Thursday, July 7, 2011

Kiswahili ndio ufunguo wa maendeleo yetu

TANZANIA miaka hamsini baada ya Uhuru ni motokaa mpya kimaendeleo ambayo mpaka leo bado linasukumwa kwa kuwa ufunguo wa kuliwasha gari hilo bado haujapatikana.

Ufunguo huo si mwingine ila ni kutaradadi kwa Kiswahili ili kitawale na kuendesha mambo yetu yote huku tukijua fika kwamba idadi ya Watanzania ambao hawatakuna wala kufanya biashara na wageni ili kuhitaji kutumia lugha nyingine ni zaidi ya asilimia 95.Kwa maneno mengine, ni asilimia tano tu au chini ya hapo ambao wanahitaji kujua lugha za kigeni.

Ili kuyakabili matatatizo au changamoto mbalimbali zinazokabili nchi na watu wetu ni lazima Kiswahili kituongoze na sio sisi tukiongoze Kiswahili. Waliojaribu kukionogza Kiswahili ili kituongoze ndio waliotufikisha hapa tulipo leo tofauti na watu wanaotumia lugha mama yao kuendeleza nchi zao.

Inaonekana jitihada za kuzibana lugha za Kienyeji nchini ili Kiswahili kitawale hazikuweza kutumika pia kuwa jibu kwa utandawazi kwa Kiswahili kutuongoza katika kukabiliana na changamoto hizo kwa sababu ya kulaghaiwa na wazungumzaji lugha ya kikoloni-Kiingereza.

Katika miaka hii ambayo nchi zinazozungumza Kiingereza zimeanza kushuka ngazi na zile zinazozungumza lugha nyingine ndio kwanza zinapanda juu na juu zaidi ni wakati muafaka wa kujiuliza kama ni sahihi kukubali kuhadaiwa na tafiti na fedha za misaada ili tuendelee kukiacha KIswahili kama lugha yatima.


ILI kusoma makala yote tuandikie SMS yenye e-mail yako: 0787-808539.

No comments:

Post a Comment