KAMA jiji hili ambalo ndilo lenye Ikulu na wizara na idara zote muhimu nchini linataka liondokane na uchafu, harufu mbaya mpaka misikitini na makanisani, kinyesi kinachozibuliwa wakati wa mvua barabarani na mandhari za kuchukiza sasa ni wakati wa kuirudisha kazi ya usafi wa jiji kwa wanajamii kwa kiasi fulani badala ya kutoa tenda na kukodisha mchakato wote kwa watu wasio na uwezo na wasiokidhi mahitaji na matakwa ya usafi wa jiji hili.
Serikali kuu na serikali za mitaa zitatakiwa kutoa ushirikiano maalum ili kufanikisha azma hii.
Tofauti na mambo mengine, ningelipendekeza kazi hii ipewe umuhimu wa juu hata machoni kwa watu wa nje wanaotaka kuisadia nchi yetu katika masuala ya utunzaji mazingira na usafi.
Kinachopendekezwa hapa ni kuachana na utitiri wa magari na matrekta mabovu katika kazi ya kukusanya na kusomba taka kuzipeleka huko zinakotupwa. Badala yake kutoa ajira pana na za kudumu kwa kina vijana wetu wenye matoroli, maguta, pikipiki, vipawatila, bajaji, mikokoteni na wilibaroo kufanya kazi ya kukusanya taka mitaani na kwenda kutupwa kwenye eneo maalum litakalokuwa na shimo kubwa la kutupwa taka zilizotenganishwa kiaina na kiufundi na kisha kuchakatwa hadi kuzalishwa bidhaa mpya inayoweza kutumika majumbani, viwandani na mashambani.
Umuhimu wa serikali kuu na serikali za mitaa ni katika kupatikana kwa maeneo maalum ya kuchimbwa mashimo hayo mitaani au kwenye kata; ujenzi wa miundo mbinu rahisi ya kukokotosha taka kuwa bidhaa hitajika; kuwaandaa vijana kimafunzo tayari kwa kazi za kutenganisha taka na kuzibeba kwenda kwenye maeneo husika; na kuhakikisha bajeti ya usafi toka serikalini na misaada ya wafadhili inaelekezwa kwenye mambo haya badala ya kuliwa na wajanja wachache huko walipo.
Italazimu pia kwa viongozi na maofisa wote wa jiji na katika wizara husika, ambao wameomba kupewa hisa na chochote na wawekezaji katika miradi mipya tarajiwa ya kurejelea taka kupewa ruhusa maalum na serikali kuu ya kuwekeza kwenye makampuni bila kutoa chochote !
Aidha wanajamii kwa kushirikiana na serikali kuu na za mitaa watapaswa kuwa na kisima cha maji kilichochimbwa kwenye eneo au kina ambacho maji hayakauki kamwe ili kuhakikisha mji unakuwa na mandhari nzuri na ya kuvutia wakati wote. Maji hayo pia yatatumika kusaidia kazi za kupooza na kulainisha bidhaa katika kituo kikuu cha kubadili taka kuwa mali na utajiri. Ndoto ya kuwa na mifumo mizuri ya kuvuna mvua itakuwa ziada ambayo si mbovu katika hili.
Kila nyumba italazimika kupatiwa pipa pacha nne au kwa maneno mengine pipa ambalo lina sehemu nne: moja kwa ajili ya kutupwa chupa na glasi: la pili kwa ajili ya kutupwa karatasi: la tatu kwa ajili ya kutupwa mabaki ya vyakula na la mwisho kwa ajili ya kutupwa taka ambazo ni hatari kwa afya ya binadamu na taka mchanganyiko nje ya hizo hapo juu.
Vijana wakusanyaji watafunzwa jinsi ya kuzihamisha taka hizo toka mapipa hayo kwenda mifuko maalum ambayo itachukua taka kwa mpangilio huo huo huo na kuzipeleka kwenye kituo kikuu cha taka kwenye mtaa au kata kwa ajili ya kurejelewa upya kuzalisha kinachowezekana kuzalishwa.
Zitakapofikishwa kituoni hapo taka zitakuwa tayari zimetenganishwa kwa utaratibu huo hapo juu na hivyo kuingizwa kwenye moja kwa moja kwenye eneo zitakazofanyiwa kazi ili kuzalisha umeme au kutoa bidhaa fulani itakayotumika kama bidhaa mpya tena madukani au sokoni. Mabaki ya vyakula yanatarajiwa kutengenezwa kuwa mbolea asili isiyo na dawa yoyote ambayo itauzwa kwenye mifuko maalum kwa wakulima na watunza bustani.
Watumishi wizara ya ardhi wataaswa kwamba ili kuleta uwiano kati ya klutenda dhambai na mema- nchini ni muhimu kwao pamoja na kuuza maeneo wazi kwa mabwanyenye wetu wapya, sasa kutoa maeneo kwa ajili ya uchimbaji mashimo makubwa ya uhifadhi wa taka zitakazochakatwa na kuwa bidhaa mpya au kuzalisha umeme kwa ajili ya faida ya wakazi walio wengi jijini.
Wataalamu wa vyama vya siasa vyenye vijiwe mjini wataombwa wautumie utaalamu huo ili kugeuza vijana wetu toka 'majoblesi alwatani', wababaishaji na kupe wenye sifa za kimataifa kubadilika kwa kukopeshwa mitaji ya kununua toroli, maguta na vifaa kama hivyo ili kuwa wakusanyaji na wabebaji taka watakaoipa heshima mpya jiji la Dar es salaam.
Wataalamu wa kupiga raia mabomu, kuvunja maandamano na mikutano wataombwa kuutumia utaalamu wao ili kuhamasisha kazi ya usombaji taka kila wakati ili pasiwe na taka hata moja mahala popote jijini kwa kasi ile ile ya upigaji mabomu ya machozi wakati wa maandamano ya upinzani, wafuasi wa dini fulani au wafanyakazi au wanafunzi.
Mameneja wa migodi wataaombwa kuazimisha magreda na makatapila kuja kuchimba mashimo hayo katika mitaa au kata mbalimbali jijini kama walivyofanikisha zoezi la uchimbaji mashimo huko Geita, North Mara na Bulyanhulu,kutegemeana na kiwango cha uzalishaji taka katika maeneo husika.
Badala ya kuwa na magari mabovu yanayosafiri umbali mrefu kuokota na kutupa taka sasa vitoroli, mikokoteni, bajaji, guta na pikipiki zitatengenezwa kwa njia ambayo kwazo zitakuwa zikipeleka taka kwenye maeneo hayo yenye mashimo na miundo mbinu maalum ya kupokea taka zilizotenganishwa na kuanza kuzifanyia mchakato ili zitoe bidhaa za aina mbalimbali na kuzalisha umeme na vitu vingine vitakavyowezekanika.
Taka zinazohitaji kutupwa mbali zitachukuliwa na magari makubwa maalum machache lakini yenye kiwango cha kimataifa kwenda kutupwa mbali kabisa na makazi ya watu na wakati mwingine hata kwenda kufukia mashimo yaliyotokana na kuchimbwa madini yetu katika mikoa ya kaskazini na kusini.
Ukiutazama mtiririko huu mzima utagundua kuwa pendekezo hili lina shabaha ya kugeuza taka kuwa mali kwa namna kadhaa. Kwanza, vijana ambao wana tatizola ajira itabidi sasa wakimbie ajira wao wenyewe. Taka zitageuka fumba na kufumbua mali, maana kila mzigo kutegemeana na aina yake utakuwa ukilipwa fedha nzuri tu mara ukifika kwenye kituo kikuu cha kuchakata taka kwenye mtaa au kata.
Aidha magari mabovu ya kusomba taka amabyo wakati mwingine badala ya kusafisha mji huuchafua yatatoweka. Takataka hizo zitazaa bidhaa ambazo wafanyabiashara na wanunuzi watanufaika kwani zina uwezekano mkubwa wa kuwa za bei rahisi zaidi kuliko nyinginezo. Kisha mbolea itakayozalishwa itakwenda kuzistawisha bustani za Ikulu na Mnazi mmoja na maeneo mengine mjini na hivyo kulipa jiji mandhari ya kukata na shoka kwa uzuri wake. Hali kadhalika, sio tu tatizo la kukatikakatika umeme jijini litakuwa historia bali mradi huu utahakikisha hata nyumba mbavu za mbwa zilizo mabondeni zinapata umeme wa kutosha na wa uhakika kila siku.
Vilevile visima vitakavyoendana na mradi huu vitawahakikishia wakazi wa kila mtaa na kata upatikanaji maji masafi ya uhakika wakati wote, wakati wanasubiri maajabu yatakayofanywa na DAWASCO miaka mitano au kumi ijayo kama bado wako hai. Hili linawezekana, cheza nafasi yako na timiza wajibu wako. Miaka hamsini baada ya uhuru hutakiwi kushindwa na jambo hili.
Wakati ninaandika makala haya watafiti wanaonisaidia wameleta habari kwamba kuna watu tayari wameanza kujituma wenyewe na kuanzisha miradi kama hii. Kama hili ni kweli basi wilaya, mkoa na wizara husika zichangamkie mara moja jambo hili. NIna hakika likipata kuungwa mkono nao ni kitu kinachowezekana na kitakalolifanya jiji la Dar es salaam kuwa jiji la kuigwa na miji mingine sio tu Tanzania bali Afrika nzima.
lle tabia ya kujifanya kuwa serikali inaweza kufanya kila kitu si kitu kizuri. Na katika miaka hii ni kitu kilichopitwa na wakati na kuwazaini wananchi huku tukijua fika tunasema uongo. Kweli Watanzania hawana fedha, yaani, ni maskini. Lakini Watanzania wana kitu kimoja ambcho thamani yake wakati mwingine ni kubwa kuliko fedha. Kitu hicho sio kingine ila akili na nguvu zao. Pakiwa na uongozi unaoona mbali na mbele na unaojua kutumia akili na nguvu hizo na kuwekeza fedha kidogo Watanzania kama watu wengine wana nafasi ya kufanya maajabu mbalimbali duniani.
Friday, November 25, 2011
Thursday, November 17, 2011
Muswada wa katiba na hatima ya nchi yetu...
AKIZUNGUMZIA uwezekano wa kuandikwa katiba mpya ya Tanzania kwa mara yake ya kwanza, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti na mwanachama wa Chama kimojawapo cha siasa nchini Tanzania, CCM, Bwana Jakaya Kikwete pamoja na mambo mengine alionesha kutamani sana kwamba katiba itakayoandikwa iweze kutufaa kwa miaka 50 kama sio 100. Hata hivyo, kile kilichowasilishwa na Waziri wake wa katiba hakikufanana kabisa na matamanio mema yake hayo.
Tofauti na msimamo huu wa mheshimiwa Rais, muswada wa serikali yake kwa bunge la Jamhuri ulidhihirisha nia ya serikali ya Chama cha Mapinduzi kuitumia fursa hiyo ili iweze kujikita vyema zaidi nchini kwa halali au haramu kisiasa kwa kuwatumia wabunge wao ambao ilionekana kama walishapewa mafunzo maalum kuhusu kinachotegemewa kutoka kwao.
Pamoja na spika wa bunge hilo kudai kwamba wanaharakati, wapinzani na waandishi wa habari wanapotosha kilicho mezani mwa wabunge, kazi nzuri ya uchambuzi wa kina iliyofanywa na Mheshimiwa Tundu Lissu (CHADEMA) ilionesha kulikuwa na uwezekano mkubwa wa wabunge wa CCM kutokuwa wameusoma muswada huo na Tundu akawa anapigia gitaa mbuzi.
Pengine wabunge wa CCM walishaambiwa kwamba ni lazima upite kama ulivyo na hakuna aliyesumbuka kuusoma kikwelikweli, lakini baadaye ilidhihirika waziwazi kwamba muswada huo ulikuwa na udhaifu mkubwa na kasoro nyingi za kimaudhui, kisheria, kisiasa na kikanuni kikatiba ambao kwa watunga sheria makini lazima wangelihitaji muda wa ziada wa kuufanyia kazi na sio kama wenzetu walivyoanza kuchangia wakiwa na uelewa 'finyu kiuzalendo' kwa kazi iliyokwa mbele yao.
Sio siri kwamba CCM inachokitaka pengine ni kujihakikishia uzima wa milele. Kitu ambacho hakiwezekani. Na haitawezekana kwa sababu hizi si zama za Nyerere, Mkapa na Mwinyi na chochote kinaweza kutokea kwa watu ambao hali ya uchumi inawawia ngumu kila kukichwa, mali asili zao zinatwaliwa bure, watu wanauawa na kubakwa migodini na wakubwa wanapora fedha, wanyama pori, miti, ardhi na rasilimali nyingine kwa jinsi wanavyotaka. Na wasichonacho wananyang'anywa hata kile kidogo walicho nacho, wakati wenye nacho wanazidi kuongezewa kila siku.
Watanzania hawatakaa wasahau kwamba kunako mwezi Novemba, mwaka 2011 baadhi ya wabunge wao kupitia CCM walipoteza fursa ya kipekee katika kuutanguliza Utanzania mbele ya nafsi na uchama wao. Matokeo ya ubinafsi na uchama wao yakawapotezea fursa hii adhimu ambayo ingeliwaweka pazuri sana katika historia ya nchi yao na watu wake.
Kilichotokea ni kwa wabunge hao wa CCM-CUF kuonesha dhahiri kuwa ni mbwa-mwitu (wawakilishi wa chama na serikali) waliovaa ngozi ya kondoo (wawakilishi wa wananchi). Kipaumbele siku hiyo hakikupewa wananchi na vizazi vyao vijavyo bali chama, matashi yake na ubinafsi wa wabunge hata kama Watanzania kwa ujumla wao watapoteza kikubwa zaidi siku zijazo.
UCCM na UCUF kwa kiasi fulani katika hili umewafanya wengi waamini kuwa wabunge wa vyama hivyo wanastahili kupata shahada ya udaktari katika uchama, usisi, umimi na katika mapambano ya maslahi na maendeleo ya wabunge binafsi.
Kwa maneno mengine, wabunge wa CCM na CUF walikuwa wakituambia kwamba vyama vyao na uongozi wa chama chao ni muhimu kuliko Utanzania wetu au utaifa wetu, watu wetu na vizazi vyetu vijavyo.
Kubwa zaidi ni lile la spika, muwakilishaji muswada na wabunge wa CCM waliochangia muswada huo kusingizia eti kuna urongo, uzushi, upotoshaji na tafsiri mbovu ya kile kilichotakiwa kuwakilishwa. Haraka aliyokuwa nayo spika, wabunge wa CCM kuchangia na mwasilisha muswada na wenzake kuliacha maswali mengi kuliko majibu. Mwisho wa siku kilio cha spika, muwasilisha mada na wabunge wa CCM na CUF kilifanana na kile kilio cha mchunga kondoo aliyekuwa akisumbua wanakijiji wenzake kwa kupiga mayowe ya MBWA MWITU, MBWA MWITU kumbe yote ilikuwa ni mzaha kama sio urongo.
Uzaini wa CCM wa kujionesha eti wana CCM na viongozi wao wanaipenda na wana uchungu sana na Tanzania kuliko watu wengine umewafanya jamaa hao kuangukia pua katika siku ambayo wengi wao hawataiashau na wao wenyewe wameamua kujizika kihistoria.
CCM na wakewenza Unguja
Baya zaidi ni lile la muswada huo kudiriki kuifanya Zanzibar kuwa sawasawa na Tanganyika isiyopo katika kuamua hatima ya nchi yetu na watu wake. Hiki ni kitendo cha waendesha utumwa, kikoloni, kibabe, kihuni na cha kidhalimu ambacho hakistahili kukubalika.
Kwani nia ya kuwapa ukubwa huu Wazanzibari wasiostahili kuupata ni kurahisisha siasa ndani ya CCM kati ya Wazanzibari na Wabara. Kwa maneno mengine, CCM imediriki kuwauza Watanganyika kwa Wazanzibari, kama walivyouza migodi ya dhahabu, ili mradi tu mambo yao yawe safi.
Ukewenza Zanzibar na Serikali ya JMT, unatuweka pabaya kitamathali na kiuyakinifu kwa kiasi cha eti watu asilimia 2 Tanzania kuamua hatima ya asilimia 98 iliyobakia.
Kwa maneno mengine, muswada huo unawageuza Wazanzibar wakoloni na Watanganyika watawaliwa katika nchi yao wenyewe. Sijui hata kama muswada huo utapita kama hili litakaa likubalike kesho na keshokutwa.
Hadhi ya Zanzibar kiukweli haina tofauti na ya mkoa wowote bara. Tofauti tu ni kuwa mikoa inabanwa kuwa huru kisiasa, kijamii na kiuchumi kwa mafaniko yake makubwa na haraka zaidi. Kilichokosekana ni uamsho kwa wakazi mikoani na uadilifu kwa serikali kuipa mikoa serikali huru zinazosimamiwa na waziri mkuu wa mkoa, baraza la mawaziri wa mkoa na wawakilishi wa mkoa na mikoa mingi tu ingeiacha Zanzibar nyuma kimaendeleo, bila ya visiwa hivyo kuona hata indiketa za mikoa hiyo kwenye mbio za ustawi wa jamii na maendeleo ya mkoa.
Itakuwa ni jambo la fedheha kama wabunge na serikali yetu baada ya kushindwa kuafikiana na wapinzani wa kweli ndani ya bunge itakuja kufanza hivyo kwa kupata shinikizo toka Marekani na EU. Jambo hili litaonesha kwamba viongozi wetu hawajaiva wala kukomaa na hakika hawastahili kuiongoza nchi hii kama kweli tunataka kuendelea na umoja na amani tuliyo nayo hivi leo. Kinachoonekana hapa ni kwamba kuna Watanzania wenye akili na uwezo mkubwa tu lakini kwa kukosa uongozi adilifu na mzuri wanashindwa kuwatumia.
Viongozi wa dini
Viongozi wa dini kama ilivyokuwa kwa wenzetu nchini Kenya wana mchango mkubwa katika kuhakikisha Tanzania inakuwa na katiba nzuri na safi na itakayowafaa Watanzania kwa muda mrefu kuliko hii ya kupandikizwa ilivyotsukuma sukuma.
Yapo mambo kadhaa ambayo viongozi wa dini wanaowatakia Watanzania na vizazi vyao amani na umoja wanaweza kuhoji na kutoa mwongozo yaende vipi kwa faida ya watu wote. Mathalani, hivi leo kanisa katoliki linafanya vizuri sana katika elimu na sekta ya afya, lakini siasa za uziwi na upofu zinaweza kuhujumu haya yote kama katiba isipohifadhi sheria na haki muhimu za kulinda kanisa, mali zake na viongozi wake. Misikiti na Makanisa yakikaa nyuma, viongozi wa dini wasije anza kulalama baadaye kwamba katiba imewapendelea hawa, au kuwaonea hawa.
Makampuni na taasisi na katiba
Makampuni na taasisi kisheria ni sawa na mtu au raia. Makampuni na taasisi zikikaa nyuma na kutokushiriki kwenye mchakato wa katiba mpya yapo masuala mengi yanayoweza kuja kuzuka baadaye kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni yakaya kuwa ni kwa hasara kubwa kwa upande wao.
Katika suala hili lal katiba mpya sisi sote ni wadau na washiriki na hakuna anayestahili kubakia kuwa mtazamaji tu au juu ya wenzake kwa namna yoyote ile.
Muswada huu kama ilivyokuwa kwa miswaada mingine dhaifu, inayovuja na dhalimu kwa wananchi na vizazi vijavyo, imedhirisha mapungugu mengi mengine katika muundo, mifumo na taratibu zetu za uongozi na uendeshaji nchi. Baadhi ya kasoro hizi ni pamoja na hatari ya kuwa na wabunge wa kuteuliwa badala ya kuchaguliwa kwenye bunge la kiwakilishi; jinsi ambavyo serikali iliyoko madarakani inaweza ikapora mamlaka na madaraka ya wananchi na kufanya mapinduzi ya kikatiba bila kuwajibishwa ipasavyo; muungano unavyozidi kuonekana kukosa maana kwa Watanganyika na kuwa mzigo usiobebeka; na ule ukweli kuwa nchi bado imo kizani na haijajaliwa kuwa na kiongozi na wanasiasa wanaoweza kututoa kwenye shimo refu la giza ambalo tumejikuta tumo leo.
Pepe: sammy.makilla@columnist.com
Tofauti na msimamo huu wa mheshimiwa Rais, muswada wa serikali yake kwa bunge la Jamhuri ulidhihirisha nia ya serikali ya Chama cha Mapinduzi kuitumia fursa hiyo ili iweze kujikita vyema zaidi nchini kwa halali au haramu kisiasa kwa kuwatumia wabunge wao ambao ilionekana kama walishapewa mafunzo maalum kuhusu kinachotegemewa kutoka kwao.
Pamoja na spika wa bunge hilo kudai kwamba wanaharakati, wapinzani na waandishi wa habari wanapotosha kilicho mezani mwa wabunge, kazi nzuri ya uchambuzi wa kina iliyofanywa na Mheshimiwa Tundu Lissu (CHADEMA) ilionesha kulikuwa na uwezekano mkubwa wa wabunge wa CCM kutokuwa wameusoma muswada huo na Tundu akawa anapigia gitaa mbuzi.
Pengine wabunge wa CCM walishaambiwa kwamba ni lazima upite kama ulivyo na hakuna aliyesumbuka kuusoma kikwelikweli, lakini baadaye ilidhihirika waziwazi kwamba muswada huo ulikuwa na udhaifu mkubwa na kasoro nyingi za kimaudhui, kisheria, kisiasa na kikanuni kikatiba ambao kwa watunga sheria makini lazima wangelihitaji muda wa ziada wa kuufanyia kazi na sio kama wenzetu walivyoanza kuchangia wakiwa na uelewa 'finyu kiuzalendo' kwa kazi iliyokwa mbele yao.
Sio siri kwamba CCM inachokitaka pengine ni kujihakikishia uzima wa milele. Kitu ambacho hakiwezekani. Na haitawezekana kwa sababu hizi si zama za Nyerere, Mkapa na Mwinyi na chochote kinaweza kutokea kwa watu ambao hali ya uchumi inawawia ngumu kila kukichwa, mali asili zao zinatwaliwa bure, watu wanauawa na kubakwa migodini na wakubwa wanapora fedha, wanyama pori, miti, ardhi na rasilimali nyingine kwa jinsi wanavyotaka. Na wasichonacho wananyang'anywa hata kile kidogo walicho nacho, wakati wenye nacho wanazidi kuongezewa kila siku.
Watanzania hawatakaa wasahau kwamba kunako mwezi Novemba, mwaka 2011 baadhi ya wabunge wao kupitia CCM walipoteza fursa ya kipekee katika kuutanguliza Utanzania mbele ya nafsi na uchama wao. Matokeo ya ubinafsi na uchama wao yakawapotezea fursa hii adhimu ambayo ingeliwaweka pazuri sana katika historia ya nchi yao na watu wake.
Kilichotokea ni kwa wabunge hao wa CCM-CUF kuonesha dhahiri kuwa ni mbwa-mwitu (wawakilishi wa chama na serikali) waliovaa ngozi ya kondoo (wawakilishi wa wananchi). Kipaumbele siku hiyo hakikupewa wananchi na vizazi vyao vijavyo bali chama, matashi yake na ubinafsi wa wabunge hata kama Watanzania kwa ujumla wao watapoteza kikubwa zaidi siku zijazo.
UCCM na UCUF kwa kiasi fulani katika hili umewafanya wengi waamini kuwa wabunge wa vyama hivyo wanastahili kupata shahada ya udaktari katika uchama, usisi, umimi na katika mapambano ya maslahi na maendeleo ya wabunge binafsi.
Kwa maneno mengine, wabunge wa CCM na CUF walikuwa wakituambia kwamba vyama vyao na uongozi wa chama chao ni muhimu kuliko Utanzania wetu au utaifa wetu, watu wetu na vizazi vyetu vijavyo.
Kubwa zaidi ni lile la spika, muwakilishaji muswada na wabunge wa CCM waliochangia muswada huo kusingizia eti kuna urongo, uzushi, upotoshaji na tafsiri mbovu ya kile kilichotakiwa kuwakilishwa. Haraka aliyokuwa nayo spika, wabunge wa CCM kuchangia na mwasilisha muswada na wenzake kuliacha maswali mengi kuliko majibu. Mwisho wa siku kilio cha spika, muwasilisha mada na wabunge wa CCM na CUF kilifanana na kile kilio cha mchunga kondoo aliyekuwa akisumbua wanakijiji wenzake kwa kupiga mayowe ya MBWA MWITU, MBWA MWITU kumbe yote ilikuwa ni mzaha kama sio urongo.
Uzaini wa CCM wa kujionesha eti wana CCM na viongozi wao wanaipenda na wana uchungu sana na Tanzania kuliko watu wengine umewafanya jamaa hao kuangukia pua katika siku ambayo wengi wao hawataiashau na wao wenyewe wameamua kujizika kihistoria.
CCM na wakewenza Unguja
Baya zaidi ni lile la muswada huo kudiriki kuifanya Zanzibar kuwa sawasawa na Tanganyika isiyopo katika kuamua hatima ya nchi yetu na watu wake. Hiki ni kitendo cha waendesha utumwa, kikoloni, kibabe, kihuni na cha kidhalimu ambacho hakistahili kukubalika.
Kwani nia ya kuwapa ukubwa huu Wazanzibari wasiostahili kuupata ni kurahisisha siasa ndani ya CCM kati ya Wazanzibari na Wabara. Kwa maneno mengine, CCM imediriki kuwauza Watanganyika kwa Wazanzibari, kama walivyouza migodi ya dhahabu, ili mradi tu mambo yao yawe safi.
Ukewenza Zanzibar na Serikali ya JMT, unatuweka pabaya kitamathali na kiuyakinifu kwa kiasi cha eti watu asilimia 2 Tanzania kuamua hatima ya asilimia 98 iliyobakia.
Kwa maneno mengine, muswada huo unawageuza Wazanzibar wakoloni na Watanganyika watawaliwa katika nchi yao wenyewe. Sijui hata kama muswada huo utapita kama hili litakaa likubalike kesho na keshokutwa.
Hadhi ya Zanzibar kiukweli haina tofauti na ya mkoa wowote bara. Tofauti tu ni kuwa mikoa inabanwa kuwa huru kisiasa, kijamii na kiuchumi kwa mafaniko yake makubwa na haraka zaidi. Kilichokosekana ni uamsho kwa wakazi mikoani na uadilifu kwa serikali kuipa mikoa serikali huru zinazosimamiwa na waziri mkuu wa mkoa, baraza la mawaziri wa mkoa na wawakilishi wa mkoa na mikoa mingi tu ingeiacha Zanzibar nyuma kimaendeleo, bila ya visiwa hivyo kuona hata indiketa za mikoa hiyo kwenye mbio za ustawi wa jamii na maendeleo ya mkoa.
Itakuwa ni jambo la fedheha kama wabunge na serikali yetu baada ya kushindwa kuafikiana na wapinzani wa kweli ndani ya bunge itakuja kufanza hivyo kwa kupata shinikizo toka Marekani na EU. Jambo hili litaonesha kwamba viongozi wetu hawajaiva wala kukomaa na hakika hawastahili kuiongoza nchi hii kama kweli tunataka kuendelea na umoja na amani tuliyo nayo hivi leo. Kinachoonekana hapa ni kwamba kuna Watanzania wenye akili na uwezo mkubwa tu lakini kwa kukosa uongozi adilifu na mzuri wanashindwa kuwatumia.
Viongozi wa dini
Viongozi wa dini kama ilivyokuwa kwa wenzetu nchini Kenya wana mchango mkubwa katika kuhakikisha Tanzania inakuwa na katiba nzuri na safi na itakayowafaa Watanzania kwa muda mrefu kuliko hii ya kupandikizwa ilivyotsukuma sukuma.
Yapo mambo kadhaa ambayo viongozi wa dini wanaowatakia Watanzania na vizazi vyao amani na umoja wanaweza kuhoji na kutoa mwongozo yaende vipi kwa faida ya watu wote. Mathalani, hivi leo kanisa katoliki linafanya vizuri sana katika elimu na sekta ya afya, lakini siasa za uziwi na upofu zinaweza kuhujumu haya yote kama katiba isipohifadhi sheria na haki muhimu za kulinda kanisa, mali zake na viongozi wake. Misikiti na Makanisa yakikaa nyuma, viongozi wa dini wasije anza kulalama baadaye kwamba katiba imewapendelea hawa, au kuwaonea hawa.
Makampuni na taasisi na katiba
Makampuni na taasisi kisheria ni sawa na mtu au raia. Makampuni na taasisi zikikaa nyuma na kutokushiriki kwenye mchakato wa katiba mpya yapo masuala mengi yanayoweza kuja kuzuka baadaye kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni yakaya kuwa ni kwa hasara kubwa kwa upande wao.
Katika suala hili lal katiba mpya sisi sote ni wadau na washiriki na hakuna anayestahili kubakia kuwa mtazamaji tu au juu ya wenzake kwa namna yoyote ile.
Muswada huu kama ilivyokuwa kwa miswaada mingine dhaifu, inayovuja na dhalimu kwa wananchi na vizazi vijavyo, imedhirisha mapungugu mengi mengine katika muundo, mifumo na taratibu zetu za uongozi na uendeshaji nchi. Baadhi ya kasoro hizi ni pamoja na hatari ya kuwa na wabunge wa kuteuliwa badala ya kuchaguliwa kwenye bunge la kiwakilishi; jinsi ambavyo serikali iliyoko madarakani inaweza ikapora mamlaka na madaraka ya wananchi na kufanya mapinduzi ya kikatiba bila kuwajibishwa ipasavyo; muungano unavyozidi kuonekana kukosa maana kwa Watanganyika na kuwa mzigo usiobebeka; na ule ukweli kuwa nchi bado imo kizani na haijajaliwa kuwa na kiongozi na wanasiasa wanaoweza kututoa kwenye shimo refu la giza ambalo tumejikuta tumo leo.
Pepe: sammy.makilla@columnist.com
Tuesday, November 8, 2011
Ndoa isiyo na tija
Ni ndoa yenye ugumba, ndoa isiyo na tija,
Hili sio la kutamba, lataka funga mkaja,
Na wengine hulichamba, wasiache kubwabwaja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ni ndoa yenye ugumba, ndoa isiyo na tija,
Wanandoa hujisomba, wakuja na wasokuja,
Utadhani ni mtumba, hujui aliyeufuja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ndoa ni kitu cha namba, kukua si rejareja,
Yataka mengi kuumba, na sio kwishia moja,
Yataka kujenga nyumba, na pengine kwenda hija,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ndoa sio kama gamba, kuvua halina haja,
Utaonwa ni mshamba, ukabakia mseja,
Ndoa kuvuta kamba, lenu wote kuwa moja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ndoa tamu ya kulamba, ikiwa rojo vioja,
Yataka hali kuvimba, ovyo vitu kutofuja,
Yataka kuvuta kamba, mbele mkajikongoja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Akiba anayekomba, upesi kumvua koja,
Na mtaji anayefuja, ni kumshusha daraja,
Maisha yataka gomba, haikubali harija,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ni ndoa yenye ugumba, ndoa isiyo na tija,
Huhasiri na unyumba, pasiwepo na umoja,
Japo mwafunga vilemba, nje watu hawana haja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Hili sio la kutamba, lataka funga mkaja,
Na wengine hulichamba, wasiache kubwabwaja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ni ndoa yenye ugumba, ndoa isiyo na tija,
Wanandoa hujisomba, wakuja na wasokuja,
Utadhani ni mtumba, hujui aliyeufuja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ndoa ni kitu cha namba, kukua si rejareja,
Yataka mengi kuumba, na sio kwishia moja,
Yataka kujenga nyumba, na pengine kwenda hija,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ndoa sio kama gamba, kuvua halina haja,
Utaonwa ni mshamba, ukabakia mseja,
Ndoa kuvuta kamba, lenu wote kuwa moja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ndoa tamu ya kulamba, ikiwa rojo vioja,
Yataka hali kuvimba, ovyo vitu kutofuja,
Yataka kuvuta kamba, mbele mkajikongoja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Akiba anayekomba, upesi kumvua koja,
Na mtaji anayefuja, ni kumshusha daraja,
Maisha yataka gomba, haikubali harija,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ni ndoa yenye ugumba, ndoa isiyo na tija,
Huhasiri na unyumba, pasiwepo na umoja,
Japo mwafunga vilemba, nje watu hawana haja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Sasa vuta nikuvute
Lazima nchi itwete, na kujakauka mate,
Watajatembea viwete, zikijageuka kete,
Na watu lazima mtote, kwa jasho pia matete,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Hali hii sasa tete, mambo vuta nikuvute,
Watu wataka wapate, si skuzote waote,
Ndoto wazitema mate, na hawataki mfute,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Ahadi kwao uwete, hungoja usiwakute,
Ni puya wazipepete, nafaka wasipukute,
Wengine msinifate, uoga jadi ya wote,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Nakukumbuka Mnete, Ujerumani usinate,
Njoo tuhidi viwete, hata kidogo waokote,
Na neema uilete, misada waipate,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Kila mtu ana kete, ataka naye apate,
Hatoishi kwa mkate, mtu anataka vyote,
Kwa hili msimsute, suteni nafsi zote,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Mtapoenda popote, chunguzeni na mtete,
Ili amani iote, fanaka iwe kwa wote,
Watu lisiwakerekete, la kukosa wao mkate,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Na hata vipi mnyate, gizani vyenu mng'ate,
Bado hudondoka mate, usingizini waote,
Kuteketea si lolote, na umauti ni wa wote,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Naomba yasinikute, nilapo wote niite,
Hata kidogo nipate, tutagawana na wote,
Na Rabana asisite, kichache aje avute,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Utupe leo mkate, peke yetu tusifute,
Na wenzetu waupate, slensi isiwapite,
Baadaye nisijute, kwa ubinafsi nisutwe,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Watajatembea viwete, zikijageuka kete,
Na watu lazima mtote, kwa jasho pia matete,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Hali hii sasa tete, mambo vuta nikuvute,
Watu wataka wapate, si skuzote waote,
Ndoto wazitema mate, na hawataki mfute,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Ahadi kwao uwete, hungoja usiwakute,
Ni puya wazipepete, nafaka wasipukute,
Wengine msinifate, uoga jadi ya wote,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Nakukumbuka Mnete, Ujerumani usinate,
Njoo tuhidi viwete, hata kidogo waokote,
Na neema uilete, misada waipate,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Kila mtu ana kete, ataka naye apate,
Hatoishi kwa mkate, mtu anataka vyote,
Kwa hili msimsute, suteni nafsi zote,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Mtapoenda popote, chunguzeni na mtete,
Ili amani iote, fanaka iwe kwa wote,
Watu lisiwakerekete, la kukosa wao mkate,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Na hata vipi mnyate, gizani vyenu mng'ate,
Bado hudondoka mate, usingizini waote,
Kuteketea si lolote, na umauti ni wa wote,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Naomba yasinikute, nilapo wote niite,
Hata kidogo nipate, tutagawana na wote,
Na Rabana asisite, kichache aje avute,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Utupe leo mkate, peke yetu tusifute,
Na wenzetu waupate, slensi isiwapite,
Baadaye nisijute, kwa ubinafsi nisutwe,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Mwvi kamwambia....
Naishangaa dunia, kuja kuumwa mwiibiwa,
Mifuko kanipekua, na mbwa kasakazia,
Mwizi ananiibia, ataka nimalizia?
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Tukio lilipotokea, wala usingedhania,
Jizi kunishambulia, na mbwawe kunivamia,
Ah, jamani ninalia, haki inshakupotea,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Shilingi kazichukua, maumivu kunachia,
Simu nayo kaizoa, na yangu dhahabu saa,
Kila nikifikiria, nazidi kuchanganyikiwa,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Mtu hakujatokea, mie kunisadia,
Kufurukuta haikua, mbwa kuning'atua,
Amtii na kumsikia, chakula anayempatia,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Hii ndiyo yetu dunia, na hizi zake hatua,
Haki viumbe wajua, sasa waweza nunua,
Wenye haki wanagwaya, ndani huja wakatiwa,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Mwivi huru anakua, na kutamba hukutambia,
Hujui utanijua, mpini nashikilia,
Mikono yako nchani, nikivuta hatarini,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Mifuko kanipekua, na mbwa kasakazia,
Mwizi ananiibia, ataka nimalizia?
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Tukio lilipotokea, wala usingedhania,
Jizi kunishambulia, na mbwawe kunivamia,
Ah, jamani ninalia, haki inshakupotea,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Shilingi kazichukua, maumivu kunachia,
Simu nayo kaizoa, na yangu dhahabu saa,
Kila nikifikiria, nazidi kuchanganyikiwa,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Mtu hakujatokea, mie kunisadia,
Kufurukuta haikua, mbwa kuning'atua,
Amtii na kumsikia, chakula anayempatia,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Hii ndiyo yetu dunia, na hizi zake hatua,
Haki viumbe wajua, sasa waweza nunua,
Wenye haki wanagwaya, ndani huja wakatiwa,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Mwivi huru anakua, na kutamba hukutambia,
Hujui utanijua, mpini nashikilia,
Mikono yako nchani, nikivuta hatarini,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
NYIE hawatawafunga, mkifunga wapinzani,
Mbona mnayabananga,hamjui mwajizaini,
Dunia geuzi anga,wajinga hawabaini,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Kutesa kwa zamu ringa, ila ujue yakini,
Wafunge watakufunga, kama haki hukuauni,
Usiombee kimbunga,kikukute mtaani,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Hujatengwa na mtenga, wajua Raskazoni,
Mpingwa huja kupinga, ikawa abautani,
Mgongwa huja kugonga, ujikute hatarini,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Sheria ukizipanga, jua na wewe undani,
Na kanuni ukitunga, jione nawe mpinzani,
Ujapoivaa khanga, usilisahau gauni,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Ukiuchonga mzinga, na nyuki wabaini,
Asali ukenda kinga, kubali na yake faini,
Porini ukenda chunga, simba usiwaamini,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Hukungwa naye mkunga, uzazi hauna dini,
Na mfungwa huja kufunga, Mandela hili aamini,
Ila sidhani kwa mwanga, iweje kuwangiwani?
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Hutwanga mtwanga unga, na hili asibaini,
Nchi yataka waganga, haitaki majinuni,
Nchi yataka kuunga, nyie vipi mwabanduani?
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Mbona mnayabananga,hamjui mwajizaini,
Dunia geuzi anga,wajinga hawabaini,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Kutesa kwa zamu ringa, ila ujue yakini,
Wafunge watakufunga, kama haki hukuauni,
Usiombee kimbunga,kikukute mtaani,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Hujatengwa na mtenga, wajua Raskazoni,
Mpingwa huja kupinga, ikawa abautani,
Mgongwa huja kugonga, ujikute hatarini,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Sheria ukizipanga, jua na wewe undani,
Na kanuni ukitunga, jione nawe mpinzani,
Ujapoivaa khanga, usilisahau gauni,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Ukiuchonga mzinga, na nyuki wabaini,
Asali ukenda kinga, kubali na yake faini,
Porini ukenda chunga, simba usiwaamini,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Hukungwa naye mkunga, uzazi hauna dini,
Na mfungwa huja kufunga, Mandela hili aamini,
Ila sidhani kwa mwanga, iweje kuwangiwani?
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Hutwanga mtwanga unga, na hili asibaini,
Nchi yataka waganga, haitaki majinuni,
Nchi yataka kuunga, nyie vipi mwabanduani?
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Waziri mkuu wa mkoa....
Nchi haitoendelea, bila mkoa huru kuwa,
Maamuzi kujifanyia, bila ya mtu kungojea,
Na awe nayo raia, sauti ya kusikiwa,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Arusha yasingetokea, leo yanayotokea,
Mkoa unatawaliwa, na chama chenye izaya,
Wajanja walipokwapua, kile wasichojivunia,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Mbeya ukiangalia, chama fulani chafaa,
Kuutawala mkoa, zingeliisha ghasia,
Uchumi wadidimia, king'ang'anizi kung'ang'ania,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Na Mwanzo nako pia, kama haya yatokea,
Uhuru wanalilia, wakazi wake mkoa,
Mambo yao kimkoa, wao wenyewe kuamua,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Wamechoka kuwekewa, viongozi wasofaa,
Na tena sio wazawa, uchungu nao hawajawa,
Angelikuwa mwana kaya, uchumi angelipaua,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Ardhi wanachukua, wa mkoa wasokuwa,
Juu walikokalia, wawekezaji wauzia,
Sasa wanagombania, ardhi kujilindia,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Mali asili tambua, ni ya wakazi wa mkoa,
Haijawa, haitakuwa, ya hao wanaopewa,
Tutaambiana ubaya, haya yakija tokea,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Tuacheni kusinzia, haja za watu kujua,
Muda usijepotea, mabaya kujatokea,
Ama chelewa chelewa, mwana hutomkumbatia!
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Maamuzi kujifanyia, bila ya mtu kungojea,
Na awe nayo raia, sauti ya kusikiwa,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Arusha yasingetokea, leo yanayotokea,
Mkoa unatawaliwa, na chama chenye izaya,
Wajanja walipokwapua, kile wasichojivunia,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Mbeya ukiangalia, chama fulani chafaa,
Kuutawala mkoa, zingeliisha ghasia,
Uchumi wadidimia, king'ang'anizi kung'ang'ania,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Na Mwanzo nako pia, kama haya yatokea,
Uhuru wanalilia, wakazi wake mkoa,
Mambo yao kimkoa, wao wenyewe kuamua,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Wamechoka kuwekewa, viongozi wasofaa,
Na tena sio wazawa, uchungu nao hawajawa,
Angelikuwa mwana kaya, uchumi angelipaua,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Ardhi wanachukua, wa mkoa wasokuwa,
Juu walikokalia, wawekezaji wauzia,
Sasa wanagombania, ardhi kujilindia,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Mali asili tambua, ni ya wakazi wa mkoa,
Haijawa, haitakuwa, ya hao wanaopewa,
Tutaambiana ubaya, haya yakija tokea,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Tuacheni kusinzia, haja za watu kujua,
Muda usijepotea, mabaya kujatokea,
Ama chelewa chelewa, mwana hutomkumbatia!
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Siasa kongwe na nzee
Mbali tuzitupilie, siasa kongwe na nzee,
Kale isituzuzue, tulipo hapo tutue,
Yajayo tutabirie, tupange tufanikiwe,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Hivi sasa tuamue, nani nchi tuwaachie,
Shughuli waifanyie, umaskini waondoe,
Watu watutumie, taifa juu lipae,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Tupumue, tusikae, mchakamchaka uwe,
Usia tukumbukie, baba taifa atoe,
Budi sisi tukimbie, acha wengine watembee,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Batabata tuwatoe, si mwendo watu uwafae,
Hatua tuzichukue, mbiombio tukimbie,
Malengo tuyafikie,dunia itushangae,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Majukumu tuyajue, kisha tushughulikie,
Katu wote tusitue, na wala tusitulie,
Nchi yataka itibiwe, na nafuu ipatiwe,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Matatizo tutatue, Watanzania wapumue,
Mbeleni tusiugue, maradhi yote yatibiwe,
Kivulini tuingie, kama walivyo wengine,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Haki tuizingatie, udikteta uvie,
Ukiritimaba tuue, na uhuru ukomae,
Ubabe tuukatae, na dola isitumiwe,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Sherehe tusherehekee, sio wajisherehekee,
Wananchi chini wasiwe, ila juu watulie,
Dunia iwasifie, wajifunze na wajue,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Kale isituzuzue, tulipo hapo tutue,
Yajayo tutabirie, tupange tufanikiwe,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Hivi sasa tuamue, nani nchi tuwaachie,
Shughuli waifanyie, umaskini waondoe,
Watu watutumie, taifa juu lipae,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Tupumue, tusikae, mchakamchaka uwe,
Usia tukumbukie, baba taifa atoe,
Budi sisi tukimbie, acha wengine watembee,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Batabata tuwatoe, si mwendo watu uwafae,
Hatua tuzichukue, mbiombio tukimbie,
Malengo tuyafikie,dunia itushangae,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Majukumu tuyajue, kisha tushughulikie,
Katu wote tusitue, na wala tusitulie,
Nchi yataka itibiwe, na nafuu ipatiwe,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Matatizo tutatue, Watanzania wapumue,
Mbeleni tusiugue, maradhi yote yatibiwe,
Kivulini tuingie, kama walivyo wengine,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Haki tuizingatie, udikteta uvie,
Ukiritimaba tuue, na uhuru ukomae,
Ubabe tuukatae, na dola isitumiwe,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Sherehe tusherehekee, sio wajisherehekee,
Wananchi chini wasiwe, ila juu watulie,
Dunia iwasifie, wajifunze na wajue,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Muungano kama hawa
Kitupu changu kibaba, japo ninaitwa baba,
Wanangu wananikaba, njaa yawapa adhaba,
Nimemlilia toba, naisubiri ratiba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba,
Kiwapi changu kiroba, nyumbani nikakibeba,
Abu, kazi ya bawaba, na mlango haujashiba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Jua njaa yake tiba, si dawa ila kushiba,
Iwe Dovya au Goba, waitaka hii tiba,
Hawaishi kwa ghiliba, utawaumbua msiba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Hata uvae majuba, njaa haina haiba,
Kwa kila mtu ni mwiba, kuzidi kuuziriba,
Na ukizikosa raba, donda huzidi mraba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Unguja si kama Pemba, Tanganyika si kisiwa,
Kukunana ni habiba, kibaba mpe kibaba,
Hukurubisha nasaba, na kuchipuka mahaba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Kazi wote kuzibeba, kubanana na kukaba,
Kutegea si haiba, husababisha msiba,
Wengine hawali riba,kuwaepusha ni toba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Kuukuza uswahiba, lazima wote kushiba,
Tuzieupuke kadhaba, na nyufa kuja ziziba,
Wafanye kazi ngariba, kutahiri waso hiba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Namshukuru Hassaba. hesabu mwenye kutamba,
Atwepushe na ghiliba, ukweli ziwe hutuba,
Pasiwe wanaoiba, wakakwaza ukuruba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Wanangu wananikaba, njaa yawapa adhaba,
Nimemlilia toba, naisubiri ratiba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba,
Kiwapi changu kiroba, nyumbani nikakibeba,
Abu, kazi ya bawaba, na mlango haujashiba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Jua njaa yake tiba, si dawa ila kushiba,
Iwe Dovya au Goba, waitaka hii tiba,
Hawaishi kwa ghiliba, utawaumbua msiba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Hata uvae majuba, njaa haina haiba,
Kwa kila mtu ni mwiba, kuzidi kuuziriba,
Na ukizikosa raba, donda huzidi mraba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Unguja si kama Pemba, Tanganyika si kisiwa,
Kukunana ni habiba, kibaba mpe kibaba,
Hukurubisha nasaba, na kuchipuka mahaba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Kazi wote kuzibeba, kubanana na kukaba,
Kutegea si haiba, husababisha msiba,
Wengine hawali riba,kuwaepusha ni toba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Kuukuza uswahiba, lazima wote kushiba,
Tuzieupuke kadhaba, na nyufa kuja ziziba,
Wafanye kazi ngariba, kutahiri waso hiba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Namshukuru Hassaba. hesabu mwenye kutamba,
Atwepushe na ghiliba, ukweli ziwe hutuba,
Pasiwe wanaoiba, wakakwaza ukuruba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Kina kabla ya uhuru
Hawa ninawaambia, kabla walozaliwa,
Uhuru kuingia, Tanganyika na Zanzibar,
Tuwatunuku hidaya, ila kuongoza baa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Mtakuwa ni raia, haki zote mtapewa,
Ila kutusimamia, hilo tunalikataa,
Nchi mmeifumua, kushonwa inatakiwa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Vijana wanatakiwa, kompyuta kuzivaa,
Ofisini wakikaa, wajua yanayotokea,
Mizubao na sinzia, kuondoka ni huria,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Twataka wanaojua, uchumi kuutibia,
Isiwe tunaugua, malale na kusinzia,
Hoja kuzichanganua, miradi ije tufaa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
KazI mmeshatufanyia, nchi ni kutuachia,
Ushauri kuutoa, pembeni mmesogea,
Nasi tutawachambulia, Tanzania kuja paa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Wenyewe kujichagua, bila jina kwangalia,
Ujuzi umejaliwa na kazi unaijua,
Ndani utajaingia, ufanye ya manufaa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Barabara kujijengea, hatua tutazichukua,
Reli kukarabatia, msaada si ruia,
Na umeme kusambaa, hiyo kazi ya siku moya,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Maji tutawamiminia, maziwani kuyavua,
Mito tutajihamia, yazidi maji kujaa,
Na misitu kuridhia, wananchi kujilindia,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Ardhi hatutaigawa, kwa wageni bila ubia,
Hati tutatishikilia, hadi kijapo kiyama,
Nani wa kutununua, na sisi wote wazawa?
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Uhuru kuingia, Tanganyika na Zanzibar,
Tuwatunuku hidaya, ila kuongoza baa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Mtakuwa ni raia, haki zote mtapewa,
Ila kutusimamia, hilo tunalikataa,
Nchi mmeifumua, kushonwa inatakiwa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Vijana wanatakiwa, kompyuta kuzivaa,
Ofisini wakikaa, wajua yanayotokea,
Mizubao na sinzia, kuondoka ni huria,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Twataka wanaojua, uchumi kuutibia,
Isiwe tunaugua, malale na kusinzia,
Hoja kuzichanganua, miradi ije tufaa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
KazI mmeshatufanyia, nchi ni kutuachia,
Ushauri kuutoa, pembeni mmesogea,
Nasi tutawachambulia, Tanzania kuja paa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Wenyewe kujichagua, bila jina kwangalia,
Ujuzi umejaliwa na kazi unaijua,
Ndani utajaingia, ufanye ya manufaa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Barabara kujijengea, hatua tutazichukua,
Reli kukarabatia, msaada si ruia,
Na umeme kusambaa, hiyo kazi ya siku moya,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Maji tutawamiminia, maziwani kuyavua,
Mito tutajihamia, yazidi maji kujaa,
Na misitu kuridhia, wananchi kujilindia,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Ardhi hatutaigawa, kwa wageni bila ubia,
Hati tutatishikilia, hadi kijapo kiyama,
Nani wa kutununua, na sisi wote wazawa?
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Kuiba kura mauaji
eri wa mali ni mwizi, wa kura ni muuaji,
Haki anaidarizi, kumpa aso na mji,
Ni msanja wa kunazi, haubebi hata maji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Anamzidi jambazi, kura anayezifoji,
Si mthamini kizazi, huyu wa wazi mkabaji,
Anajal imatanuzi, na ukubwa kuuhiji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Hana radhi ya mazi, huyu ni mgeuzaji,
Na kinyesi na ushuzi, kwake yeye upambaji,
Ukilifanya fumanizi, usiache utekaji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Ni gunia la viazi, lisilo na mbebaji,
Kunyanyuka haliwezi, hadi aje mchukuaji,
Ni chombo kisicho kazi, kutupwa ni mataraji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Tabia yake ushenzi, hata ikiwa ya jaji,
Huuzwa kwa manunuzi, haki tusijeitaraji,
Ni mbegu za maangamizi, hazifanzi uokoaji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Havistahi makuzi, ni kama mnenguaji,
Kiuno bila shimizi, ndio chazidi kuchaji,
Na ya jana sio juzi, hautaivaa beji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Kibirizi, kibirizi, mlinzi na mauaji,
Hili ni kama jinamizi, kuponya linahitaji,
Na usalama si wizi, kama hivyo hatuuhitaji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Utu sio sisimizi, watu viumbe hojaji,
Usitumiwe kama ngazi, kesho haitakufariji,
Kama umekosa kazi, kwingine tafuta mtaji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Haki anaidarizi, kumpa aso na mji,
Ni msanja wa kunazi, haubebi hata maji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Anamzidi jambazi, kura anayezifoji,
Si mthamini kizazi, huyu wa wazi mkabaji,
Anajal imatanuzi, na ukubwa kuuhiji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Hana radhi ya mazi, huyu ni mgeuzaji,
Na kinyesi na ushuzi, kwake yeye upambaji,
Ukilifanya fumanizi, usiache utekaji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Ni gunia la viazi, lisilo na mbebaji,
Kunyanyuka haliwezi, hadi aje mchukuaji,
Ni chombo kisicho kazi, kutupwa ni mataraji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Tabia yake ushenzi, hata ikiwa ya jaji,
Huuzwa kwa manunuzi, haki tusijeitaraji,
Ni mbegu za maangamizi, hazifanzi uokoaji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Havistahi makuzi, ni kama mnenguaji,
Kiuno bila shimizi, ndio chazidi kuchaji,
Na ya jana sio juzi, hautaivaa beji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Kibirizi, kibirizi, mlinzi na mauaji,
Hili ni kama jinamizi, kuponya linahitaji,
Na usalama si wizi, kama hivyo hatuuhitaji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Utu sio sisimizi, watu viumbe hojaji,
Usitumiwe kama ngazi, kesho haitakufariji,
Kama umekosa kazi, kwingine tafuta mtaji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Siasa na umafia
Yabadilika dunia, na ujanja unakua,
Ili kutokudhaniwa, jambazi polisi hua,
Vigumu kutuhumiwa, wadhifa anaopewa,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Padri ukishakua, nani atakudhania,
Zinaa ukiingia, na uchafu kukujaa,
Wengine watashukiwa, salama utabakia,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Ustadhi ukishakua, mcha Mungu wakujua,
Uovu ukipania, gizani hawatajua,
Siri utajifichia, hadi zizidi tamaa,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Na siasa nazo pia, upupu zinachukua,
Fikra zazidi via, nani anayefikiria,
Roboti utadhaia, wanayozungumzia,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Watu wasio ulua, fani wameivamia,
Kuiba waazimia, ni nani atawajua ?
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Uongozi wakikwaa, ganzi wameshajipatia,
Mbwa mwitu hujavaa, ngozi ya kondoo mliwa,
Kundini wakishaingia, kazi yao kutanua,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Wanono watajilia, tena kimya kimya,
Hakuna atayejua, hadi mtu kufichua,
Ila taifa huvia, na kuzidi kusinyaa,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Na vyama vyajatokea, udokozi kuulea,
Hazina kujaingia, kila kitu kupakua,
Pasiwe cha kubakia, ilo mifupa masalia,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Ili kutokudhaniwa, jambazi polisi hua,
Vigumu kutuhumiwa, wadhifa anaopewa,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Padri ukishakua, nani atakudhania,
Zinaa ukiingia, na uchafu kukujaa,
Wengine watashukiwa, salama utabakia,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Ustadhi ukishakua, mcha Mungu wakujua,
Uovu ukipania, gizani hawatajua,
Siri utajifichia, hadi zizidi tamaa,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Na siasa nazo pia, upupu zinachukua,
Fikra zazidi via, nani anayefikiria,
Roboti utadhaia, wanayozungumzia,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Watu wasio ulua, fani wameivamia,
Kuiba waazimia, ni nani atawajua ?
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Uongozi wakikwaa, ganzi wameshajipatia,
Mbwa mwitu hujavaa, ngozi ya kondoo mliwa,
Kundini wakishaingia, kazi yao kutanua,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Wanono watajilia, tena kimya kimya,
Hakuna atayejua, hadi mtu kufichua,
Ila taifa huvia, na kuzidi kusinyaa,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Na vyama vyajatokea, udokozi kuulea,
Hazina kujaingia, kila kitu kupakua,
Pasiwe cha kubakia, ilo mifupa masalia,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Monday, November 7, 2011
Vyama vya kisiasa Tanzania vimepitwa na wakati ? Sehemu- I
MABADILIKO yanayotokea duniani yanawawia vigumu vikongwe wa kisiasa kuyaelewa na kuyatafsiri katika mtazamo na macho ya ulimwengu wa sasa. Kama ilivyo kawaida kwa mwanadamu hatua za kwanza wanazochukua ni kupambana ili kuzuia mabadaliko hayo yasijiri makwao.
Haijawahi kutokea katika nchi yoyote ile duniani kwa mabadiliko makubwa ya kisiasa, kiuchumi na kijamii kufanyika kirahisi na bila kuwa na upinzani mkali, mkubwa na wa kutisha toka kwa wattu waoga, mbumbu, wasiojua kinachoendelea, wanaonufaika na mfumo wa hali iliyopo au wale wanaotumiwa na wanaonufaika kuwalinda wao na mali zao.
Ninasema vyama vya siasa Tanzania vimepitwa na wakati kwa sababu kile kilichozoea ukiritimba wa mfumo wa chama kimoja kinajiendesha kama wito na kazi yake kuu ni kupambana na wale wanaotaka kife; wakati wale wa iwezekanayo kuwa serikali mbadala na katika mfumo ambao si tofauti sana na wa chama kimoja katika mambo mengi, wanajiendesha kama vile kazi yao kubwa ni kuja kuingia madarakani kwa udi na uvumba. Hakuna kati yao ambaye anatoa uzito stahilifu kwa matatizo na changamoto za wananchi. Na kwa maana hii sio tu ninaona vimepitwa na wakati bali ninadhani vyama vyote havistahili hata kuwepo na nchi imekosa tu watu wanaoweza kuthubutu kuvifagia pembeni hata kabla ya uchaguzi mkuu ujao.
Mabadiliko ambayo Tanzania inastahili kuyafanya hivi sasa hayana tofauti kwa namna yoyote ile na mabadiliko mengine kama hayo yanayotokea kwingine duniani na yaliyokwishatokea pengine na katika karne nyingine huko nyuma yetu.
Tofauti tu iliyopo hivi sasa ni kuwa sisi kama watu mmoja mmoja na kitaifa hatujajipanga ipasavyo kuweza kuhakikisha kuwa mabadiliko hayo yanatokea kwa faida na manufaa yetu na sio kwa ujibari, ujivuni, kisirani na hasara kwa upande wetu.
Na katika hili kiongozi mkuu wa kujipanga kuyakabili mabadiliko anatakiwa awe ni chama cha kisiasa cnenye viongozi wanaojua watu wanataka kuelekea wapi, nchi inaelekea wapi, duniani inaelekea wapi, nani wanastahili kuwa rafiki zetu na nani hatustahili kuwaamini, kuwathamini na kuwaingiza katika siri na mambo yetu mengine.
Ni chama kinachostahili kuwa na mipango, mikakati, sera, muundo, mfumo, taratibu na kanuni za utekelezaji zinazokipa chama ukuu na nguvu juu ya mwanachama mmoja mmoja au kundi la wanachama fulani ndani ya chama husika katika mustakabali wa kujenga umoja wa chama lakini ndani ya mfumo wa demokrasia hai na inayofanya kazi. Ugonjwa wa 'ndivyotunavyofikiri' ukiachiwa kutambaa kwenye mwili-siasa wa jamii hivi leo ni dhahiri maradhi makubwa zaidi yatajitokeza na kupona kwa mgonjwa kutahitaji manabii na miujiza.
Ni chama ambacho kina 'visheni' na 'misheni' bayana ambazo wanaokiongoza hata wakikurupushwa usingizini wanavikariri bila kukosea hata neno moja.
Ni chama kinachotakiwa kuwa na mizizi yake vijijini zaidi kwa kukivewezesha vijiji na wanavijiji na sio mjini kwenye watu wachache na walioelimika vya kutosha. Ni chama ambacho ofisi zake vijijini vitakuwa ni vituo muhimu katika kazi zake mbalimbali na ofisi ambazo zina nafasi kwa ofisi za viongozi wa wilaya, mkoa na kitaifa na ukumbi wa mkutano ambao vikao vikubwa kwa vidogo vya chama vinaweza kufanyika huko bila wasiwasi na uwepo wa sehemu kama hiyo kuwa ni hamira au chachu ya maendeleo ya kijiji na wanakijiji husika.
Ni kawaida pia kinachopingwa, kupinga na kupambana na kile kinachokipinga. Lakini kwa jambo lolote ambalo wakati wake umefika ni muhali na kazi bure kulipinga. Ima-fa-ima lazima mabadiliko yanayopaswa kufanyika yatafanyika tu.
Ili kutopotezeana muda ni vyema kufunguana macho na kuhamasisha jamii kufagia yale yote yenye kunukia uzee au ukongwe usio na faida na ambayo yanaweza kusababisha kuvunjika kwa amani na umoja katika nchi hii eti tu kwa kuwa ukongwe huo unakataa mabadiliko yasitokee.
Hali ilivyo sasa ni kwamba wanasiasa waliopo wamezoea kutawala kwa kutumia mabavu na maguvu; udikteta na ukiritimba katika maamuzi na uendeshaji vyama; kusukumiza kwenye makoo ya raia zao katiba na sheria zisizokubalika; kupora mamlaka na madaraka ya wananchi kinyume na katiba; kutumia njia za haramu kupata mapato yao na ya chama; kutumia vyombo vya dola kwa faida na maslahi yake; uzaini na uongo; kununua na kuwatumia watu; kugawa na kutawala; kulea ukabila wa kichama kwa maana ya kuwabeba tu wanachama wa chama tawala kuwa viongozi na kuwaacha wasio wanachama bila kazi wala changamoto za maana katika kuendeleza wilaya au mkoa au taifa;
uroho, choyo, inda na ulafi wa hali ya juu kutaka kutawala hata pale chama husika kisipokuwa na sapoti ya kutosha; kutumia vyombo vya usalama vya taifa kwa matumizi binafsi na sio kwa maslahi ya kitaifa; kutumia vyombo vya habari kukwamisha uwazi na kudanganya badala ya kusema ukweli; Viongozi wasio na mwelekeo wa kuinufaisha nchi hii na watu bali zaidi wao wenyewe na watu wa nje, kutumia makundi ya kijamii kama vile wanawake, vijana, wazee, wazazi, wanavijiji, wanafunzi, walimu, wafanyakazi na kadhalika kwa manufaa yao na sio ya kitaifa au ya umma; kuwatumia waandishi habari kama askari wa kukodiwa kufanikisha malengo yao; kushirikiana na mafisadi na wevi kufanikisha malengo ya kichama; kuingiza udini na ukabila katika uongozi na uanachama; kutumiwa na viongozi wa nje wa serikali na makampuni kwa maslahi yao na sio ya Watanzania; kushindwa kujenga imani na kujiamini kwamba kwa kutumia rasilimali zetu wenyewe tunaweza kunufaika zaidi kuliko kudanganywa kwa misaada toka nchi za nje ambayo ni sawa na mtu kupewa perememde wewe ukaibiwa kipande cha almasi au vito vingine vyenye thamani.
Mlolongo huo hapo juu ni ushahidi tosha unaonesha ni kwa kiasi gani vyama vya kisiasa nchini Tanzania vimepitwa na wakati na vinahitaji kufa au kupona 'kusasaishwa' ili sio tu viende na wakati bali viweze kutekeleza kwa ukamilifu na usahihi zaidi majukumu yao ya kisiasa, kijamii na kitaifa.
Ili kwenda na wakati vyama vya kisiasa vinastahili pamoja na mambo mengine kuwa na wanasiasa wasioshindwa na wasiotishika katika kutumia nguvu ya hoja, uchanganuzi, uchambuzi na ubunifu katika kuongoza na wanaostawi katika kutofautiana kimawazo, kifikra na kimaono.
Lazima kila chama kihakikisha kuwepo kwa demokrasia na uhuru wa kuchagua au kuchaguliwa ndani na nje ya chama; kuruhusu kuwepo kwa katiba na sheria zilizoandikwa na wanachama au wananchi wenyewe na sio wao kama viongozi au watawala; na pia kutumia njia za halali na zinazokubalika na zisizowaumiza watu wengine kupata mapato yao na ya chama.
Ni wajibu wa chama chochote ndani au nje ya madaraka kuvhiheshimu, kushirikiana na kuvitumia vyombo vya dola kwa faida na maslahi ya umma na si watu wachache; na kujali usawa, haki na ukweli wakati wote.
Kila chama kinastahili kuthamini utu na ubinadamu wa raia wote; kujenga umoja katika tofauti za kiimani na kiitikadi; kukana na kuharamisha ukabila wa aina zote ukiwemo ule ukabila wa kichama, udugu, ujamaa na urafiki katika kazi na majukumu mengine ya kitaifa.
Chama lazima kidhibiti wakati wote uroho, choyo, inda na ulafi miongoni mwa wanachama na viongozi wake; kuwaachia wengine kutawala pale chama kisipokubalika na wakazi husika; na kutotumia vyombo vya usalama wa taifa kwa maslahi, matakwa na haja binafsi ikiwemo kuwachunguza viongozi wastaafu, wanaharakati na wanachama na viongozi wa upinzani.
KIla chama kinawajibika kutotumia vyombo vya habari kudanganya wale wenye uelewa duni wa mambo; kutowaweka waavijiji katika giza la kuelewa na kukubali kuwa demokrasia na vyama vingi ni jambo lenye manufaa kwetu kama nchi na watu; na pia kutowatumia waandishi habari kama askari wa kukodiwa kufanikisha malengo ya chama na viongozi wake.
Chama kinawajibika kutoshirikiana na matajiri na mafisadi katika kupora madini na maliasili za nchi hii; kutowagawa Watanzania katika makundi ya kijamii yanayoweza kuja kuwa hatari kwa taifa baadaye, k.m, vijana, wazee, wanafunzi, wanawake, wazazi wa chama fulani n.k.
Chama kiwe makini na kutoingiza udini na ukabila katika uongozi na uanachama; kutotumiwa na viongozi wa nje wa serikali na makampuni kwa maslahi yao na sio ya Watanzania; kufanikisha kujenga imani na kujiamini miongoni mwa Watanzania kwamba kwa kutumia watu wetu wenyewe, wazungu wasio na ajira makwao, rasilimali zetu wenyewe tunaweza kunufaika zaidi kuliko kudanganywa kwa misaada toka nchi za nje ambayo ni sawa na mtu kupewa perememde wewe ukaibiwa kipande cha almasi au vito vingine vyenye thamani na wewe ukaridhika na kuona ndiye uliyefaidi kuliko aliyefaidi kikweli.
Chama cha kisiasa sahihi na kinachostahili kuwepo katika karne ya 21 nchini Tanzania ni kile kitakachoweza kufanya mikutano yake mikubwa na midogo, kwa siku kama sio wiki kadhaa, katika kijiji chochote, mkoa wowote Tanzania kwani mikoa na vijiji hivyo vitakuwa na serikali na utawala bora unaoweza kukimu na kuruzuku mambo hayo kutokana na kuwezeshwa na chama husika na wafuasi wake na watu wengine wanaozingatia misaada kufika kule inakotakiwa na sio vinginevyo..
Haijawahi kutokea katika nchi yoyote ile duniani kwa mabadiliko makubwa ya kisiasa, kiuchumi na kijamii kufanyika kirahisi na bila kuwa na upinzani mkali, mkubwa na wa kutisha toka kwa wattu waoga, mbumbu, wasiojua kinachoendelea, wanaonufaika na mfumo wa hali iliyopo au wale wanaotumiwa na wanaonufaika kuwalinda wao na mali zao.
Ninasema vyama vya siasa Tanzania vimepitwa na wakati kwa sababu kile kilichozoea ukiritimba wa mfumo wa chama kimoja kinajiendesha kama wito na kazi yake kuu ni kupambana na wale wanaotaka kife; wakati wale wa iwezekanayo kuwa serikali mbadala na katika mfumo ambao si tofauti sana na wa chama kimoja katika mambo mengi, wanajiendesha kama vile kazi yao kubwa ni kuja kuingia madarakani kwa udi na uvumba. Hakuna kati yao ambaye anatoa uzito stahilifu kwa matatizo na changamoto za wananchi. Na kwa maana hii sio tu ninaona vimepitwa na wakati bali ninadhani vyama vyote havistahili hata kuwepo na nchi imekosa tu watu wanaoweza kuthubutu kuvifagia pembeni hata kabla ya uchaguzi mkuu ujao.
Mabadiliko ambayo Tanzania inastahili kuyafanya hivi sasa hayana tofauti kwa namna yoyote ile na mabadiliko mengine kama hayo yanayotokea kwingine duniani na yaliyokwishatokea pengine na katika karne nyingine huko nyuma yetu.
Tofauti tu iliyopo hivi sasa ni kuwa sisi kama watu mmoja mmoja na kitaifa hatujajipanga ipasavyo kuweza kuhakikisha kuwa mabadiliko hayo yanatokea kwa faida na manufaa yetu na sio kwa ujibari, ujivuni, kisirani na hasara kwa upande wetu.
Na katika hili kiongozi mkuu wa kujipanga kuyakabili mabadiliko anatakiwa awe ni chama cha kisiasa cnenye viongozi wanaojua watu wanataka kuelekea wapi, nchi inaelekea wapi, duniani inaelekea wapi, nani wanastahili kuwa rafiki zetu na nani hatustahili kuwaamini, kuwathamini na kuwaingiza katika siri na mambo yetu mengine.
Ni chama kinachostahili kuwa na mipango, mikakati, sera, muundo, mfumo, taratibu na kanuni za utekelezaji zinazokipa chama ukuu na nguvu juu ya mwanachama mmoja mmoja au kundi la wanachama fulani ndani ya chama husika katika mustakabali wa kujenga umoja wa chama lakini ndani ya mfumo wa demokrasia hai na inayofanya kazi. Ugonjwa wa 'ndivyotunavyofikiri' ukiachiwa kutambaa kwenye mwili-siasa wa jamii hivi leo ni dhahiri maradhi makubwa zaidi yatajitokeza na kupona kwa mgonjwa kutahitaji manabii na miujiza.
Ni chama ambacho kina 'visheni' na 'misheni' bayana ambazo wanaokiongoza hata wakikurupushwa usingizini wanavikariri bila kukosea hata neno moja.
Ni chama kinachotakiwa kuwa na mizizi yake vijijini zaidi kwa kukivewezesha vijiji na wanavijiji na sio mjini kwenye watu wachache na walioelimika vya kutosha. Ni chama ambacho ofisi zake vijijini vitakuwa ni vituo muhimu katika kazi zake mbalimbali na ofisi ambazo zina nafasi kwa ofisi za viongozi wa wilaya, mkoa na kitaifa na ukumbi wa mkutano ambao vikao vikubwa kwa vidogo vya chama vinaweza kufanyika huko bila wasiwasi na uwepo wa sehemu kama hiyo kuwa ni hamira au chachu ya maendeleo ya kijiji na wanakijiji husika.
Ni kawaida pia kinachopingwa, kupinga na kupambana na kile kinachokipinga. Lakini kwa jambo lolote ambalo wakati wake umefika ni muhali na kazi bure kulipinga. Ima-fa-ima lazima mabadiliko yanayopaswa kufanyika yatafanyika tu.
Ili kutopotezeana muda ni vyema kufunguana macho na kuhamasisha jamii kufagia yale yote yenye kunukia uzee au ukongwe usio na faida na ambayo yanaweza kusababisha kuvunjika kwa amani na umoja katika nchi hii eti tu kwa kuwa ukongwe huo unakataa mabadiliko yasitokee.
Hali ilivyo sasa ni kwamba wanasiasa waliopo wamezoea kutawala kwa kutumia mabavu na maguvu; udikteta na ukiritimba katika maamuzi na uendeshaji vyama; kusukumiza kwenye makoo ya raia zao katiba na sheria zisizokubalika; kupora mamlaka na madaraka ya wananchi kinyume na katiba; kutumia njia za haramu kupata mapato yao na ya chama; kutumia vyombo vya dola kwa faida na maslahi yake; uzaini na uongo; kununua na kuwatumia watu; kugawa na kutawala; kulea ukabila wa kichama kwa maana ya kuwabeba tu wanachama wa chama tawala kuwa viongozi na kuwaacha wasio wanachama bila kazi wala changamoto za maana katika kuendeleza wilaya au mkoa au taifa;
uroho, choyo, inda na ulafi wa hali ya juu kutaka kutawala hata pale chama husika kisipokuwa na sapoti ya kutosha; kutumia vyombo vya usalama vya taifa kwa matumizi binafsi na sio kwa maslahi ya kitaifa; kutumia vyombo vya habari kukwamisha uwazi na kudanganya badala ya kusema ukweli; Viongozi wasio na mwelekeo wa kuinufaisha nchi hii na watu bali zaidi wao wenyewe na watu wa nje, kutumia makundi ya kijamii kama vile wanawake, vijana, wazee, wazazi, wanavijiji, wanafunzi, walimu, wafanyakazi na kadhalika kwa manufaa yao na sio ya kitaifa au ya umma; kuwatumia waandishi habari kama askari wa kukodiwa kufanikisha malengo yao; kushirikiana na mafisadi na wevi kufanikisha malengo ya kichama; kuingiza udini na ukabila katika uongozi na uanachama; kutumiwa na viongozi wa nje wa serikali na makampuni kwa maslahi yao na sio ya Watanzania; kushindwa kujenga imani na kujiamini kwamba kwa kutumia rasilimali zetu wenyewe tunaweza kunufaika zaidi kuliko kudanganywa kwa misaada toka nchi za nje ambayo ni sawa na mtu kupewa perememde wewe ukaibiwa kipande cha almasi au vito vingine vyenye thamani.
Mlolongo huo hapo juu ni ushahidi tosha unaonesha ni kwa kiasi gani vyama vya kisiasa nchini Tanzania vimepitwa na wakati na vinahitaji kufa au kupona 'kusasaishwa' ili sio tu viende na wakati bali viweze kutekeleza kwa ukamilifu na usahihi zaidi majukumu yao ya kisiasa, kijamii na kitaifa.
Ili kwenda na wakati vyama vya kisiasa vinastahili pamoja na mambo mengine kuwa na wanasiasa wasioshindwa na wasiotishika katika kutumia nguvu ya hoja, uchanganuzi, uchambuzi na ubunifu katika kuongoza na wanaostawi katika kutofautiana kimawazo, kifikra na kimaono.
Lazima kila chama kihakikisha kuwepo kwa demokrasia na uhuru wa kuchagua au kuchaguliwa ndani na nje ya chama; kuruhusu kuwepo kwa katiba na sheria zilizoandikwa na wanachama au wananchi wenyewe na sio wao kama viongozi au watawala; na pia kutumia njia za halali na zinazokubalika na zisizowaumiza watu wengine kupata mapato yao na ya chama.
Ni wajibu wa chama chochote ndani au nje ya madaraka kuvhiheshimu, kushirikiana na kuvitumia vyombo vya dola kwa faida na maslahi ya umma na si watu wachache; na kujali usawa, haki na ukweli wakati wote.
Kila chama kinastahili kuthamini utu na ubinadamu wa raia wote; kujenga umoja katika tofauti za kiimani na kiitikadi; kukana na kuharamisha ukabila wa aina zote ukiwemo ule ukabila wa kichama, udugu, ujamaa na urafiki katika kazi na majukumu mengine ya kitaifa.
Chama lazima kidhibiti wakati wote uroho, choyo, inda na ulafi miongoni mwa wanachama na viongozi wake; kuwaachia wengine kutawala pale chama kisipokubalika na wakazi husika; na kutotumia vyombo vya usalama wa taifa kwa maslahi, matakwa na haja binafsi ikiwemo kuwachunguza viongozi wastaafu, wanaharakati na wanachama na viongozi wa upinzani.
KIla chama kinawajibika kutotumia vyombo vya habari kudanganya wale wenye uelewa duni wa mambo; kutowaweka waavijiji katika giza la kuelewa na kukubali kuwa demokrasia na vyama vingi ni jambo lenye manufaa kwetu kama nchi na watu; na pia kutowatumia waandishi habari kama askari wa kukodiwa kufanikisha malengo ya chama na viongozi wake.
Chama kinawajibika kutoshirikiana na matajiri na mafisadi katika kupora madini na maliasili za nchi hii; kutowagawa Watanzania katika makundi ya kijamii yanayoweza kuja kuwa hatari kwa taifa baadaye, k.m, vijana, wazee, wanafunzi, wanawake, wazazi wa chama fulani n.k.
Chama kiwe makini na kutoingiza udini na ukabila katika uongozi na uanachama; kutotumiwa na viongozi wa nje wa serikali na makampuni kwa maslahi yao na sio ya Watanzania; kufanikisha kujenga imani na kujiamini miongoni mwa Watanzania kwamba kwa kutumia watu wetu wenyewe, wazungu wasio na ajira makwao, rasilimali zetu wenyewe tunaweza kunufaika zaidi kuliko kudanganywa kwa misaada toka nchi za nje ambayo ni sawa na mtu kupewa perememde wewe ukaibiwa kipande cha almasi au vito vingine vyenye thamani na wewe ukaridhika na kuona ndiye uliyefaidi kuliko aliyefaidi kikweli.
Chama cha kisiasa sahihi na kinachostahili kuwepo katika karne ya 21 nchini Tanzania ni kile kitakachoweza kufanya mikutano yake mikubwa na midogo, kwa siku kama sio wiki kadhaa, katika kijiji chochote, mkoa wowote Tanzania kwani mikoa na vijiji hivyo vitakuwa na serikali na utawala bora unaoweza kukimu na kuruzuku mambo hayo kutokana na kuwezeshwa na chama husika na wafuasi wake na watu wengine wanaozingatia misaada kufika kule inakotakiwa na sio vinginevyo..
Vyama vya kisiasa Tanzania vimepitwa na wakati ? Sehemu- II
Ili 'kuvisasaisha' vyama vya kisiasa Tanzania kuna mambo kama 15 hivi yanayostahili kufanyika. Mambo hayo, yakiwemo hayo machache yaliyogusiwa hapo juu ni pamoja na mabadiliko ya miundo; mifumo kazi; uwakilishi mikoani na matawini; kuwa na wanachama hai; kuwa na vyanzo halali vya mapato; elimu isiyokoma kwa vingozi na wanachama; matumizi ya Teknohama; kutumia sayansi ya logistiki; kuwa na mipango na mikakati ya kisasa; kuwa na mbinu za kunufaika na kutohasirika na mahusiano ya kimataifa na utandawazi; kubuni njia bora za kupata viongozi; mafunzo ya menejimenti, uchumi na maarifa muhimu kwa viongozi; namna mpya za kukabiliana na matatizo na changamoto za wafuasi na wananchi kwa ujumla; na jinsi ya kuwa mwendelezaji, mwekezaji na mshiriki katika kuzitumia fursa za kimaendeleo za kiuchumi na kijamii kuanzia ngazi ya chini ya tawi hadi ya juu kitaifa kwa faida ya nchi nzima na watu wake.
( Makala haya yanauzwa; wasiliana nasi kupitia SMS : +255714265218 wakati wowote na uapata majibu chini ya saa 24.).......
( Makala haya yanauzwa; wasiliana nasi kupitia SMS : +255714265218 wakati wowote na uapata majibu chini ya saa 24.).......
Sunday, November 6, 2011
Tukubali ushoga au tuachane na nchi za Magharibi ?
ZIPO habari kwamba serikali ya Uingereza iko mbioni kuandaa utaratibu ambao nchi zinazokataa 'ushoga' , kwa maana ya mwanamme kujigeuza mwanamke na kuwa na haki ya kuolewa na kuwekwa ndani kama mke, zitakuwa zikinyimwa fedha za jamala ambazo kwa Waafrika walio wengi sio msaada ila ni sawa na kurudisha kile ambacho Waingereza na ndugu zao walikwiba, wanakwiba na wanaendelea kukwiba toka kwa Watanzania na Waafrika wengine kupitia ukoloni, ukoloni mambo leo na unyonyaji mkuu wa kibiashara na kiuchumi kimataifa.
Mama wa demokrasia duniani, Uingereza, anataka kwa mabavu kupandikiza ushoga katika nchi za Kiafrika ikiwemo Tanzania kwa kuwazaini Waafrika kwa pipi na shanga kama ilivyokuwa zamani wakati makampuni yake hayachoti tu dhahabu na madini yetu mengine bali pia hata fedha zetu kidogo zilizo katika hazina yetu.
Uingereza ndio nchi iliyoitawala Tanganyika tokea ilipomshinda Mjerumani ikisaidiwa na rafiki zake mwaka 1918-1961 bila kufikia hata nusu ya mafaniko yaliyofanywa na Mjerumani katika miaka yake 30 hivi ya kuitawala Tanganyika. Lakini ndiyo iliyofanikisha kujenga unyonyaji wa hali ya juu wa nchi hii, hadi hii leo ikiwmo kasumba ya viongozi na matajiri wetu kuwapeleka watoto wao kwenda kusomeshwa Uingereza.
Hili hata hivi linatufungua macho Watanzania kwa kutambua kwamba serikali ya Uingereza na Jumuiya ya Madola ni kama vile zinaamini kwamba zimeziweka mfukoni nchi maskini za Kiafrika na kwamba zinaweza kutumia udikteta kufosi kwenye makoo yao chochote kile wanachokitaka wao kwa kuwa ni matajiri na watu wa nchi zetu kwa kuwa maskini wakakubali kirahisi tu.
Hili huwa linawezekana kwa sababu Uingereza na Marekani huwa linawatumia watu waliosoma au kufanya kazi kwao kuja 'kuunyakua' uongozi wa nchi sio kwa sababu nyingine ila kuendeleza maslahi ya Uingereza na Marekani katika nchi husika. Katika wimbi la demokrasia katika nchi zetu hivi sasa tuwe macho sana na viongozi wa kupandikizwa kwa sababu ya nguvu ya fedha. Watu hao kwa kawaida hutumwa na mabepari wa dunia ambao ni kama asilimia 1 tu ya watu duniani kuja kukwiba utajiri wenu kwa kuunda genge la asilimia 0.005 ya mabepari na wanasiasa matapeli ndani ya nchi husika.
Kwa wasiojua dunia ya ubepari tuliyoikaribisha Tanzania ni mfumo ambao unaendeshwa na asilimia 1 tu ya matajiri duniani lakini ulio na sauti na nguvu sio tu juu ya serikali zao bali pia serikali za nchi zinazoendelea ambazo huzitegemea nchi zao. Asilimia hii moja ndiyo inayoipa nguvu asilimia nyingine kama 15-20 za mabepari wa kati wanaokuja kuwekeza katika nchi zetu na kuwanu nua viongozi na matajiri wachache nchini (labda asilimia 2-3), ili kudhulumu asilimia 97-98 ya raia wenzao kwa heri na shari.
Katika hili, mimi sina tatizo hata kidogo kuona wanawake, wazee, vijana, wafanyakazi, wakulima na makundi mengine katika jamii yakifanya uamuzi ya kuandamana na kuwapasha Waingereza na Wamarekani na wenzao kama wao kwamba hatutaki na hatukubali ushoga katika urithi, desturi, utamdauni na mila zetu za Kiafrika hapa Tanzania na kwingineko Afrika.
Ushoga kwa wale wanaoamini katika Quran Tukufu na Biblia ndiyo mambo yaliyosambaratisha nchi za Sodom na Gomorrah. Wakati kuna dalili za Marekani na nchi za Ulaya kuwa katika masahibu ya kila aina, zipo hisia kwamba Waingereza wanachotaka kukifanya ni sawa na mtu anayezama kutaka kufa na wale wanaoweza kuwasaidia na wanaotaka kumuokoa.
Ni kichekesho kwa Uingereza kuwa na msimamo kama huu katika karne ya 22, kama vile bado tupo kwenye karne za 19 au 20.
Inaonekana kama vile Uingereza na nchi nyingine tajiri bado zinaamini kwamba nchi za Kiafrika ni nchi zinazoongozwa na watu ambao uroho na tamaa yao ya misaada vinaweza kuwafanya wakubali lolote lile hata likiwa baya kwa mila, desturi, imani, utamaduni na utu wa watu wao.
Hivi leo uchumi wa Ulaya na Marekani upo kwenye misukosuko sio kwa sababu nyingine bali kwa sababu ya uchumi kukosa haya na aibu au kile kinachoitwa, 'economics without ethics', uchumi bila maadili. Na misaada toka nchi hizo nazo sasa inataka kugeuzwa kuwa ni 'aid without ethics' au misaada bila maadili. Vitu hivi tusivikubali. Na huu ni wakati wa kuwashauri Wazungu kuanza kitu kitakachoitwa uchumi na misaada yenye maadili kama masomo katika shule zao za viongozi na hasa wale wa kimataifa. (Ethiconomics na aideconomics) ili watuelewe na kutufahamu zaidi. Umaskini hauimanishi maskini kukubali kuuza roho, utu na imani yake kwa ajili ya kupewa misaada.
Lakini ni ajabu pia kwa sababu hivi sasa nchi za BRIC-Brazili, Russia, India, Uchina na bila kusahau nchi za Kiarabu, zile zilizokuwa katika ile iliyokuwa ikiitwa Urussi ya zamani, Malaysia, Indonesia, Korea Kusini, Vietnam, Japani na zile za Scandinavia nazo zinatuhitaji zaidi kuliko wao wanavyotuhitaji.
Ili kuwafunza jamaa hawa ningelishauri nchi za Kiafrika kama zilikuwa zikiwapa fursa 8 kati ya 10 Waingereza na wamarekani nchini mwao, sasa zigeuze kibao na kuyapa mataifa haya mapya na yanayokuwa kwa kasi zaidi asilimia 80 ya biashara, uwekezaji na ushirikiano kati yao na kuwabakizia wakongwe Uingereza na Marekani asilimia 20 tu, ili vitisho vyao viwe kazi bure huko tunakokwenda.
Mambo yetu Waafrika kwa kiasi kikubwa yameharibika kutokana na ukaribu na kukubali bila kujiuliza tamaduni za nje, hususan, za Kiingereza na Kimarekani. Ni dhahiri kwamba tungelikuwa tunaujali utamaduni wetu wenyewe na tukashirikiana zaidi na zaidi na nchi tofauti na hizi mbili, hivi leo labda hadithi ya Afrika isngelikuwa hii iliyopo hivi sasa.
Ni nchi za Magharibi na hususan Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Italia na Marekani ndizo zilizochangia na zinazoendelea kuchangia kudhoofisha utu, utamaduni, imani na udugu wetu kwa sababu wanazozijua vizuri kuliko sisi wenyewe. Kutokana na umaskini wetu tumeendelea kuwaganda huku wanatunyonga taratibu.
Huu ni wakati muafaka kwa viongozi wa dini na wafuasi wao nao kuja juu kiddedea na kuwaonyesha mabwana na mabibi zetu wa zamani kwamba Tanzania ya leo sio ya jana na sio nchi ya kuichezea tena!
Viongozi wa dini watumie fursa hii kuzungumza moja kwa moja na walipa kodi wa Uingereza wakiwemo Wakiristo, Waislamu na Wayahudi kuwaomba washinikize serikali ya Uingereza kuachana na wazo la kuinyima Tanzania msaada kwa sababu Tanzania haitakubali ushoga achilia mbali watu wa jinsia moja kufunga na kufungishwa ndoa.
Wakati huohuo, vyama vya siasa nchini hapa na vile vya Uingereza vianzishe vuguvugu la kudai demokrasia katika utoaji misaada na kuheshimiwa kwa haki za nchi maskini katika kulinda utu wa watu wake na mila na utamaduni wao.
Enzi za Uingereza na Marekani kutoa masharti ya kisenge na kiudhalimu kwa Waafrika ninaamini zimepita. Hivi sasa Afrika ina nafasi ya kuchagua na kukataa masharti ya kijinga na yanyochimbua mizizi na kuusambaratisha mashina yake ya utu na utamaduni wake bila sababu ya msingi. Kufuatia ujibari, jeuri na kiburi cha Marekani na Wayahudi, ingekuwa jambo zuri kama nchi za BRIC na marafiki wengine tajiri wa Afrika, zingeingilia kati na kuliziba pengo la bajeti ya UNESCO, kama Marekani itajitoa kuifadhili UNESCO eti kwa sababu Palestina imekubalika kama mwananchi kamili.
Kama mataifa haya makubwa yanaamini kweli katika demokrasia hayawezi kuwalazimisha viongozi wetu kufanya maamuzi kwa niaba yetu. Maana kufanya hivyo ni kuwafunza udikteta viongozi wetu.
Isitoshe baadhi yetu katiba zetu tayari hazikubali ushoga. Je, kwa masharti hayo ya Waingereza hawaoni moja kwa moja kwamba sio tu wanataka kuingilia sheria na katiba yetu, bali pia wanaonyesha dharau kwa serikali na watu wetu ya hali ya juu kabisa.
Wanachostahili kufanya mabwana hawa ni kuwezesha nchi zetu kuwapa fursa wananchi wao kupiga kura ya kukubali au kupinga kuingizwa au kulazimishwa kuufanya halali ushoga nchini mwao.
Kwa jinsi serikali yetu inavyojikuta mchafukoge katika masuala kama ya mkorogo katika suala la huduama za umeme, maji, afya na tiba, ustawi wa jamii na usafi; migodi na madini; ufisadi, EPA na wenzake; mawakala wanavyotumbua na kadhalika na tunavyoambiwa kuwa wanaCCM wenyewe hawaoni mtu wa kupambana na ufisadi ndani ya chama hicho hatujui ni kwa kiasi gani tunaweza kuwa na viongozi watakaoendelea kuonyesha ubabe na ufidhuli kwa wale wanaotutaka tuwe mashoga na wasenge katika dunia hii ieleekeayo kwenye maangamizi ya Sodom na Gomorrah.
Mama wa demokrasia duniani, Uingereza, anataka kwa mabavu kupandikiza ushoga katika nchi za Kiafrika ikiwemo Tanzania kwa kuwazaini Waafrika kwa pipi na shanga kama ilivyokuwa zamani wakati makampuni yake hayachoti tu dhahabu na madini yetu mengine bali pia hata fedha zetu kidogo zilizo katika hazina yetu.
Uingereza ndio nchi iliyoitawala Tanganyika tokea ilipomshinda Mjerumani ikisaidiwa na rafiki zake mwaka 1918-1961 bila kufikia hata nusu ya mafaniko yaliyofanywa na Mjerumani katika miaka yake 30 hivi ya kuitawala Tanganyika. Lakini ndiyo iliyofanikisha kujenga unyonyaji wa hali ya juu wa nchi hii, hadi hii leo ikiwmo kasumba ya viongozi na matajiri wetu kuwapeleka watoto wao kwenda kusomeshwa Uingereza.
Hili hata hivi linatufungua macho Watanzania kwa kutambua kwamba serikali ya Uingereza na Jumuiya ya Madola ni kama vile zinaamini kwamba zimeziweka mfukoni nchi maskini za Kiafrika na kwamba zinaweza kutumia udikteta kufosi kwenye makoo yao chochote kile wanachokitaka wao kwa kuwa ni matajiri na watu wa nchi zetu kwa kuwa maskini wakakubali kirahisi tu.
Hili huwa linawezekana kwa sababu Uingereza na Marekani huwa linawatumia watu waliosoma au kufanya kazi kwao kuja 'kuunyakua' uongozi wa nchi sio kwa sababu nyingine ila kuendeleza maslahi ya Uingereza na Marekani katika nchi husika. Katika wimbi la demokrasia katika nchi zetu hivi sasa tuwe macho sana na viongozi wa kupandikizwa kwa sababu ya nguvu ya fedha. Watu hao kwa kawaida hutumwa na mabepari wa dunia ambao ni kama asilimia 1 tu ya watu duniani kuja kukwiba utajiri wenu kwa kuunda genge la asilimia 0.005 ya mabepari na wanasiasa matapeli ndani ya nchi husika.
Kwa wasiojua dunia ya ubepari tuliyoikaribisha Tanzania ni mfumo ambao unaendeshwa na asilimia 1 tu ya matajiri duniani lakini ulio na sauti na nguvu sio tu juu ya serikali zao bali pia serikali za nchi zinazoendelea ambazo huzitegemea nchi zao. Asilimia hii moja ndiyo inayoipa nguvu asilimia nyingine kama 15-20 za mabepari wa kati wanaokuja kuwekeza katika nchi zetu na kuwanu nua viongozi na matajiri wachache nchini (labda asilimia 2-3), ili kudhulumu asilimia 97-98 ya raia wenzao kwa heri na shari.
Katika hili, mimi sina tatizo hata kidogo kuona wanawake, wazee, vijana, wafanyakazi, wakulima na makundi mengine katika jamii yakifanya uamuzi ya kuandamana na kuwapasha Waingereza na Wamarekani na wenzao kama wao kwamba hatutaki na hatukubali ushoga katika urithi, desturi, utamdauni na mila zetu za Kiafrika hapa Tanzania na kwingineko Afrika.
Ushoga kwa wale wanaoamini katika Quran Tukufu na Biblia ndiyo mambo yaliyosambaratisha nchi za Sodom na Gomorrah. Wakati kuna dalili za Marekani na nchi za Ulaya kuwa katika masahibu ya kila aina, zipo hisia kwamba Waingereza wanachotaka kukifanya ni sawa na mtu anayezama kutaka kufa na wale wanaoweza kuwasaidia na wanaotaka kumuokoa.
Ni kichekesho kwa Uingereza kuwa na msimamo kama huu katika karne ya 22, kama vile bado tupo kwenye karne za 19 au 20.
Inaonekana kama vile Uingereza na nchi nyingine tajiri bado zinaamini kwamba nchi za Kiafrika ni nchi zinazoongozwa na watu ambao uroho na tamaa yao ya misaada vinaweza kuwafanya wakubali lolote lile hata likiwa baya kwa mila, desturi, imani, utamaduni na utu wa watu wao.
Hivi leo uchumi wa Ulaya na Marekani upo kwenye misukosuko sio kwa sababu nyingine bali kwa sababu ya uchumi kukosa haya na aibu au kile kinachoitwa, 'economics without ethics', uchumi bila maadili. Na misaada toka nchi hizo nazo sasa inataka kugeuzwa kuwa ni 'aid without ethics' au misaada bila maadili. Vitu hivi tusivikubali. Na huu ni wakati wa kuwashauri Wazungu kuanza kitu kitakachoitwa uchumi na misaada yenye maadili kama masomo katika shule zao za viongozi na hasa wale wa kimataifa. (Ethiconomics na aideconomics) ili watuelewe na kutufahamu zaidi. Umaskini hauimanishi maskini kukubali kuuza roho, utu na imani yake kwa ajili ya kupewa misaada.
Lakini ni ajabu pia kwa sababu hivi sasa nchi za BRIC-Brazili, Russia, India, Uchina na bila kusahau nchi za Kiarabu, zile zilizokuwa katika ile iliyokuwa ikiitwa Urussi ya zamani, Malaysia, Indonesia, Korea Kusini, Vietnam, Japani na zile za Scandinavia nazo zinatuhitaji zaidi kuliko wao wanavyotuhitaji.
Ili kuwafunza jamaa hawa ningelishauri nchi za Kiafrika kama zilikuwa zikiwapa fursa 8 kati ya 10 Waingereza na wamarekani nchini mwao, sasa zigeuze kibao na kuyapa mataifa haya mapya na yanayokuwa kwa kasi zaidi asilimia 80 ya biashara, uwekezaji na ushirikiano kati yao na kuwabakizia wakongwe Uingereza na Marekani asilimia 20 tu, ili vitisho vyao viwe kazi bure huko tunakokwenda.
Mambo yetu Waafrika kwa kiasi kikubwa yameharibika kutokana na ukaribu na kukubali bila kujiuliza tamaduni za nje, hususan, za Kiingereza na Kimarekani. Ni dhahiri kwamba tungelikuwa tunaujali utamaduni wetu wenyewe na tukashirikiana zaidi na zaidi na nchi tofauti na hizi mbili, hivi leo labda hadithi ya Afrika isngelikuwa hii iliyopo hivi sasa.
Ni nchi za Magharibi na hususan Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Italia na Marekani ndizo zilizochangia na zinazoendelea kuchangia kudhoofisha utu, utamaduni, imani na udugu wetu kwa sababu wanazozijua vizuri kuliko sisi wenyewe. Kutokana na umaskini wetu tumeendelea kuwaganda huku wanatunyonga taratibu.
Huu ni wakati muafaka kwa viongozi wa dini na wafuasi wao nao kuja juu kiddedea na kuwaonyesha mabwana na mabibi zetu wa zamani kwamba Tanzania ya leo sio ya jana na sio nchi ya kuichezea tena!
Viongozi wa dini watumie fursa hii kuzungumza moja kwa moja na walipa kodi wa Uingereza wakiwemo Wakiristo, Waislamu na Wayahudi kuwaomba washinikize serikali ya Uingereza kuachana na wazo la kuinyima Tanzania msaada kwa sababu Tanzania haitakubali ushoga achilia mbali watu wa jinsia moja kufunga na kufungishwa ndoa.
Wakati huohuo, vyama vya siasa nchini hapa na vile vya Uingereza vianzishe vuguvugu la kudai demokrasia katika utoaji misaada na kuheshimiwa kwa haki za nchi maskini katika kulinda utu wa watu wake na mila na utamaduni wao.
Enzi za Uingereza na Marekani kutoa masharti ya kisenge na kiudhalimu kwa Waafrika ninaamini zimepita. Hivi sasa Afrika ina nafasi ya kuchagua na kukataa masharti ya kijinga na yanyochimbua mizizi na kuusambaratisha mashina yake ya utu na utamaduni wake bila sababu ya msingi. Kufuatia ujibari, jeuri na kiburi cha Marekani na Wayahudi, ingekuwa jambo zuri kama nchi za BRIC na marafiki wengine tajiri wa Afrika, zingeingilia kati na kuliziba pengo la bajeti ya UNESCO, kama Marekani itajitoa kuifadhili UNESCO eti kwa sababu Palestina imekubalika kama mwananchi kamili.
Kama mataifa haya makubwa yanaamini kweli katika demokrasia hayawezi kuwalazimisha viongozi wetu kufanya maamuzi kwa niaba yetu. Maana kufanya hivyo ni kuwafunza udikteta viongozi wetu.
Isitoshe baadhi yetu katiba zetu tayari hazikubali ushoga. Je, kwa masharti hayo ya Waingereza hawaoni moja kwa moja kwamba sio tu wanataka kuingilia sheria na katiba yetu, bali pia wanaonyesha dharau kwa serikali na watu wetu ya hali ya juu kabisa.
Wanachostahili kufanya mabwana hawa ni kuwezesha nchi zetu kuwapa fursa wananchi wao kupiga kura ya kukubali au kupinga kuingizwa au kulazimishwa kuufanya halali ushoga nchini mwao.
Kwa jinsi serikali yetu inavyojikuta mchafukoge katika masuala kama ya mkorogo katika suala la huduama za umeme, maji, afya na tiba, ustawi wa jamii na usafi; migodi na madini; ufisadi, EPA na wenzake; mawakala wanavyotumbua na kadhalika na tunavyoambiwa kuwa wanaCCM wenyewe hawaoni mtu wa kupambana na ufisadi ndani ya chama hicho hatujui ni kwa kiasi gani tunaweza kuwa na viongozi watakaoendelea kuonyesha ubabe na ufidhuli kwa wale wanaotutaka tuwe mashoga na wasenge katika dunia hii ieleekeayo kwenye maangamizi ya Sodom na Gomorrah.
Subscribe to:
Posts (Atom)