NI DHAHIRI suala la kuishi au kuhama mabondeni, hususan Jangwani, ni
suala 'lililosiasaishwa' na haiwezekani chama kilichoko madarakani na
serikali kuwahamisha wakazi wa maeneo haya kwa nguvu kama nguvu
inavyotumika sehemu zingine kutokana na kuhitajika kwa mtaji wa kisiasa.
Haiwezekani pia kidira, kisera, kifedha, kiteknolojia na kiuwezo kwa Dar es
salaam ambayo ni pua na mdomo na bahari kuwa na miundo mbinu
itakaloliwezesha jiji litapike maji yote ya mvua yaende baharini kama tu
imeshidwa kutapisha maji taka na ya matumizi ya kawaida kwenda baharini.
Ugumu wa hili umedhirishwa na kauli zinazopingana juu ya kuhama au
kutokuhama mabondeni zinazotolewa na viongozi wa serikali na chama
tawala. Haiwezekani katika muda mfupi na siamini kama suala hilo limo
katika kipaumbele cha serikali. Je, kiuhalisia kinachobakia kushauri ni kitu
gani ? Nitajaribu ingawa ninajua ni mtihani mkubwa kufanya hivyo katika
makala yangu leo. Ila kama kawaida tutarajie amri zisizotekelezeka na ahadi zisizotimizwa.
Kipindi cha pili cha awamu ya nne kilianza kwa bishara njemba katika
angalau za masula ya nyumba na makazi, lakini kadri muda unavyokwenda
imedhihirika kuwa hizo zilikuwa ni nguvu za soda tu.
Biashara hizo zilitokana kwanza na kuteuliwa kwa mwanamke aliyeswahi
kushika wadhifa wa juu katika shilrika la masula ya nyumba na makazi na
kauli zake za mwanzo ambazo zilionekana kama angelikuwa na uhuru wa
kufanya yale anayofikiria kichwani kwake leo angalau tungelianza angalau
kuona ishara za kuwa na mipngo miji katika nchi ambayo kwa mapana na
marefu na kwa ujumla yake ilikwishazika kabisa suala la mipango miji na
ujenzi uaoangalia na kutahadhari na yanayoweza kutokea kesho na kesho
kutwa.
Jambo moja linalochangia udhaifu katika utawala na menejimenti yetu ya
nyumba na makazi ni sheria za kubembelezana na kuvumiliana. Na siku hizi
umezuka mtindo kuwa pakijengwa kijiwe cha chama tawala mahala fulani,
basi mahala hapo panahesabika kuwa sehemu ambayo hata kama sheria
zimevunjwa, hazikuvunjwa!
Hizi ni siasa za kutafuta kupendwa na umaarufu, huku mtu akijua fika kwa
kuruhusu kinachofanyika kiendelee kufanyika basi mwisho wake ni zahama,
dhiki na vifo kwa wale wanouhurumiwa na kvumililiwa. Ninaamini wakati
umefika kwa nchi yetu kujenga heshima ya kuwa na utawala wa kisheria
ambao haushawishiwi vinginevyo na wanasiasa kwa malengo yao binafsi.
Pamoja na ujenzi wa nyumba mabondeni ipo mifano mingi ya kimaafa
maafa tu inayosubiri cheche moja tu, moto au bomu kulipuka.
Mifano hiyo ni pamoja na vituo vya zima moto na upatikanaji maji kuwa mbali
na maeneo ambayo janga la moto linaweza likazuka.
Manispaa mbalimbali za maji zimeruhusu au kuachia watu kujenga kuta au
vizuizi vya aina mbalimbali ambavyo vinaweza vikachangia si haba ukubwa
wa maafa na hasa yale ya maji na mafuriko.
Tembelea sehemu mbalimbali za jiji la Dar es salaam na utakuta makumi
kama sio mamia ya vituo vya petroli ambavyo vimejenga kando ya masoko
au ndani ya makazi ya watu.
Watalii mbalimbali hivi sasa wanahofia kuja Tanzania kutokana na
kukosekana usalama wa kutosha mabarabarani . Jambo linalosababishwa
na malori, daladala, bajaji, pikipiki, mikokoteni na vyombo vingine vya
uchukuzi kutofuata sheria zilizopo na kukosa uungwana na ustaarabu katika
maingiliano ya watu njiani.
Aidha, kumekuwa na kauli kadhaa za kisheria zisizotekelezwa juu ya hili au
lile, mojawapo likiwa ni amri inayokataza watu kuishi mabondeni toka zama
za Mzee Makamba alipokuwa mkuu wa mkoa wa jijimkoa.
Nchi haiwezi kamwe kujengwa kwa siasa za kujipendekeza, kutaka
kuonekana wema na wazuri na wengine wabaya na unafiki mwingine kama
huo. Ni lazima tufike mahala ambapo sheria zetu zinalinda na kutunza roho
za watu, kisha utamaduni, imani na mali za watu . Mengine ni uzandiki wa
kisiasa ulio na melngo binafsi dhidi ya yale yanayostahili kuwa ya umma.
Ninaamini, wakati tunatoa michango yetu kuhusu katiba yetu mpya itulinde
vipi tokana na wale tunaowapa ukubwa tutahakikisha kuwa ulinzi na
usalama wa roho za watu, utamaduni na mali zao unapewa uzito
unaostahili.
Kama azma yetu basi itakuwa ni hivyo ni dhahiri kubainisha hapa kwamba
huwezi ukalinda na kuthamini maisha ya wananchi wako kama wewe kama
serikali na mkusanyaji mkuu wa kodi na mirabaha unashindwa kuwapatia
wananchi unaowaongoza mahitaji yao ya msingi. Mahitaji hayo ya msingi ni
pmoja na nyumba na makazi bora na salama.
Nyumba kama hitaji la msingi
Kichekesho kwa wazungu na wageni wengi wanaotembelea nchi hii ni pale
wanapokuta kuwa kila Mtanzania ana mradi wa kujenga nyumba. Pengine
hawaelewi umasikini na kudunduliza kwetu na jinsi tunavyozaliana kwa
wingi, lakini bado ukweli unabakia pale pale wengi wanatushangaa
wanapoona badala ya kujenga vitu vya kututajirisha tunajenga vitu vya
kutumasikinisha.
Ukiweka siasa pembeni, nyumba ni hitaji la msingi la kila mwanadamu.
Inasemekana baada ya chakula na maji basi nyumba ni muhimu kuliko kitu
kingine. Kutokana na ukweli huu, serikali iliyokuwa makini haiwezi
kulichukulia suala hili kimzahaha mzaha au kuliona ni mzigo na kulisukuma
ili libebwe na watu wengine. Bila watu kuwa na nyumba bora na salama hata
kama watajishughulisha na mengi mazuri katika uzalishaji na ujenzi wa
nchi, fumba na kufumbua, siku moja vyote vinaweza kuoshwa au kufagiliwa
mbali na maafa ya aina hii au ile.
Serikali inayoona mbali na mbele, kwa hiyo, huwa inachukulia suala la
mipango na mikakati ya nyumba na makazi kama jiwe la msingi la
maendeleo la taifa na watu husika. Inafanya hivyo, kwa kuzingatia kuwa vita
vyote vingine vinavyokabili watu wake vikiwemo vile vya ujinga, njaa, maradhi
na umaskini ni vita vitakavyokuwa rahisi sana kuibuka kidedea kama
washindi wasioshindika.
Katika muktadha huu, hoja yangu hapa ni kwamba tusianze kumwaga
machozi ya mamba huku tukijua fika kwamba siasa zetu za kujipendekeza
zimechangia si haba kuwapotezea Watanzania wenzetu ambao kama sheria
zingelikuwa zinawalinda na rasilimali za nchi zinatumika kuwanufaisha wao
na sio vinginevyo hivi leo wasingelikuwa marehemu.
Ninasema hivyo, kwa kudhihirisha kuwa ulegevu na urojorojo wa seriikali
yetu ambayo kwa kushangaza sana inakuwa na nguvu ya kupambana na
waandamanaji toka vyama vya upinzani au wafuasi wa dini fulani
wanapotaka kuandamana au kuwasekwa ndani na kuwashtaki waandishi wa
habari kwa kutumia sheria za kidhalimu na kikoloni na zilizopitwa na wakati
kwa sababu tu waandishi hao wa habari wameandika kisichowafurahisha
wanasiasa walioko madarakani unachangia si haba nchi hii kuwa na
matatizo ya kila namna, kutokuendelea na kupiga maktaimu wakati watawala
wakidanganywa na takwimu na taarfifa za wapambe wao kwamba mambo ni
saaafii.
Mradi wa kuondokana na makazi ya mabondeni
Mathalani, kama serikali yetu ingelikuwa haifanyi kazi kisanii, basi mara tu
baada ya kutangaza marufuku ya kujenga na kuishi mabondeni
nilichotegemea kuona ni serikali hiyo kujenga nyumba za angalau chumba
kimoja na ukumbi kwa familia husika katika maeneo mengine na kisha
kupitia benki na taasisi nyingine za fedha, misaada na ukopeshaji kurejesha
gharama zake kwa kuwalipisha wananchi masikini kwa kiwango
wanachoweza kulipa hadi deni lao liishe. Je, tunakumbuka mikopo ya miaka
25 hadi 50 ya Benki ya Dunia kwa watanzania miaka ya huko nyumba.
Serikali yetu kwa kutumia utajiri, madini, mali asili zetu na kodi zetu hivi
inashindwa kufanya jambo kama hili au haina nafasi na watu wake ambao ni
maskini? Utaratibu huu utaendana hata na matarajio ya katiba ya kiutawala iliyopo na
utaanza kujenga kutoa fursa sawa kiustawi ili kuleta uwiano na usawa wa
kimaendeleo miongoni mwa Watanzania.
Hitaji la nyumba na makazi kama hitaji la msingi likishatoshelezwa, kinachobakia ni kwa wananchi kujiingiza katika ushindani mbalimbali wa kujiendeleza kielimu, kikazi, kibiashara, kihuduma, kisanaa, kimichezo na kadhalika na kuwa bora zaidi nchini na
duniani.
Kwa maneno mengine, safari ya kweli na dhati kuelekea kwenye
maendeleo ya Watanzania inakuwa ndio imeanza na sio vinginevyo.
Nyumba zilizo kwenye maeneo safi, bora na salama zitachangia sio haba
kuwapa mamilioni ya Watanzania utulivu wa akili na kiroho. Ni kitu
kitakachorahisisha miingiliano ya kijamii na kupatikana kwa huduma za
utumaji na upokeaji barua kupitia makasha nyumbani na sio ofisi za posta
mbali na waishipo watu. Hali kadhalika, kuishi kwenye makazi salama, mandhari nzuri
na yanayopendeza vitawapa Watanzania moyo wa amani, utu, huruma na mapenzi zaidi.
Na kubwa zaidi litawapa Watanzania nafasi kubwa zaidi ya kujiheshimu na
kujithamini na sio kujiona wao sio lolote sio chochote.
Nyumba bora na salama zitawapa watoto wa kimaskini nafasi ya kusoma
katika mazingira bora zaidi na kufanya vizuri zaidi katika shule na vyuo.
Nyumba bora na salama na zenye nafasi zitawapa watoto wa makini fursa
ya kuwa watundu, wenye kujaribu na wazua ujasiriamali wa kila aina siku
zote daima.
Nyumba bora, salama katika miji ambayo utawala wa kisheria sio tu
unasemekana kuwepo bali kufuatwa kwa herufi na silabi na zenye
kuhudumiwa ipasavyo na huduma zote muhimu za kijaami unaweza
kuifanya Tanzania fumba na kufumbua kuwa chaguo la watalii duniani na
mapato ya utalii peke yake yakatuwezesha kujivua nguo za mitumba ya
umaskini na kuvaa nguo mpya za raia wanaoheshimiwa, kujiheshimu na
kutoa mchango wao muhimu katika maendeleo ya dunia yao na wakati wao.
Kubwa zaidi ni lile la kwamba kuanzia hapo hayo hapo juu
yatakapozingatiwa watu wetu sio tu itakuwa ni rahisi kupata huduma zote
muhimu binadamu anazohitaji, bali kubwa zaidi maisha na mali zao
zitakuwa salama wakati wote.
Thursday, December 22, 2011
Friday, December 16, 2011
CUF na hatima ya upinzani Tanzania...
WATANZANIA mnamo mwaka 1990 waliupokea mfumo wa vyama vingi kwa matumaini makubwa ya mageuzi na mabadiliko chanya katika mfumo wao wa kisiasa, kijamii na kiuchumi. Awali CUF kilihofiwa kuwa chama chenye udini, akheri, ni dhahiri inaweza kuwa au isiwe hivyo, ila kilicho wazi ni kuwa CUF baada ya muafaka ni chama cha Kizanzibari zaidi na sio cha Kitanzania, achilia mbali kuwa cha Kitanganyika.
Watu wengi waliamini mfumo wa vyama vingi utaleta ushindani wa kweli katika siasa, uchumi, teknolojia, utamaduni na rasilimali ziendazo kwa wanajamii ili kila mtu na kila jamii ipate kilicho bora kabisa na sio kitu hafifu, dhaifu na vilivyochakachuliwa.
Hata hivyo, ushindani katika sekta nyingine ulitegemea sana kuwepo na mafanikio ya ushindani wa dhati na wa kweli katika siasa. Ushindani huo katika siasa hadi hivi wa leo haujafika, haujaonekana na kwa siasa zilizopo ndani na nje ya chama tawala haionekani kama utapatikana kwenye awamu hii.
La kusikitisha ni kuwa siasa za mfumo wa vyama vingi Tanzania zimeiga neno kwa neno siasa za Kimarekani zinazotawaliwa na wenye fedha, na wasio na fedha kuwa wasindikizaji kama sio wanunuliwaji. Na kinachopandwa hakiashirii mema kwa nchi hii na watu wake hapo baadaye.
Kubwa tunalojifunza hapa ni kwamba kutokana na kukwamishwa kuwepo kwa ushindani wa kweli wa kisiasa ndani na nje ya bunge, viongozi wetu wanawapotezea wananchi muda na nafasi nyingi na nyinginezo za kuondokana na umaskini wao kwa kutumia fursa na changamoto ambazo aghalabu huzaliwa tu katika mfumo wenye ushindani wa kweli kisiasa. Hili linapaswa lionekane na lieleweke na wote, waliomo kwenye upinzani na wanaoongoza chama tawala hivi sasa ili maamuzi yanayofaa yafanywe kwa faida ya nchi na watu wake.
Ilitegemewa kuwa vyama vya upinzani vingekuwa vingi, lakini kuna viwili au vitatu vitakavyoungana na kukipa changamoto ya kutosha chama tawala. Kiasi ambacho chama tawala kisingeweza kufanya maamuzi yoyote ya maana kiurahisi bila ushirikiano na vyama vingine na kuwaelimisha na kuwaridhisha wabunge au wawakilishi wake kwenye mazungumzo mbalimbali.
Kinachoonekana leo, hata hivyo, ni kuongezeka vyama vya siasa visivyo na kichwa wala miguu, huku vile vilivyokuwepo vikizidi kudhoofika kwa njia moja au nyingine.
Zipo sababu mbalimbali zinazotolewa kuhusu udhaifu wa upinzani. Baadhi ya viongozi wa vyama tawala wanaamini kwamba vyama hivyo vimeanzishwa kwa shinikizo la IMF na Benki ya dunia, na hili pengine linaathiri mahusiano ya chama tawala na vyama hivyo kwa chama tawala kuona ndicho pekee chenye ridhaa na uhalali kwa wananchi lakini sio vya upinzani.
Aidha, vyama vingi vya upinzani pamoja na sheria ya kuvilazimisha kuwa na wanachama angalau 200 katika angalau mikoa 10 ni vyama vilivyokosa mizizi ya kweli mijini na vijijini na vinaishi kwa kubangaizabangaiza tu. Wakati hili linatokea chama tawala kwa kushika funguo za hazina na kuwa katika nafasi ya kufanya maamuzi kadhaa kwa manufaa yake, hakina dhiki kama hiyo, ila pale kinapoingizwa mkenge kama ilivyotokea kwenye suala la rada.
Kutokana na chama tawala na viongozi wake kuwa na uwezo wa kifedha (ambao hatuna uhakika na chimbuko lake, maana hakionekani kuwa na miradi ya maana ya kukiingizia kipato na wanachama wake wengi sio walipa ada wala watoa michango mikubwa) kimetumia njaa na umaskini wa vyama vya upinzani kwa manufaa yake kwa njia mbalimbali, ambazo hatuna sababu ya kuingilia kwa undani zaidi hapa. Pamoja na hayo kutokana na siasa kuitwa mchezo mchafu tumeshuhudia mambo ambayo yanatia mashaka kuhusu ukweli na uhalali wake katika maeneo mbalimbali ya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kimaendeleo kwa ujumla.
Kisiasa kwa mfano tumeona baadhi ya vyama vikisingizia vingine udini, wakati ndivyo vinavyolea udini kwa mlango wa nyuma; tumeona uoza na ufisadi ukiswafishwa na kuitwa utakatifu; tumeona wabunge wakizomewa na kukashifiwa kwa kuwa na msimamo fulani; tumeona wabunge wakitumiwa kwa manufaa ya chama na serikali na siyo ya wananchi; tumeona watu wakisingiziwa uongo na wengine kujiita na kutaka kuonekana watakatifu na kadhalika; na juu ya yote tumewaona wanafiki na wasioitakia nchi yetu mema wakijifanya wao ndio wenye uchungu mkubwa kabisa na nchi yetu kuliko watu wengine.
CUF na Zanzibar....
Baada ya kukerwa na ugomvi wa ndugu wa Unguja na Pemba, sisi sote tulivuta pumzi na kushukuru Mungu na tukafata wahenga waliyosema: ' Ndugu wakigombana, chukua kisegerema chako uende kulima; na ndugu wanapopatana, chukua kapu lake ukavune!'
Hebu turudi nyuma kidogo, hata hivyo, je, CUF kiliundwa makusudi na mahsusi kwa ajili ya muafaka wa Zanzibar? Au nini kilichotokea?
Pamoja na ukweli kwamba cham hicho kilistahili kuwa na wanachama 200 katika kila mkoa angalau kwa mikoa 10 Tanzania bara na visiwani ni vipi chama hicho kikamezwa kabisa na Wazanzibari? Kiasi kwamba kama chama hicho hakikuhusiswa na Uzanzibari na Upemba kilikuwa kikihusishwa na Uislamu kwa heri au shari ?
Je, katika hali ambayo tunayo leo, yaani, kuwepo sio tu muafaka bali pia serikali ya Umoja wa Kizanzibari, ukweli hauonekani kwamba chama cha CUF hakikuwa chama cha Tanzania bali cha Kizanzibari?
Iweje baada ya viongozi wa Kizanzibari kupewa ubunge na vyeo mbalimbali katika serikali yao ya Umoja wa kitaifa harakati zao za kisiasa kama upinzani unaotarajiwa kuwa imara katika kuikabili CCM bara kudhoofu na kuwa hoi bin taabani?
Katika matukio ya kitaifa na hususan Bungeni, tumeona watunga sheria wa CUF kwa heri au shari wakiunga mkono au kupinga moja kwa moja lolote lile ambalo Chama tawala liliunga mkono au kupinga ?
Na hivi Hazina, Tume ya Uchaguzi na Msajili wa vyama vya siasa wanastahili kulipa CUF na CCM kama chama kimoja au vyama viwili kwa hali kama hii?
Wamasheria wanasemaje kuhusu CUF hapa Tanzania kama ni chama cha Upinzani au chama tawala au chama kilicho katikati ya hayo ?
Na Watanzania waliohadaiwa na wapanda mabasi ya muafaka wakidhani wanapelekwa kwenye upinzani imara na wa kweli wana kila haki ya kushuka na kupanda basi jengine.
Vijana wa chama ambacho kimefikia kuwauza bila wao wenyewe kujua wanauzwa ili viongozi wachache wa chama hicho wapate ukubwa na sio maendeleo ya watu na nchi yao sio laiki yao kukaa kimya labda wakose kiongozi wa kuwafungua macho na kuwaongoza kwenda kule wanakosatahili kuelekea na sio vinginevyo.
Maana ya kuwa na upinzani nchini haiwezi kubadilika. Upinzani unahitajika kama njia muhimu ya kisiasa kwa wanasiasa wa mrengo fulani kupimwa kiuwezo, kufuatiliwa, kudhibitiwa na kutathminiwa kimatendo na kimatokeo kama na wanasiasa wenzao na wananchi kwa ujumla kama wanaweza au hawawezi kazi waliyoiomba.
Huu ni mfumo ambao ukiutumia vibaya unaweza ukairuhusu nchi kutawaliwa na kuendeshwa na chuya na pumba wakati nafaka zimetupwa jalalani. Au kwa upande mwingine mfumo wa vyama vingi ni mfumo unaoweza pia kuchangia sio haba nchi kuwa na viongozi safi, wenye uwezo, wenye nia ya kujenga nchi na watu wao na wenye mitazamo na dira za kimaendeleo zinazohitajika kufikisha nchi na watu wake kule wanakotaka kwenda.
Upinzani hauwezi kustawi kama katika nchi husika bado watu wana wasiwasi kwamba upinzani ni uasi, vita na uhaini. Ni lazima watu na hasa vijijini waliko wananchi wengi wakubali kwamba mfumo wa vyama vingi ni kitu kizuri na anayeutega au kudhoofisha ni adui wa nchi na watu wake. Na kwamba upinzani si ubaya, si uasi na sio vita wala uhaini. Na kwamba vita na uhaini hutokea pale demokrasia inapohujumiwa na wale walioko madarakani kukataa kushindwa na kuwanyima washindi haki yao kwa njia halali au haramu.
Juu ya yote upinzani hauwezi kujengwa na wazee ambao daima wanalilia kupewa nishani ili watambuliwe kwa kile kisichotambulika wala kueleweka. Upinzani wa kweli utajengwa na vijana waliofunguka macho na wanaotambua kwamba nchi hii haiwezi kujengwa kwa kuigeuza shamba la bibi kama sio la nyanya, ila kwa mikoa na wilaya za nchi hii kujiendesha kama makampuni huru yenye visheni na misheni ya kile kinachostahili kuzalishwa, kuundwa au kuhudumiwa kwa ufanifu na ufanisi wa hali ya juu kwa kasi ambayo itatuwezesha kuuaga ulimwengu wa tatu kwa haraka zaidi kuliko tunavyotarajia.
Watu wengi waliamini mfumo wa vyama vingi utaleta ushindani wa kweli katika siasa, uchumi, teknolojia, utamaduni na rasilimali ziendazo kwa wanajamii ili kila mtu na kila jamii ipate kilicho bora kabisa na sio kitu hafifu, dhaifu na vilivyochakachuliwa.
Hata hivyo, ushindani katika sekta nyingine ulitegemea sana kuwepo na mafanikio ya ushindani wa dhati na wa kweli katika siasa. Ushindani huo katika siasa hadi hivi wa leo haujafika, haujaonekana na kwa siasa zilizopo ndani na nje ya chama tawala haionekani kama utapatikana kwenye awamu hii.
La kusikitisha ni kuwa siasa za mfumo wa vyama vingi Tanzania zimeiga neno kwa neno siasa za Kimarekani zinazotawaliwa na wenye fedha, na wasio na fedha kuwa wasindikizaji kama sio wanunuliwaji. Na kinachopandwa hakiashirii mema kwa nchi hii na watu wake hapo baadaye.
Kubwa tunalojifunza hapa ni kwamba kutokana na kukwamishwa kuwepo kwa ushindani wa kweli wa kisiasa ndani na nje ya bunge, viongozi wetu wanawapotezea wananchi muda na nafasi nyingi na nyinginezo za kuondokana na umaskini wao kwa kutumia fursa na changamoto ambazo aghalabu huzaliwa tu katika mfumo wenye ushindani wa kweli kisiasa. Hili linapaswa lionekane na lieleweke na wote, waliomo kwenye upinzani na wanaoongoza chama tawala hivi sasa ili maamuzi yanayofaa yafanywe kwa faida ya nchi na watu wake.
Ilitegemewa kuwa vyama vya upinzani vingekuwa vingi, lakini kuna viwili au vitatu vitakavyoungana na kukipa changamoto ya kutosha chama tawala. Kiasi ambacho chama tawala kisingeweza kufanya maamuzi yoyote ya maana kiurahisi bila ushirikiano na vyama vingine na kuwaelimisha na kuwaridhisha wabunge au wawakilishi wake kwenye mazungumzo mbalimbali.
Kinachoonekana leo, hata hivyo, ni kuongezeka vyama vya siasa visivyo na kichwa wala miguu, huku vile vilivyokuwepo vikizidi kudhoofika kwa njia moja au nyingine.
Zipo sababu mbalimbali zinazotolewa kuhusu udhaifu wa upinzani. Baadhi ya viongozi wa vyama tawala wanaamini kwamba vyama hivyo vimeanzishwa kwa shinikizo la IMF na Benki ya dunia, na hili pengine linaathiri mahusiano ya chama tawala na vyama hivyo kwa chama tawala kuona ndicho pekee chenye ridhaa na uhalali kwa wananchi lakini sio vya upinzani.
Aidha, vyama vingi vya upinzani pamoja na sheria ya kuvilazimisha kuwa na wanachama angalau 200 katika angalau mikoa 10 ni vyama vilivyokosa mizizi ya kweli mijini na vijijini na vinaishi kwa kubangaizabangaiza tu. Wakati hili linatokea chama tawala kwa kushika funguo za hazina na kuwa katika nafasi ya kufanya maamuzi kadhaa kwa manufaa yake, hakina dhiki kama hiyo, ila pale kinapoingizwa mkenge kama ilivyotokea kwenye suala la rada.
Kutokana na chama tawala na viongozi wake kuwa na uwezo wa kifedha (ambao hatuna uhakika na chimbuko lake, maana hakionekani kuwa na miradi ya maana ya kukiingizia kipato na wanachama wake wengi sio walipa ada wala watoa michango mikubwa) kimetumia njaa na umaskini wa vyama vya upinzani kwa manufaa yake kwa njia mbalimbali, ambazo hatuna sababu ya kuingilia kwa undani zaidi hapa. Pamoja na hayo kutokana na siasa kuitwa mchezo mchafu tumeshuhudia mambo ambayo yanatia mashaka kuhusu ukweli na uhalali wake katika maeneo mbalimbali ya kisiasa, kiuchumi, kijamii na kimaendeleo kwa ujumla.
Kisiasa kwa mfano tumeona baadhi ya vyama vikisingizia vingine udini, wakati ndivyo vinavyolea udini kwa mlango wa nyuma; tumeona uoza na ufisadi ukiswafishwa na kuitwa utakatifu; tumeona wabunge wakizomewa na kukashifiwa kwa kuwa na msimamo fulani; tumeona wabunge wakitumiwa kwa manufaa ya chama na serikali na siyo ya wananchi; tumeona watu wakisingiziwa uongo na wengine kujiita na kutaka kuonekana watakatifu na kadhalika; na juu ya yote tumewaona wanafiki na wasioitakia nchi yetu mema wakijifanya wao ndio wenye uchungu mkubwa kabisa na nchi yetu kuliko watu wengine.
CUF na Zanzibar....
Baada ya kukerwa na ugomvi wa ndugu wa Unguja na Pemba, sisi sote tulivuta pumzi na kushukuru Mungu na tukafata wahenga waliyosema: ' Ndugu wakigombana, chukua kisegerema chako uende kulima; na ndugu wanapopatana, chukua kapu lake ukavune!'
Hebu turudi nyuma kidogo, hata hivyo, je, CUF kiliundwa makusudi na mahsusi kwa ajili ya muafaka wa Zanzibar? Au nini kilichotokea?
Pamoja na ukweli kwamba cham hicho kilistahili kuwa na wanachama 200 katika kila mkoa angalau kwa mikoa 10 Tanzania bara na visiwani ni vipi chama hicho kikamezwa kabisa na Wazanzibari? Kiasi kwamba kama chama hicho hakikuhusiswa na Uzanzibari na Upemba kilikuwa kikihusishwa na Uislamu kwa heri au shari ?
Je, katika hali ambayo tunayo leo, yaani, kuwepo sio tu muafaka bali pia serikali ya Umoja wa Kizanzibari, ukweli hauonekani kwamba chama cha CUF hakikuwa chama cha Tanzania bali cha Kizanzibari?
Iweje baada ya viongozi wa Kizanzibari kupewa ubunge na vyeo mbalimbali katika serikali yao ya Umoja wa kitaifa harakati zao za kisiasa kama upinzani unaotarajiwa kuwa imara katika kuikabili CCM bara kudhoofu na kuwa hoi bin taabani?
Katika matukio ya kitaifa na hususan Bungeni, tumeona watunga sheria wa CUF kwa heri au shari wakiunga mkono au kupinga moja kwa moja lolote lile ambalo Chama tawala liliunga mkono au kupinga ?
Na hivi Hazina, Tume ya Uchaguzi na Msajili wa vyama vya siasa wanastahili kulipa CUF na CCM kama chama kimoja au vyama viwili kwa hali kama hii?
Wamasheria wanasemaje kuhusu CUF hapa Tanzania kama ni chama cha Upinzani au chama tawala au chama kilicho katikati ya hayo ?
Na Watanzania waliohadaiwa na wapanda mabasi ya muafaka wakidhani wanapelekwa kwenye upinzani imara na wa kweli wana kila haki ya kushuka na kupanda basi jengine.
Vijana wa chama ambacho kimefikia kuwauza bila wao wenyewe kujua wanauzwa ili viongozi wachache wa chama hicho wapate ukubwa na sio maendeleo ya watu na nchi yao sio laiki yao kukaa kimya labda wakose kiongozi wa kuwafungua macho na kuwaongoza kwenda kule wanakosatahili kuelekea na sio vinginevyo.
Maana ya kuwa na upinzani nchini haiwezi kubadilika. Upinzani unahitajika kama njia muhimu ya kisiasa kwa wanasiasa wa mrengo fulani kupimwa kiuwezo, kufuatiliwa, kudhibitiwa na kutathminiwa kimatendo na kimatokeo kama na wanasiasa wenzao na wananchi kwa ujumla kama wanaweza au hawawezi kazi waliyoiomba.
Huu ni mfumo ambao ukiutumia vibaya unaweza ukairuhusu nchi kutawaliwa na kuendeshwa na chuya na pumba wakati nafaka zimetupwa jalalani. Au kwa upande mwingine mfumo wa vyama vingi ni mfumo unaoweza pia kuchangia sio haba nchi kuwa na viongozi safi, wenye uwezo, wenye nia ya kujenga nchi na watu wao na wenye mitazamo na dira za kimaendeleo zinazohitajika kufikisha nchi na watu wake kule wanakotaka kwenda.
Upinzani hauwezi kustawi kama katika nchi husika bado watu wana wasiwasi kwamba upinzani ni uasi, vita na uhaini. Ni lazima watu na hasa vijijini waliko wananchi wengi wakubali kwamba mfumo wa vyama vingi ni kitu kizuri na anayeutega au kudhoofisha ni adui wa nchi na watu wake. Na kwamba upinzani si ubaya, si uasi na sio vita wala uhaini. Na kwamba vita na uhaini hutokea pale demokrasia inapohujumiwa na wale walioko madarakani kukataa kushindwa na kuwanyima washindi haki yao kwa njia halali au haramu.
Juu ya yote upinzani hauwezi kujengwa na wazee ambao daima wanalilia kupewa nishani ili watambuliwe kwa kile kisichotambulika wala kueleweka. Upinzani wa kweli utajengwa na vijana waliofunguka macho na wanaotambua kwamba nchi hii haiwezi kujengwa kwa kuigeuza shamba la bibi kama sio la nyanya, ila kwa mikoa na wilaya za nchi hii kujiendesha kama makampuni huru yenye visheni na misheni ya kile kinachostahili kuzalishwa, kuundwa au kuhudumiwa kwa ufanifu na ufanisi wa hali ya juu kwa kasi ambayo itatuwezesha kuuaga ulimwengu wa tatu kwa haraka zaidi kuliko tunavyotarajia.
Tusipoangalia demokrasia yetu inaweza kuwa wizi….
SI MTU mwingine ila baba wa ukomunisti, Karl Marx ambaye miaka zaidi ya 120 alitahadharisha kwamba demokrasia kama ilivyokuwa katika nchi za Magharibi ni mfumo wenye udhaifu, mapungufu na kasoro nyingi.
Alionya kwamba demokrasia isipodhibitiwa na wananchi wenyewe ikaachiwa kwa wajanja wachache katika jamii inaweza kugeuka wizi wa mchana kweupe na wa kutisha ambao umehalalishwa na una nguvu za kisheria.
Kiasi ambacho jambo likishaamuliwa huwezi kulipinga kwa kutumia sheria ila kwa njia nyingine.
Alidai wale wanaoitwa wawakilishi wa wananchi wanaweza kuamua kupiga kura ya 'ndiyo' ili kuifagia na kuisafisha hazina au Benki Kuu ya nchi ikawa nyeupe na isibakiwe hata na shilingi moja kwa ajili ya matumizi yao binafsi.
Nina wasiwasi kama huko sio kwa mfumo tulionao leo, wa demokrasia ya chama kimoja iliyojificha ndani ya mfumo wa vyama vingi kama sio tunakokwenda.
Hakuna anayepinga wabunge kupata posho na maslahi zaidi na hata kufanya israfu na kufuru ndogondogo. Kwa mfano, wabunge wenzao wa Kenya wameidhinisha bunge lao kununua viti vipya vya bunge kwa mabilioni ya fedha za Kenya. Kiti kimoja kitakuwa chanunuliwa kwa takriban shilingi milioni tatu. Piga hesabu kwa viti zaidi ya mia tatu bungeni uone mambo hayo. Tofauti na Tanzania viti hivyo havitoki nje vitatoka magereza ya Kenya ambako kuna maseremala wenye hadhi ya kimataifa. Lakini huu ni uwakilishi wa walio nacho kuwawakilisha wasio nacho, ambao wanaamini ili kufanya kazi zao vizuri na kwa starehe lazima anasa na starehe nazo ziingizwe hadi bungeni kwa namna moja au nyingine. Na matajiri kumbukeni hawatopenda wawakilishi wenu waonekane kuteseka au kuwa na maisha ya dhiki au kufanya kazi katika mazingira magumu, kwa hiyo mkiwaruhusu au msipowaruhusu wao watawafadhili bila shida. Ili kuepukana na aibu hii na fedheha ya kufadhiliwa na wenye pesa basi gharama hizo huonekana ni za lazima na zisizoepukika.
Maswali ya kujiuliza
Swali kuu la kujiuliza ni kigezo au vigezo gani vinavyotumika kihistoria na kimapokeo na katika mazingira na hali halisi au muktadha uliopo hivi leo ? Swali hili linazaa maswali yafuatayo:
. Wabunge wetu wana umuhimu na utakatifu gani wa kustahili kulipwa vizuri kuliko madaktari, wahadhiri, wahandisi, walimu, manesi na watu wengine kama hao?
. Hivi kweli hiki tunachokiona katika luninga, yaani, bunge la kusifia na kujisifia na kujipalilia na bunge la NDIIIIYO.... ndicho Watanzania watakachokubali kwacho wabunge kulipwa kihalali na sio kidhulumati ?
. Hivi bunge letu kazi yake ni kutatua matatizo ya wananchi na kuwawezesha wananchi wetu au kazi yake ni kuwapatia fursa wabunge ya kutumbua na kutanua?
. Je, badala ya kuwa na bunge moja tukawa pia na bunge la makundi ya kimaslahi, yaani, bunge la pili muda wa vikao hautafupishwa kiasi wabunge wakashughulikia matatizo yetu badala ya swahifa na swahifa za maneno na porojo?
. Hivi kila mkoa ukiwa na waziri wake mkuu, mawaziri na wawakishi wake nao wakashughulikia moja kwa moja mipango na bajeti zao bunge au mabunge ya kitaifa hayatahitaji tu wiki moja kila baada ya miezi mitatu kuzungumzia mambo makubwa ya kitaifa badala ya utaratibu wa sasa unaotudumaza badala ya kutukuza?
. Hivi na wanaopiga porojo, wanaolala, wanaozomea na kupiga vigelegele nao wanastahili posho hii?
. Mfumo wetu wa bunge hivi unalandana na ule wa kikoloni au kibepari ambao umejengwa katika hoja kuwa watu ni matajiri na sio masikini au vipi?
. Huko Malasyia viongozi wakiwemo wabunge walijipa miaka kadhaa ili kwanza wawatoe wananchi kutoka kwenye umaskini wa kutisha na kisha ndio wabunge wakaanza kulipwa vizuri na kutanua, je, wabunge wetu wanapoanza kwa kutanua kuna uwezekano wowote kweli kwa sisi kukombolewa kiuchumi na kijamii? Wanakubaliana na falsafa ya wabunge wa Malaysia au hawajaona ndani? Ukizingatia hulka au saikolojia ya binadamu, tuna ubavu wa kuifikia Malaysia hata 2100 kwa namna za posho kama hizi za wabunge wetu ?
. Kuna uwiano gani kati ya kile wabunge wanachofanikisha kiuchumi na kijamii kwa wananchi na kile wanacholipwa ?
. Je, uwezo wetu wa kukusanya kodi na kipato chetu cha kila mwaka unaturuhusu kulipa posho hii?
. Je, mabilioni ya fedha yatakayolipwa kwa namna hii hayawezi kuwekezwa kwanza katika mradi utakaozalisha ili posho hiyo itokane na kinachozalishwa na sio kuiingizia hazina shimo jipya la kuchotwa fedha kila mwaka? Hivi wabunge wetu wana akili za uwekezaji au wanazisikia tu na wanataka wawe nazo wananchi lakini si wao wenyewe?
. Je, kwanini mhadhiri, mwalimu, polisi, daktari na nesi nao wasipate posho kama hii? Hasa ukizingatia mazingira magumu wanayofanya kazi na majukumu watumishi hawa waliyonayo kwa wananchi wenzao ?
. Je, uwezo wetu wa kiakili unatufanya tujali faida au manufaa makubwa zaidi kwa idadi iliyo kubwa zaidi au kinyume cha hayo?
. Ni miradi mingapi mbadala ambayo ingesaidia watu wenye kipato cha chini kuondokana na umaskini inakwamishwa kwa hatua hii?
Sababu za baadhi ya wabunge kuridhika na hili
Wabunge nao ni binadamu na mahitaji yao yanaongezeka kutokana na ukubwa walio nao na tamaa zao za kifahari licha ya umaskini wa watu wao; wanataka kulimbikiza ili kushinda uchaguzi ujao; uwakilishi unakuwa fursa ya wao kunyanyuka kiuchumi kama sio kutajirika kirahisi zaidi na mfumo uliopo unatumika kuwanunua bila kujua ili wawasaliti wanaowawakilisha na kutetea walioko mamlakani hata katika yale yanayowahujumu wawakilishwa wao. Aidha katika mfumo ambao wizi wa kura umehalalishwa kinyemela na mbunge hachaguliwi ila kwa kugawa fedha kwanza, wawakilishi hulazimika baadaye kulipa madeni ya watu au kudunduliza tena kile kilichokuwa akiba yao walichokitumia ili wapate kura za wananchi.
Kwanini wabunge wanajisahau
. Wabunge ni binadamu na katika mfumo unaostawi kwa ubinafsi wa kichama na umimi, ubinafsi hauonekani ni kitu kibaya;
. Wabunge walio wengi hawaingii bungeni kutetea maslahi ya wengine ila kulinda na kuendeleza maslahi yao binafsi na jamaa zao;
. Katika mfumo ambao umekwaza na unakinza fani na tasnia nyingine (k.m. mishahara njiwa kwa wahadhiri, walimu, manesi na madaktari ) kimshahara au kiujira, kimasurufu na kimaslahi matokeo yake ni wengi kukimbilia siasa hata kama hawapendi siasa na wanaziona ni uchafu kwa sababu ya fedha au kipato na siyo kwa sababu ya wito;
. Wabunge hawachaguliwi tena kama wawakilishi na watetezi wa wanajamii fulani bali kama watumishi wa chama fulani;
. Mawasiliano kati ya wanaowawakilisha na wabunge huisha mara baada ya mbunge kuchaguliwa;
. Mbunge hafanyi kazi zake ili wananchi wake waneemeke na kutajirika bali kukisaidia chama chake kurudi tena madarakani;
. Nguvu ya serikali na vyombo vya serikali hutumika kukijenga chama tawala na kuvidhoofisha vyama vingine na kutokana na udhaifu wa vyama vingi wabunge kuamini kuwepo kwao kisiasa kunategemea chama tawala kushinda;
. Baadhi ya vyama vingine nyongeza ya posho inapotolewa asilimia kubwa haiendi mfukoni kwa mwakilishi bali kwa chama husika, yaani, nyongeza ya posho ni mlango mzuri wa kustawisha udokozi wa vilivyo vya serikali ili kuwajenga wanasiasa na vyama vyao, na;
. Wawakilishi walio wengi hawaujui umaskini wa wanaowawakilisha. Na wengi huishi katika ukale badala ya kuangalia hali halisi iliyopo hivi leo majimboni mwao.
Majibu ya maswali hayo hapo juu na mengine kama hayo nina hakika ndiyo yatakayoamua hatima ya wabunge na wanasiasa wetu na mustakabali wa nchi yetu bila kujali masuala ya itikadi, msimamo, mtazamo, chama na serikali iliyopo madarakani.
Tanzania tuitakayo
Tanzania tuitakayo haiwezi kupatikana kwa kuwa na wabunge walioshiba na wasiyemjua mwenye njaa, na wakuu wa mikoa wanaokokota badala ya kuongoza mikoa; kwani wao bado waamini wana njaa pia; kwa kutanguliza mbele ubinafsi badala ya jamii; na bwabwaja wa kuzungumza lakini wachache wa vitendo; na vyama na wanasiasa ambao wanajilinganisha na matajiri na kuishi kama wao kama sio kuwapita; na wanaotetea maslahi ya chama au serikali badala ya wananchi wao; na wenye fedha wanaoingia bungeni ili kutajirika zaidi na sio kuwanyanyua wanaowawaklisha; na watu wanaokubali kutumiwa na wengine kwa manufaa ya wengine na sio ya watu wao; na watu wasiojua nchi ilipo na inapotakiwa kwenda.
Ninaelewa maswali hayo hapo juu sio rahisi kuyajibu achilia mbali kuyajibu kwa haraka sana. Ila yanadhihirisha kitu kimoja, muswaada wa katiba si 'blue' wala 'green' wala 'white' paper ya serikali unahitaji muda na wasaa kuusoma na kuutafakari. Na kwamba kama wanaharakati, kazi yetu moja kubwa ni kuitumia katiba ama kuondoa vipengele vyote vinavyowapendelea kiujira na kimaslahi wale wasiozalisha na kuwakamua wanaozalisha kwa upande mmoja na kuviingiza vipengele vipya vyote vinavyohitajika ili kuondokana na dhuluma hii ya kiujira na kimapato ilioyoanzishwa na wakoloni, kulelewa na watawala wetu wa jana na sasa na likachukuliwa kama msahafu au biblia na lisilogusika au kurekebishwa na watawala wetu wa leo. Muktadha huu si msahafu, si biblia na mapinduzi hayaepukiki ili tuwe na Tanzania yenye usawa, haki, utu na ubinadamu zaidi. Tanzania mtu anayelipwa kwa kigezo cha kile alichokisomea na kuhitimu na sio kwa kubebwa kisiasa bila hoja na sababu za msingi. Mungu tusaidie!
Alionya kwamba demokrasia isipodhibitiwa na wananchi wenyewe ikaachiwa kwa wajanja wachache katika jamii inaweza kugeuka wizi wa mchana kweupe na wa kutisha ambao umehalalishwa na una nguvu za kisheria.
Kiasi ambacho jambo likishaamuliwa huwezi kulipinga kwa kutumia sheria ila kwa njia nyingine.
Alidai wale wanaoitwa wawakilishi wa wananchi wanaweza kuamua kupiga kura ya 'ndiyo' ili kuifagia na kuisafisha hazina au Benki Kuu ya nchi ikawa nyeupe na isibakiwe hata na shilingi moja kwa ajili ya matumizi yao binafsi.
Nina wasiwasi kama huko sio kwa mfumo tulionao leo, wa demokrasia ya chama kimoja iliyojificha ndani ya mfumo wa vyama vingi kama sio tunakokwenda.
Hakuna anayepinga wabunge kupata posho na maslahi zaidi na hata kufanya israfu na kufuru ndogondogo. Kwa mfano, wabunge wenzao wa Kenya wameidhinisha bunge lao kununua viti vipya vya bunge kwa mabilioni ya fedha za Kenya. Kiti kimoja kitakuwa chanunuliwa kwa takriban shilingi milioni tatu. Piga hesabu kwa viti zaidi ya mia tatu bungeni uone mambo hayo. Tofauti na Tanzania viti hivyo havitoki nje vitatoka magereza ya Kenya ambako kuna maseremala wenye hadhi ya kimataifa. Lakini huu ni uwakilishi wa walio nacho kuwawakilisha wasio nacho, ambao wanaamini ili kufanya kazi zao vizuri na kwa starehe lazima anasa na starehe nazo ziingizwe hadi bungeni kwa namna moja au nyingine. Na matajiri kumbukeni hawatopenda wawakilishi wenu waonekane kuteseka au kuwa na maisha ya dhiki au kufanya kazi katika mazingira magumu, kwa hiyo mkiwaruhusu au msipowaruhusu wao watawafadhili bila shida. Ili kuepukana na aibu hii na fedheha ya kufadhiliwa na wenye pesa basi gharama hizo huonekana ni za lazima na zisizoepukika.
Maswali ya kujiuliza
Swali kuu la kujiuliza ni kigezo au vigezo gani vinavyotumika kihistoria na kimapokeo na katika mazingira na hali halisi au muktadha uliopo hivi leo ? Swali hili linazaa maswali yafuatayo:
. Wabunge wetu wana umuhimu na utakatifu gani wa kustahili kulipwa vizuri kuliko madaktari, wahadhiri, wahandisi, walimu, manesi na watu wengine kama hao?
. Hivi kweli hiki tunachokiona katika luninga, yaani, bunge la kusifia na kujisifia na kujipalilia na bunge la NDIIIIYO.... ndicho Watanzania watakachokubali kwacho wabunge kulipwa kihalali na sio kidhulumati ?
. Hivi bunge letu kazi yake ni kutatua matatizo ya wananchi na kuwawezesha wananchi wetu au kazi yake ni kuwapatia fursa wabunge ya kutumbua na kutanua?
. Je, badala ya kuwa na bunge moja tukawa pia na bunge la makundi ya kimaslahi, yaani, bunge la pili muda wa vikao hautafupishwa kiasi wabunge wakashughulikia matatizo yetu badala ya swahifa na swahifa za maneno na porojo?
. Hivi kila mkoa ukiwa na waziri wake mkuu, mawaziri na wawakishi wake nao wakashughulikia moja kwa moja mipango na bajeti zao bunge au mabunge ya kitaifa hayatahitaji tu wiki moja kila baada ya miezi mitatu kuzungumzia mambo makubwa ya kitaifa badala ya utaratibu wa sasa unaotudumaza badala ya kutukuza?
. Hivi na wanaopiga porojo, wanaolala, wanaozomea na kupiga vigelegele nao wanastahili posho hii?
. Mfumo wetu wa bunge hivi unalandana na ule wa kikoloni au kibepari ambao umejengwa katika hoja kuwa watu ni matajiri na sio masikini au vipi?
. Huko Malasyia viongozi wakiwemo wabunge walijipa miaka kadhaa ili kwanza wawatoe wananchi kutoka kwenye umaskini wa kutisha na kisha ndio wabunge wakaanza kulipwa vizuri na kutanua, je, wabunge wetu wanapoanza kwa kutanua kuna uwezekano wowote kweli kwa sisi kukombolewa kiuchumi na kijamii? Wanakubaliana na falsafa ya wabunge wa Malaysia au hawajaona ndani? Ukizingatia hulka au saikolojia ya binadamu, tuna ubavu wa kuifikia Malaysia hata 2100 kwa namna za posho kama hizi za wabunge wetu ?
. Kuna uwiano gani kati ya kile wabunge wanachofanikisha kiuchumi na kijamii kwa wananchi na kile wanacholipwa ?
. Je, uwezo wetu wa kukusanya kodi na kipato chetu cha kila mwaka unaturuhusu kulipa posho hii?
. Je, mabilioni ya fedha yatakayolipwa kwa namna hii hayawezi kuwekezwa kwanza katika mradi utakaozalisha ili posho hiyo itokane na kinachozalishwa na sio kuiingizia hazina shimo jipya la kuchotwa fedha kila mwaka? Hivi wabunge wetu wana akili za uwekezaji au wanazisikia tu na wanataka wawe nazo wananchi lakini si wao wenyewe?
. Je, kwanini mhadhiri, mwalimu, polisi, daktari na nesi nao wasipate posho kama hii? Hasa ukizingatia mazingira magumu wanayofanya kazi na majukumu watumishi hawa waliyonayo kwa wananchi wenzao ?
. Je, uwezo wetu wa kiakili unatufanya tujali faida au manufaa makubwa zaidi kwa idadi iliyo kubwa zaidi au kinyume cha hayo?
. Ni miradi mingapi mbadala ambayo ingesaidia watu wenye kipato cha chini kuondokana na umaskini inakwamishwa kwa hatua hii?
Sababu za baadhi ya wabunge kuridhika na hili
Wabunge nao ni binadamu na mahitaji yao yanaongezeka kutokana na ukubwa walio nao na tamaa zao za kifahari licha ya umaskini wa watu wao; wanataka kulimbikiza ili kushinda uchaguzi ujao; uwakilishi unakuwa fursa ya wao kunyanyuka kiuchumi kama sio kutajirika kirahisi zaidi na mfumo uliopo unatumika kuwanunua bila kujua ili wawasaliti wanaowawakilisha na kutetea walioko mamlakani hata katika yale yanayowahujumu wawakilishwa wao. Aidha katika mfumo ambao wizi wa kura umehalalishwa kinyemela na mbunge hachaguliwi ila kwa kugawa fedha kwanza, wawakilishi hulazimika baadaye kulipa madeni ya watu au kudunduliza tena kile kilichokuwa akiba yao walichokitumia ili wapate kura za wananchi.
Kwanini wabunge wanajisahau
. Wabunge ni binadamu na katika mfumo unaostawi kwa ubinafsi wa kichama na umimi, ubinafsi hauonekani ni kitu kibaya;
. Wabunge walio wengi hawaingii bungeni kutetea maslahi ya wengine ila kulinda na kuendeleza maslahi yao binafsi na jamaa zao;
. Katika mfumo ambao umekwaza na unakinza fani na tasnia nyingine (k.m. mishahara njiwa kwa wahadhiri, walimu, manesi na madaktari ) kimshahara au kiujira, kimasurufu na kimaslahi matokeo yake ni wengi kukimbilia siasa hata kama hawapendi siasa na wanaziona ni uchafu kwa sababu ya fedha au kipato na siyo kwa sababu ya wito;
. Wabunge hawachaguliwi tena kama wawakilishi na watetezi wa wanajamii fulani bali kama watumishi wa chama fulani;
. Mawasiliano kati ya wanaowawakilisha na wabunge huisha mara baada ya mbunge kuchaguliwa;
. Mbunge hafanyi kazi zake ili wananchi wake waneemeke na kutajirika bali kukisaidia chama chake kurudi tena madarakani;
. Nguvu ya serikali na vyombo vya serikali hutumika kukijenga chama tawala na kuvidhoofisha vyama vingine na kutokana na udhaifu wa vyama vingi wabunge kuamini kuwepo kwao kisiasa kunategemea chama tawala kushinda;
. Baadhi ya vyama vingine nyongeza ya posho inapotolewa asilimia kubwa haiendi mfukoni kwa mwakilishi bali kwa chama husika, yaani, nyongeza ya posho ni mlango mzuri wa kustawisha udokozi wa vilivyo vya serikali ili kuwajenga wanasiasa na vyama vyao, na;
. Wawakilishi walio wengi hawaujui umaskini wa wanaowawakilisha. Na wengi huishi katika ukale badala ya kuangalia hali halisi iliyopo hivi leo majimboni mwao.
Majibu ya maswali hayo hapo juu na mengine kama hayo nina hakika ndiyo yatakayoamua hatima ya wabunge na wanasiasa wetu na mustakabali wa nchi yetu bila kujali masuala ya itikadi, msimamo, mtazamo, chama na serikali iliyopo madarakani.
Tanzania tuitakayo
Tanzania tuitakayo haiwezi kupatikana kwa kuwa na wabunge walioshiba na wasiyemjua mwenye njaa, na wakuu wa mikoa wanaokokota badala ya kuongoza mikoa; kwani wao bado waamini wana njaa pia; kwa kutanguliza mbele ubinafsi badala ya jamii; na bwabwaja wa kuzungumza lakini wachache wa vitendo; na vyama na wanasiasa ambao wanajilinganisha na matajiri na kuishi kama wao kama sio kuwapita; na wanaotetea maslahi ya chama au serikali badala ya wananchi wao; na wenye fedha wanaoingia bungeni ili kutajirika zaidi na sio kuwanyanyua wanaowawaklisha; na watu wanaokubali kutumiwa na wengine kwa manufaa ya wengine na sio ya watu wao; na watu wasiojua nchi ilipo na inapotakiwa kwenda.
Ninaelewa maswali hayo hapo juu sio rahisi kuyajibu achilia mbali kuyajibu kwa haraka sana. Ila yanadhihirisha kitu kimoja, muswaada wa katiba si 'blue' wala 'green' wala 'white' paper ya serikali unahitaji muda na wasaa kuusoma na kuutafakari. Na kwamba kama wanaharakati, kazi yetu moja kubwa ni kuitumia katiba ama kuondoa vipengele vyote vinavyowapendelea kiujira na kimaslahi wale wasiozalisha na kuwakamua wanaozalisha kwa upande mmoja na kuviingiza vipengele vipya vyote vinavyohitajika ili kuondokana na dhuluma hii ya kiujira na kimapato ilioyoanzishwa na wakoloni, kulelewa na watawala wetu wa jana na sasa na likachukuliwa kama msahafu au biblia na lisilogusika au kurekebishwa na watawala wetu wa leo. Muktadha huu si msahafu, si biblia na mapinduzi hayaepukiki ili tuwe na Tanzania yenye usawa, haki, utu na ubinadamu zaidi. Tanzania mtu anayelipwa kwa kigezo cha kile alichokisomea na kuhitimu na sio kwa kubebwa kisiasa bila hoja na sababu za msingi. Mungu tusaidie!
Tusipoangalia demokrasia yetu inaweza kuwa wizi….
SI MTU mwingine ila baba wa ukomunisti, Karl Marx ambaye miaka zaidi ya 120 alitahadharisha kwamba demokrasia kama ilivyokuwa katika nchi za Magharibi ni mfumo wenye udhaifu, mapungufu na kasoro nyingi.
Alionya kwamba demokrasia isipodhibitiwa na wananchi wenyewe ikaachiwa kwa wajanja wachache katika jamii inaweza kugeuka wizi wa mchana kweupe na wa kutisha ambao umehalalishwa na una nguvu za kisheria.
Kiasi ambacho jambo likishaamuliwa huwezi kulipinga kwa kutumia sheria ila kwa njia nyingine.
Alidai wale wanaoitwa wawakilishi wa wananchi wanaweza kuamua kupiga kura ya 'ndiyo' ili kuifagia na kuisafisha hazina au Benki Kuu ya nchi ikawa nyeupe na isibakiwe hata na shilingi moja kwa ajili ya matumizi yao binafsi.
Nina wasiwasi kama huko sio kwa mfumo tulionao leo, wa demokrasia ya chama kimoja iliyojificha ndani ya mfumo wa vyama vingi kama sio tunakokwenda.
Hakuna anayepinga wabunge kupata posho na maslahi zaidi na hata kufanya israfu na kufuru ndogondogo. Kwa mfano, wabunge wenzao wa Kenya wameidhinisha bunge lao kununua viti vipya vya bunge kwa mabilioni ya fedha za Kenya. Kiti kimoja kitakuwa chanunuliwa kwa takriban shilingi milioni tatu. Piga hesabu kwa viti zaidi ya mia tatu bungeni uone mambo hayo. Tofauti na Tanzania viti hivyo havitoki nje vitatoka magereza ya Kenya ambako kuna maseremala wenye hadhi ya kimataifa. Lakini huu ni uwakilishi wa walio nacho kuwawakilisha wasio nacho, ambao wanaamini ili kufanya kazi zao vizuri na kwa starehe lazima anasa na starehe nazo ziingizwe hadi bungeni kwa namna moja au nyingine. Na matajiri kumbukeni hawatopenda wawakilishi wenu waonekane kuteseka au kuwa na maisha ya dhiki au kufanya kazi katika mazingira magumu, kwa hiyo mkiwaruhusu au msipowaruhusu wao watawafadhili bila shida. Ili kuepukana na aibu hii na fedheha ya kufadhiliwa na wenye pesa basi gharama hizo huonekana ni za lazima na zisizoepukika.
Maswali ya kujiuliza
Swali kuu la kujiuliza ni kigezo au vigezo gani vinavyotumika kihistoria na kimapokeo na katika mazingira na hali halisi au muktadha uliopo hivi leo ? Swali hili linazaa maswali yafuatayo:
. Wabunge wetu wana umuhimu na utakatifu gani wa kustahili kulipwa vizuri kuliko madaktari, wahadhiri, wahandisi, walimu, manesi na watu wengine kama hao?
. Hivi kweli hiki tunachokiona katika luninga, yaani, bunge la kusifia na kujisifia na kujipalilia na bunge la NDIIIIYO.... ndicho Watanzania watakachokubali kwacho wabunge kulipwa kihalali na sio kidhulumati ?
. Hivi bunge letu kazi yake ni kutatua matatizo ya wananchi na kuwawezesha wananchi wetu au kazi yake ni kuwapatia fursa wabunge ya kutumbua na kutanua?
. Je, badala ya kuwa na bunge moja tukawa pia na bunge la makundi ya kimaslahi, yaani, bunge la pili muda wa vikao hautafupishwa kiasi wabunge wakashughulikia matatizo yetu badala ya swahifa na swahifa za maneno na porojo?
. Hivi kila mkoa ukiwa na waziri wake mkuu, mawaziri na wawakishi wake nao wakashughulikia moja kwa moja mipango na bajeti zao bunge au mabunge ya kitaifa hayatahitaji tu wiki moja kila baada ya miezi mitatu kuzungumzia mambo makubwa ya kitaifa badala ya utaratibu wa sasa unaotudumaza badala ya kutukuza?
. Hivi na wanaopiga porojo, wanaolala, wanaozomea na kupiga vigelegele nao wanastahili posho hii?
. Mfumo wetu wa bunge hivi unalandana na ule wa kikoloni au kibepari ambao umejengwa katika hoja kuwa watu ni matajiri na sio masikini au vipi?
. Huko Malasyia viongozi wakiwemo wabunge walijipa miaka kadhaa ili kwanza wawatoe wananchi kutoka kwenye umaskini wa kutisha na kisha ndio wabunge wakaanza kulipwa vizuri na kutanua, je, wabunge wetu wanapoanza kwa kutanua kuna uwezekano wowote kweli kwa sisi kukombolewa kiuchumi na kijamii? Wanakubaliana na falsafa ya wabunge wa Malaysia au hawajaona ndani? Ukizingatia hulka au saikolojia ya binadamu, tuna ubavu wa kuifikia Malaysia hata 2100 kwa namna za posho kama hizi za wabunge wetu ?
. Kuna uwiano gani kati ya kile wabunge wanachofanikisha kiuchumi na kijamii kwa wananchi na kile wanacholipwa ?
. Je, uwezo wetu wa kukusanya kodi na kipato chetu cha kila mwaka unaturuhusu kulipa posho hii?
. Je, mabilioni ya fedha yatakayolipwa kwa namna hii hayawezi kuwekezwa kwanza katika mradi utakaozalisha ili posho hiyo itokane na kinachozalishwa na sio kuiingizia hazina shimo jipya la kuchotwa fedha kila mwaka? Hivi wabunge wetu wana akili za uwekezaji au wanazisikia tu na wanataka wawe nazo wananchi lakini si wao wenyewe?
. Je, kwanini mhadhiri, mwalimu, polisi, daktari na nesi nao wasipate posho kama hii? Hasa ukizingatia mazingira magumu wanayofanya kazi na majukumu watumishi hawa waliyonayo kwa wananchi wenzao ?
. Je, uwezo wetu wa kiakili unatufanya tujali faida au manufaa makubwa zaidi kwa idadi iliyo kubwa zaidi au kinyume cha hayo?
. Ni miradi mingapi mbadala ambayo ingesaidia watu wenye kipato cha chini kuondokana na umaskini inakwamishwa kwa hatua hii?
Sababu za baadhi ya wabunge kuridhika na hili
Wabunge nao ni binadamu na mahitaji yao yanaongezeka kutokana na ukubwa walio nao na tamaa zao za kifahari licha ya umaskini wa watu wao; wanataka kulimbikiza ili kushinda uchaguzi ujao; uwakilishi unakuwa fursa ya wao kunyanyuka kiuchumi kama sio kutajirika kirahisi zaidi na mfumo uliopo unatumika kuwanunua bila kujua ili wawasaliti wanaowawakilisha na kutetea walioko mamlakani hata katika yale yanayowahujumu wawakilishwa wao. Aidha katika mfumo ambao wizi wa kura umehalalishwa kinyemela na mbunge hachaguliwi ila kwa kugawa fedha kwanza, wawakilishi hulazimika baadaye kulipa madeni ya watu au kudunduliza tena kile kilichokuwa akiba yao walichokitumia ili wapate kura za wananchi.
Kwanini wabunge wanajisahau
. Wabunge ni binadamu na katika mfumo unaostawi kwa ubinafsi wa kichama na umimi, ubinafsi hauonekani ni kitu kibaya;
. Wabunge walio wengi hawaingii bungeni kutetea maslahi ya wengine ila kulinda na kuendeleza maslahi yao binafsi na jamaa zao;
. Katika mfumo ambao umekwaza na unakinza fani na tasnia nyingine (k.m. mishahara njiwa kwa wahadhiri, walimu, manesi na madaktari ) kimshahara au kiujira, kimasurufu na kimaslahi matokeo yake ni wengi kukimbilia siasa hata kama hawapendi siasa na wanaziona ni uchafu kwa sababu ya fedha au kipato na siyo kwa sababu ya wito;
. Wabunge hawachaguliwi tena kama wawakilishi na watetezi wa wanajamii fulani bali kama watumishi wa chama fulani;
. Mawasiliano kati ya wanaowawakilisha na wabunge huisha mara baada ya mbunge kuchaguliwa;
. Mbunge hafanyi kazi zake ili wananchi wake waneemeke na kutajirika bali kukisaidia chama chake kurudi tena madarakani;
. Nguvu ya serikali na vyombo vya serikali hutumika kukijenga chama tawala na kuvidhoofisha vyama vingine na kutokana na udhaifu wa vyama vingi wabunge kuamini kuwepo kwao kisiasa kunategemea chama tawala kushinda;
. Baadhi ya vyama vingine nyongeza ya posho inapotolewa asilimia kubwa haiendi mfukoni kwa mwakilishi bali kwa chama husika, yaani, nyongeza ya posho ni mlango mzuri wa kustawisha udokozi wa vilivyo vya serikali ili kuwajenga wanasiasa na vyama vyao, na;
. Wawakilishi walio wengi hawaujui umaskini wa wanaowawakilisha. Na wengi huishi katika ukale badala ya kuangalia hali halisi iliyopo hivi leo majimboni mwao.
Majibu ya maswali hayo hapo juu na mengine kama hayo nina hakika ndiyo yatakayoamua hatima ya wabunge na wanasiasa wetu na mustakabali wa nchi yetu bila kujali masuala ya itikadi, msimamo, mtazamo, chama na serikali iliyopo madarakani.
Tanzania tuitakayo
Tanzania tuitakayo haiwezi kupatikana kwa kuwa na wabunge walioshiba na wasiyemjua mwenye njaa, na wakuu wa mikoa wanaokokota badala ya kuongoza mikoa; kwani wao bado waamini wana njaa pia; kwa kutanguliza mbele ubinafsi badala ya jamii; na bwabwaja wa kuzungumza lakini wachache wa vitendo; na vyama na wanasiasa ambao wanajilinganisha na matajiri na kuishi kama wao kama sio kuwapita; na wanaotetea maslahi ya chama au serikali badala ya wananchi wao; na wenye fedha wanaoingia bungeni ili kutajirika zaidi na sio kuwanyanyua wanaowawaklisha; na watu wanaokubali kutumiwa na wengine kwa manufaa ya wengine na sio ya watu wao; na watu wasiojua nchi ilipo na inapotakiwa kwenda.
Ninaelewa maswali hayo hapo juu sio rahisi kuyajibu achilia mbali kuyajibu kwa haraka sana. Ila yanadhihirisha kitu kimoja, muswaada wa katiba si 'blue' wala 'green' wala 'white' paper ya serikali unahitaji muda na wasaa kuusoma na kuutafakari. Na kwamba kama wanaharakati, kazi yetu moja kubwa ni kuitumia katiba ama kuondoa vipengele vyote vinavyowapendelea kiujira na kimaslahi wale wasiozalisha na kuwakamua wanaozalisha kwa upande mmoja na kuviingiza vipengele vipya vyote vinavyohitajika ili kuondokana na dhuluma hii ya kiujira na kimapato ilioyoanzishwa na wakoloni, kulelewa na watawala wetu wa jana na sasa na likachukuliwa kama msahafu au biblia na lisilogusika au kurekebishwa na watawala wetu wa leo. Muktadha huu si msahafu, si biblia na mapinduzi hayaepukiki ili tuwe na Tanzania yenye usawa, haki, utu na ubinadamu zaidi. Tanzania mtu anayelipwa kwa kigezo cha kile alichokisomea na kuhitimu na sio kwa kubebwa kisiasa bila hoja na sababu za msingi. Mungu tusaidie!
Alionya kwamba demokrasia isipodhibitiwa na wananchi wenyewe ikaachiwa kwa wajanja wachache katika jamii inaweza kugeuka wizi wa mchana kweupe na wa kutisha ambao umehalalishwa na una nguvu za kisheria.
Kiasi ambacho jambo likishaamuliwa huwezi kulipinga kwa kutumia sheria ila kwa njia nyingine.
Alidai wale wanaoitwa wawakilishi wa wananchi wanaweza kuamua kupiga kura ya 'ndiyo' ili kuifagia na kuisafisha hazina au Benki Kuu ya nchi ikawa nyeupe na isibakiwe hata na shilingi moja kwa ajili ya matumizi yao binafsi.
Nina wasiwasi kama huko sio kwa mfumo tulionao leo, wa demokrasia ya chama kimoja iliyojificha ndani ya mfumo wa vyama vingi kama sio tunakokwenda.
Hakuna anayepinga wabunge kupata posho na maslahi zaidi na hata kufanya israfu na kufuru ndogondogo. Kwa mfano, wabunge wenzao wa Kenya wameidhinisha bunge lao kununua viti vipya vya bunge kwa mabilioni ya fedha za Kenya. Kiti kimoja kitakuwa chanunuliwa kwa takriban shilingi milioni tatu. Piga hesabu kwa viti zaidi ya mia tatu bungeni uone mambo hayo. Tofauti na Tanzania viti hivyo havitoki nje vitatoka magereza ya Kenya ambako kuna maseremala wenye hadhi ya kimataifa. Lakini huu ni uwakilishi wa walio nacho kuwawakilisha wasio nacho, ambao wanaamini ili kufanya kazi zao vizuri na kwa starehe lazima anasa na starehe nazo ziingizwe hadi bungeni kwa namna moja au nyingine. Na matajiri kumbukeni hawatopenda wawakilishi wenu waonekane kuteseka au kuwa na maisha ya dhiki au kufanya kazi katika mazingira magumu, kwa hiyo mkiwaruhusu au msipowaruhusu wao watawafadhili bila shida. Ili kuepukana na aibu hii na fedheha ya kufadhiliwa na wenye pesa basi gharama hizo huonekana ni za lazima na zisizoepukika.
Maswali ya kujiuliza
Swali kuu la kujiuliza ni kigezo au vigezo gani vinavyotumika kihistoria na kimapokeo na katika mazingira na hali halisi au muktadha uliopo hivi leo ? Swali hili linazaa maswali yafuatayo:
. Wabunge wetu wana umuhimu na utakatifu gani wa kustahili kulipwa vizuri kuliko madaktari, wahadhiri, wahandisi, walimu, manesi na watu wengine kama hao?
. Hivi kweli hiki tunachokiona katika luninga, yaani, bunge la kusifia na kujisifia na kujipalilia na bunge la NDIIIIYO.... ndicho Watanzania watakachokubali kwacho wabunge kulipwa kihalali na sio kidhulumati ?
. Hivi bunge letu kazi yake ni kutatua matatizo ya wananchi na kuwawezesha wananchi wetu au kazi yake ni kuwapatia fursa wabunge ya kutumbua na kutanua?
. Je, badala ya kuwa na bunge moja tukawa pia na bunge la makundi ya kimaslahi, yaani, bunge la pili muda wa vikao hautafupishwa kiasi wabunge wakashughulikia matatizo yetu badala ya swahifa na swahifa za maneno na porojo?
. Hivi kila mkoa ukiwa na waziri wake mkuu, mawaziri na wawakishi wake nao wakashughulikia moja kwa moja mipango na bajeti zao bunge au mabunge ya kitaifa hayatahitaji tu wiki moja kila baada ya miezi mitatu kuzungumzia mambo makubwa ya kitaifa badala ya utaratibu wa sasa unaotudumaza badala ya kutukuza?
. Hivi na wanaopiga porojo, wanaolala, wanaozomea na kupiga vigelegele nao wanastahili posho hii?
. Mfumo wetu wa bunge hivi unalandana na ule wa kikoloni au kibepari ambao umejengwa katika hoja kuwa watu ni matajiri na sio masikini au vipi?
. Huko Malasyia viongozi wakiwemo wabunge walijipa miaka kadhaa ili kwanza wawatoe wananchi kutoka kwenye umaskini wa kutisha na kisha ndio wabunge wakaanza kulipwa vizuri na kutanua, je, wabunge wetu wanapoanza kwa kutanua kuna uwezekano wowote kweli kwa sisi kukombolewa kiuchumi na kijamii? Wanakubaliana na falsafa ya wabunge wa Malaysia au hawajaona ndani? Ukizingatia hulka au saikolojia ya binadamu, tuna ubavu wa kuifikia Malaysia hata 2100 kwa namna za posho kama hizi za wabunge wetu ?
. Kuna uwiano gani kati ya kile wabunge wanachofanikisha kiuchumi na kijamii kwa wananchi na kile wanacholipwa ?
. Je, uwezo wetu wa kukusanya kodi na kipato chetu cha kila mwaka unaturuhusu kulipa posho hii?
. Je, mabilioni ya fedha yatakayolipwa kwa namna hii hayawezi kuwekezwa kwanza katika mradi utakaozalisha ili posho hiyo itokane na kinachozalishwa na sio kuiingizia hazina shimo jipya la kuchotwa fedha kila mwaka? Hivi wabunge wetu wana akili za uwekezaji au wanazisikia tu na wanataka wawe nazo wananchi lakini si wao wenyewe?
. Je, kwanini mhadhiri, mwalimu, polisi, daktari na nesi nao wasipate posho kama hii? Hasa ukizingatia mazingira magumu wanayofanya kazi na majukumu watumishi hawa waliyonayo kwa wananchi wenzao ?
. Je, uwezo wetu wa kiakili unatufanya tujali faida au manufaa makubwa zaidi kwa idadi iliyo kubwa zaidi au kinyume cha hayo?
. Ni miradi mingapi mbadala ambayo ingesaidia watu wenye kipato cha chini kuondokana na umaskini inakwamishwa kwa hatua hii?
Sababu za baadhi ya wabunge kuridhika na hili
Wabunge nao ni binadamu na mahitaji yao yanaongezeka kutokana na ukubwa walio nao na tamaa zao za kifahari licha ya umaskini wa watu wao; wanataka kulimbikiza ili kushinda uchaguzi ujao; uwakilishi unakuwa fursa ya wao kunyanyuka kiuchumi kama sio kutajirika kirahisi zaidi na mfumo uliopo unatumika kuwanunua bila kujua ili wawasaliti wanaowawakilisha na kutetea walioko mamlakani hata katika yale yanayowahujumu wawakilishwa wao. Aidha katika mfumo ambao wizi wa kura umehalalishwa kinyemela na mbunge hachaguliwi ila kwa kugawa fedha kwanza, wawakilishi hulazimika baadaye kulipa madeni ya watu au kudunduliza tena kile kilichokuwa akiba yao walichokitumia ili wapate kura za wananchi.
Kwanini wabunge wanajisahau
. Wabunge ni binadamu na katika mfumo unaostawi kwa ubinafsi wa kichama na umimi, ubinafsi hauonekani ni kitu kibaya;
. Wabunge walio wengi hawaingii bungeni kutetea maslahi ya wengine ila kulinda na kuendeleza maslahi yao binafsi na jamaa zao;
. Katika mfumo ambao umekwaza na unakinza fani na tasnia nyingine (k.m. mishahara njiwa kwa wahadhiri, walimu, manesi na madaktari ) kimshahara au kiujira, kimasurufu na kimaslahi matokeo yake ni wengi kukimbilia siasa hata kama hawapendi siasa na wanaziona ni uchafu kwa sababu ya fedha au kipato na siyo kwa sababu ya wito;
. Wabunge hawachaguliwi tena kama wawakilishi na watetezi wa wanajamii fulani bali kama watumishi wa chama fulani;
. Mawasiliano kati ya wanaowawakilisha na wabunge huisha mara baada ya mbunge kuchaguliwa;
. Mbunge hafanyi kazi zake ili wananchi wake waneemeke na kutajirika bali kukisaidia chama chake kurudi tena madarakani;
. Nguvu ya serikali na vyombo vya serikali hutumika kukijenga chama tawala na kuvidhoofisha vyama vingine na kutokana na udhaifu wa vyama vingi wabunge kuamini kuwepo kwao kisiasa kunategemea chama tawala kushinda;
. Baadhi ya vyama vingine nyongeza ya posho inapotolewa asilimia kubwa haiendi mfukoni kwa mwakilishi bali kwa chama husika, yaani, nyongeza ya posho ni mlango mzuri wa kustawisha udokozi wa vilivyo vya serikali ili kuwajenga wanasiasa na vyama vyao, na;
. Wawakilishi walio wengi hawaujui umaskini wa wanaowawakilisha. Na wengi huishi katika ukale badala ya kuangalia hali halisi iliyopo hivi leo majimboni mwao.
Majibu ya maswali hayo hapo juu na mengine kama hayo nina hakika ndiyo yatakayoamua hatima ya wabunge na wanasiasa wetu na mustakabali wa nchi yetu bila kujali masuala ya itikadi, msimamo, mtazamo, chama na serikali iliyopo madarakani.
Tanzania tuitakayo
Tanzania tuitakayo haiwezi kupatikana kwa kuwa na wabunge walioshiba na wasiyemjua mwenye njaa, na wakuu wa mikoa wanaokokota badala ya kuongoza mikoa; kwani wao bado waamini wana njaa pia; kwa kutanguliza mbele ubinafsi badala ya jamii; na bwabwaja wa kuzungumza lakini wachache wa vitendo; na vyama na wanasiasa ambao wanajilinganisha na matajiri na kuishi kama wao kama sio kuwapita; na wanaotetea maslahi ya chama au serikali badala ya wananchi wao; na wenye fedha wanaoingia bungeni ili kutajirika zaidi na sio kuwanyanyua wanaowawaklisha; na watu wanaokubali kutumiwa na wengine kwa manufaa ya wengine na sio ya watu wao; na watu wasiojua nchi ilipo na inapotakiwa kwenda.
Ninaelewa maswali hayo hapo juu sio rahisi kuyajibu achilia mbali kuyajibu kwa haraka sana. Ila yanadhihirisha kitu kimoja, muswaada wa katiba si 'blue' wala 'green' wala 'white' paper ya serikali unahitaji muda na wasaa kuusoma na kuutafakari. Na kwamba kama wanaharakati, kazi yetu moja kubwa ni kuitumia katiba ama kuondoa vipengele vyote vinavyowapendelea kiujira na kimaslahi wale wasiozalisha na kuwakamua wanaozalisha kwa upande mmoja na kuviingiza vipengele vipya vyote vinavyohitajika ili kuondokana na dhuluma hii ya kiujira na kimapato ilioyoanzishwa na wakoloni, kulelewa na watawala wetu wa jana na sasa na likachukuliwa kama msahafu au biblia na lisilogusika au kurekebishwa na watawala wetu wa leo. Muktadha huu si msahafu, si biblia na mapinduzi hayaepukiki ili tuwe na Tanzania yenye usawa, haki, utu na ubinadamu zaidi. Tanzania mtu anayelipwa kwa kigezo cha kile alichokisomea na kuhitimu na sio kwa kubebwa kisiasa bila hoja na sababu za msingi. Mungu tusaidie!
Friday, November 25, 2011
Jinsi ya kuifanya Dar safi na ya kupendeza
KAMA jiji hili ambalo ndilo lenye Ikulu na wizara na idara zote muhimu nchini linataka liondokane na uchafu, harufu mbaya mpaka misikitini na makanisani, kinyesi kinachozibuliwa wakati wa mvua barabarani na mandhari za kuchukiza sasa ni wakati wa kuirudisha kazi ya usafi wa jiji kwa wanajamii kwa kiasi fulani badala ya kutoa tenda na kukodisha mchakato wote kwa watu wasio na uwezo na wasiokidhi mahitaji na matakwa ya usafi wa jiji hili.
Serikali kuu na serikali za mitaa zitatakiwa kutoa ushirikiano maalum ili kufanikisha azma hii.
Tofauti na mambo mengine, ningelipendekeza kazi hii ipewe umuhimu wa juu hata machoni kwa watu wa nje wanaotaka kuisadia nchi yetu katika masuala ya utunzaji mazingira na usafi.
Kinachopendekezwa hapa ni kuachana na utitiri wa magari na matrekta mabovu katika kazi ya kukusanya na kusomba taka kuzipeleka huko zinakotupwa. Badala yake kutoa ajira pana na za kudumu kwa kina vijana wetu wenye matoroli, maguta, pikipiki, vipawatila, bajaji, mikokoteni na wilibaroo kufanya kazi ya kukusanya taka mitaani na kwenda kutupwa kwenye eneo maalum litakalokuwa na shimo kubwa la kutupwa taka zilizotenganishwa kiaina na kiufundi na kisha kuchakatwa hadi kuzalishwa bidhaa mpya inayoweza kutumika majumbani, viwandani na mashambani.
Umuhimu wa serikali kuu na serikali za mitaa ni katika kupatikana kwa maeneo maalum ya kuchimbwa mashimo hayo mitaani au kwenye kata; ujenzi wa miundo mbinu rahisi ya kukokotosha taka kuwa bidhaa hitajika; kuwaandaa vijana kimafunzo tayari kwa kazi za kutenganisha taka na kuzibeba kwenda kwenye maeneo husika; na kuhakikisha bajeti ya usafi toka serikalini na misaada ya wafadhili inaelekezwa kwenye mambo haya badala ya kuliwa na wajanja wachache huko walipo.
Italazimu pia kwa viongozi na maofisa wote wa jiji na katika wizara husika, ambao wameomba kupewa hisa na chochote na wawekezaji katika miradi mipya tarajiwa ya kurejelea taka kupewa ruhusa maalum na serikali kuu ya kuwekeza kwenye makampuni bila kutoa chochote !
Aidha wanajamii kwa kushirikiana na serikali kuu na za mitaa watapaswa kuwa na kisima cha maji kilichochimbwa kwenye eneo au kina ambacho maji hayakauki kamwe ili kuhakikisha mji unakuwa na mandhari nzuri na ya kuvutia wakati wote. Maji hayo pia yatatumika kusaidia kazi za kupooza na kulainisha bidhaa katika kituo kikuu cha kubadili taka kuwa mali na utajiri. Ndoto ya kuwa na mifumo mizuri ya kuvuna mvua itakuwa ziada ambayo si mbovu katika hili.
Kila nyumba italazimika kupatiwa pipa pacha nne au kwa maneno mengine pipa ambalo lina sehemu nne: moja kwa ajili ya kutupwa chupa na glasi: la pili kwa ajili ya kutupwa karatasi: la tatu kwa ajili ya kutupwa mabaki ya vyakula na la mwisho kwa ajili ya kutupwa taka ambazo ni hatari kwa afya ya binadamu na taka mchanganyiko nje ya hizo hapo juu.
Vijana wakusanyaji watafunzwa jinsi ya kuzihamisha taka hizo toka mapipa hayo kwenda mifuko maalum ambayo itachukua taka kwa mpangilio huo huo huo na kuzipeleka kwenye kituo kikuu cha taka kwenye mtaa au kata kwa ajili ya kurejelewa upya kuzalisha kinachowezekana kuzalishwa.
Zitakapofikishwa kituoni hapo taka zitakuwa tayari zimetenganishwa kwa utaratibu huo hapo juu na hivyo kuingizwa kwenye moja kwa moja kwenye eneo zitakazofanyiwa kazi ili kuzalisha umeme au kutoa bidhaa fulani itakayotumika kama bidhaa mpya tena madukani au sokoni. Mabaki ya vyakula yanatarajiwa kutengenezwa kuwa mbolea asili isiyo na dawa yoyote ambayo itauzwa kwenye mifuko maalum kwa wakulima na watunza bustani.
Watumishi wizara ya ardhi wataaswa kwamba ili kuleta uwiano kati ya klutenda dhambai na mema- nchini ni muhimu kwao pamoja na kuuza maeneo wazi kwa mabwanyenye wetu wapya, sasa kutoa maeneo kwa ajili ya uchimbaji mashimo makubwa ya uhifadhi wa taka zitakazochakatwa na kuwa bidhaa mpya au kuzalisha umeme kwa ajili ya faida ya wakazi walio wengi jijini.
Wataalamu wa vyama vya siasa vyenye vijiwe mjini wataombwa wautumie utaalamu huo ili kugeuza vijana wetu toka 'majoblesi alwatani', wababaishaji na kupe wenye sifa za kimataifa kubadilika kwa kukopeshwa mitaji ya kununua toroli, maguta na vifaa kama hivyo ili kuwa wakusanyaji na wabebaji taka watakaoipa heshima mpya jiji la Dar es salaam.
Wataalamu wa kupiga raia mabomu, kuvunja maandamano na mikutano wataombwa kuutumia utaalamu wao ili kuhamasisha kazi ya usombaji taka kila wakati ili pasiwe na taka hata moja mahala popote jijini kwa kasi ile ile ya upigaji mabomu ya machozi wakati wa maandamano ya upinzani, wafuasi wa dini fulani au wafanyakazi au wanafunzi.
Mameneja wa migodi wataaombwa kuazimisha magreda na makatapila kuja kuchimba mashimo hayo katika mitaa au kata mbalimbali jijini kama walivyofanikisha zoezi la uchimbaji mashimo huko Geita, North Mara na Bulyanhulu,kutegemeana na kiwango cha uzalishaji taka katika maeneo husika.
Badala ya kuwa na magari mabovu yanayosafiri umbali mrefu kuokota na kutupa taka sasa vitoroli, mikokoteni, bajaji, guta na pikipiki zitatengenezwa kwa njia ambayo kwazo zitakuwa zikipeleka taka kwenye maeneo hayo yenye mashimo na miundo mbinu maalum ya kupokea taka zilizotenganishwa na kuanza kuzifanyia mchakato ili zitoe bidhaa za aina mbalimbali na kuzalisha umeme na vitu vingine vitakavyowezekanika.
Taka zinazohitaji kutupwa mbali zitachukuliwa na magari makubwa maalum machache lakini yenye kiwango cha kimataifa kwenda kutupwa mbali kabisa na makazi ya watu na wakati mwingine hata kwenda kufukia mashimo yaliyotokana na kuchimbwa madini yetu katika mikoa ya kaskazini na kusini.
Ukiutazama mtiririko huu mzima utagundua kuwa pendekezo hili lina shabaha ya kugeuza taka kuwa mali kwa namna kadhaa. Kwanza, vijana ambao wana tatizola ajira itabidi sasa wakimbie ajira wao wenyewe. Taka zitageuka fumba na kufumbua mali, maana kila mzigo kutegemeana na aina yake utakuwa ukilipwa fedha nzuri tu mara ukifika kwenye kituo kikuu cha kuchakata taka kwenye mtaa au kata.
Aidha magari mabovu ya kusomba taka amabyo wakati mwingine badala ya kusafisha mji huuchafua yatatoweka. Takataka hizo zitazaa bidhaa ambazo wafanyabiashara na wanunuzi watanufaika kwani zina uwezekano mkubwa wa kuwa za bei rahisi zaidi kuliko nyinginezo. Kisha mbolea itakayozalishwa itakwenda kuzistawisha bustani za Ikulu na Mnazi mmoja na maeneo mengine mjini na hivyo kulipa jiji mandhari ya kukata na shoka kwa uzuri wake. Hali kadhalika, sio tu tatizo la kukatikakatika umeme jijini litakuwa historia bali mradi huu utahakikisha hata nyumba mbavu za mbwa zilizo mabondeni zinapata umeme wa kutosha na wa uhakika kila siku.
Vilevile visima vitakavyoendana na mradi huu vitawahakikishia wakazi wa kila mtaa na kata upatikanaji maji masafi ya uhakika wakati wote, wakati wanasubiri maajabu yatakayofanywa na DAWASCO miaka mitano au kumi ijayo kama bado wako hai. Hili linawezekana, cheza nafasi yako na timiza wajibu wako. Miaka hamsini baada ya uhuru hutakiwi kushindwa na jambo hili.
Wakati ninaandika makala haya watafiti wanaonisaidia wameleta habari kwamba kuna watu tayari wameanza kujituma wenyewe na kuanzisha miradi kama hii. Kama hili ni kweli basi wilaya, mkoa na wizara husika zichangamkie mara moja jambo hili. NIna hakika likipata kuungwa mkono nao ni kitu kinachowezekana na kitakalolifanya jiji la Dar es salaam kuwa jiji la kuigwa na miji mingine sio tu Tanzania bali Afrika nzima.
lle tabia ya kujifanya kuwa serikali inaweza kufanya kila kitu si kitu kizuri. Na katika miaka hii ni kitu kilichopitwa na wakati na kuwazaini wananchi huku tukijua fika tunasema uongo. Kweli Watanzania hawana fedha, yaani, ni maskini. Lakini Watanzania wana kitu kimoja ambcho thamani yake wakati mwingine ni kubwa kuliko fedha. Kitu hicho sio kingine ila akili na nguvu zao. Pakiwa na uongozi unaoona mbali na mbele na unaojua kutumia akili na nguvu hizo na kuwekeza fedha kidogo Watanzania kama watu wengine wana nafasi ya kufanya maajabu mbalimbali duniani.
Serikali kuu na serikali za mitaa zitatakiwa kutoa ushirikiano maalum ili kufanikisha azma hii.
Tofauti na mambo mengine, ningelipendekeza kazi hii ipewe umuhimu wa juu hata machoni kwa watu wa nje wanaotaka kuisadia nchi yetu katika masuala ya utunzaji mazingira na usafi.
Kinachopendekezwa hapa ni kuachana na utitiri wa magari na matrekta mabovu katika kazi ya kukusanya na kusomba taka kuzipeleka huko zinakotupwa. Badala yake kutoa ajira pana na za kudumu kwa kina vijana wetu wenye matoroli, maguta, pikipiki, vipawatila, bajaji, mikokoteni na wilibaroo kufanya kazi ya kukusanya taka mitaani na kwenda kutupwa kwenye eneo maalum litakalokuwa na shimo kubwa la kutupwa taka zilizotenganishwa kiaina na kiufundi na kisha kuchakatwa hadi kuzalishwa bidhaa mpya inayoweza kutumika majumbani, viwandani na mashambani.
Umuhimu wa serikali kuu na serikali za mitaa ni katika kupatikana kwa maeneo maalum ya kuchimbwa mashimo hayo mitaani au kwenye kata; ujenzi wa miundo mbinu rahisi ya kukokotosha taka kuwa bidhaa hitajika; kuwaandaa vijana kimafunzo tayari kwa kazi za kutenganisha taka na kuzibeba kwenda kwenye maeneo husika; na kuhakikisha bajeti ya usafi toka serikalini na misaada ya wafadhili inaelekezwa kwenye mambo haya badala ya kuliwa na wajanja wachache huko walipo.
Italazimu pia kwa viongozi na maofisa wote wa jiji na katika wizara husika, ambao wameomba kupewa hisa na chochote na wawekezaji katika miradi mipya tarajiwa ya kurejelea taka kupewa ruhusa maalum na serikali kuu ya kuwekeza kwenye makampuni bila kutoa chochote !
Aidha wanajamii kwa kushirikiana na serikali kuu na za mitaa watapaswa kuwa na kisima cha maji kilichochimbwa kwenye eneo au kina ambacho maji hayakauki kamwe ili kuhakikisha mji unakuwa na mandhari nzuri na ya kuvutia wakati wote. Maji hayo pia yatatumika kusaidia kazi za kupooza na kulainisha bidhaa katika kituo kikuu cha kubadili taka kuwa mali na utajiri. Ndoto ya kuwa na mifumo mizuri ya kuvuna mvua itakuwa ziada ambayo si mbovu katika hili.
Kila nyumba italazimika kupatiwa pipa pacha nne au kwa maneno mengine pipa ambalo lina sehemu nne: moja kwa ajili ya kutupwa chupa na glasi: la pili kwa ajili ya kutupwa karatasi: la tatu kwa ajili ya kutupwa mabaki ya vyakula na la mwisho kwa ajili ya kutupwa taka ambazo ni hatari kwa afya ya binadamu na taka mchanganyiko nje ya hizo hapo juu.
Vijana wakusanyaji watafunzwa jinsi ya kuzihamisha taka hizo toka mapipa hayo kwenda mifuko maalum ambayo itachukua taka kwa mpangilio huo huo huo na kuzipeleka kwenye kituo kikuu cha taka kwenye mtaa au kata kwa ajili ya kurejelewa upya kuzalisha kinachowezekana kuzalishwa.
Zitakapofikishwa kituoni hapo taka zitakuwa tayari zimetenganishwa kwa utaratibu huo hapo juu na hivyo kuingizwa kwenye moja kwa moja kwenye eneo zitakazofanyiwa kazi ili kuzalisha umeme au kutoa bidhaa fulani itakayotumika kama bidhaa mpya tena madukani au sokoni. Mabaki ya vyakula yanatarajiwa kutengenezwa kuwa mbolea asili isiyo na dawa yoyote ambayo itauzwa kwenye mifuko maalum kwa wakulima na watunza bustani.
Watumishi wizara ya ardhi wataaswa kwamba ili kuleta uwiano kati ya klutenda dhambai na mema- nchini ni muhimu kwao pamoja na kuuza maeneo wazi kwa mabwanyenye wetu wapya, sasa kutoa maeneo kwa ajili ya uchimbaji mashimo makubwa ya uhifadhi wa taka zitakazochakatwa na kuwa bidhaa mpya au kuzalisha umeme kwa ajili ya faida ya wakazi walio wengi jijini.
Wataalamu wa vyama vya siasa vyenye vijiwe mjini wataombwa wautumie utaalamu huo ili kugeuza vijana wetu toka 'majoblesi alwatani', wababaishaji na kupe wenye sifa za kimataifa kubadilika kwa kukopeshwa mitaji ya kununua toroli, maguta na vifaa kama hivyo ili kuwa wakusanyaji na wabebaji taka watakaoipa heshima mpya jiji la Dar es salaam.
Wataalamu wa kupiga raia mabomu, kuvunja maandamano na mikutano wataombwa kuutumia utaalamu wao ili kuhamasisha kazi ya usombaji taka kila wakati ili pasiwe na taka hata moja mahala popote jijini kwa kasi ile ile ya upigaji mabomu ya machozi wakati wa maandamano ya upinzani, wafuasi wa dini fulani au wafanyakazi au wanafunzi.
Mameneja wa migodi wataaombwa kuazimisha magreda na makatapila kuja kuchimba mashimo hayo katika mitaa au kata mbalimbali jijini kama walivyofanikisha zoezi la uchimbaji mashimo huko Geita, North Mara na Bulyanhulu,kutegemeana na kiwango cha uzalishaji taka katika maeneo husika.
Badala ya kuwa na magari mabovu yanayosafiri umbali mrefu kuokota na kutupa taka sasa vitoroli, mikokoteni, bajaji, guta na pikipiki zitatengenezwa kwa njia ambayo kwazo zitakuwa zikipeleka taka kwenye maeneo hayo yenye mashimo na miundo mbinu maalum ya kupokea taka zilizotenganishwa na kuanza kuzifanyia mchakato ili zitoe bidhaa za aina mbalimbali na kuzalisha umeme na vitu vingine vitakavyowezekanika.
Taka zinazohitaji kutupwa mbali zitachukuliwa na magari makubwa maalum machache lakini yenye kiwango cha kimataifa kwenda kutupwa mbali kabisa na makazi ya watu na wakati mwingine hata kwenda kufukia mashimo yaliyotokana na kuchimbwa madini yetu katika mikoa ya kaskazini na kusini.
Ukiutazama mtiririko huu mzima utagundua kuwa pendekezo hili lina shabaha ya kugeuza taka kuwa mali kwa namna kadhaa. Kwanza, vijana ambao wana tatizola ajira itabidi sasa wakimbie ajira wao wenyewe. Taka zitageuka fumba na kufumbua mali, maana kila mzigo kutegemeana na aina yake utakuwa ukilipwa fedha nzuri tu mara ukifika kwenye kituo kikuu cha kuchakata taka kwenye mtaa au kata.
Aidha magari mabovu ya kusomba taka amabyo wakati mwingine badala ya kusafisha mji huuchafua yatatoweka. Takataka hizo zitazaa bidhaa ambazo wafanyabiashara na wanunuzi watanufaika kwani zina uwezekano mkubwa wa kuwa za bei rahisi zaidi kuliko nyinginezo. Kisha mbolea itakayozalishwa itakwenda kuzistawisha bustani za Ikulu na Mnazi mmoja na maeneo mengine mjini na hivyo kulipa jiji mandhari ya kukata na shoka kwa uzuri wake. Hali kadhalika, sio tu tatizo la kukatikakatika umeme jijini litakuwa historia bali mradi huu utahakikisha hata nyumba mbavu za mbwa zilizo mabondeni zinapata umeme wa kutosha na wa uhakika kila siku.
Vilevile visima vitakavyoendana na mradi huu vitawahakikishia wakazi wa kila mtaa na kata upatikanaji maji masafi ya uhakika wakati wote, wakati wanasubiri maajabu yatakayofanywa na DAWASCO miaka mitano au kumi ijayo kama bado wako hai. Hili linawezekana, cheza nafasi yako na timiza wajibu wako. Miaka hamsini baada ya uhuru hutakiwi kushindwa na jambo hili.
Wakati ninaandika makala haya watafiti wanaonisaidia wameleta habari kwamba kuna watu tayari wameanza kujituma wenyewe na kuanzisha miradi kama hii. Kama hili ni kweli basi wilaya, mkoa na wizara husika zichangamkie mara moja jambo hili. NIna hakika likipata kuungwa mkono nao ni kitu kinachowezekana na kitakalolifanya jiji la Dar es salaam kuwa jiji la kuigwa na miji mingine sio tu Tanzania bali Afrika nzima.
lle tabia ya kujifanya kuwa serikali inaweza kufanya kila kitu si kitu kizuri. Na katika miaka hii ni kitu kilichopitwa na wakati na kuwazaini wananchi huku tukijua fika tunasema uongo. Kweli Watanzania hawana fedha, yaani, ni maskini. Lakini Watanzania wana kitu kimoja ambcho thamani yake wakati mwingine ni kubwa kuliko fedha. Kitu hicho sio kingine ila akili na nguvu zao. Pakiwa na uongozi unaoona mbali na mbele na unaojua kutumia akili na nguvu hizo na kuwekeza fedha kidogo Watanzania kama watu wengine wana nafasi ya kufanya maajabu mbalimbali duniani.
Thursday, November 17, 2011
Muswada wa katiba na hatima ya nchi yetu...
AKIZUNGUMZIA uwezekano wa kuandikwa katiba mpya ya Tanzania kwa mara yake ya kwanza, Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti na mwanachama wa Chama kimojawapo cha siasa nchini Tanzania, CCM, Bwana Jakaya Kikwete pamoja na mambo mengine alionesha kutamani sana kwamba katiba itakayoandikwa iweze kutufaa kwa miaka 50 kama sio 100. Hata hivyo, kile kilichowasilishwa na Waziri wake wa katiba hakikufanana kabisa na matamanio mema yake hayo.
Tofauti na msimamo huu wa mheshimiwa Rais, muswada wa serikali yake kwa bunge la Jamhuri ulidhihirisha nia ya serikali ya Chama cha Mapinduzi kuitumia fursa hiyo ili iweze kujikita vyema zaidi nchini kwa halali au haramu kisiasa kwa kuwatumia wabunge wao ambao ilionekana kama walishapewa mafunzo maalum kuhusu kinachotegemewa kutoka kwao.
Pamoja na spika wa bunge hilo kudai kwamba wanaharakati, wapinzani na waandishi wa habari wanapotosha kilicho mezani mwa wabunge, kazi nzuri ya uchambuzi wa kina iliyofanywa na Mheshimiwa Tundu Lissu (CHADEMA) ilionesha kulikuwa na uwezekano mkubwa wa wabunge wa CCM kutokuwa wameusoma muswada huo na Tundu akawa anapigia gitaa mbuzi.
Pengine wabunge wa CCM walishaambiwa kwamba ni lazima upite kama ulivyo na hakuna aliyesumbuka kuusoma kikwelikweli, lakini baadaye ilidhihirika waziwazi kwamba muswada huo ulikuwa na udhaifu mkubwa na kasoro nyingi za kimaudhui, kisheria, kisiasa na kikanuni kikatiba ambao kwa watunga sheria makini lazima wangelihitaji muda wa ziada wa kuufanyia kazi na sio kama wenzetu walivyoanza kuchangia wakiwa na uelewa 'finyu kiuzalendo' kwa kazi iliyokwa mbele yao.
Sio siri kwamba CCM inachokitaka pengine ni kujihakikishia uzima wa milele. Kitu ambacho hakiwezekani. Na haitawezekana kwa sababu hizi si zama za Nyerere, Mkapa na Mwinyi na chochote kinaweza kutokea kwa watu ambao hali ya uchumi inawawia ngumu kila kukichwa, mali asili zao zinatwaliwa bure, watu wanauawa na kubakwa migodini na wakubwa wanapora fedha, wanyama pori, miti, ardhi na rasilimali nyingine kwa jinsi wanavyotaka. Na wasichonacho wananyang'anywa hata kile kidogo walicho nacho, wakati wenye nacho wanazidi kuongezewa kila siku.
Watanzania hawatakaa wasahau kwamba kunako mwezi Novemba, mwaka 2011 baadhi ya wabunge wao kupitia CCM walipoteza fursa ya kipekee katika kuutanguliza Utanzania mbele ya nafsi na uchama wao. Matokeo ya ubinafsi na uchama wao yakawapotezea fursa hii adhimu ambayo ingeliwaweka pazuri sana katika historia ya nchi yao na watu wake.
Kilichotokea ni kwa wabunge hao wa CCM-CUF kuonesha dhahiri kuwa ni mbwa-mwitu (wawakilishi wa chama na serikali) waliovaa ngozi ya kondoo (wawakilishi wa wananchi). Kipaumbele siku hiyo hakikupewa wananchi na vizazi vyao vijavyo bali chama, matashi yake na ubinafsi wa wabunge hata kama Watanzania kwa ujumla wao watapoteza kikubwa zaidi siku zijazo.
UCCM na UCUF kwa kiasi fulani katika hili umewafanya wengi waamini kuwa wabunge wa vyama hivyo wanastahili kupata shahada ya udaktari katika uchama, usisi, umimi na katika mapambano ya maslahi na maendeleo ya wabunge binafsi.
Kwa maneno mengine, wabunge wa CCM na CUF walikuwa wakituambia kwamba vyama vyao na uongozi wa chama chao ni muhimu kuliko Utanzania wetu au utaifa wetu, watu wetu na vizazi vyetu vijavyo.
Kubwa zaidi ni lile la spika, muwakilishaji muswada na wabunge wa CCM waliochangia muswada huo kusingizia eti kuna urongo, uzushi, upotoshaji na tafsiri mbovu ya kile kilichotakiwa kuwakilishwa. Haraka aliyokuwa nayo spika, wabunge wa CCM kuchangia na mwasilisha muswada na wenzake kuliacha maswali mengi kuliko majibu. Mwisho wa siku kilio cha spika, muwasilisha mada na wabunge wa CCM na CUF kilifanana na kile kilio cha mchunga kondoo aliyekuwa akisumbua wanakijiji wenzake kwa kupiga mayowe ya MBWA MWITU, MBWA MWITU kumbe yote ilikuwa ni mzaha kama sio urongo.
Uzaini wa CCM wa kujionesha eti wana CCM na viongozi wao wanaipenda na wana uchungu sana na Tanzania kuliko watu wengine umewafanya jamaa hao kuangukia pua katika siku ambayo wengi wao hawataiashau na wao wenyewe wameamua kujizika kihistoria.
CCM na wakewenza Unguja
Baya zaidi ni lile la muswada huo kudiriki kuifanya Zanzibar kuwa sawasawa na Tanganyika isiyopo katika kuamua hatima ya nchi yetu na watu wake. Hiki ni kitendo cha waendesha utumwa, kikoloni, kibabe, kihuni na cha kidhalimu ambacho hakistahili kukubalika.
Kwani nia ya kuwapa ukubwa huu Wazanzibari wasiostahili kuupata ni kurahisisha siasa ndani ya CCM kati ya Wazanzibari na Wabara. Kwa maneno mengine, CCM imediriki kuwauza Watanganyika kwa Wazanzibari, kama walivyouza migodi ya dhahabu, ili mradi tu mambo yao yawe safi.
Ukewenza Zanzibar na Serikali ya JMT, unatuweka pabaya kitamathali na kiuyakinifu kwa kiasi cha eti watu asilimia 2 Tanzania kuamua hatima ya asilimia 98 iliyobakia.
Kwa maneno mengine, muswada huo unawageuza Wazanzibar wakoloni na Watanganyika watawaliwa katika nchi yao wenyewe. Sijui hata kama muswada huo utapita kama hili litakaa likubalike kesho na keshokutwa.
Hadhi ya Zanzibar kiukweli haina tofauti na ya mkoa wowote bara. Tofauti tu ni kuwa mikoa inabanwa kuwa huru kisiasa, kijamii na kiuchumi kwa mafaniko yake makubwa na haraka zaidi. Kilichokosekana ni uamsho kwa wakazi mikoani na uadilifu kwa serikali kuipa mikoa serikali huru zinazosimamiwa na waziri mkuu wa mkoa, baraza la mawaziri wa mkoa na wawakilishi wa mkoa na mikoa mingi tu ingeiacha Zanzibar nyuma kimaendeleo, bila ya visiwa hivyo kuona hata indiketa za mikoa hiyo kwenye mbio za ustawi wa jamii na maendeleo ya mkoa.
Itakuwa ni jambo la fedheha kama wabunge na serikali yetu baada ya kushindwa kuafikiana na wapinzani wa kweli ndani ya bunge itakuja kufanza hivyo kwa kupata shinikizo toka Marekani na EU. Jambo hili litaonesha kwamba viongozi wetu hawajaiva wala kukomaa na hakika hawastahili kuiongoza nchi hii kama kweli tunataka kuendelea na umoja na amani tuliyo nayo hivi leo. Kinachoonekana hapa ni kwamba kuna Watanzania wenye akili na uwezo mkubwa tu lakini kwa kukosa uongozi adilifu na mzuri wanashindwa kuwatumia.
Viongozi wa dini
Viongozi wa dini kama ilivyokuwa kwa wenzetu nchini Kenya wana mchango mkubwa katika kuhakikisha Tanzania inakuwa na katiba nzuri na safi na itakayowafaa Watanzania kwa muda mrefu kuliko hii ya kupandikizwa ilivyotsukuma sukuma.
Yapo mambo kadhaa ambayo viongozi wa dini wanaowatakia Watanzania na vizazi vyao amani na umoja wanaweza kuhoji na kutoa mwongozo yaende vipi kwa faida ya watu wote. Mathalani, hivi leo kanisa katoliki linafanya vizuri sana katika elimu na sekta ya afya, lakini siasa za uziwi na upofu zinaweza kuhujumu haya yote kama katiba isipohifadhi sheria na haki muhimu za kulinda kanisa, mali zake na viongozi wake. Misikiti na Makanisa yakikaa nyuma, viongozi wa dini wasije anza kulalama baadaye kwamba katiba imewapendelea hawa, au kuwaonea hawa.
Makampuni na taasisi na katiba
Makampuni na taasisi kisheria ni sawa na mtu au raia. Makampuni na taasisi zikikaa nyuma na kutokushiriki kwenye mchakato wa katiba mpya yapo masuala mengi yanayoweza kuja kuzuka baadaye kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni yakaya kuwa ni kwa hasara kubwa kwa upande wao.
Katika suala hili lal katiba mpya sisi sote ni wadau na washiriki na hakuna anayestahili kubakia kuwa mtazamaji tu au juu ya wenzake kwa namna yoyote ile.
Muswada huu kama ilivyokuwa kwa miswaada mingine dhaifu, inayovuja na dhalimu kwa wananchi na vizazi vijavyo, imedhirisha mapungugu mengi mengine katika muundo, mifumo na taratibu zetu za uongozi na uendeshaji nchi. Baadhi ya kasoro hizi ni pamoja na hatari ya kuwa na wabunge wa kuteuliwa badala ya kuchaguliwa kwenye bunge la kiwakilishi; jinsi ambavyo serikali iliyoko madarakani inaweza ikapora mamlaka na madaraka ya wananchi na kufanya mapinduzi ya kikatiba bila kuwajibishwa ipasavyo; muungano unavyozidi kuonekana kukosa maana kwa Watanganyika na kuwa mzigo usiobebeka; na ule ukweli kuwa nchi bado imo kizani na haijajaliwa kuwa na kiongozi na wanasiasa wanaoweza kututoa kwenye shimo refu la giza ambalo tumejikuta tumo leo.
Pepe: sammy.makilla@columnist.com
Tofauti na msimamo huu wa mheshimiwa Rais, muswada wa serikali yake kwa bunge la Jamhuri ulidhihirisha nia ya serikali ya Chama cha Mapinduzi kuitumia fursa hiyo ili iweze kujikita vyema zaidi nchini kwa halali au haramu kisiasa kwa kuwatumia wabunge wao ambao ilionekana kama walishapewa mafunzo maalum kuhusu kinachotegemewa kutoka kwao.
Pamoja na spika wa bunge hilo kudai kwamba wanaharakati, wapinzani na waandishi wa habari wanapotosha kilicho mezani mwa wabunge, kazi nzuri ya uchambuzi wa kina iliyofanywa na Mheshimiwa Tundu Lissu (CHADEMA) ilionesha kulikuwa na uwezekano mkubwa wa wabunge wa CCM kutokuwa wameusoma muswada huo na Tundu akawa anapigia gitaa mbuzi.
Pengine wabunge wa CCM walishaambiwa kwamba ni lazima upite kama ulivyo na hakuna aliyesumbuka kuusoma kikwelikweli, lakini baadaye ilidhihirika waziwazi kwamba muswada huo ulikuwa na udhaifu mkubwa na kasoro nyingi za kimaudhui, kisheria, kisiasa na kikanuni kikatiba ambao kwa watunga sheria makini lazima wangelihitaji muda wa ziada wa kuufanyia kazi na sio kama wenzetu walivyoanza kuchangia wakiwa na uelewa 'finyu kiuzalendo' kwa kazi iliyokwa mbele yao.
Sio siri kwamba CCM inachokitaka pengine ni kujihakikishia uzima wa milele. Kitu ambacho hakiwezekani. Na haitawezekana kwa sababu hizi si zama za Nyerere, Mkapa na Mwinyi na chochote kinaweza kutokea kwa watu ambao hali ya uchumi inawawia ngumu kila kukichwa, mali asili zao zinatwaliwa bure, watu wanauawa na kubakwa migodini na wakubwa wanapora fedha, wanyama pori, miti, ardhi na rasilimali nyingine kwa jinsi wanavyotaka. Na wasichonacho wananyang'anywa hata kile kidogo walicho nacho, wakati wenye nacho wanazidi kuongezewa kila siku.
Watanzania hawatakaa wasahau kwamba kunako mwezi Novemba, mwaka 2011 baadhi ya wabunge wao kupitia CCM walipoteza fursa ya kipekee katika kuutanguliza Utanzania mbele ya nafsi na uchama wao. Matokeo ya ubinafsi na uchama wao yakawapotezea fursa hii adhimu ambayo ingeliwaweka pazuri sana katika historia ya nchi yao na watu wake.
Kilichotokea ni kwa wabunge hao wa CCM-CUF kuonesha dhahiri kuwa ni mbwa-mwitu (wawakilishi wa chama na serikali) waliovaa ngozi ya kondoo (wawakilishi wa wananchi). Kipaumbele siku hiyo hakikupewa wananchi na vizazi vyao vijavyo bali chama, matashi yake na ubinafsi wa wabunge hata kama Watanzania kwa ujumla wao watapoteza kikubwa zaidi siku zijazo.
UCCM na UCUF kwa kiasi fulani katika hili umewafanya wengi waamini kuwa wabunge wa vyama hivyo wanastahili kupata shahada ya udaktari katika uchama, usisi, umimi na katika mapambano ya maslahi na maendeleo ya wabunge binafsi.
Kwa maneno mengine, wabunge wa CCM na CUF walikuwa wakituambia kwamba vyama vyao na uongozi wa chama chao ni muhimu kuliko Utanzania wetu au utaifa wetu, watu wetu na vizazi vyetu vijavyo.
Kubwa zaidi ni lile la spika, muwakilishaji muswada na wabunge wa CCM waliochangia muswada huo kusingizia eti kuna urongo, uzushi, upotoshaji na tafsiri mbovu ya kile kilichotakiwa kuwakilishwa. Haraka aliyokuwa nayo spika, wabunge wa CCM kuchangia na mwasilisha muswada na wenzake kuliacha maswali mengi kuliko majibu. Mwisho wa siku kilio cha spika, muwasilisha mada na wabunge wa CCM na CUF kilifanana na kile kilio cha mchunga kondoo aliyekuwa akisumbua wanakijiji wenzake kwa kupiga mayowe ya MBWA MWITU, MBWA MWITU kumbe yote ilikuwa ni mzaha kama sio urongo.
Uzaini wa CCM wa kujionesha eti wana CCM na viongozi wao wanaipenda na wana uchungu sana na Tanzania kuliko watu wengine umewafanya jamaa hao kuangukia pua katika siku ambayo wengi wao hawataiashau na wao wenyewe wameamua kujizika kihistoria.
CCM na wakewenza Unguja
Baya zaidi ni lile la muswada huo kudiriki kuifanya Zanzibar kuwa sawasawa na Tanganyika isiyopo katika kuamua hatima ya nchi yetu na watu wake. Hiki ni kitendo cha waendesha utumwa, kikoloni, kibabe, kihuni na cha kidhalimu ambacho hakistahili kukubalika.
Kwani nia ya kuwapa ukubwa huu Wazanzibari wasiostahili kuupata ni kurahisisha siasa ndani ya CCM kati ya Wazanzibari na Wabara. Kwa maneno mengine, CCM imediriki kuwauza Watanganyika kwa Wazanzibari, kama walivyouza migodi ya dhahabu, ili mradi tu mambo yao yawe safi.
Ukewenza Zanzibar na Serikali ya JMT, unatuweka pabaya kitamathali na kiuyakinifu kwa kiasi cha eti watu asilimia 2 Tanzania kuamua hatima ya asilimia 98 iliyobakia.
Kwa maneno mengine, muswada huo unawageuza Wazanzibar wakoloni na Watanganyika watawaliwa katika nchi yao wenyewe. Sijui hata kama muswada huo utapita kama hili litakaa likubalike kesho na keshokutwa.
Hadhi ya Zanzibar kiukweli haina tofauti na ya mkoa wowote bara. Tofauti tu ni kuwa mikoa inabanwa kuwa huru kisiasa, kijamii na kiuchumi kwa mafaniko yake makubwa na haraka zaidi. Kilichokosekana ni uamsho kwa wakazi mikoani na uadilifu kwa serikali kuipa mikoa serikali huru zinazosimamiwa na waziri mkuu wa mkoa, baraza la mawaziri wa mkoa na wawakilishi wa mkoa na mikoa mingi tu ingeiacha Zanzibar nyuma kimaendeleo, bila ya visiwa hivyo kuona hata indiketa za mikoa hiyo kwenye mbio za ustawi wa jamii na maendeleo ya mkoa.
Itakuwa ni jambo la fedheha kama wabunge na serikali yetu baada ya kushindwa kuafikiana na wapinzani wa kweli ndani ya bunge itakuja kufanza hivyo kwa kupata shinikizo toka Marekani na EU. Jambo hili litaonesha kwamba viongozi wetu hawajaiva wala kukomaa na hakika hawastahili kuiongoza nchi hii kama kweli tunataka kuendelea na umoja na amani tuliyo nayo hivi leo. Kinachoonekana hapa ni kwamba kuna Watanzania wenye akili na uwezo mkubwa tu lakini kwa kukosa uongozi adilifu na mzuri wanashindwa kuwatumia.
Viongozi wa dini
Viongozi wa dini kama ilivyokuwa kwa wenzetu nchini Kenya wana mchango mkubwa katika kuhakikisha Tanzania inakuwa na katiba nzuri na safi na itakayowafaa Watanzania kwa muda mrefu kuliko hii ya kupandikizwa ilivyotsukuma sukuma.
Yapo mambo kadhaa ambayo viongozi wa dini wanaowatakia Watanzania na vizazi vyao amani na umoja wanaweza kuhoji na kutoa mwongozo yaende vipi kwa faida ya watu wote. Mathalani, hivi leo kanisa katoliki linafanya vizuri sana katika elimu na sekta ya afya, lakini siasa za uziwi na upofu zinaweza kuhujumu haya yote kama katiba isipohifadhi sheria na haki muhimu za kulinda kanisa, mali zake na viongozi wake. Misikiti na Makanisa yakikaa nyuma, viongozi wa dini wasije anza kulalama baadaye kwamba katiba imewapendelea hawa, au kuwaonea hawa.
Makampuni na taasisi na katiba
Makampuni na taasisi kisheria ni sawa na mtu au raia. Makampuni na taasisi zikikaa nyuma na kutokushiriki kwenye mchakato wa katiba mpya yapo masuala mengi yanayoweza kuja kuzuka baadaye kisiasa, kijamii, kiuchumi na kiutamaduni yakaya kuwa ni kwa hasara kubwa kwa upande wao.
Katika suala hili lal katiba mpya sisi sote ni wadau na washiriki na hakuna anayestahili kubakia kuwa mtazamaji tu au juu ya wenzake kwa namna yoyote ile.
Muswada huu kama ilivyokuwa kwa miswaada mingine dhaifu, inayovuja na dhalimu kwa wananchi na vizazi vijavyo, imedhirisha mapungugu mengi mengine katika muundo, mifumo na taratibu zetu za uongozi na uendeshaji nchi. Baadhi ya kasoro hizi ni pamoja na hatari ya kuwa na wabunge wa kuteuliwa badala ya kuchaguliwa kwenye bunge la kiwakilishi; jinsi ambavyo serikali iliyoko madarakani inaweza ikapora mamlaka na madaraka ya wananchi na kufanya mapinduzi ya kikatiba bila kuwajibishwa ipasavyo; muungano unavyozidi kuonekana kukosa maana kwa Watanganyika na kuwa mzigo usiobebeka; na ule ukweli kuwa nchi bado imo kizani na haijajaliwa kuwa na kiongozi na wanasiasa wanaoweza kututoa kwenye shimo refu la giza ambalo tumejikuta tumo leo.
Pepe: sammy.makilla@columnist.com
Tuesday, November 8, 2011
Ndoa isiyo na tija
Ni ndoa yenye ugumba, ndoa isiyo na tija,
Hili sio la kutamba, lataka funga mkaja,
Na wengine hulichamba, wasiache kubwabwaja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ni ndoa yenye ugumba, ndoa isiyo na tija,
Wanandoa hujisomba, wakuja na wasokuja,
Utadhani ni mtumba, hujui aliyeufuja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ndoa ni kitu cha namba, kukua si rejareja,
Yataka mengi kuumba, na sio kwishia moja,
Yataka kujenga nyumba, na pengine kwenda hija,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ndoa sio kama gamba, kuvua halina haja,
Utaonwa ni mshamba, ukabakia mseja,
Ndoa kuvuta kamba, lenu wote kuwa moja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ndoa tamu ya kulamba, ikiwa rojo vioja,
Yataka hali kuvimba, ovyo vitu kutofuja,
Yataka kuvuta kamba, mbele mkajikongoja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Akiba anayekomba, upesi kumvua koja,
Na mtaji anayefuja, ni kumshusha daraja,
Maisha yataka gomba, haikubali harija,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ni ndoa yenye ugumba, ndoa isiyo na tija,
Huhasiri na unyumba, pasiwepo na umoja,
Japo mwafunga vilemba, nje watu hawana haja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Hili sio la kutamba, lataka funga mkaja,
Na wengine hulichamba, wasiache kubwabwaja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ni ndoa yenye ugumba, ndoa isiyo na tija,
Wanandoa hujisomba, wakuja na wasokuja,
Utadhani ni mtumba, hujui aliyeufuja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ndoa ni kitu cha namba, kukua si rejareja,
Yataka mengi kuumba, na sio kwishia moja,
Yataka kujenga nyumba, na pengine kwenda hija,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ndoa sio kama gamba, kuvua halina haja,
Utaonwa ni mshamba, ukabakia mseja,
Ndoa kuvuta kamba, lenu wote kuwa moja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ndoa tamu ya kulamba, ikiwa rojo vioja,
Yataka hali kuvimba, ovyo vitu kutofuja,
Yataka kuvuta kamba, mbele mkajikongoja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Akiba anayekomba, upesi kumvua koja,
Na mtaji anayefuja, ni kumshusha daraja,
Maisha yataka gomba, haikubali harija,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Ni ndoa yenye ugumba, ndoa isiyo na tija,
Huhasiri na unyumba, pasiwepo na umoja,
Japo mwafunga vilemba, nje watu hawana haja,
Ndoa isiyo na tija, ni ndoa yenye ugumba.
Sasa vuta nikuvute
Lazima nchi itwete, na kujakauka mate,
Watajatembea viwete, zikijageuka kete,
Na watu lazima mtote, kwa jasho pia matete,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Hali hii sasa tete, mambo vuta nikuvute,
Watu wataka wapate, si skuzote waote,
Ndoto wazitema mate, na hawataki mfute,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Ahadi kwao uwete, hungoja usiwakute,
Ni puya wazipepete, nafaka wasipukute,
Wengine msinifate, uoga jadi ya wote,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Nakukumbuka Mnete, Ujerumani usinate,
Njoo tuhidi viwete, hata kidogo waokote,
Na neema uilete, misada waipate,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Kila mtu ana kete, ataka naye apate,
Hatoishi kwa mkate, mtu anataka vyote,
Kwa hili msimsute, suteni nafsi zote,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Mtapoenda popote, chunguzeni na mtete,
Ili amani iote, fanaka iwe kwa wote,
Watu lisiwakerekete, la kukosa wao mkate,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Na hata vipi mnyate, gizani vyenu mng'ate,
Bado hudondoka mate, usingizini waote,
Kuteketea si lolote, na umauti ni wa wote,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Naomba yasinikute, nilapo wote niite,
Hata kidogo nipate, tutagawana na wote,
Na Rabana asisite, kichache aje avute,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Utupe leo mkate, peke yetu tusifute,
Na wenzetu waupate, slensi isiwapite,
Baadaye nisijute, kwa ubinafsi nisutwe,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Watajatembea viwete, zikijageuka kete,
Na watu lazima mtote, kwa jasho pia matete,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Hali hii sasa tete, mambo vuta nikuvute,
Watu wataka wapate, si skuzote waote,
Ndoto wazitema mate, na hawataki mfute,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Ahadi kwao uwete, hungoja usiwakute,
Ni puya wazipepete, nafaka wasipukute,
Wengine msinifate, uoga jadi ya wote,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Nakukumbuka Mnete, Ujerumani usinate,
Njoo tuhidi viwete, hata kidogo waokote,
Na neema uilete, misada waipate,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Kila mtu ana kete, ataka naye apate,
Hatoishi kwa mkate, mtu anataka vyote,
Kwa hili msimsute, suteni nafsi zote,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Mtapoenda popote, chunguzeni na mtete,
Ili amani iote, fanaka iwe kwa wote,
Watu lisiwakerekete, la kukosa wao mkate,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Na hata vipi mnyate, gizani vyenu mng'ate,
Bado hudondoka mate, usingizini waote,
Kuteketea si lolote, na umauti ni wa wote,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Naomba yasinikute, nilapo wote niite,
Hata kidogo nipate, tutagawana na wote,
Na Rabana asisite, kichache aje avute,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Utupe leo mkate, peke yetu tusifute,
Na wenzetu waupate, slensi isiwapite,
Baadaye nisijute, kwa ubinafsi nisutwe,
Sasa vuta nikuvute, mtu ataka apate!
Mwvi kamwambia....
Naishangaa dunia, kuja kuumwa mwiibiwa,
Mifuko kanipekua, na mbwa kasakazia,
Mwizi ananiibia, ataka nimalizia?
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Tukio lilipotokea, wala usingedhania,
Jizi kunishambulia, na mbwawe kunivamia,
Ah, jamani ninalia, haki inshakupotea,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Shilingi kazichukua, maumivu kunachia,
Simu nayo kaizoa, na yangu dhahabu saa,
Kila nikifikiria, nazidi kuchanganyikiwa,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Mtu hakujatokea, mie kunisadia,
Kufurukuta haikua, mbwa kuning'atua,
Amtii na kumsikia, chakula anayempatia,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Hii ndiyo yetu dunia, na hizi zake hatua,
Haki viumbe wajua, sasa waweza nunua,
Wenye haki wanagwaya, ndani huja wakatiwa,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Mwivi huru anakua, na kutamba hukutambia,
Hujui utanijua, mpini nashikilia,
Mikono yako nchani, nikivuta hatarini,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Mifuko kanipekua, na mbwa kasakazia,
Mwizi ananiibia, ataka nimalizia?
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Tukio lilipotokea, wala usingedhania,
Jizi kunishambulia, na mbwawe kunivamia,
Ah, jamani ninalia, haki inshakupotea,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Shilingi kazichukua, maumivu kunachia,
Simu nayo kaizoa, na yangu dhahabu saa,
Kila nikifikiria, nazidi kuchanganyikiwa,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Mtu hakujatokea, mie kunisadia,
Kufurukuta haikua, mbwa kuning'atua,
Amtii na kumsikia, chakula anayempatia,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Hii ndiyo yetu dunia, na hizi zake hatua,
Haki viumbe wajua, sasa waweza nunua,
Wenye haki wanagwaya, ndani huja wakatiwa,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Mwivi huru anakua, na kutamba hukutambia,
Hujui utanijua, mpini nashikilia,
Mikono yako nchani, nikivuta hatarini,
Mwivi kamwambia mbwawe, ankamate, antafune!
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
NYIE hawatawafunga, mkifunga wapinzani,
Mbona mnayabananga,hamjui mwajizaini,
Dunia geuzi anga,wajinga hawabaini,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Kutesa kwa zamu ringa, ila ujue yakini,
Wafunge watakufunga, kama haki hukuauni,
Usiombee kimbunga,kikukute mtaani,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Hujatengwa na mtenga, wajua Raskazoni,
Mpingwa huja kupinga, ikawa abautani,
Mgongwa huja kugonga, ujikute hatarini,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Sheria ukizipanga, jua na wewe undani,
Na kanuni ukitunga, jione nawe mpinzani,
Ujapoivaa khanga, usilisahau gauni,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Ukiuchonga mzinga, na nyuki wabaini,
Asali ukenda kinga, kubali na yake faini,
Porini ukenda chunga, simba usiwaamini,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Hukungwa naye mkunga, uzazi hauna dini,
Na mfungwa huja kufunga, Mandela hili aamini,
Ila sidhani kwa mwanga, iweje kuwangiwani?
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Hutwanga mtwanga unga, na hili asibaini,
Nchi yataka waganga, haitaki majinuni,
Nchi yataka kuunga, nyie vipi mwabanduani?
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Mbona mnayabananga,hamjui mwajizaini,
Dunia geuzi anga,wajinga hawabaini,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Kutesa kwa zamu ringa, ila ujue yakini,
Wafunge watakufunga, kama haki hukuauni,
Usiombee kimbunga,kikukute mtaani,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Hujatengwa na mtenga, wajua Raskazoni,
Mpingwa huja kupinga, ikawa abautani,
Mgongwa huja kugonga, ujikute hatarini,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Sheria ukizipanga, jua na wewe undani,
Na kanuni ukitunga, jione nawe mpinzani,
Ujapoivaa khanga, usilisahau gauni,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Ukiuchonga mzinga, na nyuki wabaini,
Asali ukenda kinga, kubali na yake faini,
Porini ukenda chunga, simba usiwaamini,
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Hukungwa naye mkunga, uzazi hauna dini,
Na mfungwa huja kufunga, Mandela hili aamini,
Ila sidhani kwa mwanga, iweje kuwangiwani?
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Hutwanga mtwanga unga, na hili asibaini,
Nchi yataka waganga, haitaki majinuni,
Nchi yataka kuunga, nyie vipi mwabanduani?
Mkiwafunga wapinzani, nao hawatawafunga?
Waziri mkuu wa mkoa....
Nchi haitoendelea, bila mkoa huru kuwa,
Maamuzi kujifanyia, bila ya mtu kungojea,
Na awe nayo raia, sauti ya kusikiwa,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Arusha yasingetokea, leo yanayotokea,
Mkoa unatawaliwa, na chama chenye izaya,
Wajanja walipokwapua, kile wasichojivunia,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Mbeya ukiangalia, chama fulani chafaa,
Kuutawala mkoa, zingeliisha ghasia,
Uchumi wadidimia, king'ang'anizi kung'ang'ania,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Na Mwanzo nako pia, kama haya yatokea,
Uhuru wanalilia, wakazi wake mkoa,
Mambo yao kimkoa, wao wenyewe kuamua,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Wamechoka kuwekewa, viongozi wasofaa,
Na tena sio wazawa, uchungu nao hawajawa,
Angelikuwa mwana kaya, uchumi angelipaua,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Ardhi wanachukua, wa mkoa wasokuwa,
Juu walikokalia, wawekezaji wauzia,
Sasa wanagombania, ardhi kujilindia,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Mali asili tambua, ni ya wakazi wa mkoa,
Haijawa, haitakuwa, ya hao wanaopewa,
Tutaambiana ubaya, haya yakija tokea,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Tuacheni kusinzia, haja za watu kujua,
Muda usijepotea, mabaya kujatokea,
Ama chelewa chelewa, mwana hutomkumbatia!
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Maamuzi kujifanyia, bila ya mtu kungojea,
Na awe nayo raia, sauti ya kusikiwa,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Arusha yasingetokea, leo yanayotokea,
Mkoa unatawaliwa, na chama chenye izaya,
Wajanja walipokwapua, kile wasichojivunia,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Mbeya ukiangalia, chama fulani chafaa,
Kuutawala mkoa, zingeliisha ghasia,
Uchumi wadidimia, king'ang'anizi kung'ang'ania,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Na Mwanzo nako pia, kama haya yatokea,
Uhuru wanalilia, wakazi wake mkoa,
Mambo yao kimkoa, wao wenyewe kuamua,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Wamechoka kuwekewa, viongozi wasofaa,
Na tena sio wazawa, uchungu nao hawajawa,
Angelikuwa mwana kaya, uchumi angelipaua,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Ardhi wanachukua, wa mkoa wasokuwa,
Juu walikokalia, wawekezaji wauzia,
Sasa wanagombania, ardhi kujilindia,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Mali asili tambua, ni ya wakazi wa mkoa,
Haijawa, haitakuwa, ya hao wanaopewa,
Tutaambiana ubaya, haya yakija tokea,
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Tuacheni kusinzia, haja za watu kujua,
Muda usijepotea, mabaya kujatokea,
Ama chelewa chelewa, mwana hutomkumbatia!
Mkoa lazima uwe, na waziri mkuu wake.
Siasa kongwe na nzee
Mbali tuzitupilie, siasa kongwe na nzee,
Kale isituzuzue, tulipo hapo tutue,
Yajayo tutabirie, tupange tufanikiwe,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Hivi sasa tuamue, nani nchi tuwaachie,
Shughuli waifanyie, umaskini waondoe,
Watu watutumie, taifa juu lipae,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Tupumue, tusikae, mchakamchaka uwe,
Usia tukumbukie, baba taifa atoe,
Budi sisi tukimbie, acha wengine watembee,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Batabata tuwatoe, si mwendo watu uwafae,
Hatua tuzichukue, mbiombio tukimbie,
Malengo tuyafikie,dunia itushangae,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Majukumu tuyajue, kisha tushughulikie,
Katu wote tusitue, na wala tusitulie,
Nchi yataka itibiwe, na nafuu ipatiwe,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Matatizo tutatue, Watanzania wapumue,
Mbeleni tusiugue, maradhi yote yatibiwe,
Kivulini tuingie, kama walivyo wengine,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Haki tuizingatie, udikteta uvie,
Ukiritimaba tuue, na uhuru ukomae,
Ubabe tuukatae, na dola isitumiwe,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Sherehe tusherehekee, sio wajisherehekee,
Wananchi chini wasiwe, ila juu watulie,
Dunia iwasifie, wajifunze na wajue,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Kale isituzuzue, tulipo hapo tutue,
Yajayo tutabirie, tupange tufanikiwe,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Hivi sasa tuamue, nani nchi tuwaachie,
Shughuli waifanyie, umaskini waondoe,
Watu watutumie, taifa juu lipae,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Tupumue, tusikae, mchakamchaka uwe,
Usia tukumbukie, baba taifa atoe,
Budi sisi tukimbie, acha wengine watembee,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Batabata tuwatoe, si mwendo watu uwafae,
Hatua tuzichukue, mbiombio tukimbie,
Malengo tuyafikie,dunia itushangae,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Majukumu tuyajue, kisha tushughulikie,
Katu wote tusitue, na wala tusitulie,
Nchi yataka itibiwe, na nafuu ipatiwe,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Matatizo tutatue, Watanzania wapumue,
Mbeleni tusiugue, maradhi yote yatibiwe,
Kivulini tuingie, kama walivyo wengine,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Haki tuizingatie, udikteta uvie,
Ukiritimaba tuue, na uhuru ukomae,
Ubabe tuukatae, na dola isitumiwe,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Sherehe tusherehekee, sio wajisherehekee,
Wananchi chini wasiwe, ila juu watulie,
Dunia iwasifie, wajifunze na wajue,
Siasa kongwe na nzee, zinaturudisha nyuma.
Muungano kama hawa
Kitupu changu kibaba, japo ninaitwa baba,
Wanangu wananikaba, njaa yawapa adhaba,
Nimemlilia toba, naisubiri ratiba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba,
Kiwapi changu kiroba, nyumbani nikakibeba,
Abu, kazi ya bawaba, na mlango haujashiba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Jua njaa yake tiba, si dawa ila kushiba,
Iwe Dovya au Goba, waitaka hii tiba,
Hawaishi kwa ghiliba, utawaumbua msiba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Hata uvae majuba, njaa haina haiba,
Kwa kila mtu ni mwiba, kuzidi kuuziriba,
Na ukizikosa raba, donda huzidi mraba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Unguja si kama Pemba, Tanganyika si kisiwa,
Kukunana ni habiba, kibaba mpe kibaba,
Hukurubisha nasaba, na kuchipuka mahaba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Kazi wote kuzibeba, kubanana na kukaba,
Kutegea si haiba, husababisha msiba,
Wengine hawali riba,kuwaepusha ni toba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Kuukuza uswahiba, lazima wote kushiba,
Tuzieupuke kadhaba, na nyufa kuja ziziba,
Wafanye kazi ngariba, kutahiri waso hiba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Namshukuru Hassaba. hesabu mwenye kutamba,
Atwepushe na ghiliba, ukweli ziwe hutuba,
Pasiwe wanaoiba, wakakwaza ukuruba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Wanangu wananikaba, njaa yawapa adhaba,
Nimemlilia toba, naisubiri ratiba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba,
Kiwapi changu kiroba, nyumbani nikakibeba,
Abu, kazi ya bawaba, na mlango haujashiba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Jua njaa yake tiba, si dawa ila kushiba,
Iwe Dovya au Goba, waitaka hii tiba,
Hawaishi kwa ghiliba, utawaumbua msiba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Hata uvae majuba, njaa haina haiba,
Kwa kila mtu ni mwiba, kuzidi kuuziriba,
Na ukizikosa raba, donda huzidi mraba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Unguja si kama Pemba, Tanganyika si kisiwa,
Kukunana ni habiba, kibaba mpe kibaba,
Hukurubisha nasaba, na kuchipuka mahaba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Kazi wote kuzibeba, kubanana na kukaba,
Kutegea si haiba, husababisha msiba,
Wengine hawali riba,kuwaepusha ni toba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Kuukuza uswahiba, lazima wote kushiba,
Tuzieupuke kadhaba, na nyufa kuja ziziba,
Wafanye kazi ngariba, kutahiri waso hiba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Namshukuru Hassaba. hesabu mwenye kutamba,
Atwepushe na ghiliba, ukweli ziwe hutuba,
Pasiwe wanaoiba, wakakwaza ukuruba,
Muungano ni mahaba, au kula na kushiba?
Kina kabla ya uhuru
Hawa ninawaambia, kabla walozaliwa,
Uhuru kuingia, Tanganyika na Zanzibar,
Tuwatunuku hidaya, ila kuongoza baa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Mtakuwa ni raia, haki zote mtapewa,
Ila kutusimamia, hilo tunalikataa,
Nchi mmeifumua, kushonwa inatakiwa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Vijana wanatakiwa, kompyuta kuzivaa,
Ofisini wakikaa, wajua yanayotokea,
Mizubao na sinzia, kuondoka ni huria,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Twataka wanaojua, uchumi kuutibia,
Isiwe tunaugua, malale na kusinzia,
Hoja kuzichanganua, miradi ije tufaa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
KazI mmeshatufanyia, nchi ni kutuachia,
Ushauri kuutoa, pembeni mmesogea,
Nasi tutawachambulia, Tanzania kuja paa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Wenyewe kujichagua, bila jina kwangalia,
Ujuzi umejaliwa na kazi unaijua,
Ndani utajaingia, ufanye ya manufaa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Barabara kujijengea, hatua tutazichukua,
Reli kukarabatia, msaada si ruia,
Na umeme kusambaa, hiyo kazi ya siku moya,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Maji tutawamiminia, maziwani kuyavua,
Mito tutajihamia, yazidi maji kujaa,
Na misitu kuridhia, wananchi kujilindia,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Ardhi hatutaigawa, kwa wageni bila ubia,
Hati tutatishikilia, hadi kijapo kiyama,
Nani wa kutununua, na sisi wote wazawa?
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Uhuru kuingia, Tanganyika na Zanzibar,
Tuwatunuku hidaya, ila kuongoza baa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Mtakuwa ni raia, haki zote mtapewa,
Ila kutusimamia, hilo tunalikataa,
Nchi mmeifumua, kushonwa inatakiwa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Vijana wanatakiwa, kompyuta kuzivaa,
Ofisini wakikaa, wajua yanayotokea,
Mizubao na sinzia, kuondoka ni huria,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Twataka wanaojua, uchumi kuutibia,
Isiwe tunaugua, malale na kusinzia,
Hoja kuzichanganua, miradi ije tufaa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
KazI mmeshatufanyia, nchi ni kutuachia,
Ushauri kuutoa, pembeni mmesogea,
Nasi tutawachambulia, Tanzania kuja paa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Wenyewe kujichagua, bila jina kwangalia,
Ujuzi umejaliwa na kazi unaijua,
Ndani utajaingia, ufanye ya manufaa,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Barabara kujijengea, hatua tutazichukua,
Reli kukarabatia, msaada si ruia,
Na umeme kusambaa, hiyo kazi ya siku moya,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Maji tutawamiminia, maziwani kuyavua,
Mito tutajihamia, yazidi maji kujaa,
Na misitu kuridhia, wananchi kujilindia,
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Ardhi hatutaigawa, kwa wageni bila ubia,
Hati tutatishikilia, hadi kijapo kiyama,
Nani wa kutununua, na sisi wote wazawa?
Kina kabla ya uhuru, baibai mnapewa!
Kuiba kura mauaji
eri wa mali ni mwizi, wa kura ni muuaji,
Haki anaidarizi, kumpa aso na mji,
Ni msanja wa kunazi, haubebi hata maji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Anamzidi jambazi, kura anayezifoji,
Si mthamini kizazi, huyu wa wazi mkabaji,
Anajal imatanuzi, na ukubwa kuuhiji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Hana radhi ya mazi, huyu ni mgeuzaji,
Na kinyesi na ushuzi, kwake yeye upambaji,
Ukilifanya fumanizi, usiache utekaji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Ni gunia la viazi, lisilo na mbebaji,
Kunyanyuka haliwezi, hadi aje mchukuaji,
Ni chombo kisicho kazi, kutupwa ni mataraji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Tabia yake ushenzi, hata ikiwa ya jaji,
Huuzwa kwa manunuzi, haki tusijeitaraji,
Ni mbegu za maangamizi, hazifanzi uokoaji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Havistahi makuzi, ni kama mnenguaji,
Kiuno bila shimizi, ndio chazidi kuchaji,
Na ya jana sio juzi, hautaivaa beji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Kibirizi, kibirizi, mlinzi na mauaji,
Hili ni kama jinamizi, kuponya linahitaji,
Na usalama si wizi, kama hivyo hatuuhitaji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Utu sio sisimizi, watu viumbe hojaji,
Usitumiwe kama ngazi, kesho haitakufariji,
Kama umekosa kazi, kwingine tafuta mtaji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Haki anaidarizi, kumpa aso na mji,
Ni msanja wa kunazi, haubebi hata maji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Anamzidi jambazi, kura anayezifoji,
Si mthamini kizazi, huyu wa wazi mkabaji,
Anajal imatanuzi, na ukubwa kuuhiji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Hana radhi ya mazi, huyu ni mgeuzaji,
Na kinyesi na ushuzi, kwake yeye upambaji,
Ukilifanya fumanizi, usiache utekaji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Ni gunia la viazi, lisilo na mbebaji,
Kunyanyuka haliwezi, hadi aje mchukuaji,
Ni chombo kisicho kazi, kutupwa ni mataraji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Tabia yake ushenzi, hata ikiwa ya jaji,
Huuzwa kwa manunuzi, haki tusijeitaraji,
Ni mbegu za maangamizi, hazifanzi uokoaji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Havistahi makuzi, ni kama mnenguaji,
Kiuno bila shimizi, ndio chazidi kuchaji,
Na ya jana sio juzi, hautaivaa beji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Kibirizi, kibirizi, mlinzi na mauaji,
Hili ni kama jinamizi, kuponya linahitaji,
Na usalama si wizi, kama hivyo hatuuhitaji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Utu sio sisimizi, watu viumbe hojaji,
Usitumiwe kama ngazi, kesho haitakufariji,
Kama umekosa kazi, kwingine tafuta mtaji,
Kuiba mali ni wizi, kuiba kura mauaji!
Siasa na umafia
Yabadilika dunia, na ujanja unakua,
Ili kutokudhaniwa, jambazi polisi hua,
Vigumu kutuhumiwa, wadhifa anaopewa,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Padri ukishakua, nani atakudhania,
Zinaa ukiingia, na uchafu kukujaa,
Wengine watashukiwa, salama utabakia,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Ustadhi ukishakua, mcha Mungu wakujua,
Uovu ukipania, gizani hawatajua,
Siri utajifichia, hadi zizidi tamaa,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Na siasa nazo pia, upupu zinachukua,
Fikra zazidi via, nani anayefikiria,
Roboti utadhaia, wanayozungumzia,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Watu wasio ulua, fani wameivamia,
Kuiba waazimia, ni nani atawajua ?
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Uongozi wakikwaa, ganzi wameshajipatia,
Mbwa mwitu hujavaa, ngozi ya kondoo mliwa,
Kundini wakishaingia, kazi yao kutanua,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Wanono watajilia, tena kimya kimya,
Hakuna atayejua, hadi mtu kufichua,
Ila taifa huvia, na kuzidi kusinyaa,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Na vyama vyajatokea, udokozi kuulea,
Hazina kujaingia, kila kitu kupakua,
Pasiwe cha kubakia, ilo mifupa masalia,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Ili kutokudhaniwa, jambazi polisi hua,
Vigumu kutuhumiwa, wadhifa anaopewa,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Padri ukishakua, nani atakudhania,
Zinaa ukiingia, na uchafu kukujaa,
Wengine watashukiwa, salama utabakia,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Ustadhi ukishakua, mcha Mungu wakujua,
Uovu ukipania, gizani hawatajua,
Siri utajifichia, hadi zizidi tamaa,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Na siasa nazo pia, upupu zinachukua,
Fikra zazidi via, nani anayefikiria,
Roboti utadhaia, wanayozungumzia,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Watu wasio ulua, fani wameivamia,
Kuiba waazimia, ni nani atawajua ?
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Uongozi wakikwaa, ganzi wameshajipatia,
Mbwa mwitu hujavaa, ngozi ya kondoo mliwa,
Kundini wakishaingia, kazi yao kutanua,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Wanono watajilia, tena kimya kimya,
Hakuna atayejua, hadi mtu kufichua,
Ila taifa huvia, na kuzidi kusinyaa,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Na vyama vyajatokea, udokozi kuulea,
Hazina kujaingia, kila kitu kupakua,
Pasiwe cha kubakia, ilo mifupa masalia,
Watu kinachoibia, si chama hao 'mafia.'
Monday, November 7, 2011
Vyama vya kisiasa Tanzania vimepitwa na wakati ? Sehemu- I
MABADILIKO yanayotokea duniani yanawawia vigumu vikongwe wa kisiasa kuyaelewa na kuyatafsiri katika mtazamo na macho ya ulimwengu wa sasa. Kama ilivyo kawaida kwa mwanadamu hatua za kwanza wanazochukua ni kupambana ili kuzuia mabadaliko hayo yasijiri makwao.
Haijawahi kutokea katika nchi yoyote ile duniani kwa mabadiliko makubwa ya kisiasa, kiuchumi na kijamii kufanyika kirahisi na bila kuwa na upinzani mkali, mkubwa na wa kutisha toka kwa wattu waoga, mbumbu, wasiojua kinachoendelea, wanaonufaika na mfumo wa hali iliyopo au wale wanaotumiwa na wanaonufaika kuwalinda wao na mali zao.
Ninasema vyama vya siasa Tanzania vimepitwa na wakati kwa sababu kile kilichozoea ukiritimba wa mfumo wa chama kimoja kinajiendesha kama wito na kazi yake kuu ni kupambana na wale wanaotaka kife; wakati wale wa iwezekanayo kuwa serikali mbadala na katika mfumo ambao si tofauti sana na wa chama kimoja katika mambo mengi, wanajiendesha kama vile kazi yao kubwa ni kuja kuingia madarakani kwa udi na uvumba. Hakuna kati yao ambaye anatoa uzito stahilifu kwa matatizo na changamoto za wananchi. Na kwa maana hii sio tu ninaona vimepitwa na wakati bali ninadhani vyama vyote havistahili hata kuwepo na nchi imekosa tu watu wanaoweza kuthubutu kuvifagia pembeni hata kabla ya uchaguzi mkuu ujao.
Mabadiliko ambayo Tanzania inastahili kuyafanya hivi sasa hayana tofauti kwa namna yoyote ile na mabadiliko mengine kama hayo yanayotokea kwingine duniani na yaliyokwishatokea pengine na katika karne nyingine huko nyuma yetu.
Tofauti tu iliyopo hivi sasa ni kuwa sisi kama watu mmoja mmoja na kitaifa hatujajipanga ipasavyo kuweza kuhakikisha kuwa mabadiliko hayo yanatokea kwa faida na manufaa yetu na sio kwa ujibari, ujivuni, kisirani na hasara kwa upande wetu.
Na katika hili kiongozi mkuu wa kujipanga kuyakabili mabadiliko anatakiwa awe ni chama cha kisiasa cnenye viongozi wanaojua watu wanataka kuelekea wapi, nchi inaelekea wapi, duniani inaelekea wapi, nani wanastahili kuwa rafiki zetu na nani hatustahili kuwaamini, kuwathamini na kuwaingiza katika siri na mambo yetu mengine.
Ni chama kinachostahili kuwa na mipango, mikakati, sera, muundo, mfumo, taratibu na kanuni za utekelezaji zinazokipa chama ukuu na nguvu juu ya mwanachama mmoja mmoja au kundi la wanachama fulani ndani ya chama husika katika mustakabali wa kujenga umoja wa chama lakini ndani ya mfumo wa demokrasia hai na inayofanya kazi. Ugonjwa wa 'ndivyotunavyofikiri' ukiachiwa kutambaa kwenye mwili-siasa wa jamii hivi leo ni dhahiri maradhi makubwa zaidi yatajitokeza na kupona kwa mgonjwa kutahitaji manabii na miujiza.
Ni chama ambacho kina 'visheni' na 'misheni' bayana ambazo wanaokiongoza hata wakikurupushwa usingizini wanavikariri bila kukosea hata neno moja.
Ni chama kinachotakiwa kuwa na mizizi yake vijijini zaidi kwa kukivewezesha vijiji na wanavijiji na sio mjini kwenye watu wachache na walioelimika vya kutosha. Ni chama ambacho ofisi zake vijijini vitakuwa ni vituo muhimu katika kazi zake mbalimbali na ofisi ambazo zina nafasi kwa ofisi za viongozi wa wilaya, mkoa na kitaifa na ukumbi wa mkutano ambao vikao vikubwa kwa vidogo vya chama vinaweza kufanyika huko bila wasiwasi na uwepo wa sehemu kama hiyo kuwa ni hamira au chachu ya maendeleo ya kijiji na wanakijiji husika.
Ni kawaida pia kinachopingwa, kupinga na kupambana na kile kinachokipinga. Lakini kwa jambo lolote ambalo wakati wake umefika ni muhali na kazi bure kulipinga. Ima-fa-ima lazima mabadiliko yanayopaswa kufanyika yatafanyika tu.
Ili kutopotezeana muda ni vyema kufunguana macho na kuhamasisha jamii kufagia yale yote yenye kunukia uzee au ukongwe usio na faida na ambayo yanaweza kusababisha kuvunjika kwa amani na umoja katika nchi hii eti tu kwa kuwa ukongwe huo unakataa mabadiliko yasitokee.
Hali ilivyo sasa ni kwamba wanasiasa waliopo wamezoea kutawala kwa kutumia mabavu na maguvu; udikteta na ukiritimba katika maamuzi na uendeshaji vyama; kusukumiza kwenye makoo ya raia zao katiba na sheria zisizokubalika; kupora mamlaka na madaraka ya wananchi kinyume na katiba; kutumia njia za haramu kupata mapato yao na ya chama; kutumia vyombo vya dola kwa faida na maslahi yake; uzaini na uongo; kununua na kuwatumia watu; kugawa na kutawala; kulea ukabila wa kichama kwa maana ya kuwabeba tu wanachama wa chama tawala kuwa viongozi na kuwaacha wasio wanachama bila kazi wala changamoto za maana katika kuendeleza wilaya au mkoa au taifa;
uroho, choyo, inda na ulafi wa hali ya juu kutaka kutawala hata pale chama husika kisipokuwa na sapoti ya kutosha; kutumia vyombo vya usalama vya taifa kwa matumizi binafsi na sio kwa maslahi ya kitaifa; kutumia vyombo vya habari kukwamisha uwazi na kudanganya badala ya kusema ukweli; Viongozi wasio na mwelekeo wa kuinufaisha nchi hii na watu bali zaidi wao wenyewe na watu wa nje, kutumia makundi ya kijamii kama vile wanawake, vijana, wazee, wazazi, wanavijiji, wanafunzi, walimu, wafanyakazi na kadhalika kwa manufaa yao na sio ya kitaifa au ya umma; kuwatumia waandishi habari kama askari wa kukodiwa kufanikisha malengo yao; kushirikiana na mafisadi na wevi kufanikisha malengo ya kichama; kuingiza udini na ukabila katika uongozi na uanachama; kutumiwa na viongozi wa nje wa serikali na makampuni kwa maslahi yao na sio ya Watanzania; kushindwa kujenga imani na kujiamini kwamba kwa kutumia rasilimali zetu wenyewe tunaweza kunufaika zaidi kuliko kudanganywa kwa misaada toka nchi za nje ambayo ni sawa na mtu kupewa perememde wewe ukaibiwa kipande cha almasi au vito vingine vyenye thamani.
Mlolongo huo hapo juu ni ushahidi tosha unaonesha ni kwa kiasi gani vyama vya kisiasa nchini Tanzania vimepitwa na wakati na vinahitaji kufa au kupona 'kusasaishwa' ili sio tu viende na wakati bali viweze kutekeleza kwa ukamilifu na usahihi zaidi majukumu yao ya kisiasa, kijamii na kitaifa.
Ili kwenda na wakati vyama vya kisiasa vinastahili pamoja na mambo mengine kuwa na wanasiasa wasioshindwa na wasiotishika katika kutumia nguvu ya hoja, uchanganuzi, uchambuzi na ubunifu katika kuongoza na wanaostawi katika kutofautiana kimawazo, kifikra na kimaono.
Lazima kila chama kihakikisha kuwepo kwa demokrasia na uhuru wa kuchagua au kuchaguliwa ndani na nje ya chama; kuruhusu kuwepo kwa katiba na sheria zilizoandikwa na wanachama au wananchi wenyewe na sio wao kama viongozi au watawala; na pia kutumia njia za halali na zinazokubalika na zisizowaumiza watu wengine kupata mapato yao na ya chama.
Ni wajibu wa chama chochote ndani au nje ya madaraka kuvhiheshimu, kushirikiana na kuvitumia vyombo vya dola kwa faida na maslahi ya umma na si watu wachache; na kujali usawa, haki na ukweli wakati wote.
Kila chama kinastahili kuthamini utu na ubinadamu wa raia wote; kujenga umoja katika tofauti za kiimani na kiitikadi; kukana na kuharamisha ukabila wa aina zote ukiwemo ule ukabila wa kichama, udugu, ujamaa na urafiki katika kazi na majukumu mengine ya kitaifa.
Chama lazima kidhibiti wakati wote uroho, choyo, inda na ulafi miongoni mwa wanachama na viongozi wake; kuwaachia wengine kutawala pale chama kisipokubalika na wakazi husika; na kutotumia vyombo vya usalama wa taifa kwa maslahi, matakwa na haja binafsi ikiwemo kuwachunguza viongozi wastaafu, wanaharakati na wanachama na viongozi wa upinzani.
KIla chama kinawajibika kutotumia vyombo vya habari kudanganya wale wenye uelewa duni wa mambo; kutowaweka waavijiji katika giza la kuelewa na kukubali kuwa demokrasia na vyama vingi ni jambo lenye manufaa kwetu kama nchi na watu; na pia kutowatumia waandishi habari kama askari wa kukodiwa kufanikisha malengo ya chama na viongozi wake.
Chama kinawajibika kutoshirikiana na matajiri na mafisadi katika kupora madini na maliasili za nchi hii; kutowagawa Watanzania katika makundi ya kijamii yanayoweza kuja kuwa hatari kwa taifa baadaye, k.m, vijana, wazee, wanafunzi, wanawake, wazazi wa chama fulani n.k.
Chama kiwe makini na kutoingiza udini na ukabila katika uongozi na uanachama; kutotumiwa na viongozi wa nje wa serikali na makampuni kwa maslahi yao na sio ya Watanzania; kufanikisha kujenga imani na kujiamini miongoni mwa Watanzania kwamba kwa kutumia watu wetu wenyewe, wazungu wasio na ajira makwao, rasilimali zetu wenyewe tunaweza kunufaika zaidi kuliko kudanganywa kwa misaada toka nchi za nje ambayo ni sawa na mtu kupewa perememde wewe ukaibiwa kipande cha almasi au vito vingine vyenye thamani na wewe ukaridhika na kuona ndiye uliyefaidi kuliko aliyefaidi kikweli.
Chama cha kisiasa sahihi na kinachostahili kuwepo katika karne ya 21 nchini Tanzania ni kile kitakachoweza kufanya mikutano yake mikubwa na midogo, kwa siku kama sio wiki kadhaa, katika kijiji chochote, mkoa wowote Tanzania kwani mikoa na vijiji hivyo vitakuwa na serikali na utawala bora unaoweza kukimu na kuruzuku mambo hayo kutokana na kuwezeshwa na chama husika na wafuasi wake na watu wengine wanaozingatia misaada kufika kule inakotakiwa na sio vinginevyo..
Haijawahi kutokea katika nchi yoyote ile duniani kwa mabadiliko makubwa ya kisiasa, kiuchumi na kijamii kufanyika kirahisi na bila kuwa na upinzani mkali, mkubwa na wa kutisha toka kwa wattu waoga, mbumbu, wasiojua kinachoendelea, wanaonufaika na mfumo wa hali iliyopo au wale wanaotumiwa na wanaonufaika kuwalinda wao na mali zao.
Ninasema vyama vya siasa Tanzania vimepitwa na wakati kwa sababu kile kilichozoea ukiritimba wa mfumo wa chama kimoja kinajiendesha kama wito na kazi yake kuu ni kupambana na wale wanaotaka kife; wakati wale wa iwezekanayo kuwa serikali mbadala na katika mfumo ambao si tofauti sana na wa chama kimoja katika mambo mengi, wanajiendesha kama vile kazi yao kubwa ni kuja kuingia madarakani kwa udi na uvumba. Hakuna kati yao ambaye anatoa uzito stahilifu kwa matatizo na changamoto za wananchi. Na kwa maana hii sio tu ninaona vimepitwa na wakati bali ninadhani vyama vyote havistahili hata kuwepo na nchi imekosa tu watu wanaoweza kuthubutu kuvifagia pembeni hata kabla ya uchaguzi mkuu ujao.
Mabadiliko ambayo Tanzania inastahili kuyafanya hivi sasa hayana tofauti kwa namna yoyote ile na mabadiliko mengine kama hayo yanayotokea kwingine duniani na yaliyokwishatokea pengine na katika karne nyingine huko nyuma yetu.
Tofauti tu iliyopo hivi sasa ni kuwa sisi kama watu mmoja mmoja na kitaifa hatujajipanga ipasavyo kuweza kuhakikisha kuwa mabadiliko hayo yanatokea kwa faida na manufaa yetu na sio kwa ujibari, ujivuni, kisirani na hasara kwa upande wetu.
Na katika hili kiongozi mkuu wa kujipanga kuyakabili mabadiliko anatakiwa awe ni chama cha kisiasa cnenye viongozi wanaojua watu wanataka kuelekea wapi, nchi inaelekea wapi, duniani inaelekea wapi, nani wanastahili kuwa rafiki zetu na nani hatustahili kuwaamini, kuwathamini na kuwaingiza katika siri na mambo yetu mengine.
Ni chama kinachostahili kuwa na mipango, mikakati, sera, muundo, mfumo, taratibu na kanuni za utekelezaji zinazokipa chama ukuu na nguvu juu ya mwanachama mmoja mmoja au kundi la wanachama fulani ndani ya chama husika katika mustakabali wa kujenga umoja wa chama lakini ndani ya mfumo wa demokrasia hai na inayofanya kazi. Ugonjwa wa 'ndivyotunavyofikiri' ukiachiwa kutambaa kwenye mwili-siasa wa jamii hivi leo ni dhahiri maradhi makubwa zaidi yatajitokeza na kupona kwa mgonjwa kutahitaji manabii na miujiza.
Ni chama ambacho kina 'visheni' na 'misheni' bayana ambazo wanaokiongoza hata wakikurupushwa usingizini wanavikariri bila kukosea hata neno moja.
Ni chama kinachotakiwa kuwa na mizizi yake vijijini zaidi kwa kukivewezesha vijiji na wanavijiji na sio mjini kwenye watu wachache na walioelimika vya kutosha. Ni chama ambacho ofisi zake vijijini vitakuwa ni vituo muhimu katika kazi zake mbalimbali na ofisi ambazo zina nafasi kwa ofisi za viongozi wa wilaya, mkoa na kitaifa na ukumbi wa mkutano ambao vikao vikubwa kwa vidogo vya chama vinaweza kufanyika huko bila wasiwasi na uwepo wa sehemu kama hiyo kuwa ni hamira au chachu ya maendeleo ya kijiji na wanakijiji husika.
Ni kawaida pia kinachopingwa, kupinga na kupambana na kile kinachokipinga. Lakini kwa jambo lolote ambalo wakati wake umefika ni muhali na kazi bure kulipinga. Ima-fa-ima lazima mabadiliko yanayopaswa kufanyika yatafanyika tu.
Ili kutopotezeana muda ni vyema kufunguana macho na kuhamasisha jamii kufagia yale yote yenye kunukia uzee au ukongwe usio na faida na ambayo yanaweza kusababisha kuvunjika kwa amani na umoja katika nchi hii eti tu kwa kuwa ukongwe huo unakataa mabadiliko yasitokee.
Hali ilivyo sasa ni kwamba wanasiasa waliopo wamezoea kutawala kwa kutumia mabavu na maguvu; udikteta na ukiritimba katika maamuzi na uendeshaji vyama; kusukumiza kwenye makoo ya raia zao katiba na sheria zisizokubalika; kupora mamlaka na madaraka ya wananchi kinyume na katiba; kutumia njia za haramu kupata mapato yao na ya chama; kutumia vyombo vya dola kwa faida na maslahi yake; uzaini na uongo; kununua na kuwatumia watu; kugawa na kutawala; kulea ukabila wa kichama kwa maana ya kuwabeba tu wanachama wa chama tawala kuwa viongozi na kuwaacha wasio wanachama bila kazi wala changamoto za maana katika kuendeleza wilaya au mkoa au taifa;
uroho, choyo, inda na ulafi wa hali ya juu kutaka kutawala hata pale chama husika kisipokuwa na sapoti ya kutosha; kutumia vyombo vya usalama vya taifa kwa matumizi binafsi na sio kwa maslahi ya kitaifa; kutumia vyombo vya habari kukwamisha uwazi na kudanganya badala ya kusema ukweli; Viongozi wasio na mwelekeo wa kuinufaisha nchi hii na watu bali zaidi wao wenyewe na watu wa nje, kutumia makundi ya kijamii kama vile wanawake, vijana, wazee, wazazi, wanavijiji, wanafunzi, walimu, wafanyakazi na kadhalika kwa manufaa yao na sio ya kitaifa au ya umma; kuwatumia waandishi habari kama askari wa kukodiwa kufanikisha malengo yao; kushirikiana na mafisadi na wevi kufanikisha malengo ya kichama; kuingiza udini na ukabila katika uongozi na uanachama; kutumiwa na viongozi wa nje wa serikali na makampuni kwa maslahi yao na sio ya Watanzania; kushindwa kujenga imani na kujiamini kwamba kwa kutumia rasilimali zetu wenyewe tunaweza kunufaika zaidi kuliko kudanganywa kwa misaada toka nchi za nje ambayo ni sawa na mtu kupewa perememde wewe ukaibiwa kipande cha almasi au vito vingine vyenye thamani.
Mlolongo huo hapo juu ni ushahidi tosha unaonesha ni kwa kiasi gani vyama vya kisiasa nchini Tanzania vimepitwa na wakati na vinahitaji kufa au kupona 'kusasaishwa' ili sio tu viende na wakati bali viweze kutekeleza kwa ukamilifu na usahihi zaidi majukumu yao ya kisiasa, kijamii na kitaifa.
Ili kwenda na wakati vyama vya kisiasa vinastahili pamoja na mambo mengine kuwa na wanasiasa wasioshindwa na wasiotishika katika kutumia nguvu ya hoja, uchanganuzi, uchambuzi na ubunifu katika kuongoza na wanaostawi katika kutofautiana kimawazo, kifikra na kimaono.
Lazima kila chama kihakikisha kuwepo kwa demokrasia na uhuru wa kuchagua au kuchaguliwa ndani na nje ya chama; kuruhusu kuwepo kwa katiba na sheria zilizoandikwa na wanachama au wananchi wenyewe na sio wao kama viongozi au watawala; na pia kutumia njia za halali na zinazokubalika na zisizowaumiza watu wengine kupata mapato yao na ya chama.
Ni wajibu wa chama chochote ndani au nje ya madaraka kuvhiheshimu, kushirikiana na kuvitumia vyombo vya dola kwa faida na maslahi ya umma na si watu wachache; na kujali usawa, haki na ukweli wakati wote.
Kila chama kinastahili kuthamini utu na ubinadamu wa raia wote; kujenga umoja katika tofauti za kiimani na kiitikadi; kukana na kuharamisha ukabila wa aina zote ukiwemo ule ukabila wa kichama, udugu, ujamaa na urafiki katika kazi na majukumu mengine ya kitaifa.
Chama lazima kidhibiti wakati wote uroho, choyo, inda na ulafi miongoni mwa wanachama na viongozi wake; kuwaachia wengine kutawala pale chama kisipokubalika na wakazi husika; na kutotumia vyombo vya usalama wa taifa kwa maslahi, matakwa na haja binafsi ikiwemo kuwachunguza viongozi wastaafu, wanaharakati na wanachama na viongozi wa upinzani.
KIla chama kinawajibika kutotumia vyombo vya habari kudanganya wale wenye uelewa duni wa mambo; kutowaweka waavijiji katika giza la kuelewa na kukubali kuwa demokrasia na vyama vingi ni jambo lenye manufaa kwetu kama nchi na watu; na pia kutowatumia waandishi habari kama askari wa kukodiwa kufanikisha malengo ya chama na viongozi wake.
Chama kinawajibika kutoshirikiana na matajiri na mafisadi katika kupora madini na maliasili za nchi hii; kutowagawa Watanzania katika makundi ya kijamii yanayoweza kuja kuwa hatari kwa taifa baadaye, k.m, vijana, wazee, wanafunzi, wanawake, wazazi wa chama fulani n.k.
Chama kiwe makini na kutoingiza udini na ukabila katika uongozi na uanachama; kutotumiwa na viongozi wa nje wa serikali na makampuni kwa maslahi yao na sio ya Watanzania; kufanikisha kujenga imani na kujiamini miongoni mwa Watanzania kwamba kwa kutumia watu wetu wenyewe, wazungu wasio na ajira makwao, rasilimali zetu wenyewe tunaweza kunufaika zaidi kuliko kudanganywa kwa misaada toka nchi za nje ambayo ni sawa na mtu kupewa perememde wewe ukaibiwa kipande cha almasi au vito vingine vyenye thamani na wewe ukaridhika na kuona ndiye uliyefaidi kuliko aliyefaidi kikweli.
Chama cha kisiasa sahihi na kinachostahili kuwepo katika karne ya 21 nchini Tanzania ni kile kitakachoweza kufanya mikutano yake mikubwa na midogo, kwa siku kama sio wiki kadhaa, katika kijiji chochote, mkoa wowote Tanzania kwani mikoa na vijiji hivyo vitakuwa na serikali na utawala bora unaoweza kukimu na kuruzuku mambo hayo kutokana na kuwezeshwa na chama husika na wafuasi wake na watu wengine wanaozingatia misaada kufika kule inakotakiwa na sio vinginevyo..
Vyama vya kisiasa Tanzania vimepitwa na wakati ? Sehemu- II
Ili 'kuvisasaisha' vyama vya kisiasa Tanzania kuna mambo kama 15 hivi yanayostahili kufanyika. Mambo hayo, yakiwemo hayo machache yaliyogusiwa hapo juu ni pamoja na mabadiliko ya miundo; mifumo kazi; uwakilishi mikoani na matawini; kuwa na wanachama hai; kuwa na vyanzo halali vya mapato; elimu isiyokoma kwa vingozi na wanachama; matumizi ya Teknohama; kutumia sayansi ya logistiki; kuwa na mipango na mikakati ya kisasa; kuwa na mbinu za kunufaika na kutohasirika na mahusiano ya kimataifa na utandawazi; kubuni njia bora za kupata viongozi; mafunzo ya menejimenti, uchumi na maarifa muhimu kwa viongozi; namna mpya za kukabiliana na matatizo na changamoto za wafuasi na wananchi kwa ujumla; na jinsi ya kuwa mwendelezaji, mwekezaji na mshiriki katika kuzitumia fursa za kimaendeleo za kiuchumi na kijamii kuanzia ngazi ya chini ya tawi hadi ya juu kitaifa kwa faida ya nchi nzima na watu wake.
( Makala haya yanauzwa; wasiliana nasi kupitia SMS : +255714265218 wakati wowote na uapata majibu chini ya saa 24.).......
( Makala haya yanauzwa; wasiliana nasi kupitia SMS : +255714265218 wakati wowote na uapata majibu chini ya saa 24.).......
Sunday, November 6, 2011
Tukubali ushoga au tuachane na nchi za Magharibi ?
ZIPO habari kwamba serikali ya Uingereza iko mbioni kuandaa utaratibu ambao nchi zinazokataa 'ushoga' , kwa maana ya mwanamme kujigeuza mwanamke na kuwa na haki ya kuolewa na kuwekwa ndani kama mke, zitakuwa zikinyimwa fedha za jamala ambazo kwa Waafrika walio wengi sio msaada ila ni sawa na kurudisha kile ambacho Waingereza na ndugu zao walikwiba, wanakwiba na wanaendelea kukwiba toka kwa Watanzania na Waafrika wengine kupitia ukoloni, ukoloni mambo leo na unyonyaji mkuu wa kibiashara na kiuchumi kimataifa.
Mama wa demokrasia duniani, Uingereza, anataka kwa mabavu kupandikiza ushoga katika nchi za Kiafrika ikiwemo Tanzania kwa kuwazaini Waafrika kwa pipi na shanga kama ilivyokuwa zamani wakati makampuni yake hayachoti tu dhahabu na madini yetu mengine bali pia hata fedha zetu kidogo zilizo katika hazina yetu.
Uingereza ndio nchi iliyoitawala Tanganyika tokea ilipomshinda Mjerumani ikisaidiwa na rafiki zake mwaka 1918-1961 bila kufikia hata nusu ya mafaniko yaliyofanywa na Mjerumani katika miaka yake 30 hivi ya kuitawala Tanganyika. Lakini ndiyo iliyofanikisha kujenga unyonyaji wa hali ya juu wa nchi hii, hadi hii leo ikiwmo kasumba ya viongozi na matajiri wetu kuwapeleka watoto wao kwenda kusomeshwa Uingereza.
Hili hata hivi linatufungua macho Watanzania kwa kutambua kwamba serikali ya Uingereza na Jumuiya ya Madola ni kama vile zinaamini kwamba zimeziweka mfukoni nchi maskini za Kiafrika na kwamba zinaweza kutumia udikteta kufosi kwenye makoo yao chochote kile wanachokitaka wao kwa kuwa ni matajiri na watu wa nchi zetu kwa kuwa maskini wakakubali kirahisi tu.
Hili huwa linawezekana kwa sababu Uingereza na Marekani huwa linawatumia watu waliosoma au kufanya kazi kwao kuja 'kuunyakua' uongozi wa nchi sio kwa sababu nyingine ila kuendeleza maslahi ya Uingereza na Marekani katika nchi husika. Katika wimbi la demokrasia katika nchi zetu hivi sasa tuwe macho sana na viongozi wa kupandikizwa kwa sababu ya nguvu ya fedha. Watu hao kwa kawaida hutumwa na mabepari wa dunia ambao ni kama asilimia 1 tu ya watu duniani kuja kukwiba utajiri wenu kwa kuunda genge la asilimia 0.005 ya mabepari na wanasiasa matapeli ndani ya nchi husika.
Kwa wasiojua dunia ya ubepari tuliyoikaribisha Tanzania ni mfumo ambao unaendeshwa na asilimia 1 tu ya matajiri duniani lakini ulio na sauti na nguvu sio tu juu ya serikali zao bali pia serikali za nchi zinazoendelea ambazo huzitegemea nchi zao. Asilimia hii moja ndiyo inayoipa nguvu asilimia nyingine kama 15-20 za mabepari wa kati wanaokuja kuwekeza katika nchi zetu na kuwanu nua viongozi na matajiri wachache nchini (labda asilimia 2-3), ili kudhulumu asilimia 97-98 ya raia wenzao kwa heri na shari.
Katika hili, mimi sina tatizo hata kidogo kuona wanawake, wazee, vijana, wafanyakazi, wakulima na makundi mengine katika jamii yakifanya uamuzi ya kuandamana na kuwapasha Waingereza na Wamarekani na wenzao kama wao kwamba hatutaki na hatukubali ushoga katika urithi, desturi, utamdauni na mila zetu za Kiafrika hapa Tanzania na kwingineko Afrika.
Ushoga kwa wale wanaoamini katika Quran Tukufu na Biblia ndiyo mambo yaliyosambaratisha nchi za Sodom na Gomorrah. Wakati kuna dalili za Marekani na nchi za Ulaya kuwa katika masahibu ya kila aina, zipo hisia kwamba Waingereza wanachotaka kukifanya ni sawa na mtu anayezama kutaka kufa na wale wanaoweza kuwasaidia na wanaotaka kumuokoa.
Ni kichekesho kwa Uingereza kuwa na msimamo kama huu katika karne ya 22, kama vile bado tupo kwenye karne za 19 au 20.
Inaonekana kama vile Uingereza na nchi nyingine tajiri bado zinaamini kwamba nchi za Kiafrika ni nchi zinazoongozwa na watu ambao uroho na tamaa yao ya misaada vinaweza kuwafanya wakubali lolote lile hata likiwa baya kwa mila, desturi, imani, utamaduni na utu wa watu wao.
Hivi leo uchumi wa Ulaya na Marekani upo kwenye misukosuko sio kwa sababu nyingine bali kwa sababu ya uchumi kukosa haya na aibu au kile kinachoitwa, 'economics without ethics', uchumi bila maadili. Na misaada toka nchi hizo nazo sasa inataka kugeuzwa kuwa ni 'aid without ethics' au misaada bila maadili. Vitu hivi tusivikubali. Na huu ni wakati wa kuwashauri Wazungu kuanza kitu kitakachoitwa uchumi na misaada yenye maadili kama masomo katika shule zao za viongozi na hasa wale wa kimataifa. (Ethiconomics na aideconomics) ili watuelewe na kutufahamu zaidi. Umaskini hauimanishi maskini kukubali kuuza roho, utu na imani yake kwa ajili ya kupewa misaada.
Lakini ni ajabu pia kwa sababu hivi sasa nchi za BRIC-Brazili, Russia, India, Uchina na bila kusahau nchi za Kiarabu, zile zilizokuwa katika ile iliyokuwa ikiitwa Urussi ya zamani, Malaysia, Indonesia, Korea Kusini, Vietnam, Japani na zile za Scandinavia nazo zinatuhitaji zaidi kuliko wao wanavyotuhitaji.
Ili kuwafunza jamaa hawa ningelishauri nchi za Kiafrika kama zilikuwa zikiwapa fursa 8 kati ya 10 Waingereza na wamarekani nchini mwao, sasa zigeuze kibao na kuyapa mataifa haya mapya na yanayokuwa kwa kasi zaidi asilimia 80 ya biashara, uwekezaji na ushirikiano kati yao na kuwabakizia wakongwe Uingereza na Marekani asilimia 20 tu, ili vitisho vyao viwe kazi bure huko tunakokwenda.
Mambo yetu Waafrika kwa kiasi kikubwa yameharibika kutokana na ukaribu na kukubali bila kujiuliza tamaduni za nje, hususan, za Kiingereza na Kimarekani. Ni dhahiri kwamba tungelikuwa tunaujali utamaduni wetu wenyewe na tukashirikiana zaidi na zaidi na nchi tofauti na hizi mbili, hivi leo labda hadithi ya Afrika isngelikuwa hii iliyopo hivi sasa.
Ni nchi za Magharibi na hususan Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Italia na Marekani ndizo zilizochangia na zinazoendelea kuchangia kudhoofisha utu, utamaduni, imani na udugu wetu kwa sababu wanazozijua vizuri kuliko sisi wenyewe. Kutokana na umaskini wetu tumeendelea kuwaganda huku wanatunyonga taratibu.
Huu ni wakati muafaka kwa viongozi wa dini na wafuasi wao nao kuja juu kiddedea na kuwaonyesha mabwana na mabibi zetu wa zamani kwamba Tanzania ya leo sio ya jana na sio nchi ya kuichezea tena!
Viongozi wa dini watumie fursa hii kuzungumza moja kwa moja na walipa kodi wa Uingereza wakiwemo Wakiristo, Waislamu na Wayahudi kuwaomba washinikize serikali ya Uingereza kuachana na wazo la kuinyima Tanzania msaada kwa sababu Tanzania haitakubali ushoga achilia mbali watu wa jinsia moja kufunga na kufungishwa ndoa.
Wakati huohuo, vyama vya siasa nchini hapa na vile vya Uingereza vianzishe vuguvugu la kudai demokrasia katika utoaji misaada na kuheshimiwa kwa haki za nchi maskini katika kulinda utu wa watu wake na mila na utamaduni wao.
Enzi za Uingereza na Marekani kutoa masharti ya kisenge na kiudhalimu kwa Waafrika ninaamini zimepita. Hivi sasa Afrika ina nafasi ya kuchagua na kukataa masharti ya kijinga na yanyochimbua mizizi na kuusambaratisha mashina yake ya utu na utamaduni wake bila sababu ya msingi. Kufuatia ujibari, jeuri na kiburi cha Marekani na Wayahudi, ingekuwa jambo zuri kama nchi za BRIC na marafiki wengine tajiri wa Afrika, zingeingilia kati na kuliziba pengo la bajeti ya UNESCO, kama Marekani itajitoa kuifadhili UNESCO eti kwa sababu Palestina imekubalika kama mwananchi kamili.
Kama mataifa haya makubwa yanaamini kweli katika demokrasia hayawezi kuwalazimisha viongozi wetu kufanya maamuzi kwa niaba yetu. Maana kufanya hivyo ni kuwafunza udikteta viongozi wetu.
Isitoshe baadhi yetu katiba zetu tayari hazikubali ushoga. Je, kwa masharti hayo ya Waingereza hawaoni moja kwa moja kwamba sio tu wanataka kuingilia sheria na katiba yetu, bali pia wanaonyesha dharau kwa serikali na watu wetu ya hali ya juu kabisa.
Wanachostahili kufanya mabwana hawa ni kuwezesha nchi zetu kuwapa fursa wananchi wao kupiga kura ya kukubali au kupinga kuingizwa au kulazimishwa kuufanya halali ushoga nchini mwao.
Kwa jinsi serikali yetu inavyojikuta mchafukoge katika masuala kama ya mkorogo katika suala la huduama za umeme, maji, afya na tiba, ustawi wa jamii na usafi; migodi na madini; ufisadi, EPA na wenzake; mawakala wanavyotumbua na kadhalika na tunavyoambiwa kuwa wanaCCM wenyewe hawaoni mtu wa kupambana na ufisadi ndani ya chama hicho hatujui ni kwa kiasi gani tunaweza kuwa na viongozi watakaoendelea kuonyesha ubabe na ufidhuli kwa wale wanaotutaka tuwe mashoga na wasenge katika dunia hii ieleekeayo kwenye maangamizi ya Sodom na Gomorrah.
Mama wa demokrasia duniani, Uingereza, anataka kwa mabavu kupandikiza ushoga katika nchi za Kiafrika ikiwemo Tanzania kwa kuwazaini Waafrika kwa pipi na shanga kama ilivyokuwa zamani wakati makampuni yake hayachoti tu dhahabu na madini yetu mengine bali pia hata fedha zetu kidogo zilizo katika hazina yetu.
Uingereza ndio nchi iliyoitawala Tanganyika tokea ilipomshinda Mjerumani ikisaidiwa na rafiki zake mwaka 1918-1961 bila kufikia hata nusu ya mafaniko yaliyofanywa na Mjerumani katika miaka yake 30 hivi ya kuitawala Tanganyika. Lakini ndiyo iliyofanikisha kujenga unyonyaji wa hali ya juu wa nchi hii, hadi hii leo ikiwmo kasumba ya viongozi na matajiri wetu kuwapeleka watoto wao kwenda kusomeshwa Uingereza.
Hili hata hivi linatufungua macho Watanzania kwa kutambua kwamba serikali ya Uingereza na Jumuiya ya Madola ni kama vile zinaamini kwamba zimeziweka mfukoni nchi maskini za Kiafrika na kwamba zinaweza kutumia udikteta kufosi kwenye makoo yao chochote kile wanachokitaka wao kwa kuwa ni matajiri na watu wa nchi zetu kwa kuwa maskini wakakubali kirahisi tu.
Hili huwa linawezekana kwa sababu Uingereza na Marekani huwa linawatumia watu waliosoma au kufanya kazi kwao kuja 'kuunyakua' uongozi wa nchi sio kwa sababu nyingine ila kuendeleza maslahi ya Uingereza na Marekani katika nchi husika. Katika wimbi la demokrasia katika nchi zetu hivi sasa tuwe macho sana na viongozi wa kupandikizwa kwa sababu ya nguvu ya fedha. Watu hao kwa kawaida hutumwa na mabepari wa dunia ambao ni kama asilimia 1 tu ya watu duniani kuja kukwiba utajiri wenu kwa kuunda genge la asilimia 0.005 ya mabepari na wanasiasa matapeli ndani ya nchi husika.
Kwa wasiojua dunia ya ubepari tuliyoikaribisha Tanzania ni mfumo ambao unaendeshwa na asilimia 1 tu ya matajiri duniani lakini ulio na sauti na nguvu sio tu juu ya serikali zao bali pia serikali za nchi zinazoendelea ambazo huzitegemea nchi zao. Asilimia hii moja ndiyo inayoipa nguvu asilimia nyingine kama 15-20 za mabepari wa kati wanaokuja kuwekeza katika nchi zetu na kuwanu nua viongozi na matajiri wachache nchini (labda asilimia 2-3), ili kudhulumu asilimia 97-98 ya raia wenzao kwa heri na shari.
Katika hili, mimi sina tatizo hata kidogo kuona wanawake, wazee, vijana, wafanyakazi, wakulima na makundi mengine katika jamii yakifanya uamuzi ya kuandamana na kuwapasha Waingereza na Wamarekani na wenzao kama wao kwamba hatutaki na hatukubali ushoga katika urithi, desturi, utamdauni na mila zetu za Kiafrika hapa Tanzania na kwingineko Afrika.
Ushoga kwa wale wanaoamini katika Quran Tukufu na Biblia ndiyo mambo yaliyosambaratisha nchi za Sodom na Gomorrah. Wakati kuna dalili za Marekani na nchi za Ulaya kuwa katika masahibu ya kila aina, zipo hisia kwamba Waingereza wanachotaka kukifanya ni sawa na mtu anayezama kutaka kufa na wale wanaoweza kuwasaidia na wanaotaka kumuokoa.
Ni kichekesho kwa Uingereza kuwa na msimamo kama huu katika karne ya 22, kama vile bado tupo kwenye karne za 19 au 20.
Inaonekana kama vile Uingereza na nchi nyingine tajiri bado zinaamini kwamba nchi za Kiafrika ni nchi zinazoongozwa na watu ambao uroho na tamaa yao ya misaada vinaweza kuwafanya wakubali lolote lile hata likiwa baya kwa mila, desturi, imani, utamaduni na utu wa watu wao.
Hivi leo uchumi wa Ulaya na Marekani upo kwenye misukosuko sio kwa sababu nyingine bali kwa sababu ya uchumi kukosa haya na aibu au kile kinachoitwa, 'economics without ethics', uchumi bila maadili. Na misaada toka nchi hizo nazo sasa inataka kugeuzwa kuwa ni 'aid without ethics' au misaada bila maadili. Vitu hivi tusivikubali. Na huu ni wakati wa kuwashauri Wazungu kuanza kitu kitakachoitwa uchumi na misaada yenye maadili kama masomo katika shule zao za viongozi na hasa wale wa kimataifa. (Ethiconomics na aideconomics) ili watuelewe na kutufahamu zaidi. Umaskini hauimanishi maskini kukubali kuuza roho, utu na imani yake kwa ajili ya kupewa misaada.
Lakini ni ajabu pia kwa sababu hivi sasa nchi za BRIC-Brazili, Russia, India, Uchina na bila kusahau nchi za Kiarabu, zile zilizokuwa katika ile iliyokuwa ikiitwa Urussi ya zamani, Malaysia, Indonesia, Korea Kusini, Vietnam, Japani na zile za Scandinavia nazo zinatuhitaji zaidi kuliko wao wanavyotuhitaji.
Ili kuwafunza jamaa hawa ningelishauri nchi za Kiafrika kama zilikuwa zikiwapa fursa 8 kati ya 10 Waingereza na wamarekani nchini mwao, sasa zigeuze kibao na kuyapa mataifa haya mapya na yanayokuwa kwa kasi zaidi asilimia 80 ya biashara, uwekezaji na ushirikiano kati yao na kuwabakizia wakongwe Uingereza na Marekani asilimia 20 tu, ili vitisho vyao viwe kazi bure huko tunakokwenda.
Mambo yetu Waafrika kwa kiasi kikubwa yameharibika kutokana na ukaribu na kukubali bila kujiuliza tamaduni za nje, hususan, za Kiingereza na Kimarekani. Ni dhahiri kwamba tungelikuwa tunaujali utamaduni wetu wenyewe na tukashirikiana zaidi na zaidi na nchi tofauti na hizi mbili, hivi leo labda hadithi ya Afrika isngelikuwa hii iliyopo hivi sasa.
Ni nchi za Magharibi na hususan Uingereza, Ujerumani, Ufaransa, Italia na Marekani ndizo zilizochangia na zinazoendelea kuchangia kudhoofisha utu, utamaduni, imani na udugu wetu kwa sababu wanazozijua vizuri kuliko sisi wenyewe. Kutokana na umaskini wetu tumeendelea kuwaganda huku wanatunyonga taratibu.
Huu ni wakati muafaka kwa viongozi wa dini na wafuasi wao nao kuja juu kiddedea na kuwaonyesha mabwana na mabibi zetu wa zamani kwamba Tanzania ya leo sio ya jana na sio nchi ya kuichezea tena!
Viongozi wa dini watumie fursa hii kuzungumza moja kwa moja na walipa kodi wa Uingereza wakiwemo Wakiristo, Waislamu na Wayahudi kuwaomba washinikize serikali ya Uingereza kuachana na wazo la kuinyima Tanzania msaada kwa sababu Tanzania haitakubali ushoga achilia mbali watu wa jinsia moja kufunga na kufungishwa ndoa.
Wakati huohuo, vyama vya siasa nchini hapa na vile vya Uingereza vianzishe vuguvugu la kudai demokrasia katika utoaji misaada na kuheshimiwa kwa haki za nchi maskini katika kulinda utu wa watu wake na mila na utamaduni wao.
Enzi za Uingereza na Marekani kutoa masharti ya kisenge na kiudhalimu kwa Waafrika ninaamini zimepita. Hivi sasa Afrika ina nafasi ya kuchagua na kukataa masharti ya kijinga na yanyochimbua mizizi na kuusambaratisha mashina yake ya utu na utamaduni wake bila sababu ya msingi. Kufuatia ujibari, jeuri na kiburi cha Marekani na Wayahudi, ingekuwa jambo zuri kama nchi za BRIC na marafiki wengine tajiri wa Afrika, zingeingilia kati na kuliziba pengo la bajeti ya UNESCO, kama Marekani itajitoa kuifadhili UNESCO eti kwa sababu Palestina imekubalika kama mwananchi kamili.
Kama mataifa haya makubwa yanaamini kweli katika demokrasia hayawezi kuwalazimisha viongozi wetu kufanya maamuzi kwa niaba yetu. Maana kufanya hivyo ni kuwafunza udikteta viongozi wetu.
Isitoshe baadhi yetu katiba zetu tayari hazikubali ushoga. Je, kwa masharti hayo ya Waingereza hawaoni moja kwa moja kwamba sio tu wanataka kuingilia sheria na katiba yetu, bali pia wanaonyesha dharau kwa serikali na watu wetu ya hali ya juu kabisa.
Wanachostahili kufanya mabwana hawa ni kuwezesha nchi zetu kuwapa fursa wananchi wao kupiga kura ya kukubali au kupinga kuingizwa au kulazimishwa kuufanya halali ushoga nchini mwao.
Kwa jinsi serikali yetu inavyojikuta mchafukoge katika masuala kama ya mkorogo katika suala la huduama za umeme, maji, afya na tiba, ustawi wa jamii na usafi; migodi na madini; ufisadi, EPA na wenzake; mawakala wanavyotumbua na kadhalika na tunavyoambiwa kuwa wanaCCM wenyewe hawaoni mtu wa kupambana na ufisadi ndani ya chama hicho hatujui ni kwa kiasi gani tunaweza kuwa na viongozi watakaoendelea kuonyesha ubabe na ufidhuli kwa wale wanaotutaka tuwe mashoga na wasenge katika dunia hii ieleekeayo kwenye maangamizi ya Sodom na Gomorrah.
Sunday, October 9, 2011
Tumuenzi vipi Mwalimu Nyerere miaka 12 baada ya kifo chake....
YAPO mengi tunayoweza kuzungumza kama njia za kumuenzi Baba wa Taifa, Julius K. Nyerere miaka 12 baada ya kifo chake. Binafsi ninaamini haya nitakayoyaorodhesha hapa chini yanaweza kuwa ni changamoto ambazo kwazo tunaweza kumuenzi kikwelikweli kiongozi huyo wa Afrika na siyo Tanzania pekee.
Kitu cha kwanza, ni kuirithi na kuiboresha visheni aliyokuwa nayo baba taifa kuhusu Tanzania na Afrika na nafasi yao katika dunia hii ya ubepari na utandawazi.
Mwalimu anatarajia kuwa viongozi wa nchi hii waliotangulia na wa sasa, watachangia sio haba kuleta umoja wa Afrika Mashariki na wa ule wa Afrika na kwamba katika maeneo hayo yote, Tanzania, itakuwa mstari wa mbele na sio vinginevyo. Tuliyoyaona hivi karibuni ni kinyume cha hivyo. Tanzania imekuwa mstari wa mbele katika kuenzi na kufuata na pengine hata kutetea maslahi ya nchi kubwa duniani kama vile Marekani na Uingereza; na ya mwisho katika kuenzi na kutetea yale yanayohusu wananchi wa Afrika, lakini mstari wa mbele katika kutetea maslahi ya viongozi fulani wa Afrika, hata kama viongozi wao wanawatendea isivyo haki wananchi wao. Siamini kama jambo hili linamfurahisha baba wa taifa huko aliko. Nyerere aliwaweka wananchi wa Afrika mbele na sio viongozi wao! Maana alijifunza mengi kutokana na viongozi wababe wa Nigeria, Uganda na Kongo.
Utu, uungwana, ubinadamu na kutopenda makuu ni baadhi ya sifa alizokuwa nazo baba wa taifa. Inatia mashaka kama sifa hizi bado zinaenziwa na viongozi wetu walioko madarakani na viongozi wastaafu. Na matokeo yake yanaonekana kila kona ya nchi, nayo ni yale wananchi kukosa imani na siasa na wanasiasa kiasi cha asilimia chini ya 30 ya wananchi wa Igunga wanaostahili kupiga kura kujitokeza katika zoezi hili. Hapa kuna mambo na wala sio jambo. Ni vizuri viongozi walioko na waliokuwepo enzi hizo wajichunguze, wachunguze wengine na wachunguzane ili kujua kama kile tunachowatendea wananchi wa Tanzania kinaleta jumla na majibu yanayokubalika au tunawapotezea tu wananchi wakati wao.
Azimio la Arusha lina mambo mengi ambayo kwayo Mwalimu Nyerere anaweza akaenziwa miaka mingi baada ya kizazi hiki kinachotawala na kitakachotawala baada ya kuondoka duniani. Mambo hayo ni pamoja na kuenzi elimu ya kujitegemea; kuzuia kukua kupindukia kwa tofauti kati ya walionacho na wasionacho kiutawala na kikodi na sio kimaguvu; kuwapa uhuru wakulima na wazalishaji mali wengine; kufufua kisomo cha watu wazima; kujenga siasa za demokrasia ya kijamii ambayo inawaruhusu watu kuwa na sauti kuliko serikali kuu; na kuwaendeleza vijana wa Kitanzania kushika nafasi zao wanazostahili kama viongozi wa dunia katika miaka ya ubepari na utandawazi.
Maendeleo vijijini. Baba wa taifa aliwajali sana wakulima na wanavijiji. Ingawa jaribio lake la kuanzisha vijiji vya kisasa kupitia ujamaa vijijini lilishindwa, siyo yeye aliyeshindwa bali ni Watanzania na hususan viongozi waliomfuatia. Wakati vijiji vya ujamaa vya Israel 'Kibutz' leo ni vijiji vya kisasa na kivutio cha utalii kikubwa nchini, swali ni, je, waliomfuatia Nyerere waliamini na wanaamini kwamba vijiji bado haviwezi kuendelezwa kwa faida ya wanavijiji na nchi kwa ujumla, maana maneno ni mengi kuliko vitendo pale suala la maendeleo vijijini linapozungumziwa. Ninaimani kwamba bado maendeleo vijijini ni ufunguo wa nchi hii kutoka nchi ya ulimwengu wa nne na kuwa nchi ya angalau ulimwengu wa tatu.
Madaraka mikoani. Mwalimu tofauti na viongozi waliomfuatia na waliopo alitambua kwamba kadri Watanzania wengi wanavyoelimika na kufunguliwa macho na teknolojia mpya basi watazidi kudai haki na uhuru wa kutawala mambo yao wenyewe. Kwa kulitambua hili ndio maana akaanzisha sera ya madaraka mikoani kwa maana kwamba sio mikoa tu bali pia wilaya, tarafa na vijiji na kata vingelikuwa na maamuzi ya mwisho kuhusu jinsi ya kuendesha kiuchumi na kijamii maeneo yao bila kuingiliwa bila sababu na serikali kuu. Hivi sasa, inaelekea kwamba pamoja na kubadili majina na mbwembwe za kila aina mipango na sera inayozingatia kiukweli madaraka mikoani hamna na mambo yanajiendea tu kwa kudra ya Mwenyezi Mungu. Hili lina hatari kubwa ya shinikizo la mabadiliko sasa kutoka kwa wananchi wenyewe, na hasa pale serikali itakapoendelea kuchelewa na kukosa msukumo wa sio tu kupanga bali kusimamia na kudhibiti zoezi zima la madaraka mikoani kwa faida ya wakazi wa miko na nchi nzima.
Mojawapo ya sifa kubwa aliyokuwa nayo Baba wa taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ni kuwachukulia wanawe wa kuzaa kama sehemu ya wanawe wa kutawala. Wakina Anna, Rose na Madaraka hawakuwazidi kitu watoto wengine wa Kitanzania. Kinachojitokeza sasa si hivyo. Na hili kila mtu analijua na hatuna sababu ya kuliongelea na hususan katika chama tawala ambapo tunaona dhahiri mashindano ya baadhi ya viongozi kuwarithisha watoto wao uongozi wa chama na pengine nchi bila kujali wana uwezo au hawana uwezo. Tungevuta hatua moja nyuma na kutafakari yale yanayotokea huko Uarabuni na jinsi nchi yetu inavyoweza kuathirika kama baadhi ya wazazi viongozi wataendelea na msimamo na mtazamo walio nao sasa.
Elimu. Nyerere alichukulia elimu kama haki ya kila mtoto wa Kitanzania. Alijua nchi ni masikini. Na wale waliopewa elimu kwake walifananishwa na wanavijiji kwenye vijiji vyenye njaa waliopewa chakula chote na kijiji ili kwenda kijiji cha mbali kutafuta chakula cha kuja kuwanusuru watu wake. Mtazamo na msimamo wetu hivi leo ni tofauti. Kwa Watanzania wengi hivi leo elimu ni ufunguo wa kuzidisha ubinafsi wao na kujionesha wao, watoto wao na familia zao ni bora kuliko za Watanzania wengine. Na elimu na malezi ya watoto leo yanaelekea pengine kutokana na sera ya ubinafsishaji kubinafsishwa zaidi kwa madhara makubwa baadaye kwa taifa na mustakabali wake.
Kiongozi anayeona giza tu katika handaki la elimu ana tatizo. Kwa kuwa anaona giza hawezi tena kuongoza watu wakaiona nuru.
Kwa kuwa elimu haina mwisho, tatizo sio wingi wa wenye digrii mbili, madaktari na maprofesa bali kile watu hao wanachopangiwa ili kuitoa Tanzania kwenye nchi ya ulimwengu wa nne na kuifanya nchi ya ulimwengu wa tatu.
Uchumi uwe mikononi mwa Watanzania. Kama kuna jambo ambalo Nyerere alisikitika kutokuliona basi pengine ni lile la kuona uchumi wa Tanzania ukiwa chini ya Watanzania wenyewe na sio chini ya wawekezaji na wageni toka nje tu. Kumuenzi Nyerere lazima viongozi na nchi iwe na mipango na sera zinazolenga 'kuutanzania' uchumi na maendeleo yetu kwa kiasi kikubwa zaidi.
Kubwa zaidi ni lile la elimu tunayoitoa kulenga kutatua matatizo ya Watanzania na sio vinginevyo. Ni kichekesho hivi leo kuwa na wasomi wasiojua kutengeneza kitu chochote tunachokitumia, wahandisi wasioweza kutengeneza barabara wala reli wala madaraja; wahandisi umeme wasioweza kujiunga wakatatua matatizo ya umeme ya Watanzania; wahandisi wa maji wanaoshindwa kutupa huduma ya kuridhisha ya maji; wahandisi wanaoshindwa kutujengea bandari na viwanja vya ndege vizuri na salama na vyenye kufanana na mazingira na utamaduni wetu na kadhalika.
Teknolojia, sayansi na kwenda na wakati. Nyerere alienzi sana sayansi na teknolojia na hususan kwa maendeleo vijijini. Ili kumuenzi ni lazima tuhakikishe kuwa teknolojia na sayansi zilizopo nchini hivi leo zinarahisishiwa kufika na kutumiwa huko vijijini kwa faida ya Wanavijiji na wakulima na nchi kwa ujumla.
Jamii na Kujitegemea. Sifa ambayo hakuna kiongozi mwingine wa Tanzania amewahi kuipata ni ile ya Nyerere kuwa kiongozi pekee aliyetambua kwamba hatuwezi kutegemea fedha kwa maendeleo yetu. Kwa maneno yake mwenyewe: Fedha sio msingi wa maendeleo! Ni kwa kutambua hili ndio maana mwalimu akawa anapigia debe sana mchango wa hali na mali toka kwa wananchi katika maendeleo yao wenyewe. Serikali inayojiweka katika nafasi kwamba inaweza kuwafanzia kila kitu Watanzania sio serikali inayowatakia mema Watanzania. Inakotupeleka ni kule ambako leo Ugiriki inakokanyaga. Je, huku ndiko tunakotaka kwenda?
Mali asili, madini na uwekezaji. Mwalimu angelitamani sana kuona maliasili yetu, madini na majaliwa mengine yanatumika kwa faida ya Watanzania wote na sio kwa faida ya wawekezaji wachache, mangimeza wa serikali na vibarakala wao. Hali ilivyo hivi leo, hili linaonekana kuwa mbali sana na viongozi wetu wote, wastaafu kwa waliopo wanaokena zaidi kujali kujinufaisha wao na jamaa zao na sio Watanzania wote kwa ujumla kwa hatari na mikosi mingi isiyostahili kabisa kuwepo.
Umoja wa Afrika wenye maslahi ya wananchi na
sio ya viongozi wabovu kulindana. Kama mwanzilishi wa Umoja wa Afrika siamini kama mwalimu alitaka AU iwe klabu ya viongozi wazuri kwa wabaya kulindana na kupeana muda zaidi kuwagandamiza Waafrika wenzao. Mtazamo na mategemeo ya mwalimu yalikuwa kuona nchi za Kiafrika zikitawaliwa na viongozi wenye uchungu na wananchi wao na wasiotumiwa na viongozi au nchi za nje kuwanyonya na kuwagandamiza watu wao. Mwalimu akifufuka leo atasikitika kukuta hata zile nchi zilizosaidiwa na Tanzania kuwa huru na viongozi waliosomeshwa hapa Tanzania wamo katika mkumbo wa uroho wa madaraka, udikteta na kuwanyonya, kuwatesa, kuwadhulumu na kuwagandamiza watu wao.
Kama kuna kitu kitakachomkasirisha Baba wa taifa ni kukuta Tanzania ya leo ina viongozi wa juu wa kitaifa wastaafu ambao pamoja na usomi wao kwa sababu za kibinafsi wanaoendeleza siasa za kichama na wanajiingiza kuvuruga umoja na amani ya taifa hili.
Kitu cha kwanza, ni kuirithi na kuiboresha visheni aliyokuwa nayo baba taifa kuhusu Tanzania na Afrika na nafasi yao katika dunia hii ya ubepari na utandawazi.
Mwalimu anatarajia kuwa viongozi wa nchi hii waliotangulia na wa sasa, watachangia sio haba kuleta umoja wa Afrika Mashariki na wa ule wa Afrika na kwamba katika maeneo hayo yote, Tanzania, itakuwa mstari wa mbele na sio vinginevyo. Tuliyoyaona hivi karibuni ni kinyume cha hivyo. Tanzania imekuwa mstari wa mbele katika kuenzi na kufuata na pengine hata kutetea maslahi ya nchi kubwa duniani kama vile Marekani na Uingereza; na ya mwisho katika kuenzi na kutetea yale yanayohusu wananchi wa Afrika, lakini mstari wa mbele katika kutetea maslahi ya viongozi fulani wa Afrika, hata kama viongozi wao wanawatendea isivyo haki wananchi wao. Siamini kama jambo hili linamfurahisha baba wa taifa huko aliko. Nyerere aliwaweka wananchi wa Afrika mbele na sio viongozi wao! Maana alijifunza mengi kutokana na viongozi wababe wa Nigeria, Uganda na Kongo.
Utu, uungwana, ubinadamu na kutopenda makuu ni baadhi ya sifa alizokuwa nazo baba wa taifa. Inatia mashaka kama sifa hizi bado zinaenziwa na viongozi wetu walioko madarakani na viongozi wastaafu. Na matokeo yake yanaonekana kila kona ya nchi, nayo ni yale wananchi kukosa imani na siasa na wanasiasa kiasi cha asilimia chini ya 30 ya wananchi wa Igunga wanaostahili kupiga kura kujitokeza katika zoezi hili. Hapa kuna mambo na wala sio jambo. Ni vizuri viongozi walioko na waliokuwepo enzi hizo wajichunguze, wachunguze wengine na wachunguzane ili kujua kama kile tunachowatendea wananchi wa Tanzania kinaleta jumla na majibu yanayokubalika au tunawapotezea tu wananchi wakati wao.
Azimio la Arusha lina mambo mengi ambayo kwayo Mwalimu Nyerere anaweza akaenziwa miaka mingi baada ya kizazi hiki kinachotawala na kitakachotawala baada ya kuondoka duniani. Mambo hayo ni pamoja na kuenzi elimu ya kujitegemea; kuzuia kukua kupindukia kwa tofauti kati ya walionacho na wasionacho kiutawala na kikodi na sio kimaguvu; kuwapa uhuru wakulima na wazalishaji mali wengine; kufufua kisomo cha watu wazima; kujenga siasa za demokrasia ya kijamii ambayo inawaruhusu watu kuwa na sauti kuliko serikali kuu; na kuwaendeleza vijana wa Kitanzania kushika nafasi zao wanazostahili kama viongozi wa dunia katika miaka ya ubepari na utandawazi.
Maendeleo vijijini. Baba wa taifa aliwajali sana wakulima na wanavijiji. Ingawa jaribio lake la kuanzisha vijiji vya kisasa kupitia ujamaa vijijini lilishindwa, siyo yeye aliyeshindwa bali ni Watanzania na hususan viongozi waliomfuatia. Wakati vijiji vya ujamaa vya Israel 'Kibutz' leo ni vijiji vya kisasa na kivutio cha utalii kikubwa nchini, swali ni, je, waliomfuatia Nyerere waliamini na wanaamini kwamba vijiji bado haviwezi kuendelezwa kwa faida ya wanavijiji na nchi kwa ujumla, maana maneno ni mengi kuliko vitendo pale suala la maendeleo vijijini linapozungumziwa. Ninaimani kwamba bado maendeleo vijijini ni ufunguo wa nchi hii kutoka nchi ya ulimwengu wa nne na kuwa nchi ya angalau ulimwengu wa tatu.
Madaraka mikoani. Mwalimu tofauti na viongozi waliomfuatia na waliopo alitambua kwamba kadri Watanzania wengi wanavyoelimika na kufunguliwa macho na teknolojia mpya basi watazidi kudai haki na uhuru wa kutawala mambo yao wenyewe. Kwa kulitambua hili ndio maana akaanzisha sera ya madaraka mikoani kwa maana kwamba sio mikoa tu bali pia wilaya, tarafa na vijiji na kata vingelikuwa na maamuzi ya mwisho kuhusu jinsi ya kuendesha kiuchumi na kijamii maeneo yao bila kuingiliwa bila sababu na serikali kuu. Hivi sasa, inaelekea kwamba pamoja na kubadili majina na mbwembwe za kila aina mipango na sera inayozingatia kiukweli madaraka mikoani hamna na mambo yanajiendea tu kwa kudra ya Mwenyezi Mungu. Hili lina hatari kubwa ya shinikizo la mabadiliko sasa kutoka kwa wananchi wenyewe, na hasa pale serikali itakapoendelea kuchelewa na kukosa msukumo wa sio tu kupanga bali kusimamia na kudhibiti zoezi zima la madaraka mikoani kwa faida ya wakazi wa miko na nchi nzima.
Mojawapo ya sifa kubwa aliyokuwa nayo Baba wa taifa, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ni kuwachukulia wanawe wa kuzaa kama sehemu ya wanawe wa kutawala. Wakina Anna, Rose na Madaraka hawakuwazidi kitu watoto wengine wa Kitanzania. Kinachojitokeza sasa si hivyo. Na hili kila mtu analijua na hatuna sababu ya kuliongelea na hususan katika chama tawala ambapo tunaona dhahiri mashindano ya baadhi ya viongozi kuwarithisha watoto wao uongozi wa chama na pengine nchi bila kujali wana uwezo au hawana uwezo. Tungevuta hatua moja nyuma na kutafakari yale yanayotokea huko Uarabuni na jinsi nchi yetu inavyoweza kuathirika kama baadhi ya wazazi viongozi wataendelea na msimamo na mtazamo walio nao sasa.
Elimu. Nyerere alichukulia elimu kama haki ya kila mtoto wa Kitanzania. Alijua nchi ni masikini. Na wale waliopewa elimu kwake walifananishwa na wanavijiji kwenye vijiji vyenye njaa waliopewa chakula chote na kijiji ili kwenda kijiji cha mbali kutafuta chakula cha kuja kuwanusuru watu wake. Mtazamo na msimamo wetu hivi leo ni tofauti. Kwa Watanzania wengi hivi leo elimu ni ufunguo wa kuzidisha ubinafsi wao na kujionesha wao, watoto wao na familia zao ni bora kuliko za Watanzania wengine. Na elimu na malezi ya watoto leo yanaelekea pengine kutokana na sera ya ubinafsishaji kubinafsishwa zaidi kwa madhara makubwa baadaye kwa taifa na mustakabali wake.
Kiongozi anayeona giza tu katika handaki la elimu ana tatizo. Kwa kuwa anaona giza hawezi tena kuongoza watu wakaiona nuru.
Kwa kuwa elimu haina mwisho, tatizo sio wingi wa wenye digrii mbili, madaktari na maprofesa bali kile watu hao wanachopangiwa ili kuitoa Tanzania kwenye nchi ya ulimwengu wa nne na kuifanya nchi ya ulimwengu wa tatu.
Uchumi uwe mikononi mwa Watanzania. Kama kuna jambo ambalo Nyerere alisikitika kutokuliona basi pengine ni lile la kuona uchumi wa Tanzania ukiwa chini ya Watanzania wenyewe na sio chini ya wawekezaji na wageni toka nje tu. Kumuenzi Nyerere lazima viongozi na nchi iwe na mipango na sera zinazolenga 'kuutanzania' uchumi na maendeleo yetu kwa kiasi kikubwa zaidi.
Kubwa zaidi ni lile la elimu tunayoitoa kulenga kutatua matatizo ya Watanzania na sio vinginevyo. Ni kichekesho hivi leo kuwa na wasomi wasiojua kutengeneza kitu chochote tunachokitumia, wahandisi wasioweza kutengeneza barabara wala reli wala madaraja; wahandisi umeme wasioweza kujiunga wakatatua matatizo ya umeme ya Watanzania; wahandisi wa maji wanaoshindwa kutupa huduma ya kuridhisha ya maji; wahandisi wanaoshindwa kutujengea bandari na viwanja vya ndege vizuri na salama na vyenye kufanana na mazingira na utamaduni wetu na kadhalika.
Teknolojia, sayansi na kwenda na wakati. Nyerere alienzi sana sayansi na teknolojia na hususan kwa maendeleo vijijini. Ili kumuenzi ni lazima tuhakikishe kuwa teknolojia na sayansi zilizopo nchini hivi leo zinarahisishiwa kufika na kutumiwa huko vijijini kwa faida ya Wanavijiji na wakulima na nchi kwa ujumla.
Jamii na Kujitegemea. Sifa ambayo hakuna kiongozi mwingine wa Tanzania amewahi kuipata ni ile ya Nyerere kuwa kiongozi pekee aliyetambua kwamba hatuwezi kutegemea fedha kwa maendeleo yetu. Kwa maneno yake mwenyewe: Fedha sio msingi wa maendeleo! Ni kwa kutambua hili ndio maana mwalimu akawa anapigia debe sana mchango wa hali na mali toka kwa wananchi katika maendeleo yao wenyewe. Serikali inayojiweka katika nafasi kwamba inaweza kuwafanzia kila kitu Watanzania sio serikali inayowatakia mema Watanzania. Inakotupeleka ni kule ambako leo Ugiriki inakokanyaga. Je, huku ndiko tunakotaka kwenda?
Mali asili, madini na uwekezaji. Mwalimu angelitamani sana kuona maliasili yetu, madini na majaliwa mengine yanatumika kwa faida ya Watanzania wote na sio kwa faida ya wawekezaji wachache, mangimeza wa serikali na vibarakala wao. Hali ilivyo hivi leo, hili linaonekana kuwa mbali sana na viongozi wetu wote, wastaafu kwa waliopo wanaokena zaidi kujali kujinufaisha wao na jamaa zao na sio Watanzania wote kwa ujumla kwa hatari na mikosi mingi isiyostahili kabisa kuwepo.
Umoja wa Afrika wenye maslahi ya wananchi na
sio ya viongozi wabovu kulindana. Kama mwanzilishi wa Umoja wa Afrika siamini kama mwalimu alitaka AU iwe klabu ya viongozi wazuri kwa wabaya kulindana na kupeana muda zaidi kuwagandamiza Waafrika wenzao. Mtazamo na mategemeo ya mwalimu yalikuwa kuona nchi za Kiafrika zikitawaliwa na viongozi wenye uchungu na wananchi wao na wasiotumiwa na viongozi au nchi za nje kuwanyonya na kuwagandamiza watu wao. Mwalimu akifufuka leo atasikitika kukuta hata zile nchi zilizosaidiwa na Tanzania kuwa huru na viongozi waliosomeshwa hapa Tanzania wamo katika mkumbo wa uroho wa madaraka, udikteta na kuwanyonya, kuwatesa, kuwadhulumu na kuwagandamiza watu wao.
Kama kuna kitu kitakachomkasirisha Baba wa taifa ni kukuta Tanzania ya leo ina viongozi wa juu wa kitaifa wastaafu ambao pamoja na usomi wao kwa sababu za kibinafsi wanaoendeleza siasa za kichama na wanajiingiza kuvuruga umoja na amani ya taifa hili.
Sunday, September 25, 2011
Elimu: Jamii na serikali muhimu kushirikiana kwa maendeleo zaidi.
UUNGWANA, pamoja na mambo mengine ni kuona na kusifu kile ambacho mmojawetu ameweza kukifanikisha katika maisha yake kwa faida ya wanajamii wenzake. Mojawapo ni mchango wa serikali katika maendeleo ya elimu hususan ule ambao umechangiwa na uongozi wa awamu ya nne toka uingie madarakani 2005.
Hakuna kilicho kamili katika dunia hii. Ndio maana mafanikio katika sekta ya elimu nchini hivi sasa yanaibua mijadala mingi inayobainisha udhaifu na kasoro zilizopo, wingi wa mawazo na mapendekezo mbalimbali juu ya nini kifanyike na kadhalika.
Mafanikio yaliyopatikana katika elimu Tanzania hadi wa leo, yanaiweka Tanzania katika nafasi nzuri ya kuwa na zaidi ya watoto milioni 1.5 katika shule za msingi, milioni moja katika shule za sekondari na laki mbili au tatu katika vyuo vikuu kila mwaka. Kinachotakiwa ni kujipanga vizuri kwa kukuza ushirikiano kati ya serikali, sekta binafsi na wanajamii kwenye maeneo shule au vyuo vilivyoko.
Elimu kama zilivyo sekta nyingine inahitaji rasilimali watu bora zaidi; majengo na rasilimali zisizo hai, safi, nzuri na bora na zinaboreshwa kila siku; uongozi au menejimenti bora zaidi kila siku; mafanikio makubwa zaidi katika matokeo ya kazi za watumishi katika sekta husika na matokeo mazuri ya kimasomo kwa upande wa wanafunzi.
Katika baadhi ya nchi za Kiafrika kama ilivyo kwenye nchi nyingi zinazoendelea, tabia moja mbaya sana imekuwa ikikubalika bila kuhojiwa na tabia hiyo kwa kiasi kikubwa inachangia zaidi matatizo kuliko kupatikana kwa ufumbuzi wa matatizo. Inadumaza maendeleo ya watu na jamii, wakati mwingine hata wakubwa wa nchi bila kujua kinachoendelea.
Tabia hiyo siyo nyingine ila ni ile ya serikali na chama tawala kujifanya ndio taasisi pekee zenye uwezo wa kifedha, kiufundi, kiutaalamu, kimamlaka na kirasilimali kuwezesha jambo lolote kufanyika na kwamba eti wanajamii hawana uono au uwezo kama huo ambao chama tawala na serikali yake walio nao.
Huu ni uzushi, utapeli, ulaghai na uongo mtupu. Wanaostahili kuwa na uwezo, fedha na rasilimali ni wanajamii wenyewe kupitia kodi zao mbalimbali zinazowezesha kuwepo kwa serikali. Serikali kama yalivyo makundi mengine katika jamii ni kundi la watu wa matumizi na hata wakati mwingine matanuzi yasiyoisaidia kitu jamii.
Upo ulazima wa kuwaelimisha watu juu ya ukweli huu, uwezo, nguvu na rasilimali walizonazo na jinsi utofauti katika hili unavyoweza kuwaondoa wananchi kutoka hali ya uhitaji na unyonge na kuwaweka sio tu kwenye nafasi ya kujitosheleza katika mahitaji yao ya msingi bali pia katika nafasi nzuri na isiyoterereka ya kuhoji utendaji, ufanisi na ufanifu wa serikali, viongozi wake na wa chama tawala.
Ili uamsho huu uweze kufanya kazi na kuzaa matunda yanayotarajiwa ni muhimu kwa taasisi zisizo za kiserikali na wanaharakati wote kwa ujumla kuwa na programu za kuwaamsha wananchi kwa kuwabainishia kuwa wao ndio wenye uwezo wa kubadili maisha yao na vizazi vyao na sio vinginevyo. Na rasilimali zote za nchi zinastahili kuwa zao na zinazochangia kuleta mabadiliko tarajiwa.
Si haki nchi iuze almasi au dhahabu au ardhi yake kisha wananchi wadanganywe kwa pipi, halua, chandalua zenye dawa na kondomu!!!
Ili sekta ya elimu iweze kupata mafanikio ni lazima wazazi waambiwe, watambue na wakubali kwamba wao binafsi wana mchango mkubwa katika shule na vyuo vilivyopo. Na kwamba ili mchango huu uanze kupatikana na kufanya kazi ni lazima wawe na taasisi, uongozi, mifumo na taratibu zinazofanya kazi. Bila hivyo, itakuwa sio rahisi kwa uwezo na nguvu waliyonayo kuonekana dhahiri, kukubalika na kuheshimiwa na washikadau wengine ikiwemo serikali, wahisani na taasisi binafsi na za kidini.
Kwa mfano, hivi leo panahitajika haraka sana: 'Taasisi ya Wazazi wenye Wanafunzi Mashuleni na Vyuoni' kuliko wakati mwingine wowote huko nyuma ili kutetea na kulinda maslahi ya wazazi na watoto wao wanaosoma katika taasisi mbalimbali ikiwemo usalama kwenye taasisi hizo, ubora wa elimu, mafunzo na walimu au wahadhiri, ubora wa malazi, ubora wa vyakula, usalama wa maji na haki na uhalali wa ada na gharama nyingine zinazolipwa ili wazazi kupuka kutapeliwa na shule za msingi, shule za sekondari, vyuo na vyuo vikuu feki au vibabaishaji.
Jamii inaweza isiridhike na shule na vyuo vilivyopo na ikaamua kuwekeza na kuanzisha shule na vyuo vyake ambavyo vitakuwa bora zaidi kuliko ilivyo hivi sasa. Jambo hili si jipya duniani. Baadhi yaWamarekani walipoanza kuchakachua elimu na kutoa elimu isiyohitajika na soko la ajira, jamii mbalimbali za KImarekani zilianza kuanzisha shule za msingi za kijamii na kisha wakaanzisha sekondari na vyuo vikiuu vya kijamii na hivi leo taasisi hizo ni kati ya zile zinazong'ara nchini Marekani.
Lakini ilimradi vile vilivyopo vinajikusuru, basi ni vizuri zaidi Taasisi kama hiyo ya wazazi wenye wanafunzi wanaosoma ikawepo ili kusimamia, kushinikiza na kutoa chachu ya mabadiliko, ukuaji na maendeleo kwa taasisi zote za elimu zilizopo.
Ni muhimu pia serikali kutambua kwamba haina ubavu, nguvu, rasilimali na mitaji ya kutosha kuweza kufanya kila kitu peke yake kwa yote yale wananchi wanayoyahitaji. Kwa namna moja au nyingine, lazima ikiri hadharani, kama ilivyofanya kwa kuinyima ukiritimba TANESCO, juu ya lile lililoonekana kushindwa kuendelea kwa serikali kulibeba achilia mbali kulifufua shirika hilo na hivyo kufungua milango kwa watu wa ndani na nje kuwekeza katika uzalishaji, usambazaji na uuzaji umeme kama soko huru linavyotushuritisha.
Ndivyo inavyotakiwa pia kwa serikali mapema iwezekanavyo
kutoa wito kwa wananchi kila inapowezekana kuwekeza, kuendesha, kusimamia na kusaidia shule zilizopo kwenye maeneo yao kwa faida ya nchi na watu wake. Kwa maneno mengine, serikali inapaswa kutamka bila kusita kwamba wazazi na wanajamii kwa ujumla wana sababu, uwezo na shuruti ya kusaidia kwa hali na mali, maendeleo ya shule za kata na nyinginezo ili kuboresha sio tu hali za shule husika bali pia utawala au menejimenti na matokeo ya mitihani ya shule husika kimkoa, kitaifa na kimataifa. Shule, kwa maneno mengine, 'sio shule za serikali tu' ni shule za wananchi au wanajamii wa maeneo husika.
Wanajamii ndio wanaoweza kusifanya zifanye vizuri na kufanikiwa au kuziangusha. Upo ushahidi wa kutosha kwamba ushiriki wa wanajamii katika usimamizi na uendeshaji wa shule huchangia sio haba kupunguza matatizo mbalimbali yanayokabili shule, walimu na wanafunzi.
Na kwamba mchango wa hali na mali wa wanajamii katika maeneo hayo unahitajika na unakubalika. Wanajamii wakishirikiana na walimu au wahadhiri na wakuu wa taasisi husika wanaweza 'wakakomisheni 'tafiti mbalimbali ili kuona nini kinachoendelea, kisichostahili kuwepo na ukubwa au upana wa pengo lililopo na mabadiliko yanayotakikana,ili kuongeza ubora katika sekta ya elimu kwenye maeneo mbalimbali.
Baadhi ya mambo ya kutafiti na kufanyia kazi ni pamoja na je, Idadi ya masomo yaliyopo ni sahihi? Mitaala na silabasi zilizopo zinakidhi haja zetu? Je, masomo hayo yana manufaa kimaisha? Je, yatamsaidia mwanafunzi wa leo kuja kujiajiri au kuajiriwa? Je, sio vyema wanafunzi
kuchagua masomo machache kuendana na kipaji, uwezo wa mwanafunzi na kile anachokipenda kuwa katika maisha yake hapo baadaye?
Aidha ni lazima kupata majibu kwa maswali kama, je, alama za kiwango cha kufaulu ni sahihi na cha haki?
Je, kurudia darasa kiwango cha kufaulu kisipofikiwa sio jambo zuri na kwa faida ya mwanfunzi kuliko kuwa na mwanafunzi anayeingia darasa la pili lakini hana uwezo wa mwanafunzi wa chekechea ?
Je, idadi ya wanafunzi darasani ni sawa? Je, idadi ya walimu waliopo katika shule ni sawa? Je, muundo na mifumo iliyopo inaruhusu viranja, viongozi na wasimamizi wa shule kufanya kazi bila uonevu au upendeleo? Je chakula, kifungua kinywa, maji na lishe ya wanafunzi inaendana na hali ya maisha leo? Je, majengo na huduma stahilivu yana viwango vinavyokubalika na vinaendelea kuboreshwa kila siku, au shule au vyuo havina sera ya uchakavu na majengo yao yanatisha na kusikitisha? Na, je, mtoto wa Kimalawi au Kizambia au Kikongo au Kirundi au Kinyarwanda achilia mbali Kiganda na Kikenya anaweza kujiunga na shule au vyuo vyote na wazazi wake wakaridhika kwa elimu na huduma za msingi atakazopata?
Je, unyapara na hususan ule wa ukaguzi katika sekta ya elimu sio kitu chema na kinachohitajika wakati wote?
Na ni kwa mikakati na mbinu gani zinazoweza kutumika ili kuboesha kipato cha walimu na maupurupu yao bila kuwalazimisha kutafuta njia za mikato na zisizo na tija kitaifa na kijamii?
Je, katika jiji kama Dar es salaam kupanga ratiba za masomo ya shule za msingi na sekondari kuanza saa 12 alfajiri na kukoma kwenye saa sita au saba hakutapunguza tatizo la kunyanyapaliwa wanafunzi na wenye daladala na hivyo kuathiri maendeleo ya darasani na kwenye mitihani ? Na je, kuwa na kalenda ya shule na vyuo vyote katika elimu kwa masomo, likizo, sikukuu mitihani, michezo, michuano ya michezo mbalimbali, safari za kimasomo, muda wa masomo kwa vitendo, ukarabati, ukaguzi, ununuzi na usambazaji wa vitabu ni jambo litakalosaidia maendeleo ya elimu au la?
Je, kupunguza masaa ya shule au kuyagawa kati ya mafunzo na michezo hakutachangia kumkuza mtoto kimwili na kiakili kwa mapana na marefu zaidi?
Je, wanajamii wenye elimu, ujuzi, maarifa na uwezo mbalimbali ambao sio walimu hawawezi kufanyiwa utaratibu wa kusaidia kufundisha pale kusiko na walimu wa kutosha?
Haya ni baadhi ya masuala ambayo yanaweza kuzungumzwa, kufanyiwa utafiti na makundi husika ya shinikizo katika elimu kuiwajibisha serikali iliyopo madarakani kufanya yale yanayohitajika na yanayowezekana bila ulegevu, uoga, uvivu, ubabaishaji, 'usiasaishaji', au ucheleweshaji wa aina yoyote? Ni kwa namna hii tu ndipo tutakapoweza kutoa majibu sahihi kwa changamoto zilizoko katika sekta ya elimu na mafunzo nchini kwa faida ya kizazi cha sasa na kizazi kijacho.Baba wa Taifa, J.K.Nyerere alituasa fedha si msingi wa maendeleo. Yapo yawezayo kufanywa kwa fedha na yapo yanayoweza kufanywa kwa utashi, akili, bidii, juhudi na nguvu za wanajamii husika.
Tukitegemea fedha kwa kila kitu hatutafika mbali.
Hakuna kilicho kamili katika dunia hii. Ndio maana mafanikio katika sekta ya elimu nchini hivi sasa yanaibua mijadala mingi inayobainisha udhaifu na kasoro zilizopo, wingi wa mawazo na mapendekezo mbalimbali juu ya nini kifanyike na kadhalika.
Mafanikio yaliyopatikana katika elimu Tanzania hadi wa leo, yanaiweka Tanzania katika nafasi nzuri ya kuwa na zaidi ya watoto milioni 1.5 katika shule za msingi, milioni moja katika shule za sekondari na laki mbili au tatu katika vyuo vikuu kila mwaka. Kinachotakiwa ni kujipanga vizuri kwa kukuza ushirikiano kati ya serikali, sekta binafsi na wanajamii kwenye maeneo shule au vyuo vilivyoko.
Elimu kama zilivyo sekta nyingine inahitaji rasilimali watu bora zaidi; majengo na rasilimali zisizo hai, safi, nzuri na bora na zinaboreshwa kila siku; uongozi au menejimenti bora zaidi kila siku; mafanikio makubwa zaidi katika matokeo ya kazi za watumishi katika sekta husika na matokeo mazuri ya kimasomo kwa upande wa wanafunzi.
Katika baadhi ya nchi za Kiafrika kama ilivyo kwenye nchi nyingi zinazoendelea, tabia moja mbaya sana imekuwa ikikubalika bila kuhojiwa na tabia hiyo kwa kiasi kikubwa inachangia zaidi matatizo kuliko kupatikana kwa ufumbuzi wa matatizo. Inadumaza maendeleo ya watu na jamii, wakati mwingine hata wakubwa wa nchi bila kujua kinachoendelea.
Tabia hiyo siyo nyingine ila ni ile ya serikali na chama tawala kujifanya ndio taasisi pekee zenye uwezo wa kifedha, kiufundi, kiutaalamu, kimamlaka na kirasilimali kuwezesha jambo lolote kufanyika na kwamba eti wanajamii hawana uono au uwezo kama huo ambao chama tawala na serikali yake walio nao.
Huu ni uzushi, utapeli, ulaghai na uongo mtupu. Wanaostahili kuwa na uwezo, fedha na rasilimali ni wanajamii wenyewe kupitia kodi zao mbalimbali zinazowezesha kuwepo kwa serikali. Serikali kama yalivyo makundi mengine katika jamii ni kundi la watu wa matumizi na hata wakati mwingine matanuzi yasiyoisaidia kitu jamii.
Upo ulazima wa kuwaelimisha watu juu ya ukweli huu, uwezo, nguvu na rasilimali walizonazo na jinsi utofauti katika hili unavyoweza kuwaondoa wananchi kutoka hali ya uhitaji na unyonge na kuwaweka sio tu kwenye nafasi ya kujitosheleza katika mahitaji yao ya msingi bali pia katika nafasi nzuri na isiyoterereka ya kuhoji utendaji, ufanisi na ufanifu wa serikali, viongozi wake na wa chama tawala.
Ili uamsho huu uweze kufanya kazi na kuzaa matunda yanayotarajiwa ni muhimu kwa taasisi zisizo za kiserikali na wanaharakati wote kwa ujumla kuwa na programu za kuwaamsha wananchi kwa kuwabainishia kuwa wao ndio wenye uwezo wa kubadili maisha yao na vizazi vyao na sio vinginevyo. Na rasilimali zote za nchi zinastahili kuwa zao na zinazochangia kuleta mabadiliko tarajiwa.
Si haki nchi iuze almasi au dhahabu au ardhi yake kisha wananchi wadanganywe kwa pipi, halua, chandalua zenye dawa na kondomu!!!
Ili sekta ya elimu iweze kupata mafanikio ni lazima wazazi waambiwe, watambue na wakubali kwamba wao binafsi wana mchango mkubwa katika shule na vyuo vilivyopo. Na kwamba ili mchango huu uanze kupatikana na kufanya kazi ni lazima wawe na taasisi, uongozi, mifumo na taratibu zinazofanya kazi. Bila hivyo, itakuwa sio rahisi kwa uwezo na nguvu waliyonayo kuonekana dhahiri, kukubalika na kuheshimiwa na washikadau wengine ikiwemo serikali, wahisani na taasisi binafsi na za kidini.
Kwa mfano, hivi leo panahitajika haraka sana: 'Taasisi ya Wazazi wenye Wanafunzi Mashuleni na Vyuoni' kuliko wakati mwingine wowote huko nyuma ili kutetea na kulinda maslahi ya wazazi na watoto wao wanaosoma katika taasisi mbalimbali ikiwemo usalama kwenye taasisi hizo, ubora wa elimu, mafunzo na walimu au wahadhiri, ubora wa malazi, ubora wa vyakula, usalama wa maji na haki na uhalali wa ada na gharama nyingine zinazolipwa ili wazazi kupuka kutapeliwa na shule za msingi, shule za sekondari, vyuo na vyuo vikuu feki au vibabaishaji.
Jamii inaweza isiridhike na shule na vyuo vilivyopo na ikaamua kuwekeza na kuanzisha shule na vyuo vyake ambavyo vitakuwa bora zaidi kuliko ilivyo hivi sasa. Jambo hili si jipya duniani. Baadhi yaWamarekani walipoanza kuchakachua elimu na kutoa elimu isiyohitajika na soko la ajira, jamii mbalimbali za KImarekani zilianza kuanzisha shule za msingi za kijamii na kisha wakaanzisha sekondari na vyuo vikiuu vya kijamii na hivi leo taasisi hizo ni kati ya zile zinazong'ara nchini Marekani.
Lakini ilimradi vile vilivyopo vinajikusuru, basi ni vizuri zaidi Taasisi kama hiyo ya wazazi wenye wanafunzi wanaosoma ikawepo ili kusimamia, kushinikiza na kutoa chachu ya mabadiliko, ukuaji na maendeleo kwa taasisi zote za elimu zilizopo.
Ni muhimu pia serikali kutambua kwamba haina ubavu, nguvu, rasilimali na mitaji ya kutosha kuweza kufanya kila kitu peke yake kwa yote yale wananchi wanayoyahitaji. Kwa namna moja au nyingine, lazima ikiri hadharani, kama ilivyofanya kwa kuinyima ukiritimba TANESCO, juu ya lile lililoonekana kushindwa kuendelea kwa serikali kulibeba achilia mbali kulifufua shirika hilo na hivyo kufungua milango kwa watu wa ndani na nje kuwekeza katika uzalishaji, usambazaji na uuzaji umeme kama soko huru linavyotushuritisha.
Ndivyo inavyotakiwa pia kwa serikali mapema iwezekanavyo
kutoa wito kwa wananchi kila inapowezekana kuwekeza, kuendesha, kusimamia na kusaidia shule zilizopo kwenye maeneo yao kwa faida ya nchi na watu wake. Kwa maneno mengine, serikali inapaswa kutamka bila kusita kwamba wazazi na wanajamii kwa ujumla wana sababu, uwezo na shuruti ya kusaidia kwa hali na mali, maendeleo ya shule za kata na nyinginezo ili kuboresha sio tu hali za shule husika bali pia utawala au menejimenti na matokeo ya mitihani ya shule husika kimkoa, kitaifa na kimataifa. Shule, kwa maneno mengine, 'sio shule za serikali tu' ni shule za wananchi au wanajamii wa maeneo husika.
Wanajamii ndio wanaoweza kusifanya zifanye vizuri na kufanikiwa au kuziangusha. Upo ushahidi wa kutosha kwamba ushiriki wa wanajamii katika usimamizi na uendeshaji wa shule huchangia sio haba kupunguza matatizo mbalimbali yanayokabili shule, walimu na wanafunzi.
Na kwamba mchango wa hali na mali wa wanajamii katika maeneo hayo unahitajika na unakubalika. Wanajamii wakishirikiana na walimu au wahadhiri na wakuu wa taasisi husika wanaweza 'wakakomisheni 'tafiti mbalimbali ili kuona nini kinachoendelea, kisichostahili kuwepo na ukubwa au upana wa pengo lililopo na mabadiliko yanayotakikana,ili kuongeza ubora katika sekta ya elimu kwenye maeneo mbalimbali.
Baadhi ya mambo ya kutafiti na kufanyia kazi ni pamoja na je, Idadi ya masomo yaliyopo ni sahihi? Mitaala na silabasi zilizopo zinakidhi haja zetu? Je, masomo hayo yana manufaa kimaisha? Je, yatamsaidia mwanafunzi wa leo kuja kujiajiri au kuajiriwa? Je, sio vyema wanafunzi
kuchagua masomo machache kuendana na kipaji, uwezo wa mwanafunzi na kile anachokipenda kuwa katika maisha yake hapo baadaye?
Aidha ni lazima kupata majibu kwa maswali kama, je, alama za kiwango cha kufaulu ni sahihi na cha haki?
Je, kurudia darasa kiwango cha kufaulu kisipofikiwa sio jambo zuri na kwa faida ya mwanfunzi kuliko kuwa na mwanafunzi anayeingia darasa la pili lakini hana uwezo wa mwanafunzi wa chekechea ?
Je, idadi ya wanafunzi darasani ni sawa? Je, idadi ya walimu waliopo katika shule ni sawa? Je, muundo na mifumo iliyopo inaruhusu viranja, viongozi na wasimamizi wa shule kufanya kazi bila uonevu au upendeleo? Je chakula, kifungua kinywa, maji na lishe ya wanafunzi inaendana na hali ya maisha leo? Je, majengo na huduma stahilivu yana viwango vinavyokubalika na vinaendelea kuboreshwa kila siku, au shule au vyuo havina sera ya uchakavu na majengo yao yanatisha na kusikitisha? Na, je, mtoto wa Kimalawi au Kizambia au Kikongo au Kirundi au Kinyarwanda achilia mbali Kiganda na Kikenya anaweza kujiunga na shule au vyuo vyote na wazazi wake wakaridhika kwa elimu na huduma za msingi atakazopata?
Je, unyapara na hususan ule wa ukaguzi katika sekta ya elimu sio kitu chema na kinachohitajika wakati wote?
Na ni kwa mikakati na mbinu gani zinazoweza kutumika ili kuboesha kipato cha walimu na maupurupu yao bila kuwalazimisha kutafuta njia za mikato na zisizo na tija kitaifa na kijamii?
Je, katika jiji kama Dar es salaam kupanga ratiba za masomo ya shule za msingi na sekondari kuanza saa 12 alfajiri na kukoma kwenye saa sita au saba hakutapunguza tatizo la kunyanyapaliwa wanafunzi na wenye daladala na hivyo kuathiri maendeleo ya darasani na kwenye mitihani ? Na je, kuwa na kalenda ya shule na vyuo vyote katika elimu kwa masomo, likizo, sikukuu mitihani, michezo, michuano ya michezo mbalimbali, safari za kimasomo, muda wa masomo kwa vitendo, ukarabati, ukaguzi, ununuzi na usambazaji wa vitabu ni jambo litakalosaidia maendeleo ya elimu au la?
Je, kupunguza masaa ya shule au kuyagawa kati ya mafunzo na michezo hakutachangia kumkuza mtoto kimwili na kiakili kwa mapana na marefu zaidi?
Je, wanajamii wenye elimu, ujuzi, maarifa na uwezo mbalimbali ambao sio walimu hawawezi kufanyiwa utaratibu wa kusaidia kufundisha pale kusiko na walimu wa kutosha?
Haya ni baadhi ya masuala ambayo yanaweza kuzungumzwa, kufanyiwa utafiti na makundi husika ya shinikizo katika elimu kuiwajibisha serikali iliyopo madarakani kufanya yale yanayohitajika na yanayowezekana bila ulegevu, uoga, uvivu, ubabaishaji, 'usiasaishaji', au ucheleweshaji wa aina yoyote? Ni kwa namna hii tu ndipo tutakapoweza kutoa majibu sahihi kwa changamoto zilizoko katika sekta ya elimu na mafunzo nchini kwa faida ya kizazi cha sasa na kizazi kijacho.Baba wa Taifa, J.K.Nyerere alituasa fedha si msingi wa maendeleo. Yapo yawezayo kufanywa kwa fedha na yapo yanayoweza kufanywa kwa utashi, akili, bidii, juhudi na nguvu za wanajamii husika.
Tukitegemea fedha kwa kila kitu hatutafika mbali.
Subscribe to:
Posts (Atom)