao. Ubora na kile mtu anachoweza kukifanya katika kutimiza lengo lililoko mbele yake ndio kitu muhimu kuliko vyote. Na kiongozi bora, hatokei hata mara moja, kuwalaumu walio chini yake kwamba wameshindwa kazi fulani. Wakishindwa ina maana ni yeye ameshindwa na sio walio chini yake. Aghalabu, kiongozi mzuri na bora, huwaongoza watu kwa namna ambayo watu wao wanapofanikisha malengo fulani basi watu hao kwa pamoja husema, 'tumeweza, tumeshinda!' na sio kiongozi wetu ameweza, ameshinda!
Kiongozi bora na hususan akiwa wa wilaya au mkoa au nchi hupaswa kujua mambo ambayo mkoa wenyewe unastahili kutengeneza au kuzalisha na yale ambayo kwa muda fulani yapasa kuyapata toka kwa wengine.
Ni kichekesho kwa nchi kuwa na mpango unaotaka kuongeza asilimia ya nyumba zinazopata umeme toka asilimia 5 hadi asilimia ishirini na tano au hamsini, bila ya kuwa na mpango wa uzalishaji mashine, vifua umeme, mitambo na zanatepe mbalimbali zinazohitajika ili nchi yenyewe ijitegemee angalau kwa asilimia 80 kwa vitu vinavyohitajika kuzalisha, kusambaza na kuunganisha umeme nchini.
Kama nilivyodokeza huko nyuma, jambo hili sasa ni rahisi na jepesi kuliko wakati wowote katika historia ya nchi yetu na maendeleo yetu. Maana, hakuna sheria inayosema ili tuendelee lazima tuwatumie tu Watanzania au raia wetu hata kama hawajui na hawajasomea kazi inayotaka kufanyika. Na eti, hata kama kuna wahandisi au mafundi wa umeme,, maprofesa wa umeme, washauri, wanafunzi na watafiti wa masuala ya uzalishaji umeme wasio na kazi wala mafunzo kwa vitendo nchini na nchi za nje lazima tutegemee shirika moja tu nchini kutunusuru na balaa na maafa yanayoikumba nchi na watu wetu leo.
Kutokuona na kutozithamini na kutozitumia rasilimali watu zilizotapakaa huko Marekani, Ulaya Magharibi, Ulaya Mashariki, Russia ya zamani na kwingineko kutafuta ufumbuzi wa matatizo yetu mbalimbali ya kijamii, kiuchumi na kiteknolojia
ni jambo ambalo tutakaa na kuja kulijutia baada ya muda si mrefu kutoka sasa.
Miaka mingi iliyopita kulikuwa na Baba Baa na Baba Waa. Wote wawili walikuwa na mashamba makubwa yenye mimea ya kila aina pamoja na maeneo wazi, yaani, yasiyopandwa chochote. Msimu wa kilimo ulivyofika, Baba Baa alikuwa akiwatafuta vibarua wa kikwao tu, hakutaka wageni walime shamba lake. Aliamini hawajui kulima.Lakini mwenziwe Baba Waa aliwamwagia ajira Warundi, wamakonde, wasafwa, Wanyarandwa bila kubagua. Katika mchanganyiko huu wa watu wenye asili mbalimbali shamba la Baba Waa sio tu lililimwa vizuri bali lilinufaika na mimea mipya, njia mpya za kilimo, kama vile kupiga matuta na kadhalika. Hivi leo wajukuu wa Baba Baa hawana lolote maana shamba lilimshinda na hatimaye akaliuza. Wajukuu wa Baba Baa wangali na shamba la babu yao, na Mungu kawaongezea zaidi kwa kuwa na viwanda, maduka na mahoteli ya kitalii! Tafakari! Akili kichwani mwako!
Monday, July 11, 2011
M a l e z i y a w a t o t o h a y a e n d a n i n a t u n a k o t a k a k w e n d a
BILA shaka toka nchi hii ianze kuukumbatia ubepari, soko huria na utandawazi tumeanza kuona mabadiliko makubwa sana katika tabia za watoto na vijana wa KItanzania.
Taifa la watu waliokuwa wema, wapole, wenye huruma, heshima na adabu limeanza kuwa kitu tofauti kabisa. Na hakuna anayeonekana kutaka kukemea huku kukengeuka. Sio vyombo vyetu vya habari au dini zetu wala sio serikali isiyokuwa na dini.
Aghalabu wengi hushtuka kutokana na utovu wa adabu, ukosefu wa heshima na hulka za kiajabuajabu ambazo inadaiwa ni kwenda na wakati.
Kwa namna fulani hali hii inatokana na kukua kwa kasi kwa ubinafsi na watu kujiamini kuwa wanaweza wakajitosheleza kwa kila kitu na wakawalea watoto wao bila msaada wa mtu mwingine.
Matokeo yake hivi leo sio tu kwamba watoto hao wanakuwa kero na maudhi kwa watu wengine lakini hata kwa wazazi wao wenyewe.
Pengine huu ni wakati muafaka wa kuvuta hatua moja nyuma na kujiuliza kama malezi haya ya leo kweli ndiyo yatakayolifikisha taifa letu pale tunapotaka liende ?
Nina wasiwasi mkubwa kama malezi haya kweli ndiyo yanayowafaa watoto wetu. Na kamwe waoto hawawezi kulaumiwa bali ni wazazi wao, viongozi wao wa dini, jamii yao, wanasiasa wao, na taifa lao.
Wazazi ndio wanaoshika usukani hata kama sio moja kwa moja. Na wao wanapochelea kuikosoa serikali na viongozi wao kwamba wanapeleka upogo kizazi kijacho hawatakuwa na kuwamlaumu ila kujilaumu wenyewe.
Pengine upofu huu unatokana na uchu wa viongozi wa dini kupata waumini ndivyo sivyo ili mradi sadaka inayopatikana ni kubwa na wao wanaishi maisha ya kifahari? Au pengine upofu huu unatokana na kukosa chama huru cha wazazi na viongozi wa wazazi wasio wanasiasa. Au pengine upofu huu unatokana na ubinafsi na tamaa ya kuonekana tofauti na watu wengine.
Potelea mbali sababu iwayo, lakini ukweli unabakia palepale kwamba kauli na vitendo vyetu leo ndivyo vinavyosaidia kurithisha tabia, hulka na mienendo ambayo sisi wazazi tulio wengi tunaonekana kuirithia.
Kauli na vitendo vya mzazi wa Kitanzania leo vimetawaliwa na vinatafiriwa na umimi na ubinafsi wa hali ya juu iwe nyumbani, kazini, njiani au michezoni. Na kiongozi mmoja alilipalilia hili kwa kiasi kikubwa pale alipowaambia Watanzania kuwa: ' Kila mtu atabeba msalaba wake mwenyewe!'
Lakini tunachoshindwa kujua sisi wazazi ni kuwa mtoto huzaliwa hana tabia yenye uhakika. Na tabia ni matokeo ya kuzungukwa na wazazi wake na jamii yake na yale yanayomtokea katika maisha yake. Na kama shamba lako halina magugu (kwa maana huna watoto wenye tabia mbaya) lakini aghalabu utakuwa umezungukwa na mashamba yenye magugu (majirani wenye watoto kisirani) na hivyo hatimaye magugu pia huingia shambani kwako kwa kushtukizia na kwa athari mbaya zaidi. Maana, wanao ni weupe na hawana wanalolijua.
Hebu, tuangalie sampuli kadhaa za wazazi na jinsi wanavyoathiri viongozi wa kesho na keshokutwa. Tuanze na huyu masikini aliyeko barabarani na ana watoto kadhaa. Watoto hao hawaendi shule bali wanamsaidia mzazi wao kazi. Kwa kuwa kazi ya baba au mama ni ombaomba, wanamsaidia kuomba kama mzazi wao. Hebu fikiria wewe mwenyewe je huyu atakuwa Mtanzania wa aina gani akiwa mtu mzima?
Baadhi ya wazzazi tunalia machozi ya mamba. Tunajifanya tuna uchungu sana na mayatima. Tunaanzisha vituo vya kulea mayatima. Lakini ukiangalia kwa undani vituo hivyo havina dhati ya kuwalea mayatima hao bali kumpatia mwenye kituo utajiri wa haraka haraka. Hivi kweli watoto waliotoka katika mateso ya uyatima au mama wa kambo wakakutana na kadhia kama hii watakuwa na utu gani. Na kwa nini yatima alelewe kwenye kituo. Kuna yatima wangapi Tanzania? HIvi haiwezekani kwa watu wenye uwezo kuwachukua na kuwalea mayatima hawa majumbani mwao ili wawe na maisha yaliyofanana na ya watoto wenye wazazi wawili? Hatujui dini yako inasemaje, wlala thawabu utakazopata au madhambi utakayofutiwa, lakini kitendo hiki kitahakikisha kuwepo kwa taifa bora zaidi kuliko hali ikiwa kinyume cha hivyo.
Aina nyingine ya wazazi ni wale wa tabaka la chini kimaisha. Wazazi hawa aidha wanafanya kazi au wana biashara fulani au ni wakulima. Lakini kutokana na ugumu wa maisha baba anaamua kuwa mlevi, wengine wanazidisha starehe ili wasahau maumivu na wengine wanakwepa majukumu yao kama wazazi. Si uongo, ulevi noma. Familia nyingi zinasambaratika kutokana na baba na balaa zaidi hata mama kuwa walevi. Je, matangazo kwenye redio na televisheni yanatosha kuwafanya wazazi hawa wapunguze idadi ya sigara na chupa za bia wanazosaidia serikali kuongeza bajeti yake?
Umewahi kukutana na mtoto wa mlevi au baba asiyejua majukumu yake kwa familia yake ? Nguo chakavu na chafu, kapauka (hana mafuta ya kujipaka), midomo mikavu (hakupata kifungua kinywa asubuhi), hana begi labda mfuko wa marlboro na kadhalika. Ikionesha dalili kwamba hakuna kitu kinachoitwa ustawi wa jamii hapa nchini na kama kipo basi hakifanyi kazi. Kimekufa. Je, taasisi hiyo inasaia kujenga chuki, husuda na roho mbaya miongoni mwa watoto kama hawa au inajenga amani na umoja wa kesho?
Kuna wazazi wa lile tabaka la pili ambao juzi na jana walikuwa na hali nzuri kiasi, wana nyumba, gari na wanakula milo 3 kwa siku. Lakini toka peteroli na bei ya vyakula ianze kupaa juu kuliko roketi na shilingi kuzidi kuporomoka maamuzi magumu yanabidi kufanyika. Kuweka gari peteroli na kula ugali kwa matembere au....
La ajabu, katika familia hizi tofauti na wenzetu kwingineko Afrika Mashariki pamoja na jamaa hawa kuwa na intaneti hakuna anayewafundisha wanawe ujasiriamali, ubunifu na uzuzi wa mambo mapya. Tunalea 'Kisukuma' baba linafanya kazi zote na wake na watoto wake kazi yao ni kula tu. Na jinsi mtu anavyolisha watu wengi ndivyo anavyozidi kuwa maarufu.
Lakini ni dhahiri kuwa vijana wa miaka 14 sio watoto tena. Hawa ni watu wanaoweza kufunzwa jinsi ya kushiriki moja au mawili ya faida kwao na wazazi wao leo na kesho. Tunapojenga utegemezi wa kupita kiasi mwishowe ni kuwa na nyumba zinazofanana na zile za Uswahilini pale Kariakoo. Utamkuta baba na mama, watoto wo wa kiume wanne na sita wa kike. Na hao watoto sita wa kike wote wamezalia nyumnbani na wajuku wanalelewa na bibi na babu. Kazi kweli! Uzazi wa namna hii ni chanzo kikubwa cha umasikini wa uzeeni. Na kama serikali ina nia ya kweli ya kuwasaidia wazee basi ianze kwa kuwapunguzia wazazi wa namna hii mzigo kama huu.
Ni wazazi hawa pia wanaotujali kwa kutuletea kizazi kipya na bidhaa zao. IKiwemo muziki wa kuiga au wa kinyani toka Marekani, kuvaa suruali inayoacha nusu ya makalio nje au sketi na vigauni ambavyo vinaacha sentimeta chache tu kuona sehemu nyeti-kwa kisingizio cha kwenda na wakati. Na baba na mama nyumbani wanawaunga mkono watoto wao. Mwisho wa yote humjui mzazi ni nani na mtoto ni yupi. Wote ngoma sawa. Balaa na mikosi ikianza kila mtu anaanza kumlaumu Muumba, maana hata kuomba tena hawajui. Uhuru huu usiokuwa na mipaka sio uhuru unaowasaidia vijana wetu wala taifa letu. Ya ngoswe muachieni ngose. Nina hakika tukiuenzi Uafrika wetu na kutunza adabu na heshima yetu basi tutakuwa na bidhaa bora zaidi na zinakubalika kimataifa kuliko ilivyo sasa. Msaada wa vyombo vya habari katika hili ni muhimu sana.
Halafu, tuna wazazi wa tabaka la tatu au matajiri wakubwa au vizito. Hawa wanaajiri, hawaajiriwi. Wana viwanda, biashara kubwa au shule au vyuo au hospitali na kadhalika. Kutokana na wingi wa mali hata watoto wao wa miaka 10 huchukua magari na kuingia nayo barabarani. Kwa kuwa sina utajiri wa kiasi hicho, labda niulize tu hivi mzazi kumfanya mwanawe aamini utajiri wake ni utajiri wa mwanawe pia kunamsaidia au kunambomoa kijana wake. Aidha, kwa viongozi au vigogo wa kisiasa wanaojua kazi moja tu ya kufundisha watoto wao-siasa, je, kutaka mwanao awe kama wewe kunamsaidia au kunamdumaza mwanao. Na je, ulicho wewe ndicho anachoweza kuwa yeye ? Baadhi ya wazazi ndio wanaomiliki televisheni. Tuwaulize wanaridhika kwa wajukuu zao kuona kile kinachooneshwa ?
Awe ni mtoto wa masikini au tajiri, mwenye wazazi au yatima, mwenye akili au mjinga, mweupe au mweusi, Mkiristo au Mwislamu hawa wote ni watoto wetu na hii ni nchi yetu na haya ndiyo malezi yetu. Swali la mwisho ni je hii amani na huu umoja tunaojivunia sana hapa Afrika watavirithi kwa malezi haya ?
Taifa la watu waliokuwa wema, wapole, wenye huruma, heshima na adabu limeanza kuwa kitu tofauti kabisa. Na hakuna anayeonekana kutaka kukemea huku kukengeuka. Sio vyombo vyetu vya habari au dini zetu wala sio serikali isiyokuwa na dini.
Aghalabu wengi hushtuka kutokana na utovu wa adabu, ukosefu wa heshima na hulka za kiajabuajabu ambazo inadaiwa ni kwenda na wakati.
Kwa namna fulani hali hii inatokana na kukua kwa kasi kwa ubinafsi na watu kujiamini kuwa wanaweza wakajitosheleza kwa kila kitu na wakawalea watoto wao bila msaada wa mtu mwingine.
Matokeo yake hivi leo sio tu kwamba watoto hao wanakuwa kero na maudhi kwa watu wengine lakini hata kwa wazazi wao wenyewe.
Pengine huu ni wakati muafaka wa kuvuta hatua moja nyuma na kujiuliza kama malezi haya ya leo kweli ndiyo yatakayolifikisha taifa letu pale tunapotaka liende ?
Nina wasiwasi mkubwa kama malezi haya kweli ndiyo yanayowafaa watoto wetu. Na kamwe waoto hawawezi kulaumiwa bali ni wazazi wao, viongozi wao wa dini, jamii yao, wanasiasa wao, na taifa lao.
Wazazi ndio wanaoshika usukani hata kama sio moja kwa moja. Na wao wanapochelea kuikosoa serikali na viongozi wao kwamba wanapeleka upogo kizazi kijacho hawatakuwa na kuwamlaumu ila kujilaumu wenyewe.
Pengine upofu huu unatokana na uchu wa viongozi wa dini kupata waumini ndivyo sivyo ili mradi sadaka inayopatikana ni kubwa na wao wanaishi maisha ya kifahari? Au pengine upofu huu unatokana na kukosa chama huru cha wazazi na viongozi wa wazazi wasio wanasiasa. Au pengine upofu huu unatokana na ubinafsi na tamaa ya kuonekana tofauti na watu wengine.
Potelea mbali sababu iwayo, lakini ukweli unabakia palepale kwamba kauli na vitendo vyetu leo ndivyo vinavyosaidia kurithisha tabia, hulka na mienendo ambayo sisi wazazi tulio wengi tunaonekana kuirithia.
Kauli na vitendo vya mzazi wa Kitanzania leo vimetawaliwa na vinatafiriwa na umimi na ubinafsi wa hali ya juu iwe nyumbani, kazini, njiani au michezoni. Na kiongozi mmoja alilipalilia hili kwa kiasi kikubwa pale alipowaambia Watanzania kuwa: ' Kila mtu atabeba msalaba wake mwenyewe!'
Lakini tunachoshindwa kujua sisi wazazi ni kuwa mtoto huzaliwa hana tabia yenye uhakika. Na tabia ni matokeo ya kuzungukwa na wazazi wake na jamii yake na yale yanayomtokea katika maisha yake. Na kama shamba lako halina magugu (kwa maana huna watoto wenye tabia mbaya) lakini aghalabu utakuwa umezungukwa na mashamba yenye magugu (majirani wenye watoto kisirani) na hivyo hatimaye magugu pia huingia shambani kwako kwa kushtukizia na kwa athari mbaya zaidi. Maana, wanao ni weupe na hawana wanalolijua.
Hebu, tuangalie sampuli kadhaa za wazazi na jinsi wanavyoathiri viongozi wa kesho na keshokutwa. Tuanze na huyu masikini aliyeko barabarani na ana watoto kadhaa. Watoto hao hawaendi shule bali wanamsaidia mzazi wao kazi. Kwa kuwa kazi ya baba au mama ni ombaomba, wanamsaidia kuomba kama mzazi wao. Hebu fikiria wewe mwenyewe je huyu atakuwa Mtanzania wa aina gani akiwa mtu mzima?
Baadhi ya wazzazi tunalia machozi ya mamba. Tunajifanya tuna uchungu sana na mayatima. Tunaanzisha vituo vya kulea mayatima. Lakini ukiangalia kwa undani vituo hivyo havina dhati ya kuwalea mayatima hao bali kumpatia mwenye kituo utajiri wa haraka haraka. Hivi kweli watoto waliotoka katika mateso ya uyatima au mama wa kambo wakakutana na kadhia kama hii watakuwa na utu gani. Na kwa nini yatima alelewe kwenye kituo. Kuna yatima wangapi Tanzania? HIvi haiwezekani kwa watu wenye uwezo kuwachukua na kuwalea mayatima hawa majumbani mwao ili wawe na maisha yaliyofanana na ya watoto wenye wazazi wawili? Hatujui dini yako inasemaje, wlala thawabu utakazopata au madhambi utakayofutiwa, lakini kitendo hiki kitahakikisha kuwepo kwa taifa bora zaidi kuliko hali ikiwa kinyume cha hivyo.
Aina nyingine ya wazazi ni wale wa tabaka la chini kimaisha. Wazazi hawa aidha wanafanya kazi au wana biashara fulani au ni wakulima. Lakini kutokana na ugumu wa maisha baba anaamua kuwa mlevi, wengine wanazidisha starehe ili wasahau maumivu na wengine wanakwepa majukumu yao kama wazazi. Si uongo, ulevi noma. Familia nyingi zinasambaratika kutokana na baba na balaa zaidi hata mama kuwa walevi. Je, matangazo kwenye redio na televisheni yanatosha kuwafanya wazazi hawa wapunguze idadi ya sigara na chupa za bia wanazosaidia serikali kuongeza bajeti yake?
Umewahi kukutana na mtoto wa mlevi au baba asiyejua majukumu yake kwa familia yake ? Nguo chakavu na chafu, kapauka (hana mafuta ya kujipaka), midomo mikavu (hakupata kifungua kinywa asubuhi), hana begi labda mfuko wa marlboro na kadhalika. Ikionesha dalili kwamba hakuna kitu kinachoitwa ustawi wa jamii hapa nchini na kama kipo basi hakifanyi kazi. Kimekufa. Je, taasisi hiyo inasaia kujenga chuki, husuda na roho mbaya miongoni mwa watoto kama hawa au inajenga amani na umoja wa kesho?
Kuna wazazi wa lile tabaka la pili ambao juzi na jana walikuwa na hali nzuri kiasi, wana nyumba, gari na wanakula milo 3 kwa siku. Lakini toka peteroli na bei ya vyakula ianze kupaa juu kuliko roketi na shilingi kuzidi kuporomoka maamuzi magumu yanabidi kufanyika. Kuweka gari peteroli na kula ugali kwa matembere au....
La ajabu, katika familia hizi tofauti na wenzetu kwingineko Afrika Mashariki pamoja na jamaa hawa kuwa na intaneti hakuna anayewafundisha wanawe ujasiriamali, ubunifu na uzuzi wa mambo mapya. Tunalea 'Kisukuma' baba linafanya kazi zote na wake na watoto wake kazi yao ni kula tu. Na jinsi mtu anavyolisha watu wengi ndivyo anavyozidi kuwa maarufu.
Lakini ni dhahiri kuwa vijana wa miaka 14 sio watoto tena. Hawa ni watu wanaoweza kufunzwa jinsi ya kushiriki moja au mawili ya faida kwao na wazazi wao leo na kesho. Tunapojenga utegemezi wa kupita kiasi mwishowe ni kuwa na nyumba zinazofanana na zile za Uswahilini pale Kariakoo. Utamkuta baba na mama, watoto wo wa kiume wanne na sita wa kike. Na hao watoto sita wa kike wote wamezalia nyumnbani na wajuku wanalelewa na bibi na babu. Kazi kweli! Uzazi wa namna hii ni chanzo kikubwa cha umasikini wa uzeeni. Na kama serikali ina nia ya kweli ya kuwasaidia wazee basi ianze kwa kuwapunguzia wazazi wa namna hii mzigo kama huu.
Ni wazazi hawa pia wanaotujali kwa kutuletea kizazi kipya na bidhaa zao. IKiwemo muziki wa kuiga au wa kinyani toka Marekani, kuvaa suruali inayoacha nusu ya makalio nje au sketi na vigauni ambavyo vinaacha sentimeta chache tu kuona sehemu nyeti-kwa kisingizio cha kwenda na wakati. Na baba na mama nyumbani wanawaunga mkono watoto wao. Mwisho wa yote humjui mzazi ni nani na mtoto ni yupi. Wote ngoma sawa. Balaa na mikosi ikianza kila mtu anaanza kumlaumu Muumba, maana hata kuomba tena hawajui. Uhuru huu usiokuwa na mipaka sio uhuru unaowasaidia vijana wetu wala taifa letu. Ya ngoswe muachieni ngose. Nina hakika tukiuenzi Uafrika wetu na kutunza adabu na heshima yetu basi tutakuwa na bidhaa bora zaidi na zinakubalika kimataifa kuliko ilivyo sasa. Msaada wa vyombo vya habari katika hili ni muhimu sana.
Halafu, tuna wazazi wa tabaka la tatu au matajiri wakubwa au vizito. Hawa wanaajiri, hawaajiriwi. Wana viwanda, biashara kubwa au shule au vyuo au hospitali na kadhalika. Kutokana na wingi wa mali hata watoto wao wa miaka 10 huchukua magari na kuingia nayo barabarani. Kwa kuwa sina utajiri wa kiasi hicho, labda niulize tu hivi mzazi kumfanya mwanawe aamini utajiri wake ni utajiri wa mwanawe pia kunamsaidia au kunambomoa kijana wake. Aidha, kwa viongozi au vigogo wa kisiasa wanaojua kazi moja tu ya kufundisha watoto wao-siasa, je, kutaka mwanao awe kama wewe kunamsaidia au kunamdumaza mwanao. Na je, ulicho wewe ndicho anachoweza kuwa yeye ? Baadhi ya wazazi ndio wanaomiliki televisheni. Tuwaulize wanaridhika kwa wajukuu zao kuona kile kinachooneshwa ?
Awe ni mtoto wa masikini au tajiri, mwenye wazazi au yatima, mwenye akili au mjinga, mweupe au mweusi, Mkiristo au Mwislamu hawa wote ni watoto wetu na hii ni nchi yetu na haya ndiyo malezi yetu. Swali la mwisho ni je hii amani na huu umoja tunaojivunia sana hapa Afrika watavirithi kwa malezi haya ?
Friday, July 8, 2011
Sabasaba: Dhana na Upeo wake vipanuliwe
Maonyesho kama yale ya Sabasaba kama yakiangaliwa upya na eneo kubwa zaii kupatikana yanaweza kuwa ni kivutio kikubwa cha utalii, wawekezaji na biashara kubwa kubwa duniani.
Katika kujipanga upya huko, kwanza, eneo jipya litafutwe ambako kutajengwa uwanja mpya utakaofaa uitwe Dar es salaam Internationl Expo -Tanzania.
Maonyesho haya yawe ni ya kimataifa. Yaani, bidhaa, tekhonhama na mitambo mbalimbali itakayooneshwa hapo iwe ni ile inayoweza kununuliwa na nchi zote zinazotuzunguka.
Uwanja huu unastahili kuwa ni wa ubora wa kimataifa na ingelikuwa ni vyema upatiwe kiwanja kipya ambacho kitaweza kuwa ni kijiji cha kudumu kwa maonyesho ya expo mbalimbali.
Wakati huo huo, kila mkoa unastahili kuwa na maonyesho yake ya sabasaba wakati ule ule yale ya Dar es salaam yanapofanyika.
Katika kufanya hivyo tutadhihirishia umma kwamba Dar es salaam sio Tanzania, na Tanzania sio Dar es salaam. Ajira zitaongezeka na kusambaa kwa sababu sasa patahitajika makundi 30 ya wawakilishi kwa kila Kampuni nchini kwenda katika mikoa 30 ya Tanzania. Kubwa zaidi, mikoa inayolala kwa kukosa kujua kuwepo kwa bidhaa na vifaa vya aina ambazo zinaweza kuwafanya waondokane na umaskini wao haitakaa ilale tena maana sabasaba kila mwaka itaizindua. Ndivyo inavyostahili pia kuwa kwa maonyesho ya nanenane. Yasiendelee kufanyika kisiasa bali yawe kweli ni maonyesho ya Expo-Kilimo International. Hali kadhalika mikoa nayo iwe na maonyesho yao kwa kadri ya uwezo, changamoto na matarajio yao.
Maonyesho yote haya yajikite kwanza na awali ya yote katika matatizo ya Watanzania, yawe ya kiuchumi, kijamii, kiutamaduni au kiteknolojia.
Kazi yake kubwa iwe ni kuoesha kipya kilichovumbuliwa na Watanzania na watu wengine ambacho kinaweza kuwa ufumbuzi wa tatizo au shida fulani. Kwa hiyo, miaka inavyokwenda matatizo ya Biashara, Kilimo na Viwanda yatakuwa yakipatiwa majibu yake katika maonyesho hayo.
Ni muhimu kwa maeneo kuwamakubwa zaidi na shughuli nzima iwe ni kivutio sio tu kwa wananchi wa kawaida, bali wawekezaji nawatalii pia. Hii iwe sawa na sherehe kubwa ya wiki nzima kitaifa ambako Watanzania watakuwa wakitafakari majibu ya matatizo yao na changamoto ambazo bado zinawakabili kuelekea kwenye dunia ya pili baada ya kugura ile ya kwanza.
Dhana nzima ya mashindano haya inapotezwa kwa kuangalia eti banda gani ni zuri na linalopendeza zaidi. Ninaamini wakati umefika kuvibadili vigezo vya ushindi na kuwachagua washindi kutokana na jinsi ambavyo banda husika limejitahidi kupata jibu sahihi kwa tatizo fulani linalowakabili Tanzania. Kwa mfano, bado tunanunua pampu za maji toka nje, je, zawadi si apewe aliyetengeneza pampu hiyo hapa nchini -iwe Mtanzania au mgeni!
Tuna tatizo la kupata zana za uchimbaji madini na hususan kwa wachimbaji wadogo, je, kwanini zawadi hiyo asipewe mtu atakayevumbua zana au mashine za kuchimba madini hapa nchini?
Tuna tatizo la uzalishaji na upatikanaji umeme, je, kwanini mzawadiwa asiwe ni Mtanzania au mgeni aliyekuja kuwekeza nchini na akaweza kuzalisha umeme kwa njia mbadala na umeme huo ukawa wa gharama nafuu zaidi.
Tuna matatizo ya kuzalisha magari, malori na mabasi yetu wenyewe kwanini zawadi zisiende kwa wale wa kwanza kabisa kutengeneza gari la Kitanzania hata kama teknolojia nzima itaazimwa au kuibwa nje?
Hivi atakayetengeneza trekta dogo la Kitanzania kwa kuazima teknolojia ya nje na ikawezekana trekta hilo kuuzwa kwa chini ya shilingi milioni mbili huyu si ndiye anayestahili kuwa mshindi kwenye Sabasaba Expo ijayo?
Watoto mashuleni hawana madeski, vitabu na vifaa vya kujifunzia vya kila aina. Je, kwanini zawadi wasipate wale watakaokuja na ufumbuzi wa matatizo hayo.
Mahospitali yetu yanafungwa na huduma kusimama kila kona nchini. Je, ushindani utakaofaa si ule wa utengenezaji wa zana na vifaa mbalimbali vya mahospitali hapa nchini ili viuzwe kwingineko kwa bei nafuu kuliko vinavyotoka nchi za nje? Maana, ukiwa na teknolojia duni katika hospitali au chuo ndivyo pia shule yenye inavyokuwa duni na ovyo kihali na kimazingira. Teknolojia ya kisasa inalazimisha usasa kwa kiwango cha juu ikiwemo usafi, mandhari na mazingira bora zaidi.
Mambo mengi yako ndani ya uwezo wetu. Kinachotakiwa ni kuona kwamba keki ya taifa inagawika kwa namna ambayo wajasiriamali na wazalishaji mali mbalimbali nao wanapata kitu cha uhakika ili kuleta mabadiliko tuliyokusudia nchini.
Nia na sababu ya kuwepo kwa maonyesho ya sabasaba ilikuwa ni kuiwezesha nchi kuwa na kipimamaendeleo kitakachoonesha jana tulikuwa wapi na leo tumefikia wapi. Lakini tukiwa mwaka nenda, mwaka rudi tunaonesha vilevile vya juzi basi kuna walakini mkubwa hapo. Utandawazi na makuzi ya teknolojia hayaturuhusu kuwa goigoi na wenda pole kiasi hicho.
Kiwanja kipya cha sabasaba lazima kiwe kikubwa kweli kiasi cha
kuwa na uwanja wa ndege mdogo, kituo cha treni, kituo cha basi, mabohari na vingine kama hivyo. Hili likifanyika foleni za kutisha zitakuwa historia maeneo ya Temeke. Na ili kuanza kutekeleza azma njema ya kutenga maeneo ya biashara na makazi ya wau au maofisi ni vyema kama uwanja wa Sabasaba hivi sasa utafanywa kuwa ni TEMEKE PUBLIC SHOPPING PLAZA AND SUPERMARKETS.
Uwanja mpya lazima uwe pia na hoteli ya hadhi ya kitalii kwa maana ya nyota 5 kwenda mbele. Uwanja wa golfu wa kisasa kabisa na vilevile uwanja wa mbio za langalanga (Formula 1) ili kutumika kwa uwanja huo mara kwa mara uwe ni kitu cha uhakika.
Wakati wa maonesho ni vyema uwanja huo ukawa na redio stesheni na TV ya maalum kwa ajili ya mawasiliano. Kwa upande mwingine kutakuwa na eneo la Tovuti au Intaneti ambako wafanyabiashara na wajasiriamali wa kila aina na rika watapata fursa ya kujifunza kufanya kazi zao kwa kutumia Teknohama.
Katika kufanya mabadiliko haya makubwa ni muhimu
kuwashirikisha watu wa nje kama Wajerumani, Wajapani na Wachina waliokubuhu katika mambo ya 'expo'.
Katika kujipanga upya huko, kwanza, eneo jipya litafutwe ambako kutajengwa uwanja mpya utakaofaa uitwe Dar es salaam Internationl Expo -Tanzania.
Maonyesho haya yawe ni ya kimataifa. Yaani, bidhaa, tekhonhama na mitambo mbalimbali itakayooneshwa hapo iwe ni ile inayoweza kununuliwa na nchi zote zinazotuzunguka.
Uwanja huu unastahili kuwa ni wa ubora wa kimataifa na ingelikuwa ni vyema upatiwe kiwanja kipya ambacho kitaweza kuwa ni kijiji cha kudumu kwa maonyesho ya expo mbalimbali.
Wakati huo huo, kila mkoa unastahili kuwa na maonyesho yake ya sabasaba wakati ule ule yale ya Dar es salaam yanapofanyika.
Katika kufanya hivyo tutadhihirishia umma kwamba Dar es salaam sio Tanzania, na Tanzania sio Dar es salaam. Ajira zitaongezeka na kusambaa kwa sababu sasa patahitajika makundi 30 ya wawakilishi kwa kila Kampuni nchini kwenda katika mikoa 30 ya Tanzania. Kubwa zaidi, mikoa inayolala kwa kukosa kujua kuwepo kwa bidhaa na vifaa vya aina ambazo zinaweza kuwafanya waondokane na umaskini wao haitakaa ilale tena maana sabasaba kila mwaka itaizindua. Ndivyo inavyostahili pia kuwa kwa maonyesho ya nanenane. Yasiendelee kufanyika kisiasa bali yawe kweli ni maonyesho ya Expo-Kilimo International. Hali kadhalika mikoa nayo iwe na maonyesho yao kwa kadri ya uwezo, changamoto na matarajio yao.
Maonyesho yote haya yajikite kwanza na awali ya yote katika matatizo ya Watanzania, yawe ya kiuchumi, kijamii, kiutamaduni au kiteknolojia.
Kazi yake kubwa iwe ni kuoesha kipya kilichovumbuliwa na Watanzania na watu wengine ambacho kinaweza kuwa ufumbuzi wa tatizo au shida fulani. Kwa hiyo, miaka inavyokwenda matatizo ya Biashara, Kilimo na Viwanda yatakuwa yakipatiwa majibu yake katika maonyesho hayo.
Ni muhimu kwa maeneo kuwamakubwa zaidi na shughuli nzima iwe ni kivutio sio tu kwa wananchi wa kawaida, bali wawekezaji nawatalii pia. Hii iwe sawa na sherehe kubwa ya wiki nzima kitaifa ambako Watanzania watakuwa wakitafakari majibu ya matatizo yao na changamoto ambazo bado zinawakabili kuelekea kwenye dunia ya pili baada ya kugura ile ya kwanza.
Dhana nzima ya mashindano haya inapotezwa kwa kuangalia eti banda gani ni zuri na linalopendeza zaidi. Ninaamini wakati umefika kuvibadili vigezo vya ushindi na kuwachagua washindi kutokana na jinsi ambavyo banda husika limejitahidi kupata jibu sahihi kwa tatizo fulani linalowakabili Tanzania. Kwa mfano, bado tunanunua pampu za maji toka nje, je, zawadi si apewe aliyetengeneza pampu hiyo hapa nchini -iwe Mtanzania au mgeni!
Tuna tatizo la kupata zana za uchimbaji madini na hususan kwa wachimbaji wadogo, je, kwanini zawadi hiyo asipewe mtu atakayevumbua zana au mashine za kuchimba madini hapa nchini?
Tuna tatizo la uzalishaji na upatikanaji umeme, je, kwanini mzawadiwa asiwe ni Mtanzania au mgeni aliyekuja kuwekeza nchini na akaweza kuzalisha umeme kwa njia mbadala na umeme huo ukawa wa gharama nafuu zaidi.
Tuna matatizo ya kuzalisha magari, malori na mabasi yetu wenyewe kwanini zawadi zisiende kwa wale wa kwanza kabisa kutengeneza gari la Kitanzania hata kama teknolojia nzima itaazimwa au kuibwa nje?
Hivi atakayetengeneza trekta dogo la Kitanzania kwa kuazima teknolojia ya nje na ikawezekana trekta hilo kuuzwa kwa chini ya shilingi milioni mbili huyu si ndiye anayestahili kuwa mshindi kwenye Sabasaba Expo ijayo?
Watoto mashuleni hawana madeski, vitabu na vifaa vya kujifunzia vya kila aina. Je, kwanini zawadi wasipate wale watakaokuja na ufumbuzi wa matatizo hayo.
Mahospitali yetu yanafungwa na huduma kusimama kila kona nchini. Je, ushindani utakaofaa si ule wa utengenezaji wa zana na vifaa mbalimbali vya mahospitali hapa nchini ili viuzwe kwingineko kwa bei nafuu kuliko vinavyotoka nchi za nje? Maana, ukiwa na teknolojia duni katika hospitali au chuo ndivyo pia shule yenye inavyokuwa duni na ovyo kihali na kimazingira. Teknolojia ya kisasa inalazimisha usasa kwa kiwango cha juu ikiwemo usafi, mandhari na mazingira bora zaidi.
Mambo mengi yako ndani ya uwezo wetu. Kinachotakiwa ni kuona kwamba keki ya taifa inagawika kwa namna ambayo wajasiriamali na wazalishaji mali mbalimbali nao wanapata kitu cha uhakika ili kuleta mabadiliko tuliyokusudia nchini.
Nia na sababu ya kuwepo kwa maonyesho ya sabasaba ilikuwa ni kuiwezesha nchi kuwa na kipimamaendeleo kitakachoonesha jana tulikuwa wapi na leo tumefikia wapi. Lakini tukiwa mwaka nenda, mwaka rudi tunaonesha vilevile vya juzi basi kuna walakini mkubwa hapo. Utandawazi na makuzi ya teknolojia hayaturuhusu kuwa goigoi na wenda pole kiasi hicho.
Kiwanja kipya cha sabasaba lazima kiwe kikubwa kweli kiasi cha
kuwa na uwanja wa ndege mdogo, kituo cha treni, kituo cha basi, mabohari na vingine kama hivyo. Hili likifanyika foleni za kutisha zitakuwa historia maeneo ya Temeke. Na ili kuanza kutekeleza azma njema ya kutenga maeneo ya biashara na makazi ya wau au maofisi ni vyema kama uwanja wa Sabasaba hivi sasa utafanywa kuwa ni TEMEKE PUBLIC SHOPPING PLAZA AND SUPERMARKETS.
Uwanja mpya lazima uwe pia na hoteli ya hadhi ya kitalii kwa maana ya nyota 5 kwenda mbele. Uwanja wa golfu wa kisasa kabisa na vilevile uwanja wa mbio za langalanga (Formula 1) ili kutumika kwa uwanja huo mara kwa mara uwe ni kitu cha uhakika.
Wakati wa maonesho ni vyema uwanja huo ukawa na redio stesheni na TV ya maalum kwa ajili ya mawasiliano. Kwa upande mwingine kutakuwa na eneo la Tovuti au Intaneti ambako wafanyabiashara na wajasiriamali wa kila aina na rika watapata fursa ya kujifunza kufanya kazi zao kwa kutumia Teknohama.
Katika kufanya mabadiliko haya makubwa ni muhimu
kuwashirikisha watu wa nje kama Wajerumani, Wajapani na Wachina waliokubuhu katika mambo ya 'expo'.
Thursday, July 7, 2011
Kiswahili ndio ufunguo wa maendeleo yetu
TANZANIA miaka hamsini baada ya Uhuru ni motokaa mpya kimaendeleo ambayo mpaka leo bado linasukumwa kwa kuwa ufunguo wa kuliwasha gari hilo bado haujapatikana.
Ufunguo huo si mwingine ila ni kutaradadi kwa Kiswahili ili kitawale na kuendesha mambo yetu yote huku tukijua fika kwamba idadi ya Watanzania ambao hawatakuna wala kufanya biashara na wageni ili kuhitaji kutumia lugha nyingine ni zaidi ya asilimia 95.Kwa maneno mengine, ni asilimia tano tu au chini ya hapo ambao wanahitaji kujua lugha za kigeni.
Ili kuyakabili matatatizo au changamoto mbalimbali zinazokabili nchi na watu wetu ni lazima Kiswahili kituongoze na sio sisi tukiongoze Kiswahili. Waliojaribu kukionogza Kiswahili ili kituongoze ndio waliotufikisha hapa tulipo leo tofauti na watu wanaotumia lugha mama yao kuendeleza nchi zao.
Inaonekana jitihada za kuzibana lugha za Kienyeji nchini ili Kiswahili kitawale hazikuweza kutumika pia kuwa jibu kwa utandawazi kwa Kiswahili kutuongoza katika kukabiliana na changamoto hizo kwa sababu ya kulaghaiwa na wazungumzaji lugha ya kikoloni-Kiingereza.
Katika miaka hii ambayo nchi zinazozungumza Kiingereza zimeanza kushuka ngazi na zile zinazozungumza lugha nyingine ndio kwanza zinapanda juu na juu zaidi ni wakati muafaka wa kujiuliza kama ni sahihi kukubali kuhadaiwa na tafiti na fedha za misaada ili tuendelee kukiacha KIswahili kama lugha yatima.
ILI kusoma makala yote tuandikie SMS yenye e-mail yako: 0787-808539.
Ufunguo huo si mwingine ila ni kutaradadi kwa Kiswahili ili kitawale na kuendesha mambo yetu yote huku tukijua fika kwamba idadi ya Watanzania ambao hawatakuna wala kufanya biashara na wageni ili kuhitaji kutumia lugha nyingine ni zaidi ya asilimia 95.Kwa maneno mengine, ni asilimia tano tu au chini ya hapo ambao wanahitaji kujua lugha za kigeni.
Ili kuyakabili matatatizo au changamoto mbalimbali zinazokabili nchi na watu wetu ni lazima Kiswahili kituongoze na sio sisi tukiongoze Kiswahili. Waliojaribu kukionogza Kiswahili ili kituongoze ndio waliotufikisha hapa tulipo leo tofauti na watu wanaotumia lugha mama yao kuendeleza nchi zao.
Inaonekana jitihada za kuzibana lugha za Kienyeji nchini ili Kiswahili kitawale hazikuweza kutumika pia kuwa jibu kwa utandawazi kwa Kiswahili kutuongoza katika kukabiliana na changamoto hizo kwa sababu ya kulaghaiwa na wazungumzaji lugha ya kikoloni-Kiingereza.
Katika miaka hii ambayo nchi zinazozungumza Kiingereza zimeanza kushuka ngazi na zile zinazozungumza lugha nyingine ndio kwanza zinapanda juu na juu zaidi ni wakati muafaka wa kujiuliza kama ni sahihi kukubali kuhadaiwa na tafiti na fedha za misaada ili tuendelee kukiacha KIswahili kama lugha yatima.
ILI kusoma makala yote tuandikie SMS yenye e-mail yako: 0787-808539.
Subscribe to:
Posts (Atom)