Naishangaa dunia, kuja kuumwa mwiibiwa,
Mifuko kanipekua, na mbwa kasakazia,
Mwizi ananiibia, ataka nimalizia?
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Tukio lilipotokea, wala usingedhania,
Jizi kunishambulia, na mbwawe kunivamia,
Ah, jamani ninalia, haki inshakupotea,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Shilingi kazichukua, maumivu kunachia,
Simu nayo kaizoa, na yangu dhahabu saa,
Kila nikifikiria, nazidi kuchanganyikiwa,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Mtu hakujatokea, mie kunisadia,
Kufurukuta haikua, mbwa kuning'atua,
Amtii na kumsikia, chakula anayempatia,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Hii ndiyo yetu dunia, na hizi zake hatua,
Haki viumbe wajua, sasa waweza nunua,
Wenye haki wanagwaya, ndani huja wakatiwa,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Mwivi huru anakua, na kutamba hukutambia,
Hujui utanijua, mpini nashikilia,
Mikono yako nchani, nikivuta hatarini,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Tuesday, November 8, 2011
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment