Sunday, January 5, 2014
Rai kwa rasimu ya pili ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Kwanza, ninapoingeza Tume ya Warioba (Rasimu ya Katiba ya JMT) kwa kazi yao nzuri ambayo kila mtu ameiona na wakati huohuo kuwarai Watanzania wenzangu kumuenzi kiongozi huyu na timu yake, sasa na siku zijazo na kuhakikisha wanakuwepo kitwasira katika sebule kuu za taifa letu kwa ajili ya kumbukumbu kwa vizazi vijavyo.
Kazi iliyobakia kwetu sisi wananchi ninaamini ni kama kung'arisha kitu ambacho utengenezaji wake umeshakamailika na imebakia tu mambo tudogotudogo hapa na pale kuikamilisha.
Katika makala haya nitaangazia mambo machache tu ambayo kwa uoni wangu wa haraka haraka nadhani yanahitaji kuangaliwa kwa undani zaidi wakati wa mikutano ya Bunge la Kuboresha Rasimu ya Katiba mpya.
Mapato yatakayotokana na gesi, petroli na madini yetu ni lazima yaelekezwe kwenye elimu. Sioni ibara ifuatayo kwanini isisomeke kama ifuatavyo, yaani kifungu
42. (b) kingelisomeka kama: "kupata elimu bora ya msingi na sekondari.....yaani.
Kuhusu Haki ya elimu lazima itangaze pia kwamba pamoja na yaliyomo hivi sasa ni
haki kwa taasisi yoyote ile inayotoa elimu kutoa elimu yoyote ile kwa lugha mwenye au wenye taasisi na walengwa wanayoitaka; katika kujenga usawa kati ya mikoa, kila mkoa utakuwa na angalau chuo kimoja kikuu cha umma; na kwamba elimu toka chekechea hadi sekondari itatolewa kwa gharama za pato la taifa hususan kutokana na utajiri weu wa madini na mali asili kwa faida ya wengi; na kwamba elimu itakayotolewa italenga siku zote kuwawezesha vijana wa nchi kutatua matatizo ya nchi na watu wao na hivyo kukuza ajira kwa kuboresha maisha ya waliio wengi.
Pamoja nayaliyomo katika ibara ya 44 ingelifaa yaongezwe pia kwamba ni jukumu la serikali kuu kuwajengea vijana mazingira ya kujiajiri wenyewe kwa kujifunza kuwa wabunifu, wavumbuzi na kujiingiza katika ujasiriamali na taifa kwa kutumia hazina yake itawajengea mazingira ya kuweza kukopeshwa na kupata nyenzo nyenginezo za kuwasaidia kujiajiri na kujitegemea....lengo likiwa ni kupunguza idadi ya mashine, magari na mitambo tunayonunua toka nje kwa sisi wenyewe kuvitengeneza hapa hapa nchini baadhi ya vitu hivyo.
Tunaijua hali ya nchi yetu na mapungufu yake, je, Tunu za kitaifa zilizoanishwa zinatutosha au ingelifaa pia tuongeze tunu nyengine kama:
utamaduni, mila na desturi chanya mbalimbali na usasaishaji wake;
ukweli; uaminifu; usafi; ubunifu na uvumbuzi na udhibiti kamilifu na bora wa majukumu na kazi kubwa kwa ndogo nchini.
Nina wasiwasi pia kama sifa anazostahili kuwa nazo mtu anayestahili kugombea urais kama zimeainishwa katika rasimu hii. Labda zimefutika kwenye nakala yangu, maana ukweli sikuziona. Je, tutapata kiongozi bora kama rais wa muungano bila ya kujua tunahitaji mtu wa aina au namna gani?
Ibara ya 32 inayozungumzia uhuru wa imani ya dini kwa baadhi ya watu inaonekana kuning'inia. Baadhi ya maswali yanayoulizwa ni je inajitosheleza bila kuzungumzia masuala kama: hakuna taasisi au chombo chochote kitakachopewa na katiba au sheria chini ya katiba hii ukiritimba juu waumini wa imani au dini yoyote ile iwayo; viongozi wa ksiasa na kiserikali hawataruhusiwa kwa namna yoyote ile kuwachagulia waumini viongozi wao; kwa imani zinazopenda serikali na wafadhili watasaidia kuwajengea waumini miundo na mifumo ya kuendesha mambo yao ili kuendana na wakati; serikali na wahisani wa ndani na nje wanastahili kusaidia kila imani kukamilisha masuala yao ya ibada kwa kuwa na taasisi na watu wanaochangia ukamilikaji wa ibada zao; na kwamba sio tu haitaonekana bali haitakubalika kwa kikundi chochote katika jamii kuishawishi serikali kuinyima imani fulani ya kidni kuwa na mifumo, miundo na rasilimali watu muhimu wanaohitajika kukamilisha imani yake.
Wale wanaosema kwamba suala la Mahakama ya Kadhi, mathalani, sio la muungano ni muhimu wafafanue kama katiba ya muungano ni katiba mama, au ni katiba za Tanganyika na Zanzibar ndio katiba mama?
Ni dhahiri kutokana na miaka mingi ya utawala wa mfumo wa chama kimoja, muda unahitajika pia kuwabadili kimawazo na kivitendo baadhi ya watendaji watakaokuwa wamezoea kuwa watumishi wa umma na wakati huo watumishi wa chama cha kisiasa....
Kwa yale mambo ambayo yanayonekana yanaweza kuwa chanzo cha kutokuelewana miongoni mwetu, fujo au ghasia au kusababisha 'tokomeza' nyingine kama yasiporekebishwa sasa hivi, ni vyema yaanze mara moja....
Kuhusu uhuru wa vyombo vya habari, bunge letu kwa kushirikiana na mabunge mengine ya Afrika Mashariki yatatunga sheria moja ili kuoanisha mitazamo yetu na kuvipa vyombo vya habari kutimiza wajibu wake kwa jamii zetu bila mikwaruzano na serikali isiyo ya lazima.
Kiujumla kuna vifungu kadhaa katika rasimu hiyo ambavyo kwa faida za baadaye za kisheria ni muhimu kupanuliwa zaidi ili kile kinacholengwa hatimaye kipatikane kiurahisi bila shida kwa walengwa wa katiba hii mpya.
Vifungu vingi vinavyohsu mamlaka, haki na wajibu wa wananchi na wale watakaowatawala ni lazima vifafanuliwe zaidi ili kuondokana na kosa kubwa linalotokea kwenye katiba yoyote mpya, nalo sio lingine ila lile la kuzusha migongano inayokuja kuleta ukinzani mgumu mbele ya mahakama panapokuja kuzuka tatizo ambalo misingi yake haikufafanuliwa ipasavyo.
Ingawa Tume ya Jaji Warioba imependekeza pawe na miaka minne hivi ya mpito, kwa upande wangu ninaona ingelifaa yale yanayowezekana kufanyika leo leo, yafanyike, na yale ambayo kwa namna fulani yanastahili kufanyiwa kazi zaidi ndiyo yacheleweshwe.
Rasimu imekaa kimya pia juu ya suala la madaraka mikoani au mikoa iliyo huru kiuchumi na haja ya kupunguza utititri wa wakuu wa wilaya nchini. NInaamini wajumbe wa bunge la katiba wataendelea kulishughulikia ili kupata muafaka wenye manufaa kwa Watanzania.
Je, ni muhimu Uchaguzi Mkuu ujao ufanyike 2015. NInadhani sio lazima. Kama nikiruhusiwa, ningelipendekeza kwamba Rais Jakaya Kikwete angeongezewa miaka miwili 2005-2007 ambacho kitaitwa kipindi cha mpito cha kukamilisha kazi ya katiba iliyosalia. Katika muda huu pengine Mheshimiwa Kikwete atambulike kama Rais wa muda wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na kazi yake kubwa itakuwa kuzisaidia Tanganyika na Zanzibar kama nchi mbili katika muungano mpya kupata viongozi wanaofaa. Kwa maoni yangu Uchaguzi Mkuu wa Tanganyika, Zanzibar na ule wa Muungano wa Tanzania ungestahili kufanyika Januari 2007. Na kuanzia hapo mwaka wetuu wa kifedha ubadilishwe pia na kuanzia Januari na kuishia Disemba ili kupunguza matatizo yanayoendana na mwaka wa kifedha tunaotumia kwa hivi sasa.
Tutakachokikosa hapa zaidi ni kutokuwa na chaguzi zinazofanyika kwa miaka inayoishia 0 au 5.
Wengi waliofanya haraka ya kutaka kuikamilisha katiba na wakati huoo kuendesha uchaguzi mkuu kwingineko Afrika wamejikuta na matatizo mengi kuliiko walivyotegemea.
Ninaamini kama pendekezo langu litakubalika basi Tanzania itapata muda wa kutosha kufanya maandalizi na marekebisho muhimu yatakayozisaidia nchi zetu mbili na serikali ya muungano kuanza vizuri na kuepuka shinikizo na songombingo zisizo za lazima.
NI dhahiri kama teuzi kadhaa za watu muhimu; na kwamba mawaziri hawatatokana tena na wabunge; na kwamba kutakuwa na Tume Huru ya Uchaguzi na wagombea huru kwa nafasi mbalimbali ni jambo litakalohitaji muda wa kutosha.
Friday, August 23, 2013
Reli ya Tanga- Taveta - Arusha igeuzwe Chuo Kikuu cha Ujenzi wa Reli nchini...
HOJA yangu binafsi leo ni kwamba Tanzania baada ya miaka hamsini ya
uhuru haina sababu ya kutegemea nchi nyingine duniani katika ujenzi wa
baadhi ya miundombinu yake na uwepo wa viwanda vinavozalisha mitambo
na mashine muhimu katika maendeleo yake ya kiuchumi na kijamii na
ujenzi wa nchi kwa ujumla. Vijana wengi niliowauliza walimaka: '
Na kufuatia uamuzi wa Kenya kujenga upya reli yake kati ya Mombsa na Malabo kwa msaada wa Wachina, huku Rwanda na Burundi nazo kupitisha mizigo yake kupitia Kenya, upo uwezekano mkubwa wa ujenzi wa bandari ya Bagamoyo kuwa ghalibure na hasara na mzigo usiobebeka kwa kizazi kijacho. Itakuwa ni busara na hekima kutumia njia mbadala za ujenzi wa reli zetu nchini na badala ya kuviongezea vizazi vijanvyo mzigo wa madeni kuvipunguzia zigo hilo ogepewa. Badala ya kuzungumzia serikali mbili, haya ndiyo mambo ambayo vijana wa Tanzania kuonesha wako mbele ya vijana wengine wa Kiafrika walikuwa wanapaswa kuzungumzia. Na sio kuzungumzia mikakati ya kuua kabisa matumaini ya umoja wa Afrika ili kuzima kiu na kushibisha njaa ya leo.
Ujenzi wa reli kwa akili zetu wenyewe na rasilimali zetu wenyewe sio tu utaondosha baadhi ya matatizo yetu bali utawapa vijana wa nchi hii kuwa wajenzi wa reli waanzilishi hapa Afrika. Ili tuwe nchi bora na nchi mali lazima viongozi na wananchi wetu tuone mbali kuliko jirani wanaotuzunguka.
Tunacheleweshwa mno!' Na kwamba uwekezaji mkubwa unaostahili kufanywa
na nchi inayotaka kuendelea kikweli kweli ni katika vijana wake na sio
tu ardhi , migodi na viwanda.
Katika miaka hamsini ya mwanzo kutokana na kukosa watu waliosoma,
shule na vyuo stahilifu, raia wanaojijua na sababu ya kuwepo kwao,
wajasirimali, vijana wabunifu, mitaji, masoko, teknolojia muafaka na
mitandao ya kusaidiana kufanikisha azma fulani palikuwa hapana njia
ila kuvumilia tu kutegemea watu wengine watujengee nchi yetu huku sisi
wenyewe tukijifunza.
Hoja yangu inapewa nguvu na makali na ukweli kwamba tumeshajifunza
kiasi cha kutosha sasa; tuna shule na vyuo stahilifu; na wapo wasomi
nje na ndani ya nchi wanaotaka kuchangia kwa hali na mali kutatua
matatizo ya watu na nchi yao pindi wanapowezeshwa na kurahisishiwa
kufanza hivyo. Vijana wengi wa Kiafrika wamechoka kuona wanabwebwa na
kudekezwa na kunyimwa kufanza mengi kama vile wao ni watoto na
wazungu au wageni wengine ndio watu wazima. Wanataka kuonyesha utundu
wao, kujaribu, kuthubutu na hatimaye kuweza kuanza kutoa mchango kwa
maendeleo ya nchi na watu wake haraka iwezekanavyo. Wakati huko
Chinana kwingineko Asia, vijana wa miaka 18 wanaanzisha miradi na
kuwa na kampuni zao wenywe, hapa Tazania ndio kwanza tunamficha kijana
shuleni asome, kisha afeli na kukata tamaa na maisha.
Isitoshe hivi leo dunaini kuna mitandao na rasilimali za kielimu,
kiujuzi na kimaarifa za kila aina kumuwezesha mwanadamu kuunda
chochote anachokitaka; teknolojia zinatafutwa kwenye intaneti kirahisi;
soko kwa ajili ya miundombinu ya namna hii bado bikra kabisa Afrika;
kuna taasisi za kila aina kuwawezesha vijana kupata mtaji mradi tu
wapate mdhamini; nchi ina vijana wabunifu ambao vipaji vyao vinahitaji
kuengwaengwa na kuendelezwa kidogo tu, pasina ubabaishaji,unafiki,
kumjua huyu ni wa nani na yule si wa nani, wala upendeleao;
wengi wa vijana wetu leo ni watu wanaojitambua kuwa sababu ya kuwepo
kwao sio starehe na anasa bali kubwa zaidi na la mwanzo kabisa ni
kusaidia nchi yao kuondokana na umaskini, ujinga na mardhi, na hali
kadhalika elimu na vipaji vya ujasiriamali na maarifa ya kiuchumi na
kiteknohama vinachipua kama uyogakila kona nchini.
La kujiuliza baada ya miaka hamsini ya uhuru ni je, elimu
tunayoendelea kuitoa hapa nchini inasaidia nchi kwa kiasi gani kutatua
matatizo ya nchi na watu wake?
Nchi yetu ina matatizo mbalimbali yakiwemo yale ya
usafiri na uchukuzi- ikiwemo uundaji na utengenezaji wa reli, meli,
ndege, vyombo vingine vya usafiri na uchukuzi, bandari, barabara,
viwanja vya ndege, chakula, maji, nishati nafuu na rahisi kutumika, na
viwanda mama na viwanda vidogovidogo.
Nchi yetu bado inahitaji pia nyumba bora kwa ajili ya wanacnhi wake
na hasa vijijini; shule, hospitali, vijiji na miji safi na bora
zaidi. Achilia upatikanaji kirahisi wa maji, umeme na huduma za usafi
na utunzaji mazingira nchini.Aidha, tunahitaji kuzlisha mazao na
bidhaa mbalimbali kwa kiwango cha kimataifa na vile vile ktuoa huduma
zinazokubalika kimataifa ili tusipate ulazima wa kujitengenza na kuwa
wasafi pale mgeni ajapo kututembelea kwa usafi na mazingira bora kuwa
ni sehemu ya maisha yetu ya kila siku.
Nitazungumzia leo tatizo moja tu, lakini ninaamini fikra za ufumbuzi
wa tatizo hilo zinaweza pia kutumika kwenye kutatua matatizo ya mahaa
na aina nyingine kiurahisi kama itavyowezekana katika hili.
Yeyote anayetembelea miji au vijij kando ya reli ya Tanga-Kahe-
Taveta- Arusha kam vile vya Mkumbara, Hedaru, Pongwe, Magunga, Mombo,
Korogwe, Makanya, Chekereni, Himo, Uchira, Kahe, Mtakuja, Kiyungi,
Rongoi, Rundugai, KIA, USA River na kadhalika hakosi kuona nini hali
ya sehemu na maeneo hayo ingekuwaje laiti Shirika husika la reli
lingelikuwa bado linatoa huduma zake na hasa katika ubebaji mizigo na
mifugo.
Jambo hili tukilifanza kwa njia ya utegemezi na kusubiri h isani ya
wafadhili litatuchukua miaka kama sio miongo kadhaa. Lakini jambo hili
hili tukijifunga kibwebwe na kulianzishia shule au chuo cha ujenzi wa
reli kwa kuitumia njia hiyohiyo ya reli ya Tanga-Moshi-Taveta na
Arusha linaweza sio tu kufnyika haraka, lakini pia likawa ndio mwanzo
wa Tanzania kuachana na kuzitegemea nchi nyingine katika uundaji wake
wa magarimoshi na utengenezaji wa njia zake za reli.
Chuo hiki kinaweza kuanza kwa vifaa vilevile ambavyo bado vipo kwenye
maeneo ya shirika hilo kwenye mikoa husika. Kwa kutumia mabehewa ya
zamani na mahema vijana wakaanza mwaka wa kwanza kwa kujifunza masomo
ya msingi katika uhandisi wa njia za reli na uundaji garimoshi.
Wakishajifunza sayansi, mahesabu na teknolojia za msingi vijana hao
katika mwaka wa pili wanaanza kazi ya kulaza reli upya katika njia
husika kwa kutumia viberenge huku wakisadiana mafundi wa kulipwa na
kujitolea kutoka sehemu mbalimbali duniani ambako huko kwao hivi leo
hawana ajira na wanangojea fursa kama hii kwa hamu sana.
Mwaka unaofuata kwa kusaidiwa na serikali na watu wanaoipenda nchi
yetu popote kule duniani vijana wanaanza kufufua au kukarabati
mabehewa na vichwa vya treni huku mipango ikiandaliwa kimkakati kuwa
na karakana au viwanda bora zaidi vya kufanyia kazi hiyo kwa
kuwatumia wafanyakazi wa zamani katika sekta za reli ndani na nje ya
nchi. Msaada huu utawezeshwa zaidi kwa kuwa na mawasiliano ya uhakika
kati ya wahadhiri na wanafunzi chuoni hapo na mabingwa wa reli
kimataifa kupitia simu za mkononi na nyenzo kama facebook. Badala ya
facebook kuzipindua nchi zetu, sasa itatumika kuleta mapinduzi ya
kujitegemea kiufundi na kitaalamu katika nchi zetu.
Baada ya hapo huduma inaanza kwa uchukuzi wa mizigo na mifugo kwanza
kabla usafirishaji binadamu haujaanza huku vijana wakijifunza
menejimenti na utawala au uendeshaji bora wa sekta ya reli nchini na
Afrika kwa ujumla. Hili likifanyika, wakati huo huo chuo kinaanza
kujitangaza na kutafuta tenda za ujenzi wa reli katika nchi kama
Kongo, Afrika ya kati, Chad, Zambia, Angola na kwingineko duniani
ikiwemo India, Urussi, Amerika ambayo njia zake za reli zimechakaa
kupita kiasi.
Wakishamaliza mafunzo ya bashara na menejimenti kuu, sasa vijana
watajimwaga kusomea masomo kama vile menejimenti ya operesheni,
logistiki, uboreshaji safari za treni kwa kuwa na treni ziendazo kasi
na kutumia umeme, utafiti na uvumbuzi muafaka katika kuendeleza na
kuimarisha uchukuzi na usafirishaji kwa kutumia reli na masuala
mengine ya kitaifa na kimataifa yatakayochangia katika kuifanya nchi
kuwa mfano na kitovu cha ujenzi reli asili hapa Afrika.
Vijana wanaopitia mchakato huu pindi wanapohitimu sio tu watapata
vyeti vinayotambulika kimataifa, lakini, chuo na wabia wake kibiashara
kinamwajiri papo kwa hapo. Inawezekana kweli kwamba nipo kwenye ndoto,
lakini muamuzi mzuri wa hili ni kijana wa Tanzania asiyekuwa na ajira
hivi sasa. Tumuulize, hli linawezekana au haliwezekani?
Sunday, July 28, 2013
Bomu linalosubiri kulipuka Afrika: Tofauti ya walionacho na wasionacho..
Kabla ya 2010 dunia ilijikita zaidi katika kushughulikia changamoto zilizosababishwa na athari au madhara yanayosababishwa na walimwengu kwa hali ya hewa na mazingira duniani. Kuanzia muongo wa pili wa karne ya ishirini na moja, hata hivyo, mtazamo na mwelekeo wa wanauchumi na wanajamii kwa ujumla umekuwa ukiegema zaidi upande wa namna au jinsi ambayo masuala ya kiuchumi na kijamii yanavyoweza kuhatarisha sio tu maisha ya mwanadamu, bali hata kuzidisha uwezekano wa athari mbaya dhidii ya mazingira na hali ya hewa kuongezeka.
Katika makala ya leo tutajikita zaidi katika suala la kukua tofauti za kipato au kiuchumi kati ya wale wenye nacho na wasionacho.
Tafiti zilizofanywa na Prof. Joseph E. Stiglitz wa Chuo Kikuu cha Columbia cha nchini Marekani, ni kazi nzuri inayokuja wakati muafaka katika kuitahadharisha dunia kuwa mfumo wa ubepari usiodhibtiwa budi utazipeleka nchi na dunia kubaya. Na kwamba upo umuhimu wa kujitoa kimasomaso kuja na sera ambazo hazitaipelekea Afrika kujikuta kwenye masahibu ambayo baadhi ya nchi za Ulaya na Asia leo zinalazimika kuyafungia kibwebwe.
Mfano wa nchi ambazo zinajenga mfano mzuri wa kuigwa katika kudhibiti pendo kati ya walionacho na wasionacho ni nchi za Skandinavia. Nchi hizo hazina muujiza wowote ila tu ni kule kuanzisha kwao na kutunza mikakati na sera ambazo wanazitumia kuzuia kulipuka kwa tofauti kubwa katika kipato cha watu wa kima cha juu na wale wa chini. Sera hizi hubainika na wengi duniani kama mfumo wa ujamaa wa kidemokrasia.
Laiti Tanzania isingetupa moja kwa moja siasa ya Ujamaa na Kujitegemea leo tusingekuwa na cha kuandika hapa. Hasara yetu ni sawa na ile ya mwogeshaji mwana, kumtupa mwana na maji machafu aliyeogeshewa.
Nchi zinazoathirika zaidi ni zile zenye kukosa azma na sera kwa malengo ya kisiasa na kijamii yaliyo dhahiri na yanayokubalika kama dawa mujarabu kwa tofauti za kiuchumi na kipato katika jamii husika.
Aidha, vijiji kusahaulika kimaendeleo kwa kukosa mipango ya kuvisaidia kupata uongozi au menejimenti bora ikiwemo ile ya rasilimali watu, usimamiaji uzalishaji mali, utafutaji mitaji na masoko Ujamaa, ubepari ni jambo jengine linaloendelea kuchangia kukua kwa tofauti za kipato hususan kati ya watu wa mijini na wale wa vijiini. Sera zozote zinazochania kumnyang'anya masikini hata kile kidogo alichonacho sio chachu ya kudumisha amani na umoja katika jamii husika.
Katika nchi nyingi zilizoanza na kuendelea na ubepari tofauti hizi husababishwa kwa kiasi kikubwa kwa baadhi ya watu aidha kuzaliwa katika utajiri au ukubwa au nafasi zenyemlo na wengi wengine katika umaskini, hivyo kuwapa wale wa kwanza mtaji wa kiuzawa na vilevile kutokana na tofauti za kiajira na kielimu na uweledi wa kiteknolojia na utaalamu wa tasnia husika.
Katika nchi zilizokuwa zikifuata ujamaa tofauti hizi zinazaliwa na watawala waliokuwa wajamaa kugeuka mabepari kwa kunufaika na mali zilizokuwa za umma huku wakigwaya kukiri kwa wananchi wao kuwa wao na nchi sasa ni ya kibepari na sio tena ya kijamaa; utumishi unaojali zaidi uswahiba na udugu na sio tija na ufanisi; utegemezi wa upendeleo, rushwa na teni pasenti kwa vyama tawala badala ya njia halali za mapato; wanasiasa kununuliwa na matajiri na fisadi; mabenki na taasisi nyingine za fedha kuwa chini ya wanasiasa wanaotawala; misaada toka nje kuwanufaisha watawala kuliko wananchi; kukosa uwazi na uwajibikaji katika usimamizi wa mipango, mikataba, siasa na sera za nchi husika; kusaini mikataba mibovu kwa faida ya chama na watu binafsi na sio kwa faida ya umma; kukosekana ushindani wa kweli wa kidemokrasia kisiasa na kiuchumi;kuwanyima fursa wapinzani wa kisiasa na watawala au watu wao kupewa fursa hizo; uwepo wa makampuni yasiyotozwa kodi tosha na ambayo yanaweza kuzaini umma na yenyewe kutengeneza mabilioni kama sio matrilioni katika muda mfupi tu bila udhibiti na ukaguzi wa uhakika toka kwa wanaohusika na ardhi na maliasili za nchi kuwafaa zaidi watawala, wageni na wenye nacho na sio mwananchi wa kawaida.
Jambo jengine linachangia si haba kukuza pengo kati ya walio nacho na wasio nacho ni lile la kukosa vigezo vinavyokubalika katika ajira na ujira. Kwenye nchi nyingi waliosoma sana na wenye ujuzi mkubwa zaidi ndio hulipwa kidogo lakini wasiosoma bali wana vyeo wao wakafaidi ujira, masurufu na maduhuli makubwa zaidi.
Nchi nyingi maskini kama vile Tanzania zina matatizo pia ya kushindwa kuwa na sera na mipango inayofanya kazi katka masuala ya matumizi na ugawanyaji pato la taifa kitaifa, kijamii mbalimbali na kati ya tasnia na makundi kazi mbalimbali katika jamii.
Kosa lingine linalochangia kukua kwa pengo kati ya walionacho na wasio nacho ni kushindwa kuipa mali asili yetu kama ardhi, madini, mimea na watu wetu thamani stahilifu na inayoweza kuwanyanyua watu wetu kiuchumi na kimapato kwa njia moja au nyengine.
Udhaifu katika menejimenti ya uchumi wa nchi na hasa uzalishaji mali na ujasiriamli ikiwemo, mathalani, fursa ya kuviongoza vijiji kiuchumi na kimapato zaidi nayo inachangia tatizo hili si haba. Kuna wanaodai kuwa vijiji na wanavijiji wakiboreshewa tu masuala ya menejimenti na utawala nchi inaweza kupunguza nusu ya umaskini wake kwa haraka zaidi kuliko inavyotarajiwa na hasa panapokuwa na uwekezaji unaolenga kutmia kile wanakiji walichonacho katika kuwasaidia kupata maendeleo makubwa zaidi.
Siasa za WB, IMF ambazo leo zinakataliwa na Ulaya na Amerika wanaopitia matatizo yaleyale kama yetu zinahitaji pia kukataliwa waziwazi kwani zinachangia hatari ya kutuletea matatizo makubwa zaidi siku za usoni.
Ipo haja ya kuangalia upya, baada ya nchi yetu sasa, kugundua mali asili mpya kama gesi, mafuta ya peteroli na madini salama kuvunwa ya aina mbalimbali ni kwa jinsi gani Tanzania inaweza kurejea tena kwenye mfumo mzuri uliodhibiti vilivyo tofauti ya kipato na kiutajiri kati ya watu wetu kama vile utoaji elimu bure; utoaji huduma za afya bure; kutoa ruzuku katika huduma muhimu kama zile za maji na umeme, usafirishaji na uchukuzi; kuwatunza maskini, yatima na wajane kwa kujitolea na nyenginezo kama hizo.
Benki Kuu na vyombo vyetu vya fedha lazima zibadilike ili kuwa vyombo vya kupunguza pengo kati ya walichonachona wasionacho kwa namna moja au nyengine. Na kuu katika hili ni kuhakikisha kuna mifuko maalum ya kusaidia miradi kwa wanavjiji, vijana, wanafunzi wanaomaliza shule na wanatafuta kujiajiri na watu kama hao kwa kuiga mifano iliyofanikiwa ndani na nje ya nchi ili kzungusha pato la taifa na kutoa fursa kubwa zaidi ya uwekezaji wa wazawa nchini.
Tuesday, April 23, 2013
Migogoro ya Kiimani matunda ya kukosa uongozi jumuishi, bora na adilifu kijamii, kiuchumi, kidini na kisiasa
NCHI zote ambazo asili na utu wao unatawakali mbele ya vitu vingine duniani ndizo zilizotulia na zilizoepuka machafuko na migogoro ya kijamii na kiimani kwa kiasi kikubwa. Kuanzia Uarabuni, Uchina, India, Urussi, Vietnam, Malaysia, Indonedia, Ufilipino na kddhalika.
Matatizo katika nchi hizi yanakuja pale mataifa haya yanapoanza kuzainiwa na kuacha kutanguliza asili, historia na utu wao kwanza na wakakubali kutanguliza kitu kingine mbele iwe dini au maslahi fulani au ukabila au ueneokijiografia au uchama na kadhalika.
Utaifa, historia, desturi na utamaduni wa watu vinapopewa hadhi stahilifu husaidia sana na kuiepusha nchi kukwepa pepo za ushawishi na mbadaliko ya kimtazamo kutokana na kuingiliana na watu wa asili na tamaduni nyingine.
Migogoro ya kiimani Afrika na hususan Tanzania ni matunda ya kuurudisha nyuma Utanzania na Uafrika wetu na kutanguliza maslahi ya kiitikadi na kibinafsi miongoni mwetu na hasa kati ya viongozi wetu.
Hili nalo kwa maoni yangu linasababishwa na kushindwa kutambua kwamba uongozi bora ni jambo la ushirika kiushauri na la pamoja. Ukijenga ukiritimba katika uongozi mara nyingi unaharibu, badala ya kutengeneza.
Kila jamii ina aina mbalimbali ya viongozi. Kuna viongozi wa kiseriikali, kisiasa, kiimani, kimila/kiutamaduni, kiuchumi/kibiashara, kiteknolojia na kadhalika. Pale viongozi wa kiutawala au wa kisiasa wanapoona kwamba wao ndio tu wanaostahili kuitawala jamii na sio viongozi wa aina nyingine, basi migogoro katika jamii hiyo haiishi na imani ya wananchi kwa viongozi wao hao hupungua kwa kiasi kikubwa.
Katika hili yapo mengi ya kumuiga mwasisi wa taifa hili, Mwalimu J.K. Nyerere na moja kubwa ni kwamba hakusita kuwaita na kuwaambia waziwazi na bayana viongozi wa kiimaniya kwamba mpaka we0katika hili ni huu hapa na msivuke mstari huu. Maana Mwalimu aliutanguliza kwanza Uafrika na Utanzania wake kabla ya kitu kingine. Kuutanguliza Utanzania, Uafrika na utu wetu mbele ya kttu kingine ndiyo nguzo ya kwanza ya amani na umoja wetu. Athubutu mwingine kutwambia vingine. Ninaona katika hili, hivi leo kuna udhaifu mkubwa miongoni mwa viongozi wetu.
Endapo tunataka kuondokana na migogoro inayolinyemelea taifa letu kwa hivi sasa ni lazima tuukubali ukweli huu hapo juu na kuanza kuandaa mifumo na miundo ambayo itawapa viongozi wote katika sehemu na ngazi zote nafasi ya kuchangia maendeleo ya nchi na watu wetu.
Kinachoonekana kwa hivi sasa ni kwa viongozi wetu mbalimbali kuchomwa moyo zaidi na kujihusisha na vidonda na vipele na sio chanzo halisi cha gonjwa la kukosa sio tu amani bali upendo, ushirikiano na kuaminiana kati ya wanacnhi wetu kama ilivyokuwa kwenye awamu ya kwanza ya serikali ya Tanzania.
Ieleweke hakuna Mtanzania mmoja aliyekuwa na akili kuliko Watanzania wote wakiwekwa pamoja na anayeamini hivyo sio tu anajidanganya ila yeye ni tatizo kubwa. Akili ni nywele na kila mtu ana zake.
Taaluma, uwezo na kushindwa kujifunza kutokana na historia na watu wengine kwa ujumla ninaamini ni jambo moja linalochangia kuwepo kwa migogoro ya kiimani ambayo isingelikuwepo kwenye miaka ya sabini na themanini hapa nchini kutokana na dini kuwa mikononi mwa viongozi walioisoma jamii vyena ma waliojitahidi kutoa mchango wao katika kuifanya jamii yetu kuwa kitu kimoja.
Hizo ni enzi ninazozikumbuka wakati wa viongozi kama Hemedi bin Juma, Kadinali Rugambwa, Askofu Moshi, Askofu Sangu na viongozi wa dini nyingine ndogo kwa kubwa waliojua kutenga kilichokua cha Kaizari na kilichokuwa cha Mungu. Leo tuna mamia ya watu wanajiona wao ni bora mara mia ya viongozi wao. Lakini tukumbuke pamoja na yote uongozi ni zawadi kwa wema au ubaya toka Kwa Mungu.
Katika miaka hii kwa bahati mbaya sana kila sekta inaingiliwa na wanasiasa, matajiri na watu kama hao wanaotaka kuwatumia watu wengine kujitajirisha, kujenga umaarufu na wakati mwingine kuihadaa na kuigombanisha jamii kwa maslahi yao binafsi na sio maslahi ya walio wengi. Izingatiwe kwamba katika taifa lolote kuna asilimia ya watu 97 wanaofikiri kwa moyo na ni asilimia chini ya 3 wanaofikiri kwa akili. Ni asilimia hii 3 ndiyo ambayo aghalabu inayozusha matatizo ya kila aina. Huwa wanadhani wanajua, kumbe hawajui kitu. Wanajihadaa wao wenyewe na wale wanaowahadaa kwa hasara ya nchi na watu wake.
Ipo haja ya kuwa na Taasisi ya Kuwafunza viongozi wote wawe wa kisiasa au kidini au kibiashara mahala pamoja juu ya nadharia na dhana na imani na kanuni za msingi zitakazochangia kutuunganisha badala ya kutugawa. Kwa namna hii, kila kiongozi nchini wa kundi lolote lile atajifunza lililo sawa kufanza na lisilo sawa kulifanza pale anapoteta au kufanya jambo lolote lile hadharani.
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ingelipitia kwa mara nyingine tena uwepo wa 'World Conference of Religions for Peace' hapa nchini (taasisi muhimu sana inayopuuzwa kiasi cha kutisha) na kuona ni kwa namna taasisi hiyo inaweza kushikishwa na kuwezeshwa kufikia malengo na madhumuni yake ambayo kwa mapana na marefu ni hayo hayo au pengine zaidi ya hayo aliyogusia na anayoyahofia mheshimiwa Kikwete katika hotuba yake ya hivi karibuni.
Kinachoonekana hapa nchini ni kwamba kuna watu na taasisi kabakaba ambazo zikiachwa kupuuzwa na zikashirikishwa katika changamoto na vilio vyetu mbalimbali vya kila siku, taasisi na watu hao wanaweza kutoa mchango wenye thamani na faida kubwa kwa nchi na watu wetu. Tuzinduaneni na tufanye kweli, lawana na hotuba zisizokwisha na zisizobadili kitu haziwezi kutufaa kwa lolote.
Kisiasa ni muhimu kupitia upya na sera zinapendelea wanachama wa chama fulani na kubagua wa vyama vingine. Wanasiasa wakifanya hivyo, je, watu wa Mungu nao watahesabika wamefanya kosa na wao wakifanya ubaguzi kama huo? Wanasiasa wetu waelewe kuwa demokrasia na mfumo kamili, unapouwekea vikwazo upande mmoja, unachangia pia kuvuruga na kwignine usikokujua.
Unafiiki na undumilakuwili ambao aghalabu unachangia mara kwa mara isijulikane kama hivi leo wanasiasa hapawanasema kweli au uongo hauwezi kutusaidia katika changamoto zilizo mbele yetu. Lazima viongozi wa dini na kisiasa wakubaliane kwamba nchi yetu haiwezi kujengwa juu ya misingi ya uongo, Kujitia uziwi na upofu unapoambiwa kweli, ubinafsi, kufikiri kwa moyo badala ya akili, kujigeuza kifaurongo, uzushi, kupakazina, umbeya, hadaa na uzaini wa kidizaini na kisanii bali katika misingi ya ukweli, uwazi, haki, usawa wa kisheria na uwajibikaji na vinginevyo ni kujidanganya kwa hasara ya walio wengi.
Kwa kuanzia nawatafadhalisha viongozi wetu wote kujua ni mahala gani au wapi pa kusema yanayowahusu viongozi na wapi pa kumwaga mtama mbele ya kuku au bata wote.
Ikiwa hivi tutakuwa na viongozi ambao mikono yao inafungwa na mikono ya viongozi wengine nchini na inakuwa ni rahisi kuwafuatilia na kuwadhibiti wanakosea na kuwatoa kwenye kundi la uongozi.
Hatua hii italiepushia taifa madhara kama tunayoyaona kwingine Afrika. Mimi kama mwananchi wa kawaida nawatafadhalisha viongozi wetu kabla hawajafungua mdomo kutuambia chochote basi wazungumze wenyewe kwa wenyewe kwanza, wapime na kutathmini nini itakuwa atahri yake wanacnhi watakapofafanuliwa jambo hilo.
Hatari kubwa ninayoiona kwa amani na umoja wa Tanzania sio kitu kingine ila midomo na kauli za viongozi wetu (kwa maana hiyo pana), kwamba kipo watakachokisema kitakachotuleta madhara makubwa kama ilivyo kwa watakachoacha kukisema nacho kikatuleta shari kubwa pia. Ninaamini viongozi wote kwa pamoja wana dhamana ya kulizungumzia hili na kujifunza kutoka kwa wengine itifakizinazoendana na matamshi yanayogusa sehemu kubwa ya watu wetu au taifa kwa ujumla wake. Viongozi wanapokuwa kitu kimoja katika kuongoza wale wanaostahili kuongozwa wana uwezo mkubwa zaidi wa kujenga amani na umoja kuliko vinginevyo. Mungu ibariki imani zetu, Mungu tubariki Tanzania na Afrika na tujalie kuutanguliza Utanzania na
Thursday, February 21, 2013
Mambo Yatakayonusuru Amani na Umoja Miaka hii na Ijayo..
AMANI na umoja hapa Tanzania una kila sababu ya kuendele
kuwepo ili mradi tu mambo yafuatayo yanaheshimiwa, hayawi tu sera bali yanakuwa vitendo vya kila
siku na wote kwa pamoja tukawa tunakataa kwenda kinyume na kauli na ahadi za
kitaifa kuhusu masuala husika.
Kwanza
viongozi na raia lazima kujiheshimu, kuheshimu wengine na kuheshimiana. Huwezi
ukaendelea kuwadhalilisha wengine au kufanya vitendo vinavyohalalisha
kudhalilishwa wengine na wewe ukaamini kuwa utaendelea kuheshimika. Kiongozi
yeyote wa Tanzania atakayekubali Mtanzania yeyote kudhalilishwa ndani au nje ya
nchi na yeyote yule awaye basi huwa mchangiaji katika hatima ya uvunjikaji
amani na umoja wa nchi.
Mtu
mmoja mmoja, vikundi vya watu, wapangaji, wenye nyumba, wenye mji, wanamtaa,
wanakijiji na wanamji kwa ujumla wao ni sehemu ya Tanzania. Kila mmoja wao ana
wajibu na ana haki zake. Kitendo chochote kinachoruhusu au kuendelea kuruhusu
mtu au watu fulani kununua na kuuza haki za wengine ni kitendo kinachonuiwa na
kinachodhamiria kuvunja amani na umoja wetu. Kisikubalike
Uhuru
wa kweli kwa mtu mmoja mmoja na makundi au jumuiya ya watu pasina uhuru huo
kuingilia uhuru wa wengine. Uhuru ndicho kitu kinachompa uwezo mwananchi au
raia awaye kufanya maamuzi kwa kuangalia maslahi yake na kikundi chake bila ya
kurubuniwa, kuzainiwa, kununuliwa au kushawishiwa kufanza hivyo kwa pesa au
upendeleo wowote uwao. Nchi huru hujengwa na watu huru haijengwi na watu wa kununuliwa au watumwa wa
mtu fulani.
Kama
nchi, Tanzania tunapwaya mno katika medani za ukweli na uaminifu kama watu
binafsi na dhamana tunazopewa kutunza na wenzeu. UOngo haujengi nchi, aghalabu
uongo hubomoa na kausambaratisha watu, vyama na nchi. Ni muhimu katika
uandikaji wa katiba yetu tukarejea suala la kuwa na maadili muhimu ya kitaifa.
Maadili hayo pamoja na mambo mengine yahusu: ukweli kama tabia inayokubalika na wote; uaminifu;
usafi wa mazingira, miili na mioyo yetu; uchapakazi na uwajibikaji wa kiwango
cha juu; tabia ya kujisomea na kujiendeleza baada ya kumaliza shule/vyuo;
kujitolea kusaidia wengine; kujitegemea kama jamii kama hali inaruhusu na ndio
njia peikee ya kutatua tatizo la kijamii na kujitahidi kuongoza kwa vitendo na
sio porojo na maneno.
Hali
ilivyo hivi sasa ni kwamba kuna matajiri na wakubwa wengine wanaojiweka juu ya
sheria na wengi wengine kuwa chini ya sheria. Amani na umoja wetu lazima kufa
kama hapatakuwa na usawa mbele ya sheria kwa wote viongozi kwa raia.
Tusikubali
visingizio vya kihaki za kibinadamu na kisheria kukwamisha mapambano dhidi ya
rushwa. Kwa vigezo na bishara zote mla rushwa na fisadi huonekana maili kumi
toka pale alipo na wala sio siri. Tukiidharau rushwa na kukubali itutawale sisi
kama taifa na sio sisi kuitawala rushwa tutakuwa tumeshindwa katika safari ya
ustawi na maendeleo ya watu wetu kabla hata ya kuanza safari yenyewe.
Kujilinda na kuwa na maofisa habari na mawasiliano pia
wahariri wa habari na waandishi ambao pamoja na
uchanga wao wanajifanya ni
watakatifu na wanajua kilicho bora zaidi kwa nchi na watu wake. Hali katika
kufanya hivyo wakawa ndio wanaopanda
mbegu za ushetani na balaa kwa nchi na watu
wake .
-Kupigwa vita rushwa na ufisadi
Kama
hatutaenzi ahadi na amri mbalimbali ambazo ni sahihi na za haki basi kitaifa
tutakuwa tunabomoa msingi wa amani na umoja wetu. Baada ya kusema hivyo, ni
lazima kwa wakubwa wetu sio tu kuchungua mambo pale tatizo linapotokea bali pia
kuchungua kwa makini, kina na mapana malalamiko yoyote nchini ambayo yanaashiria
kuwepo tatizo kati ya mtu na mtu au watu na watu. Mambo haya yakichukuliwa
kijuujuu yatatufiksha pabaya, kwani yana uwezekano mkubwa wa kuweka umoja na
amani yetu rehani katika mikono ya wachache kwa wema au ila.
Huko
nyuma Watanzania walikuwa wepesi wa kuitana ndugu au komredi. Kuzuka na kukua kwa matabaka kati yetu
kumeanza kunyemelea na kuuharibu udugu na ujamaa huo. Ni muhimu kuangalia kwa
kutumia njia zozote ziwezekanazo tunarudisha
upendo na kukubalika kwa makundi mbalimbali katika jamii na sio kama
hivi sasa ambapo baadhi ya watumishi wa
umma wameanza kuonekana kama maadui na aghalabu wako juu ya sheria za nchi na
maeneo mbalimbali. Udugu na mahusiano mema huzaa kile kinachoitwa mtaji wa
kijamii. Mtaji huu usipokuweko mbio za manendeleo kwa jamii yoyote iwayo hatima
yake ni kuishia sakafuni.
Tuepuke
tabia ya kuwadharau , kuwashusha h adhi na kuwakwaza wengine hadharani pasina
sababu ya msingi ila kwa mtu kujipendekeza na kujionyesha kwa wenzake kwamba
yeye ni mkereketwa na anayewashwa zaidi kuliko wenzako na hasa katika jambo
muktalifuni na lisilokubalika ukweli
wake na watu alimu na wenye uadilifu. Tabia ya kuikweza na kujionyesha wewe
safi na bora kuliko wengine hujenga
chuki na inda isiyo na tija. Aghalabu anayejikweza na kukwaza wenzake
huonekana mbaya, mbinafsi, adui na huchukiwa na wenigi hata na wale anaodhania
wanamshabikia na kumpenda. Maana leo ni yule, kesho aweza wageukia wao.
Kumezuka
tabia ya baadhi ya wanasiasa na matajiri kuwanunua Watanzania wengine kwa sababu moja au
nyingine. Jambo hili sio tu linarudisha
uhadimu kwa watu wetu kupitia mlango wa nyuma bali ni sababu moja kubwa
inayochangia kuua na kuumaliza udugu na umoja wetu, kwa kuwa watu wanaonunuliwa
ni rahisi sana kutumika kufanya lolote lile liwalo, liwe jema au baya mradi
wanalipa deni lao.
Katika
miaka hii ya kugundulika kwa rasilimali mbalimbali nchini upo umuhimu wa kuwa
na fomula ya kitaifa itakayogawa rasilimali na mapato yanayotokana nazo kwa
namna ambayo kule inakopatikana wanaona wanastahili kupata wanachopata na
wengine kugawiwa au kunufaika na kile kinachobakia, ikiwemo serikali na vyombo
vyake pia.
Upo
uwezekano mkubwa wa amani na umoja wetu kudumu kama mambo niliyoorodhoshea hapo
juu yatafanyiwa maamuzi sio kiimla bali kwa kuwashirikisha wahusika au wabia
katika masuala mbalimbali na kufikia maamuzi ambayo yanachangia wote kujiona ni
washindi na hakuna mshindwa.
Kwenye
jamii ya mpito kama ilivyo yetu aghalabu umoja hujengwa kwa kuwa na madaraja
kati ya walionacho na wasio nacho. Aidha kila kinachoonekana kuwa ni kizuizi
katika ukombozi wa wasionacho huwa kinang'olewa haraka kwa faida ya wote.
Rasilimali
zetu ni nyingi na za kutosha. Kinachokosekana ni uongozi, utu na ubinadamu wa kuweza kutumia akili na maarifa
tuliyopewa na Mola ili rasilimali hizo ziweze kutufaa sote bila ya wengine
kutengwa na kusahauliwa. Hii ina maana katika sifa kubwa amabyo viongozi wetu
kuanzia vijijini hadi kitaifa wangepaswa kuwa nayo ni ile ya kukosa kabisa
ubainafsi wenye uharibifu.
Hatuwezi
kuwapata kina Nyerere wengine (watu waliokuwa wanajisahau wao wenywe na familia
zao na kumtanguliza mbele Mtanzania kwanza) lakini tukiwa na maadili bora,
kupata viongozi wenye kudhibiti ubinafsi wao kwa masalahi ya walio wengii ni
kitu kinachowezekana kabisa. Kuna mifano mingi duniani inayoonesha kwamba nchi
zilizochipukia na kuwa tajiri katika miaka ya hivi karibuni ziliongozwa na
viongozi walionyima wao na kuwanufaisha watu wao kwanza, na sio waliowanyima na
kuwakwaza watu wao ili wao wajinufaishe kwanza.
Tanzania katika nchi nyingi za Kiafrika ipo katika nafasi ya
kipekee kuendelea kudumisha amani na umoja wa watu wake kama isipofuata
msaragambo na kuiga yanayotokea katika nchi nyingine za Kiafrika na kwingineko
duniani kwa kuwa na utaratibu wa wazi na usio na usiri katika kuzungumzia mambo
mbalimbali yanayoonekana kuwa ni chanzo cha mtafaruku na maelewano kati ya
Watanzania katika siku zijazo.
Tabia
ya mbuni haifai kwa nchi kama yetu, yaani, kuingiza kichwa chetu kwenye
mchanga, kisha tukajifanya kama vile kwa kuwa hatuoni hatari inayokuja, basi
tukifijificha hatari hiyo haitatugusa na eti tukabakia salama. Athari, hatari
na matishio mbalimbali kwa amani na
umoja wetu lazima tupambane navyo ana kwa ana.
Elimu, Mitaala na Utatuaji Matatizo ya Watu na Nchi
Nia na madhumuni ya insha hii ni kujaribu kuwashawishi
Watanzania kuona kwamba elimu yetu sasa hivi inaendeshwa kwa namna ambayo haina
uhusiano kabisa na matatizo yanayokabili nchi na watu wetu.
Ninavyoelewa
mimi sababu kubwa ya kuwepo kwa elimu ni kusaidia kudumisha daraja la maarifa,
nadharia, ujuzi na uzoefu wa waliotangulia na wanaowafatia katika jamii fulani.
Jamii
isiyoweza kurithisha toka kizazi kimoja kwenda kingine maarifa, elimu,
teknolojia, mila, desturi na utamaduni wake kiujumla inayozikusanya muongo
baada ya muongo sio jamii yenye uhakika wa kuwepo na kuendelea kuwepo katika
siku zijazo.
Urithishaji
huu unajumlisha pia urithishwaji wa kizazi kimoja na kingine mbinu, njia na
mikakati ya kushughulikia matatizo makubwa na madogo yanayokabili mtu mmoja
mmoja na jamii nzima kwa ujumla.
Inaaminika
kwamba nusu ya matatizo ya jamii fulani huhesabika yamekwisha au
yameishatatuliwa kama jamii hiyo itakuwa inawafunza vijana wake pamoja na elimu
nyinginezo elimu ya kutafuta ufumbuzi wa matatizo yanayoikablili jamii husika.
Mafunzo haya hutolewa sio tu kinadharia bali pia kwa
vitendo. Unapotenganisha nadharia na
vitndo katika elimu, basi jamii husika huwa inapoteza jambo muhimu sana katika
wakati muafaka na sio rahisi kulipata jambo hilo tena katika siku zijazo.
Kuna
wanaoamini kwamba nusu ya matatizo ya Tanzania yanaweza kwisha kwa kuwa na
mitaala inayolenga kutatua matatizo yake ya kijamii na kiuchumi.
Matatizo ya kimaendeleo yanayowakabili Watanzania walio
wengi ni pamoja na uadimu kama sio ukosefu wa maji, chakula na nyumba. Aidha
kuna udhaifu katika elimu, tiba na afya kiasi kwamba watoto wa Kitanzania
wanaendelea bado kusomeshwa nchi jirani na Ulaya au Asia; wakati huo huo
wagonjwa wa Kitanzania wanaendelea kutibiwa
nje.
Kuna
tatizo la kukosa matunzo kwa wazee,
mayatima na watoto wa mitaani. Vilevile
yapo matatizo ya kiulinzi na usalama, uhalifu yanayotishia sio tu usalama wa
raia mmoja mmoja bali amani na utulivu katika jamii ikiwemo kuongezeka kwa
vitendo vya wivi na ubakaji pamoja na kuwa na sheria kali dhidi ya vitendo
hivyo.
Aidha
yapo matatizo katika ujenzi na upanuzi au ujengaji upya wa barabara, reli,
madaraja, uchimbaji madini, bandari, viwanja vya ndege na ujenzi wa uendelezaji
wa miundombinu mingine.
Kiutamaduni
na Kiteknolojia tuna matatizo ya kuoanisha maendeleo ya teknolojia na mila na
desturi zetu ili kupunguza gharama na kurahisisha ufanifu na ufanisi katika
maeneo mengineyo ya maisha, kazi, sanaa, utunzi wa vitabu, filamu, michezo na
burudani.
Kijamii
na kiuchumi matatizo makubwa ni katika ujasiriamali, mikopo na urudishaji wake,
mipango, uratibu, uongozi, usimamizi na udhibiti wa mambo kiutawala,
kimaandishi na kiteknolojia. Hali
kadhalika kuna masuala ya menejimenti na uendeshaji bora wa michezo, sanaa na
uchumiwa utoaji au uuzaji huduma. Aidha kuna changamoto katika uchimbaji na
utunzaji au uangalizi wa visima vya maji, bomba, pampu, mashamba ya kisasa,
uvuvi na ufugaji wa kisasa, utunzaji na ulinzi wa wanyama pori, nege na viumbe
wengine, matumizi bora na makubwa zaidi ya rasilimali nchi kavu, rasilimali
kwenye baharini na kwenye maji kwa faida ya wengi na sio wachache.
Elimu
yetu kwa mapana na marefu sasa hivi imeelekezwa katika kujifunza vitu kama
historia, sayansi kama sayansi, uraia, jiografia, hesabu, lugha na mambo kama hayo.
Kwa maoni yangu masomo yote yanayotolewa hivi sasa iwe kwa shule za msingi au
sekondari yanaweza kuangukia ndani ya masomo matatu makubwa: Maarifa ya Namba
na Takwimu; Maarifa ya Kunadika na Mawasiliano na Maarifa ya Maisha, Sayansi na
Mazingira.
Fani
hizo hapo juu zikipata msukumo wa kuwekwa kwenye mtandao kwa lugha ya Kiswahili
na Kiingereza kama itakavyoandikwa na Watanzania wenyewe ni maeneo yanayoweza
kutawaliwa kielimu vyema na mwanafunzi yeyote awaye.
Hayo
kwa upande wangu ndiyo yangelikuwa masomo ya msingi kuanzia chekechea hadi
sekondari na yakawa ni lazima kuwepo kwenye kila mchepuo kwenye maeneo hayo.
Masomo
yanayotakiwa kupangwa kama ziada itakayotofautisha kati ya mchepuo wa mweleko
fulani na mwingine ni mtatizo yalioorodheshwa hapo juu.
Kwa
mpangilio huo mwanafunzi, mathalani,
katika kundi la kwanza la matatizo ya uadimu na ughali wa maji, chakula,
nyumba na kadhalika atakuwa akijishughulisha na kujifunza jinsi ambavyo
matatizo hayo yanaweza kupunguzwa au kumalizwa nchini. Ni elimu inayomhakikisha
kijana nafasi ya kujiajiri au kuajiriwa kwa sababu elimu hiyo itakazia nguvu
zaidi katika vitendo na sio nadharia tu.
Mchepuo
mwingine unaweza ukaelekeza nguvu zake katika kujifunza na kurahisisha kuelewa
matatizo ya elimu (elimu nayo pia huwa tatizo na lazima kufunzwa na kufanyiwa
tafiti dahari ili kuboreshwa mara kwa mara),
tiba na afya wataanza kugangana
na mbinu, stadi na maarifa za ualimu au ufundishaji na uangalizi au utabibu
mahospitalini na katika zahanati mbalimbali nzhini zisizo na watumishi wa
kutosha.
Wanafunzi
wengine na hususan katika shule za msingi wataelekezwa kutokan na mapenzi na
mwelekeo wao katika kujifunza na kulielewa tatizo la matunzo kwa wazee, wajane,
mayatima na watoto wa mitaani ili waje kubobea sio tu katika nadharia bali
vitendo vya kulipunguza au kuondosha kabisa tatizo hilo.
Wale
wanaopendelea mambo ya ujenzi na miundombinu wataanza kupigwa msasa toka shule
za msingi kwa kujifunza juu ya umuhimu, kazi na faida za nyumba, barabara, reli, madaraja, visima, bandari
na viwanja vya ndege, vituo vya kisasa mipakani na usafiri na uchukuzi
kiujumla. Kwa namna hii, mtoto hata akimaliza darasa la saba anaweza kuanza
kufanya kazi katika eneo hilo na akawa anajiendeleza katika fani yake
pasipokuwa na wasiwasi wa kuchanganya kimasomo au kimitaala. Maana elimu hapa
inakuwa ikishughulika na tatizo lilipo, linaloeleweka na linaonekana na kila
mtu katika jamii.
Mcherpuo
mmoja muhimu utakuwa ule wa kuwapa watoto kuanzia chekechea fursa ya kuonyesha
vipaji vyao katika nyanja za sanaa, kuimba, kucheza ngoma na kukatika viuno,
kuigiza, kuchekesha, uchezaji mpira wa vikapu na michezo mingine na mambo kama
hayo. Kwa kuwa mtoto anaelekezwa kulekule anakokutaka inakuwa ni rahisi kijana
wa Kitanzania kuanza kuonyesha vitu vyake akingali bado mdogo na hivyo kumpa
nafasi ya kufanza makubwa zaidi hapo baadaye.
Mabadiliko
ya mitaala katika miaka hii pia lazima iwe na mchepuo wa uongozi, utawala,
biashara na menejimenti ya vitu hivyo. Ni vizuri hili likaanzia shule za msingi
kiasi kwamba mtoto wa Kitanzania akimaliza darasa la saba anakuwa sawa na mtoto
wa Kimarekani aliyesomea B.B.A. au hata M.B.A. (unacheka?) nina hakika hili
linawezekana kwa kuwa watoto wa Kitanzania kutokana na mzingira yao magumu
wanaisoma na kuilewa dunia haraka kuliko watu wa nje katika hili.
Mwanafunzi
anayemaliza masomo katika mchepuo huu atakuwa na uwezo wa kusimamia biashara ya
wazazi wake kwa namna bora zaidi kuliko wazazi
hao, na upo uwezekano mkubwa wa mchepuo huu kuzalisha viongozi bora
zaidi kwa vyama, vijiji na taasisi nyingine kuliko hali ilivyo hivi sasa.
Ninakubaliana
na wale wote wanaodai kwamba ilikuwa ni makosa kuondoa elimu ya ujamaa na kujitegemea mashuleni. Lakini
kama ikirudishwa, ninashauri ingerudishwa kwa mapana na kina zaidi kwa
kuzingatia ulazima wa kuoanisha matatizo ya jamii leo na elimu inayowapatia
watu wake.
Nionavyo
mimi, Vyuo vya VETA vinastahili kuitia makali au kuinoa zaidi elimu vijana wetu
watakayoipata shule za msingi na sio kuwa mahala pa kuanzia tu vitu vipya kwao.
Nikiwa na maana kwamba shule zetu zote za msingi zinahitaji maabara na karakana
za useremala, uashi, umakenika na ufundi mwingine ili ziwe kamili na sio
nusunusu kama zilivyo leo. Hali ingelikuwa hivyo, leo tusingekuwa na shule za
msingi zisizokuwa na madawati na vyoo vya kutosha, na zenye madarasa na majengo
mengine yasiyofikia viwango.
Copyright
© 2013 Sammy W.I. Makilla. All Rights Reserved.
Saturday, February 16, 2013
Ujamaa na Kujitegemea Bado una Nafasi Vijijini na mashuleni
KIHISTORIA watu wa mjini hawajawahi kuwa watu wanaotamani na kupenda ujamaa. Miji jinsi ilivyo imejengwa katika msingi wa ubinafsi na kila mtu na lweke. Na kwa miaka mingi ijayo hilo ndilo litakaloendelea kwa ubepari kuwa wenye sura mbaya na makucha makali zaidi.
Mtu aneyeuchukia ujamaa eti kwa sababu tu Warussi wameutupa na wajamaa wa jana wameanza kukumbatia baadhi ya sera za kibepari ni mtu asiyejua maana halisi ya ubepari. Ni mtu anayehitaji kujitambua na kuijua jamii yake na hasa ile ya vijijini na shida na dhiki zao mbalimbali.
Anakuwa hivyo kama anavyokuwa kwa sababu anadanganyika na mng'aro wa dhahabu ubepari unaonyesha kwa nje, bila kujua kilichoko ndani wala sio shaba achilia mbali madini ya fedha.
Tumeshaufungulia mlango, na hakuna namna ambayo tutaweza kuuzuia. Labda, angalau tukubaliane na na kina Raila Oginga na wenzake (watangulizi maarufu katika ubepari) kuwa nchi zetu sasa zinastahili kuwa na sera na dira ya Ujamaa wa Kidemokrasia (Sosho-demokrasia), ha hivyo kupunguza ushetani na makali yaliyomo katika ubepari kwa faida ya wasionacho katika jamii yetu.
Hata hivyo, hali ya maisha vijijini katika sehemu mbalimbali za Tanzania nilizotembelea na wanakoishi watu masikini na wa kawaida na sio viongozi au jamaa za viongozi kila feli, kila mtihani, kila tatizo na kila fursa inapiga mayowe ya kuwa pasipo ujamaa na kujitegemea miongoni mwa wanavijiji maisha huko tuendako yatakuwa magumu na yasiyo na huruma hata kidogo.
Hili linakuwa hivyo, kwa kuwa nchi yetu bado haijawa na sera inayomfanya mwanakijiji anufaike na ardhi yake na kile kilichomo ndani yake kama viongozi wa juu wanavyonufaika.
Aidha, pamoja na kuwepo kwa teknolojia ya habari na mawasiliano bado inawachukua wanavijiji muda mrefu kujua kinachotokea mkoani mwao achilia mbali nchini kwao na duniani kwa ujumla.
Vilevile, pamoja na kuwa na vitu kama TASAF na NGOs mbalimbali zenye madhumuni na nia ya kuwasaidia wanavijiji kutatua matatizo yao bado muundo na mifumo ya taasisi hizo imekaa kuwanufaisha zaidi watu wa mjini kuliko wa vijijini.
Tafiti zinaonyesha kwamba jitihada za kuwaamsha na kuwafunza wanavijiji umuhimu wa ushirika zinaharibiwa na tamaa za viongozi wao na mabepari uchwara wsnaoishi au kuchanganyikana nao.
Watu wanashangaa kusikia kwamba dhana na nadharia ya ushirikishwaji watu nchini hapa pamoja na kuleta ufanisi wa aina fulani haikutoka kwenye ile ngazi ya chini kabisa katika ushirikishwaji watu kwa kutumia modeli ya ushirikishwaji watu iliyobuniwa na Mjapani kutoka Chuo Kikuu cha Kobe aitwaye Etsuko Okazaki. Hatua hiyo siyo nyingine ila ni ile ya uanasesere wa kuchezewa na wanasiasa na viongozi wa serikali za mkoa na kitaifa. Hatua za juu katika ngazi hiyo ya ushirikishwaji watu ni pamoja na tiba, kuarifiiwa, ushauri, kubembelewa, ubia, ukaimishwaji na nguvu ya umma.
Matatizo yanayokabili vijiji vyetu nchini ni pamoja na tatizo la maji; dhikiya chakula na lishe bora; ukosefu wa nyumba bora kwa wananchi walio wengi na uzalishaji mali kwa njia dhaifu na zisizo na ufanifu na ufanisi wa kutosha. Na kutokana na hili bado shughuli za kilimo, ufugaji pamoja na ule wa nyuki, uvuvi, uchimbaji madini na matumizi ya rasilimali ardhi na bahari kwa ujumla ni dhaifu na zisizowasaidia kitu wanavijiji katika kubadili ubora wa maisha yao na kuwa yenye heri na mafanikio zaidi.
Matatizo mengine ni kutokuwepo kwa biashara zenye manufaa zaidi kwa wanavijiji na mwelekeo wa kuchangia kuwafanza kwanza wazalishe kitu na ndio watumie; kutokuwepo huduma za uhakika zinazoweza kupunguza umaskini vijijini k.m. utaalii wa vijijini na wa kiutamaduni; matatizo ya mejengo, vifaa na walimu kwa shule nyingi vijijini; huduma dhaifu ya tiba na Afya vijijini; uadimu wa
umeme na nishati mbalimbali; na
Usafirishaji na Uchukuzi wenye matatizo kedekede na hivyo kusababisha hatari na hasara kwa wanavijiji walio wengi.
Nichukulie tatizo moja tu nchini-maji. Tatizo hili, ninavyoamini, linaweza kutatuliwa kiurahisi ikiwa wanavijiji wenyewe wanajifunza na kubadilika na kuwa ndio viongozi wa maendeleo yao badala ya kuwategemea watu kutoka kwenye kata au tarafa au wilaya au mkoa au hata taifa kuja kuwasaidia.
Wenyewe wakishaamua kusimama kidedea inakuwa ni rahisi kuamua, kupanga na kutekeleza kile wanachokiamua. Na hili huwa ni rahisi zaidi pale wanakijiji wote kwa pamoja wanapokuwa kitu kimoja na sio baadhi yao kukubali kuzainiwa na wale wenye tamaa za uongozi na njaa yao binafsi.
Huko nyuma nimewahi kupendekeza njia mbalimbali za wanavijiji kupata maji huko waliko vijijini pasina ya kutembea mbali au kuhangaika sana. Njia mojawapo ni kuchimba bwawa pale penye chanzo cha maji na vilevile kwa ajili ya kutega maji ya mvua badala ya kuyaachia yote kwenda baharini. Njjia nyingine ni kuchimba kisima pale wataalamu wanapothibitisha kuwa maji hayapo mbali na uso wa dunia. Katika sehemu zenye maziwa jirani na wao upo umuhimu wa wahandisi wa Kitanzania kuamka na kuvumbua njia ambazo kwazo kwa maziwa yaliyo na kina cha chini wao wanaweza kuchimba mtaro chini kwa chini na kuvuta maji hadi nchi kavu. Wale wanaoishi pembeni na bahari huu ni wakati wa baadhi yao kurudi shule na kujifuna kutoka kwa wenzetu jinsi wanavyobadili maji ya chumvi hadi maji hayo kutumika kunyweshwa mashamba na bustani na kusaidia pia katika matumizi ya nyumbani.
Ukiyaangalia yote haya ni mambo yanayohitaji vichwa vilivyotulia na watu wanaokubali kwamba changamoto na fursa nyingi walizonazao zinalazimisha kuwepo kwa ushirikishwaji na kujitolea kwa namna moja au nyingine. Na kwamba bila ushirikiano wa walio wengi vijijini ippo hatari kubwa ya vijiji kubaki kama vilivyo hivi leo hata baada ya muongo mmoja ujao.
Maendeleo ya vijiji vyetu yamekwaza na viongozi wetu. Ambao kufatia Azimio la Zanzibar wamekuwa 'bize' kushughulika na mambo yote mengine na sio ujenzi na uendelezaji vijiji. Kwa namna moja au nyingine kwa miaka kadhaa sasa isipokuwa kwa vijiji viongozi wetu wanakotokea vijiji vingine vimeingizwa kwenye kabati kama sio kaburi la sahau.
Jambo la kushangaza ni kwamba matatizo mengi yanayoikabili miji yetu hivi leo yanasababishwa uongozi kushindwa kutoa msaada na nyenzo (wakati mwingine vimilioni vichache tu) ili kuwawezesha wanavijiji kuhama kwenye umaskini wa kutupwa na kuwa watu wanaojitegemea.
Kama kuna jambo moja ambalo ningeliwaomba wanaoendesha ukusanyaji maoni juu ya katiba mpya ni kutia shadidi katika kile kifungu kinachozungumziwa uwiano wa kimaendeleo kati ya sehemu moja na nyingine ili pawe na mikakati, sera na kanuni zilizo fasaha na wazi juu ya kushughulikia ujenzi na maendele oi ya vijiji vyetu. Ninazungumza hivyo nikiwa na uhakika kwamba nusu ya matatizo ya mjini yatakuwa yamekwisha kama vijiji vyetu vitatapatiwa angalau kwa kuanzia mahitaji yote ya msingi na ushirikiano kiungozi na kiutawala unaoweza kuwatoa wanavijiji pale walipo na kuwafikisha mahala ambapo sisi sote wa mjini na vijijini tunaweza kujivunia.
Jambo moja linalohitaji kupewa uzito wa kipekee hivi sasa ni kuangalia uwezekano wa kuwa na viongozi na watendaji bora wa vijiji bila kujali mtu anatokea wapi.
Inashangaza kwamba pamoja na kuwa na vyuo vya maendeleo vijijini kasi ya maendeleo vijijini imezidi kwenda chini mwaka hata mwaka. Aidha, elimu inayotolewa na vyuo kama hivyo haiendani na wakati au wanaozalishwa na vyuo hivyo hawaendi kuwa viongozi wa vijiji bali wanaselea humu humu mjini kama wahitimu katika masuala mengine. Kama ilivyo kwa vijiji basi mengi pia ya kijamaa na kujitegemea yanaweza kufanzwa shuleni na vyuoni kwa manufaa ya wanafunzi, wazazi wao na nchi yao. Hata kama baada ya shule vijana wataamua kufata ubepari na sio ujamaa.
Ninaamini kwamba jambo litakalochochea ari, mwamko na msukumo wa maendeleo kwa watu wa vijijini ni rasilimali watu. Wakati umefika huko vijijini wanavijiji kuwa na viongozi bora na sio bora viongozi.
Ukweli ni kuwa hata tukiwa na viongozi wazuri kiasi gani katika ngazi za juu lakini huko vijijini uongozi ukawa dhaifu kupita kiasi hatutaweza kuendelea kiwelikweli. Jambo hili likiunganishwa na ufanyaji kazi kidhati kwa mashirika yanayosemekana kazi yake ni kusaidia maendeleo vijijini na kisha wanakijiji wakafunzwa namna za kukopesheka kama wawekezaji wanaokuja kupewa ardhi kwenye vijiji vyao wanavyopewa mikopo kiurahisi kwa kutumia ardhi hiyo hiyo, basi maendeleo ya vijiji vyetu hayatabakia katika ruia zetu tu! Aidha, bila kusita wala kutafuna maneno huu ni wakati wa serikali zetu za mitaa na serikali kuu kuhakikisha kwamba wale wanaoishi katika maeneo mbalimbali hapa nchini wananufaishwa na na tathmini mpya ya mali asili na rasilimali zao nyingine na kwamba mali hizo kuanzia sasa zitakuwa zinahesabika kama mtaji wao kieneo na kitaifa na hivyo kuwaruhsu kunufaika kihisa na kifedha na rasilimali kama hizo na isiwe tu wanaonufaika na hili ni viongozi wa juu na wanasiasa nchini.
Subscribe to:
Posts (Atom)